Kwa hiyo kauli yao, hao magaidi hawaoni wamejigeuza kuwa maadui na nchi zote zenye raia wao ndani ya Israel?
Ajabu kuna wajinga wanaotetea ushetani unaofanywa na hawa magaidi, wakati wao wenyewe wanakiri kuua raia wasio raia wa Israel, tena wasio na hatia.
Hamas ni kundi lenye wanachama wajinga sana. Kutumia utetezi ukiwemo Nyerere kuwaunga mkono Palestina, Nyerere niliyemjua angewalaani hawa wahuni mchana kweupe, kama alivyowaunga mkono hao Palestina, hakuwa mnafiki.
Au kusema Vita ina "collateral damage", na mwingine wowote ni ujinga mtupu, mbona hatujaskia Israel wakiwaua raia wasio wa nchi yao kwa makusudi kama wafanyavyo Hamas?
- Kwanini hao magaidi wa Hamas wasiwe wanatoa ultimatum, kwa raia wasio wa Israel kuondoka kabla hawajaanza kuwateka na kuwaua?
Huo utetezi wa collateral damage unathibitisha Hamas ni wendawazimu, ningeuelewa kidogo endapo bomu lingetupwa sehemu liue mpaka raia wasio husika, lakini sio kuwachagua kabisa, kisha kuwapiga risasi individually. Never.
Hata kama mnasema vita haina macho, lakini mtambue wanaoipigana wana macho, tusifiche maovu ya hao wahuni kwa sababu zozote, wakemewe.
Sent from my SM-G900H using
JamiiForums mobile app