Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Majibu ya Uchunguzi yako wapi ?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ya ndani yanazidi kuwekwa Wazi johnthebaptist
-
“Timu ya uchunguzi [kuhusu bandari] iliteuliwa na Hayati Magufuli. Kimsingi ni mwendelezo wa kazi, sio kitu ambacho kimekurupuka ghafla, ni mchakato wa muda mrefu wa serikali kuhakikisha tunakuwa na bandari yenye ufanisi.”
Kwa RaisMajibu ya Uchunguzi yako wapi ?
Kwanini asihusike Mkuu. Mambo yanatia hasira haya.Yani nilivyoona Rostam Aziz amerudi basi nilijisemea tu huyu mtu safari hii ana hasira kuliko mwanzoni.
Sasa anatuibia mpaka bundle za Tigo, yani ukiweka GB moja usithubutu kufunguwa video utakoma ubishi, kwenye hili la DP kama Rostam hausiki mninyonge nife.
Umepiga mulemuleWanafikiri, au wameshauriwa, au wamedanganywa??
Hapana kwa yote. Ni wapuuzi!
Wamepuuza Wananchi, wanawachonganisha Wananchi.
Kwa uhakika mkubwa, hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kamati iliyosemwa na iliyoanzishwa wakati wa JPM, kwamba ilipewa jukumu la kutafuta ufanisi wa Bandari na mapitio ya mkataba huo. Hakuna.
Inatosha kusema kwamba ufanisi wowote uliotafutwa ulikuwa kwa njia yoyote au sura au fomu, ukaguzi wa mkataba mkononi.
Ila, pia ni kwa asili, kwamba utawala wowote ukiwa unataka kuboresha baadhi kama si wote wa mashirika yake yote na kuongeza au kuboresha ufanisi huwa wanafanya hivyo ili(mashirika-hapa bandari) waweze kufuata sera ambazo ziko mkononi na kwamba inaona kufanya hivyo kuwa na manufaa na tija kwa muda mrefu, kwa mustakabhali wa Nchi. Na uhakika, kuwatwisha DPW haikuwa sera wala nia ya Uongozi chini ya JPM
Sio sahihi kwa mleta mada, au Johari kutaka kuunganisha juhudi za kuongeza ufanisi wa kamati zilizoundwa huko nyuma na Udhaifu wa serikali hii.
CCM hii madarakani ni Lazima wapumzishwe. Ni Lazima kwa Usalama na Mustakabhali wa Nchi. Huu upotoshaji wa hali hii, inadhihirisha , kama wadau wengine wanaodai humu kuwa kuna Jinamizi katika mkataba huo.
Nani kafanya activation ya mkataba? Kulikua na ulazima gan wa kuridhia jambo ambalo halina afya kwa Taifa? Why wasilaumiwe hawa waliopo. Cz DP world hawajaanza utendaji!!Sasa aangushiwe kwani yeye alikua mwenyekiti wa kijiji au rais wa nchi? Mbona migodi alibinafsisha au siyo rasilimali hiyo.
Wewe unasema jambo halina afya umeona matokeo ya uwekezaji huo wa bandari angalau hata kwa miezi 6?Nani kafanya activation ya mkataba? Kulikua na ulazima gan wa kuridhia jambo ambalo halina afya kwa Taifa? Why wasilaumiwe hawa waliopo. Cz DP world hawajaanza utendaji!!
Afya nayoisemea ni ya stage ya kimkataba! Ndan kuna mamb hayana afya kwa Taifa... Duration, terms and conditions!! Soma iyooo!!Wewe unasema jambo halina afya umeona matokeo ya uwekezaji huo wa bandari angalau hata kwa miezi 6?
Haswa.Kwenye hili mama hakwepi hata anunue vichawa vingine waongeze nguvu kumtetea, ila wanatanzania wa miaka 10 iliyopita siyo kama wa leo, wanajua na wanaouwezo wa kuhoji inapobidi!
Mambo yamebadirika mno
Narudia tena, kuendelea kumsingizia Magufuli leo, ni dhahiri kwamba kosa wanalo ila hawataki kujitokeza kuomba poo!
Yawezekana mkataba huo hujausoma ndio maana umetoa hoja yako hiyo ambayo ni kinyume kabisa na hoja zinazopinga uwekezaji huo. Mimi nitaendelea kupinga huo uwekezaji kwa mkataba huo ulivyo wa hovyo hata ukirekebishwa.Tatizo tunamuona JPM kuwa ni shujaa wa taifa na tumeshalipa tafsiri potofu suala zima la DP World.
Tunadhani SSH kwa maamuzi yake mwenyewe alienda Dubai na kuingia mikataba, tunasahau kuwa hawa wawili ni wateuliwa wa chama kimoja cha siasa. Wanatekeleza ilani moja ya uchaguzi.
Tumembagua na kumtusi SSH tukisahau chanzo halisi cha huu mradi ni nani, tukashindwa hata kujiuliza gharama kubwa ya ujenzi wa SGR kwa kuilinganisha na mradi huu wa waarabu.
Siasa kuzitafakari inamtaka mtu atulize kichwa chake vizuri.
Ni DP-W.Kwani wanaoitaka bandari ni wandengereko?
Kwenda kuonana moja kwa moja na bunge naamini ni taratibu tu kulingana na ukubwa wa mradi wenyewe.Hii sio biashara ya kitoto. SGR kwa sehemu kubwa imejengwa kuhudumia mradi wa aina hii.Yawezekana mkataba huo hujausoma ndio maana umetoa hoja yako hiyo ambayo ni kinyume kabisa na hoja zinazopinga uwekezaji huo. Mimi nitaendelea kupinga huo uwekezaji kwa mkataba huo ulivyo wa hovyo hata ukirekebishwa.
DPW kama ina nia ya dhati kuwekeza Tanzania, ipitie ama kwenye Kituo cha Uwekezaji (Tanzania Investment Centre) au iingie ubia na Mamlaka ya Bandari (Tanzania Ports Authority) ambapo tayari wana MoU. Njia zote 2 zina taratibu zake, lakini siyo kuingiza Serikali Kuu (kwa maana ya nchi) kwenye mkataba usio na kikomo, labda kama nyuma ya pazia kuna jambo ambalo ni Rais mwenyewe tu analijua kwa agenda yake ya siri.
SGR ni mradi wa kimkakati unaotekelezwa na Serikali, hivyo basi, huwezi kulinganisha na mkataba unaoiweka DPW kama mwekezaji. SGR ikikamilika na kama Mamlaka ya Reli (Tanzania Railway Authority) itaona kuna tija kuingia ubia na mwekezaji kutoka nje, itafanya hivyo kwa Sheria, Taratibu na Kanuni zilizopo.
Mimi sipingi uwekezaji bandari na mahitaji ya kupanuka bandari kulingana na mahitaji ya ukubwa wa mizigo hasa SGR ikianza kazi. Ninapinga ni mkataba wa IGA isipokuwa DPW iingie ubia na TPA kwa Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo. Serikali isimamie tu huo mkataba unatekelezwa ipasavyoKwenda kuonana moja kwa moja na bunge naamini ni taratibu tu kulingana na ukubwa wa mradi wenyewe.Hii sio biashara ya kitoto. SGR kwa sehemu kubwa imejengwa kuhudumia mradi wa aina hii.
Na reli hiyo kumbuka ilivyokutana na upinzani wakati inaanza kujengwa, Huko Rwanda Kagame keshajenga na kufungua Dry Port kwa ajili ya kuweka mzigo unaotoka pale pale Rwanda na mwingine kutoka DRC.
Kusema kwamba hakuna ukomo ni suala la uelewa juu ya kipi kisicho na ukomo. Ule mkataba MAMA uliopelekwa bungeni hauna ukomo lakini ile itakayosainiwa kwa ajili ya kuanza kwa biashara itakuwa na ukomo kulingana na mazingira yenyewe ya kibiashara.
Tuweke Kumbukumbu sawa...Rostam wlirudi kipindi Cha Jiwe! Unakumbuka mdogo wake alipkamatwa na nyara za aserikali..baadaye Jiwe akamwachia!Yani nilivyoona Rostam Aziz amerudi basi nilijisemea tu huyu mtu safari hii ana hasira kuliko mwanzoni.
Sasa anatuibia mpaka bundle za Tigo, yani ukiweka GB moja usithubutu kufunguwa video utakoma ubishi, kwenye hili la DP kama Rostam hausiki mninyonge nife.
Kwa Nini Mkataba wa Mama usiwe na Ukomo!?Bwana Chawa Mwandamizi.Kwenda kuonana moja kwa moja na bunge naamini ni taratibu tu kulingana na ukubwa wa mradi wenyewe.Hii sio biashara ya kitoto. SGR kwa sehemu kubwa imejengwa kuhudumia mradi wa aina hii.
Na reli hiyo kumbuka ilivyokutana na upinzani wakati inaanza kujengwa, Huko Rwanda Kagame keshajenga na kufungua Dry Port kwa ajili ya kuweka mzigo unaotoka pale pale Rwanda na mwingine kutoka DRC.
Kusema kwamba hakuna ukomo ni suala la uelewa juu ya kipi kisicho na ukomo. Ule mkataba MAMA uliopelekwa bungeni hauna ukomo lakini ile itakayosainiwa kwa ajili ya kuanza kwa biashara itakuwa na ukomo kulingana na mazingira yenyewe ya kibiashara.
Mpaka mmeingia kutaja jina la Magufuli ili liwasaidie kuwaamini mnachoongea...Hatutawaamini kamwe!😂😂😂😂 ya ndani yanazidi kuwekwa Wazi johnthebaptist
-
“Timu ya uchunguzi [kuhusu bandari] iliteuliwa na Hayati Magufuli. Kimsingi ni mwendelezo wa kazi, sio kitu ambacho kimekurupuka ghafla, ni mchakato wa muda mrefu wa serikali kuhakikisha tunakuwa na bandari yenye ufanisi.”
Hili hapa chimbuko la Mkataba 'tata' wa Bandari, hawa wanacho cha kutueleza!
Nimeamua kuwadokeza watanzania jambo hili. Kujua chimbuko ni mwanzo wa kujua suluhisho la tatizo, kama lipo. Kwa ubobevu wangu kiutumishi serikalini na chamani, nimefuatilia na kujua chimbuko la mkataba huu 'tata' wa bandari kati ya Serikali yetu na ile ya UAE ikiwakilishwa na kampuni ya DP...www.jamiiforums.com
Kwa statement hii maana yake huu mkataba unashida, mbona watu wanakimbia kuwajibishwa, ?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ya ndani yanazidi kuwekwa Wazi johnthebaptist
-
“Timu ya uchunguzi [kuhusu bandari] iliteuliwa na Hayati Magufuli. Kimsingi ni mwendelezo wa kazi, sio kitu ambacho kimekurupuka ghafla, ni mchakato wa muda mrefu wa serikali kuhakikisha tunakuwa na bandari yenye ufanisi.”
Hili hapa chimbuko la Mkataba 'tata' wa Bandari, hawa wanacho cha kutueleza!
Nimeamua kuwadokeza watanzania jambo hili. Kujua chimbuko ni mwanzo wa kujua suluhisho la tatizo, kama lipo. Kwa ubobevu wangu kiutumishi serikalini na chamani, nimefuatilia na kujua chimbuko la mkataba huu 'tata' wa bandari kati ya Serikali yetu na ile ya UAE ikiwakilishwa na kampuni ya DP...www.jamiiforums.com