Halima na wenzake lazima watoboe. Msijidanganye kama watoto. Ukweli utajulikana nani alipeleka barua NEC

Kwa hiyo aliyetolewa mahabusu aliwekewa dhamana na Tume? Ni vigumu kuamini uchaguzi ilikuwa halali kwa matukio kabla ya uchaguzi akiwemo mgombea wa ccm kuchukua form ya mgombea urais kwa staili ile.Alihofu nini wakati alikuwa kipenzi cha wanyonge?
 
Naomba chondechonde msijitungie maneno yenu..mtaadhibiwa na Sheria ya mtandao

..hata wanaosema kina Halima wamefoji barua nao wanajitungia maneno.

..kwani imethibitishwa na nani kwamba kina Halima wamefoji barua?

..madai yangu yanatokana na taarifa za Cdm kwamba Nec wameshindwa kuwapa ushirikiano kuhusu barua / nyaraka za uteuzi wa kina Halima.

..Ndio maana mimi kwa mtizamo wangu naamini kina Halima hawakuwa na barua na hawakuteuliwa na Nec.
 
..Pascal maelezo yako sio ya kweli.

..Unapotosha, tena unafanya makusudi.

..hakuna kikao cha CC ya Cdm kilichoketi baada ya uchaguzi wa 2020 na kuteua wanachama 19 kuwa wabunge wa viti maalum.

..Katibu Mkuu Mnyika amesema hajawahi kusaini barua Halima na wenzake waende bungeni.

..Msemaji wa Cdm amedai Nec imeshindwa kuwapatia nyaraka zilizotumika kuwateua kina Halima.

..Kwa maelezo hayo, we have no other option, zaidi ya ku-conclude kwamba kina Halima hawakuteuliwa na chama wala tume kuwa wabunge wa viti maalum.

..Watu wanahangaika kutafuta " barua " na " aliyegushi" wakati hakukuwa na kitu kama hicho.
 
Mr. Famine is unfortunately on a wrong footing.
 
Mbona wakati mwingine unawaangusha wanasheria wenzio Pascal Mayalla ?!.

Kama walianguka vibaya kwa mujibu wa kauli yako. WalipataJe viti 19 vya bure ?! Je ni kweli mbunge hata wa kuchaguliwa jimboni akinyang'anywa uanachama ubunge wake hukoma ?!. Je viti maalumu akina Sophia Simba, alietimuliwa kwa usaliti wa kumuunga mkono Lowasa ubunge wao hukoma baada ya kutimuliwa uanachama ?!.

P. Kwanini Cdm idhibitiwe kutokuwadhibiti wanachama wake ?!. Yana mwisho. Bahati mbaya watu hawataki kujifunza .
 
Wew umethibitisha vipi kuwa hayo maelezo ya Mayala niya kweli? Maana alivyoandika utazani yeye ni alikuwa mjumbe au ni mjumbe wa vikao vyote vya maamuzi vya chadema.
Ukizielewa taratibu za upatikanaji wa hao wajumbe wala haikusumbui. Utaelewa fika jinsi walivyopatikana
 
Sasa hayo ndio majina yaliopelekwa?
 
Vipi bwana njaa bado hawajakupa teuzi?
 
..Pascal maelezo yako sio ya kweli.

..Unapotosha, tena unafanya makusudi.

..hakuna kikao cha CC ya Cdm kilichoketi baada ya uchaguzi wa 2020 na kuteua wanachama 19 kuwa wabunge wa viti maalum.
Uteuzi wa wabunge maalum kutoka vyama vyote na majina yanapelekwa NEC 30 days kabla ya uchaguzi. Chadema waliteua majina yao na kuyawasisha NEC, ni kikao gani kiliteua na kina nani waliteuliwa, that is purely Chadema internal matters, kitu cha muhimu hapa ni barua authentic bonafide genuine kutoka Chadema kwenda NEC ilipeleka hayo majina!. Barua hiyo iliandikwa na nani na kusainiwa na nani hayo sio yangu, hoja yangu ni majina halali 19 ya wanachama halali wa Chadema yalitua NEC na NEC ikawapa authentic bonafide genuine certificates za uteuzi na kuwapeleka bungeni, hivyo Bunge limepokea wabunge 19 halali kutoka NEC, wakaapishwa na sasa ni Wabunge halali kabisa bonafide genuine mpaka sasa!.
.Katibu Mkuu Mnyika amesema hajawahi kusaini barua Halima na wenzake waende bungeni.
Kitu muhimu kinacho matter kwenye any official confirmations ni authentication of the office bearers, as long as barua ni official letter yenye letter head ya Chadema, sio fake letter, sio forgery bali ni authentic bonafide genuine letter from Chadema to NEC, hata kama haijasainiwa na KM, ni barua authentic bonafide genuine na halali.

NB. Mfanyakazi yoyote wa Chadema mwenye access to official communication anaweza kuandika barua authentic bonafide genuine kwenye letter head ya Chadema na kufoji saini ya KM, JJMNYIKA, kwa kujifanya it's an official letter, na kuiwasilisha NEC kujifanya imetoka Chadema. If this is the case, then this is forgery na ni Jinai.

Baada ya KM JJMNYIKA kujua yeye hajaandika barua yoyote kuwateua the next step ilikuwa ni JJMnyika kuripoti polisi kuhusu jinai hiyo, uchunguzi wa kijinai ungefanyika na Chadema kuuthibisha hiyo barua ya uteuzi ni forgery, wala hata wiki wasingemaliza, NEC ndio ingetengua uteuzi wao!.
Kitendo cha Chedema kuripoti popote forgery yoyote ni uthibitisho they know the letters ni authentic bonafide genuine.
Msemaji wa Cdm amedai Nec imeshindwa kuwapatia nyaraka zilizotumika kuwateua kina Halima.
Chadema ipeleke nyaraka za uteuzi NEC, zipokelewe, wateuliwe, waapishwe, halafu wewe wewe urudi NEC kuiomba barua kutoka chama chake, hata ningekuwa mimi, why nikupe?, si copy unayo?, kama kweli hukuandika na huna copy hiyo maana yake ni forgery,the right thing was to report.

Kama Chadema wangeripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai ufanyike, Chadema would have been saved with the letter from Chadema to NEC na hapo ndipo Chadema angethibitisha barua hiyo ni forgery.
Kwa maelezo hayo, we have no other option, zaidi ya ku-conclude kwamba kina Halima hawakuteuliwa na chama
Uteuzi haufanywi kwa imani wala maneno bali maandishi. Nakuambia barua authentic bonafide genuine ya uteuzi wa wabunge hao 19 toka Chadema ipo!
wala tume kuwa wabunge wa viti maalum.
Barua authentic bonafide genuine certificates za uteuzi kutoka Tume kwenda Bungeni kuwateua zipo na ndio maana Bungeni wameapishwa.
Watu wanahangaika kutafuta " barua " na " aliyegushi" wakati hakukuwa na kitu kama hicho.
The government works on black and white, bila papers there is nothing government is done!. Barua zipo na hakuna forgery yoyote ila kuna uhuni fulani!.
P
 
Nimekuelewa Mkuu Pasco asietaka kuelewa awezi kukuelewa
 
Kushinda kwa akina Halima Mdee sii jambo jibya kwani Serikali, Bunge na Mahakama walishazoea kuvunja katiba hasa wakati wa ERA iliyopita haya ni marudio na mazoea tu sii jipya. Halitastajabisha lolote. Nawaonea sana huruma viongozi watakaokuwa wamevunja katiba maisha yao baada ya ajiira dhamira zao zitawasuta sana. Katiba mpya ikija na kutekelezwa inavyostahili hii nchi itakuwa Taifa bora kabisa with power to develop is high speed.
 
Mkuu JokaKuu, kuna kitu kimoja hapa naweza kukubaliana na wewe, kwenye democracy changa, matokeo ya uchaguzi, does not depends on votes casted but the votes counted, hivyo determinants ya ushindi is not the vote cast but he who counted the votes.

Wewe Joka ukishindana na Kuu, kura zikahesabiwa ukapata kura 90, Kuu akapata kura 10, msimamizi wa uchaguzi akatangaza matokeo Joka amepata kura 10, Kuu amepata kura 90, mshindi ni Kuu, then Kuu ndiye mshindi.

Hivyo kama NEC imetoa tuu zile certificate za uteuzi wa hao wabunge 19 wa Chadema, bila barua yoyote kuwateua toka Chadema, then hii sindio the biggest for forgery ya mwaka kwa serikali yetu!. Kwanini mpaka sasa Chadema hawajachukua hatua?.
P
 

..Kikao cha kamati kuu ya Cdm hakikuketi baada ya uchaguzi mkuu kuteua wanachama 19 kwa ajili ya viti maalum.

..Kwa msingi huo nakubaliana na wewe kuna UHUNI umefanyika ktk uteuzi wa kina Halima.

..NEC for 2 yrs wameshindwa kuthibitisha kwa kuonyesha barua ya forgery iliyowateua kina Halima. My humble conclusion ni kuwa hakuna kitu kama hicho.

..Hivyo kwa mtizamo wangu UHUNI uliofanyika ni kina Halima kuwezeshwa kwenda moja kwa moja bungeni na kuapa.

..Barua toka Cdm kwenda NEC haipo.
 

..Chadema wamechukua hatua.

..Wamewafukuza wanachama wao walioshiriki uhuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…