Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Je, yuko wapi kwa sasa na anafanya nini.?!
Magariz,
Daisy
sijaonananae kwa kipindi kirefu lakini yeye akifanya kazi na
moja ya mashirika ya kimataifa nje ya Tanzania.

Kwa sasa sijui yuko wapi.
 
Mkuu Maalim
Mohamed Saidasante kwa taarifa, kutujulisha kumbe enzi zile ni Nyerere ndio alikuwa anatia watu jela na kuwafunga tuu!, ila haikusemwa watu hao waliofungwa na Nyerere, walikuwa wanafunguliwa na nani kutoka vifungo hivyo vya Nyerere?!. Mimi nilidhani ungesema ni serikali ya Nyerere!, kumbe ni Nyerere!, asante!.

Kwa msio jua kilichotokea Zanzibar baada ya mapinduzi yale matukufu ya 1964, wapinzani wa Karume walikuwa wana vanish into thin air, hata unywele haukuonekana (taarrifa zisizothibitishwa zilisema walininginizwa majiwe shingoni, kutiwa ndani ya magunia na kutoswa baharini). Kufuatia Mwalimu Nyerere kuwa ni mcha Mungu, hakuridhishwa na kinachoendelea kule, hivyo ili kuwanusuru waliotofautiana na Karume, aliwachukua na kuwafunga huku bara ambayo hiyo ndio salama yao!, hivyo ndivyo Nyerere alivyowanusu wengi akiwemo Col. Mafudha, Abrahman Mohamed Babu na baadhi ya Makomredi, vinginevyo saa hizi, tungekuwa tunazungumza mengine!.

Kiukweli shukrani ya punda ni mateke!, asingekuwa Nyerere na Muungano, baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sijui ingelikuwaje kwa race fulani kule Zanzibar, halocust ingekuwa ni afadhali maana angalau ulipatikana japo mfupa au hata majivu!, Zanzibar hata unyayo tuu ulipokanya mara ya mwisho,usingeonekana, sii unywele wala ukucha!. Badala ya kushukuru ndio kwanza watu humu wanabeza!.

Kwa amsiomjua Nyerere, japo nchi yetu ina adhabu ya kifo, katika utawala wake wa miaka 23, alisaini hati moja tuu ya kunyongwa kwa Mwamwindi!. Aliyefuatia ni swala tano!, uliza alisaini hati ngapi na watu wakanyongwa!.

Vitu vingine bora tuacheni tuu!, harakati za kumtangaza Nyerere ni Mwenye Heri, zinaendelea!.

Pasco
Pasco,
Unataka kupiga ala bila kujifunza chromatics.
Unataka kuizungumza historia ya Zanzibar bila kusoma historia yenyewe.

Lakini kubwa ni kuwa hata ''intellect,'' yako ni tatizo kidogo maana hata
mtu akikusoma hili linamtokea dhahiri kabisa.

Ataliona jinsi michango yako inavyokosa mantiki na matokeo yake ni haya
ya kuchanganya mambo.

Unachokijua wewe ni, ''mapinduzi matukufu,'' huna kingine.

Nikikuwekea mabandiko ya kukufikirisha unapotea kwa muda kisha unaibuka
na jambo lingine kabisa lile unalikimbia.

Ni kweli waliofungwa jela za Bara walinusurika kuuawa.
Lakini iweje umshukuru mtu aliyekukata mkono kwa kukurudishia kidole gumba?

Jana nilikuwa Zanzibar kutoa mada kuhusu Sheikh Hassan bin Amir.
Walionialika ni Mwinyi Baraka Foundation.

DSCN0876.JPG


Kongamano la Mwinyi Baraka Foundation 12 June 2016 Ukumbi wa Baytul Amiyn

Sheikh Hassan bin Amir ni Mzanzibari na alishiriki katika kuunda TANU na ni
mmoja wa wajumbe wa TAA Political Sub Committee 1950 wajunbe wengine
wakiwa, Dr. Kyaruzi, Abdul Sykes, Stephen Mhando, Hamza Mwapachu,
Said Chaurembo
na John Rupia.

Sheikh Hassan bin Amir ndiyo aliyiongoza TANU kuwa ''a nationalist secularist
party,'' baada ya kufanya mkutano wa siri Mtaa wa Pemba Dar es Salaam na
baadhi ya viongozi wa TANU mwaka wa 1955 wakiwamo Rajab Diwani, Sheikh
Abdallah Chaurembo, Sheikh Nurdin Hussein
na wengineo.

Sheikh Hassan bin Amir alikuwa Mufti wa Tanganyika hadi alipofukuzwa na
Nyerere mwaka wa 1968 na kurudishwa Zanzibar na kupigwa marufuku

kukanyagaTanganyika baada ya ''mgogoro,'' wa East African Muslim Welfare
Society (EAMWS) uliopelekea kuundwa BAKWATA.

Lakini baada ya Sheikh Hassan kufariki mwaka wa 1979 Nyerere alihudhuria
hitma yake Msikiti wa Mtoro alialikwa na Sheikh Abdallah Chaurembo na
Sheikh Kassim Juma.

Mimi nilikuwapo hapo msiktini siku hiyo.

Ikiwa huyajui haya kwa undani maisha utahangaika na historia ya Tanganyika
kwani huu ndiyo msingi unaosimamisha si historia ya Nyerere bali historia nzima
ya uhuru wa Tanganyika na baada yake.

Pasco,
Hebu jitulize na isome historia kwanza kabla hujataka kupambana na mimi.
Watoto wa mjini wana Kiswahili chao.

Wanasema, ''Mimi si saizi yako.''
Maana ukinivaa utapwaya.
 
Pasco,
Unachokijua wewe ni, ''mapinduzi matukufu,'' huna kingine.

Ni kweli waliofungwa jela za Bara walinusurika kuuawa.
Lakini iweje umshukuru mtu aliyekukata mkono kwa kukurudishia kidole gumba?

Pasco,
Hebu jitulize na isome historia kwanza kabla hujataka kupambana na mimi.
Watoto wa mjini wana Kiswahili chao.

Wanasema, ''Mimi si saizi yako.''
Maana ukinivaa utapwaya.
Mkuu Maalim Mohamed Said, kwanza nakiri sina nijuacho, na sio zaizi yako, na hata hayo Mapinduzi Matukufu nimeyajua kwa kusoma tuu na kuhadithiwa!.

Sipambani na wewe bali tunatofautiana tuu kwa mmoja wetu kuwalisha watu urongo humu, na baadhi yetu kukataa kuumeza urongo huo !.

Dini zumetufunzwa kuwa na shukani katika madogo ili tuweze kupewa makubwa!, ni Nyerere ndiye aliyetupatia uhuru, kwa hili pekee hana budi kuenziwa na kushukuiwa daima!. Wengine hatuna uvumilivu wa kuona licha ya kutangulia mbele ya haki, kila uchao, unakuja humu na posti zako za udini ulikubuhu mtu kisha kumbeza!.

Kama mtu amehukumiwa kifo kwa upanga, na sheria ya upanga ule ni kupigwa kwa pigo moja tuu!, inapotokea yule mkata upanga akakuepushia kifo na badala ya kukata shingo, upanga ukashukia kwenye mkono na kukata mkono hivyo kuepuka kifo, mtu aliyesalimika kifo, atamshukuru mchinjaji kwa kumuepushia kifo badala ya kumlaani kwa kumkata mkono!.

Hao walionusuishwa kifo na Nyerere huko walipo wanamshukuru Nyerere, who are you kumbeza kila uchao?!.

Mimi japo sii mwanazuoni na sii mwandishi kuyaandika yote niliyoyasikia, lakini nimezungumza na Sheikh Mkuu Hemed Bin Jumaa Bin Hemed, Sheikh Kassim Bin Juma, Sheikh Nurdin, Sheikh Yahya Hussein, Sheikh Comorean, Sheikh Jabir, Omar Matata na wengine wengi, misimamo yao naijua na shukrani zao kwa Nyerere nazijua huku waliko wanakusoma na kukushangaa jinsi unavyombeza humu!.

Maadam wewe wasema ''Mimi si saizi yako, ukinivaa utapwaya", kiukweli nimekuvaa na nimepwaya and here I rest my case!, endelea kulisha watu urongo, wa kumeza watameza, wa kutema watatema hadi watakapotokea saizi yako ndio labda watatunusuru na urongo wenye kupandikiza mbegu za chuki za udini kwa kisingizio cha kuhifadhi historia!

Asante.

Pasco
 
Mkuu Maalim Mohamed Said, kwanza nakiri sina nijuacho, na sio zaizi yako, na hata hayo Mapinduzi Matukufu nimeyajua kwa kusoma tuu na kuhadithiwa!.

Sipambani na wewe bali tunatofautiana tuu kwa mmoja wetu kuwalisha watu urongo humu, na baadhi yetu kukataa kuumeza urongo huo !.

Dini zumetufunzwa kuwa na shukani katika madogo ili tuweze kupewa makubwa!, ni Nyerere ndiye aliyetupatia uhuru, kwa hili pekee hana budi kuenziwa na kushukuiwa daima!. Wengine hatuna uvumilivu wa kuona licha ya kutangulia mbele ya haki, kila uchao, unakuja humu na posti zako za udini ulikubuhu mtu kisha kumbeza!.

Kama mtu amehukumiwa kifo kwa upanga, na sheria ya upanga ule ni kupigwa kwa pigo moja tuu!, inapotokea yule mkata upanga akakuepushia kifo na badala ya kukata shingo, upanga ukashukia kwenye mkono na kukata mkono hivyo kuepuka kifo, mtu aliyesalimika kifo, atamshukuru mchinjaji kwa kumuepushia kifo badala ya kumlaani kwa kumkata mkono!.

Hao walionusuishwa kifo na Nyerere huko walipo wanamshukuru Nyerere, who are you kumbeza kila uchao?!.

Mimi japo sii mwanazuoni na sii mwandishi kuyaandika yote niliyoyasikia, lakini nimezungumza na Sheikh Mkuu Hemed Bin Jumaa Bin Hemed, Sheikh Kassim Bin Juma, Sheikh Nurdin, Sheikh Yahya Hussein, Sheikh Comorean, Sheikh Jabir, Omar Matata na wengine wengi, misimamo yao naijua na shukrani zao kwa Nyerere nazijua huku waliko wanakusoma na kukushangaa jinsi unavyombeza humu!.

Maadam wewe wasema ''Mimi si saizi yako, ukinivaa utapwaya", kiukweli nimekuvaa na nimepwaya and here I rest my case!, endelea kulisha watu urongo, wa kumeza watameza, wa kutema watatema hadi watakapotokea saizi yako ndio labda watatunusuru na urongo wenye kupandikiza mbegu za chuki za udini kwa kisingizio cha kuhifadhi historia!

Asante.

Pasco
Pasco,
Hakuna anaekataa kuwa Mwalimu Nyerere ndiye aliyeoongoza mapambano dhidi
ya Waingereza.

Historia hii imeandikwa na sote tunaikubali ila ninachosema mimi ni kuwa mbona
hakuwa peke yake katika mapambano hayo?

Licha ya hilo kuwa hakuwa peke yake ninachosema mimi ni kuwa mapambano ya
kudai uhuru yalianza kabla yake.

Na kuthibitisha hilo ndipo nikaandika kitabu cha Abdul Sykes nikitumia njia ya
''biographical approach.''

Nimekuwekea Kamati ya Siasa katika TAA ambayo Abdul Sykes aliipa jina la TAA
Political Subcommittee kama nyaraka zake zinavyoonyesha na hii ilikuwa 1950.
(Annual Report of the Secretary of Tanganyika African Association, 7 January, 1951.
Sykes' Papers).

Katika taarifa hii Abdul kaeleza mengi kuhusu juhudi za kuja na chama cha siasa.
Soma kitabu changu yote nimeeleza kwa urefu na mapana yake.

Nyaraka hizi zipo na sasa zina umri wa miaka 66 na zilikuwa mikononi kwa marehemu
Ally Sykes hadi alipofariki.

Abdul Sykes awe muongo mkweli uwe wewe kwa kuzungumza na Omari Matata
ambae hakuna anaemjua katika historia ya Tanganyika?

Nyerere hakuweko katika kamati hii.
Nimekuwekea majina ya wanakamati wote na hawa ndiyo waliouanda TANU 1954.

Lipi la uongo nililosema mimi.

Sasa ngoja nije katika saikolojia ya watu unaodai kuwa ulizungumzanao kuhusu
historia ya TANU.

Labda hukuwa unajijua wala hukuwa unajua hali ya wakati ule ulipozungumzanao.

Kwa watu hawa kama Sheikh Kassim Juma na Nurdin Hussein wewe ulikuwa
mpelelezi umetumwa kuwachimba na ndiyo maana wakakufurahisha kwa kukupa lile
ambalo ndilo lililokuwa likitakiwa liwe.

Mimi Sheikh Kassim ni kaka yangu.
Aliwekwa ndani na hiki ni kisa mashuhuri.

Kuna khutba imepewa jina, ''Leo Nitataja Majina.''

Siku alipotoa khutba hii mimi nilikuwapo ilikuwa katika khutba ya Ijumaa Msikiti wa
Mtoro huu ndiyo wakati ule alipokuwa anapambana na serikali kuhusu madhila ya
bucha za nguruwe.

Hiyo ndiyo siku hadharani Waislam walimsikia Sheikh Kassim akieleza historia ya
Abdul Sykes na Nyerere katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Jiulize kipi kilichomfanya Sheikh Kassim kuvunja mwiko siku ile?
Mwiko uliokuwa umehifadhiwa kwa zaidi ya miaka 40?

Siku ile pia alimtaja na Rajab Diwani.

Mimi nimeishi ndani ya historia hii na hao wote ninaokutajia wakinijua
na mimi nikiwajua ingawa nilikuwa kijana na mdogo kwao wote.

Nawafahamu vizuri kila mmoja wao na misimamo yao ya siasa.

Pasco,

Wewe ni mgeni kwa watu hawa.

Sheikh Nurdin Hussein ni mzee wangu.
Nawajua wanae tumekua sote Kariakoo.

Sheikh Nurdin Hussein alihidhuria mkutano ule wa Mtaa wa Pemba
wa 1955 ambao Sheikh Hassan bin Amir alitoa wazo kuwa TANU
ichukue kwa makusudi mwelekeo wa ''nationalist-secularist party.''

Nina hakika Sheikh Nurdin alikuficha haya hakukueleza kwa kuwa
hakuwa anakuamini wala kukufahamu umetokea wapi.

Sheikh Nurdin aliwekwa ndani na Nyerere na kupelekwa uhamishoni
Ngombezi labda hilo pia hakukueleza.

Sheikh Ali Comorian rika langu mchezo wetu mmoja.

Baba yake Sheikh Ali Mzee Comorian alifungwa na Nyerere wakati
Sheikh Hassan bin Amir alipokamatwa na kufukuzwa Tanganyika 1968.

Kwa wote hao niliokutajia mimi si ''outsider,'' kama wewe.
Hawa ukienda wewe kutaka kuwauliza historia ya TANU tayari ushawatisha.

Hao wengine katika masheikh uliowataja wala sioni kama ipo haja ya kusema
lolote.

Mwisho mimi sijapatapo kumbeza Nyerere siwezi kukosa adabu kiasi hicho
na kama una ushahidi wa hili ulete hapa barzani watu wote waushuhudie.

Ila mimi siwezi kumpa Nyerere sifa isiyokuwa yake wala siwezi kumdhulumu
kwa lile ambalo kwa hakika anastahili kusifiwa.

Historia ya TANU na kudai uhuru wa Tanganyika ni mimi niliyokuja kuikamilisha.

Pasco,
Nakuwekea kumbukumbu muhimu:

zApILRPZVET4pBs1oE8itiDZuHryxTdV4FHl6x9q-mMF9bfHRYCjzaMzJfBzrYoNDwvjCmqKtHS8FYHylQO_6QoWZVI18TZ1K5IBIeZ4R0xyRrRbIEQ23SE9RWXnf_5ooFKqIVrc2dQa9Di4Gr8P6MdbWmtT6umAzVoLCr9Hz2ovWDVGXE72KWZJh3tB8r4pdVAwgDJkMszKnpKOuOhbtHueD1gciQgAwWfICMIY9ItHRtVxyVUIJ96qkCZ3CKDt20SBV-aa6CqmjD4pBO0YyzGxYRNGcbGzqbK7z5f8_NL1cG6VCnD6nE4MERTe2QavlJ8etw-VLVVsrhWkJecH07g63oCNxEoPTMvaOisOtqiOhfYvtN3uCbjA7Nk8SK8AVs0tbF3nUMTsCxZv5JJI4Vwj2McQElDoUxQIldzd0moMIaGiotTLb4NnWG_FGvlLgkp6IVJYGb2wzITqLBBJjjX1Mr4BZxBSdLBBvvWnSVqn2IB8cq055djqsQPT-hqq_WrNURn0MhpYezQ4HXyN1iaR3qGjDnPNhi9C2WDTD7w=w858-h643-no

Sheikh Kassim siku alipotolewa jela hapa ni Msikiti wa Mtoro

Ingia hapa usome historia ya Sheikh Kassim bin Juma hii ni mada niliwasilisha Chuo Kikuu
Cha Kenyatta, Nairobi:

Mohamed Said: Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma (1940 – 1994) And the Dar es Salaam Pork Riots of 1993
 
Pasco,
Hakuna anaekataa kuwa Mwalimu Nyerere ndiye aliyeoongoza mapambano dhidi
ya Waingereza.

Historia hii imeandikwa na sote tunaikubali ila ninachosema mimi ni kuwa mbona
hakuwa peke yake katika mapambano hayo?

Licha ya hilo kuwa hakuwa peke yake ninachosema mimi ni kuwa mapambano ya
kudai uhuru yalianza kabla yake.

Na kuthibitisha hilo ndipo nikaandika kitabu cha Abdul Sykes nikitumia njia ya
''biographical approach.''

Nimekuwekea Kamati ya Siasa katika TAA ambayo Abdul Sykes aliipa jina la TAA
Political Subcommittee kama nyaraka zake zinavyoonyesha na hii ilikuwa 1950.
(Annual Report of the Secretary of Tanganyika African Association, 7 January, 1951.
Sykes' Papers).

Katika taarifa hii Abdul kaeleza mengi kuhusu juhudi za kuja na chama cha siasa.
Soma kitabu changu yote nimeeleza kwa urefu na mapana yake.

Nyaraka hizi zipo na sasa zina umri wa miaka 66 na zilikuwa mikononi kwa marehemu
Ally Sykes hadi alipofariki.

Abdul Sykes awe muongo mkweli uwe wewe kwa kuzungumza na Omari Matata
ambae hakuna anaemjua katika histori ya Tanganyika?

Nyerere hakuweko katika kamati hii.
Nimekuwekea majina ya wanakamati wote na hawa ndiyo waliouanda TANU 1954.

Lipi la uongo nililosema mimi.

Sasa ngoja nije katika saikolojia ya watu unaodai kuwa ulizungumzanao kuhusu
historia ya TANU.

Labda hukuwa unajijua wala hukuwa unajua hali ya wakati ule ulipozungumzanao.

Kwa watu hawa kama Sheikh Kassim Juma na Nurdin Hussein wewe ulikuwa
mpelelezi umetumwa kuwachimba na ndiyo maana wakakufurahisha kwa kukupa lile
ambalo ndilo lililokuwa likitakiwa liwe.

Mimi Sheikh Kassim ni kaka yangu.
Aliwekwa ndani na hiki ni kisa mashuhuri.

Kuna khutba imepewa jina, ''Leo Nitataja Majina.''

Siku alipotoa khutba hii mimi nilikuwapo ilikuwa katika khutba ya Ijumaa Msikiti wa
Mtoro huu ndiyo wakati ule alipokuwa anapambana na serikali kuhusu madhila ya
bucha za nguruwe.

Hiyo ndiyo siku hadharani Waislam walimsikia Sheikh Kassim akieleza historia ya
Abdul Sykes na Nyerere katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Jiulize kipi kilichomfanya Sheikh Kassim kuvunja mwiko siku ile?
Mwiko uliokuwa umehifadhiwa kwa zaidi ya miaka 40?

Siku ile pia alimtaja na Rajab Diwani.

Mimi nimeishi ndani ya historia hii na hao wote ninaokutajia wakinijua
na mimi nikiwajua ingawa nilikuwa kijana na mdogo kwao wote.

Nawafahamu vizuri kila mmoja wao na misimamo yao ya siasa.

Pasco,

Wewe ni mgeni kwa watu hawa.

Sheikh Nurdin Hussein ni mzee wangu.
Nawajua wanae tumekua sote Kariakoo.

Sheikh Nurdin Hussein alihidhuria mkutano ule wa Mtaa wa Pemba
wa 1955 ambao Sheikh Hassan bin Amir alitoa wazo kuwa TANU
ichukue kwa makusudi mwelekeo wa ''nationalist-secularist party.''

Nina hakika Sheikh Nurdin alikuficha haya hakukueleza kwa kuwa
hakuwa anakuamini wala kukufahamu umetokea wapi.

Sheikh Nurdin aliwekwa ndani na Nyerere na kupelekwa uhamishoni
Ngombezi labda hilo pia hakukueleza.

Sheikh Ali Comorian rika langu mchezo wetu mmoja.

Baba yake Sheikh Ali Mzee Comorian alifungwa na Nyerere wakati
Sheikh Hassan bin Amir alipokamatwa na kufukuzwa Tanganyika 1968.

Kwa wote hao niliokutajia mimi si ''outsider,'' kama wewe.
Hawa ukienda wewe kutaka kuwauliza historia ya TANU tayari ushawatisha.

Hao wengine katika masheikh uliowataja wala sioni kama ipo haja ya kusema
lolote.

Mwisho mimi sijapatapo kumbeza Nyerere siwezi kukosa adabu kiasi hicho
na kama una ushahidi wa hili ulete hapa barzani watu wote waushuhudie.

Ila mimi siwezi kumpa Nyerere sifa isiyokuwa yake wala siwezi kumdhulumu
kwa lile ambalo kwa hakika anastahili kusifiwa.

Historia ya TANU na kudai uhuru wa Tanganyika ni mimi niliyokuja kuikamilisha.

Pasco,
Nakuwekea kumbukumbu muhimu:

zApILRPZVET4pBs1oE8itiDZuHryxTdV4FHl6x9q-mMF9bfHRYCjzaMzJfBzrYoNDwvjCmqKtHS8FYHylQO_6QoWZVI18TZ1K5IBIeZ4R0xyRrRbIEQ23SE9RWXnf_5ooFKqIVrc2dQa9Di4Gr8P6MdbWmtT6umAzVoLCr9Hz2ovWDVGXE72KWZJh3tB8r4pdVAwgDJkMszKnpKOuOhbtHueD1gciQgAwWfICMIY9ItHRtVxyVUIJ96qkCZ3CKDt20SBV-aa6CqmjD4pBO0YyzGxYRNGcbGzqbK7z5f8_NL1cG6VCnD6nE4MERTe2QavlJ8etw-VLVVsrhWkJecH07g63oCNxEoPTMvaOisOtqiOhfYvtN3uCbjA7Nk8SK8AVs0tbF3nUMTsCxZv5JJI4Vwj2McQElDoUxQIldzd0moMIaGiotTLb4NnWG_FGvlLgkp6IVJYGb2wzITqLBBJjjX1Mr4BZxBSdLBBvvWnSVqn2IB8cq055djqsQPT-hqq_WrNURn0MhpYezQ4HXyN1iaR3qGjDnPNhi9C2WDTD7w=w858-h643-no

Sheikh Kassim siku alipotolewa jela hapa ni Msikiti wa Mtoro

Mzee Mohammed Said, umesema huwezi kumpa sifa isiyositahiri Nyerere wala huwezi kumkosea adabu kwa kiasi anachokisema Pasco, lakini mtu akikaa akasoma mabandiko yako kwa utulivu na akili iliyowazi (open mind), atakuelewa kabisa mlengo wa maandishi yako. Mimi sina tatizo na maandishi yako kwa sababu kwanza kabisa najitambua na natumbua mnachokidai tangu siku nyingi sana. Pasco anasema maandishi yako yamejaa udini na kumdharau Nyerere kwa sababu mbili tu :kwanza, mihadhara mingi na hii historia unalotaka tuiamini kuwa ndo ya kweli inafanyika kwa asilimia kubwa misikitini (na wewe ni shahidi). Je, kizazi chenye uhalali wa kufahamu historia sahihi ya kupigania uhuru wa Tanganyika ni waislam pekee!? Pili :makongamano yenu mengi yanawalenga vijana wa kiislam na huko ndo mnaanza kuelezea negativite kuhusu Nyerere na uhuru wa Tanganyika, Je, hao wengine walioshiriki Jamii isiyokuwa ya Kiislam hawana haki ya kufahamu mchango wao!? Au kuelezea hiyo historia ya "kweli" kwa wengine mtakosa thawabu!? Kitu kingine unachotakiwa kusema kwa ukweli ambao naamini unakuuma kuusema na ndio maana hutaki kuusema ni kwamba NYERERE HAKUJIPELEKA TAA! ALITWA NA ALIOMBWA NA HAO WAZEE WALIOKUWA WANAFANYA HIZO HARAKATI ZA KUTAKA UHURU. SASA TWAMBIE, NI KOCHA GANI DUNIANI ANANUNUA MCHEZAJI ASIYEKUWA NA UWEZO WA ZIADA!? mchango mkubwa wa Nyerere upo, utaendelea kuwepo na wala hautaweza kuufuta kwani hata hao waliomuita hawakumbeza kama unavyojaribu kufanya wewe! Ingekuwa unachosema kina Afya katika Jamii usingekisemea kwenye majumba ya ibada na wanafamilia wa majumba hayo huku ukifahamu kabisa hao ni sehemu ndogo sana ya wanafamilia wanaohitaji kufahamu hao wapigania uhuru wengine na michango yao. Sio dhambi kwani sote tunafahamu uhuru haukupiganiwa na mtu mmoja, lakini hao wengine walikuwa na kiongozi wao! Na mwisho wa siku katika kikosi ukubali ukatae KIONGOZI ndio anayebeba kombe juu! Stop negativite towards Nyerere, be free to appreciate his work!
 
Mzee Mohammed Said, umesema huwezi kumpa sifa isiyositahiri Nyerere wala huwezi kumkosea adabu kwa kiasi anachokisema Pasco, lakini mtu akikaa akasoma mabandiko yako kwa utulivu na akili iliyowazi (open mind), atakuelewa kabisa mlengo wa maandishi yako. Mimi sina tatizo na maandishi yako kwa sababu kwanza kabisa najitambua na natumbua mnachokidai tangu siku nyingi sana. Pasco anasema maandishi yako yamejaa udini na kumdharau Nyerere kwa sababu mbili tu :kwanza, mihadhara mingi na hii historia unalotaka tuiamini kuwa ndo ya kweli inafanyika kwa asilimia kubwa misikitini (na wewe ni shahidi). Je, kizazi chenye uhalali wa kufahamu historia sahihi ya kupigania uhuru wa Tanganyika ni waislam pekee!? Pili :makongamano yenu mengi yanawalenga vijana wa kiislam na huko ndo mnaanza kuelezea negativite kuhusu Nyerere na uhuru wa Tanganyika, Je, hao wengine walioshiriki Jamii isiyokuwa ya Kiislam hawana haki ya kufahamu mchango wao!? Au kuelezea hiyo historia ya "kweli" kwa wengine mtakosa thawabu!? Kitu kingine unachotakiwa kusema kwa ukweli ambao naamini unakuuma kuusema na ndio maana hutaki kuusema ni kwamba NYERERE HAKUJIPELEKA TAA! ALITWA NA ALIOMBWA NA HAO WAZEE WALIOKUWA WANAFANYA HIZO HARAKATI ZA KUTAKA UHURU. SASA TWAMBIE, NI KOCHA GANI DUNIANI ANANUNUA MCHEZAJI ASIYEKUWA NA UWEZO WA ZIADA!? mchango mkubwa wa Nyerere upo, utaendelea kuwepo na wala hautaweza kuufuta kwani hata hao waliomuita hawakumbeza kama unavyojaribu kufanya wewe! Ingekuwa unachosema kina Afya katika Jamii usingekisemea kwenye majumba ya ibada na wanafamilia wa majumba hayo huku ukifahamu kabisa hao ni sehemu ndogo sana ya wanafamilia wanaohitaji kufahamu hao wapigania uhuru wengine na michango yao. Sio dhambi kwani sote tunafahamu uhuru haukupiganiwa na mtu mmoja, lakini hao wengine walikuwa na kiongozi wao! Na mwisho wa siku katika kikosi ukubali ukatae KIONGOZI ndio anayebeba kombe juu! Stop negativite towards Nyerere, be free to appreciate his work!
Uncle Jei Jei,
Kwanza umenifurahisha kwa utulivu wako wa fikra na kuleta hoja kiungwana.
Kusema kuwa naandika udini labda mimi niwe sijui maana ya udini.

Kitabu cha Abdulwahid Sykes kimefanyiwa ''review,'' na wasomi maarufu duniani
katika historia ya Africa kama John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

llFXnOXMTFIyyOhjvYkHPDcotW3x2mWcyHEjzsGugtI0YhUM0gkAiD1ajYG29SO7d-6PRV00QraxujBuDukuJl3R7i7Y5IfRtGBwUvhQ3_4083FV0fBD97cqIyW7jfSCuILauY1-AINDfCDDG8Y-f5mw4iG0_16MFV_FsFPy_D3RkT4fZvnJTi6ee_WDFSGYbPDGK4Yr112KsSHFJDcgjrFCIYh8w3clpDQxiEMLCq0TcS17TriMumLUUisNgb2PcDmPyKkq0i0iUaZ4Hx7j4oZAv1YoFotlVd3qATtshs4FZCiUW0N3lmRHJPt_DT_xf25G9ZYYRNlWe1qVk-0LtulziDt4gYvssr3tq1nepqFVCFMLKha4BuLPifojvRmKWMAC280pU6jvE1S9fqLPWRRcYpxkz-62fbFBT-oqi2re_gTJS3I1zpmwdpjQZ4vvU8caS4RdwQiOCWCu_Ohi1dj8diXrHh7ETdSCtdsARb8gkwHI9lc-4k2NSDNi_aMmzEujfckdpjmx6Fhi28D43F_M1tswDGPmoNI_1QMUp7jYK8n-9zfLRj99PwLKtNsgSWnNQ1tjdjcAu37NOfTZkquj31WPHhQ=w1035-h690-no

James Brenan na mimi Dar es Salaam

Hakuna hata mahali pamoja wamesema kuwa kuna udini ndani ya kitabu hicho.

Wote kwa umoja wao wamekubaliana kuwa ni kitabu kilichosahihisha historia ya
Tanganyika.

Hawa hawakuishia hapo.

Baadhi yao wamenialika kwenye vyuo vyao nikatoe muhadhara na nimekwenda na
kufanya hivyo.

Prof. James Giblin kanialika University of Iowa na niliitika mwaliko na nimezungumza
chuoni kwake.

mxeIPzcZWz2fVo-iAF61vlZzZ3Z_XP0d0jVw1sKgYbXm1PaUdPfXXuHxLSCAfY-vK9xarLMFz0jPlj_dk-5T4-WZejHZoYW6X9TfSkrYOyMbawLKCLfXhY_afZlia4um5M7utZcF6JebRRR1mJ3RJ7tz4SUsVkq_LdscPols5vh8pfLtvEhkBRd_kICnTyHb8orMK1K8YV5H8TDZTXHPKkWxov6aQ5CAZ-Z2md3liNN9DbZfSj-wsvaFw0aArggV5emzXJ5qVZMX6dxqZsp5zeTJVrS-S1mAXzSxz2fQauiHwZHULxA1Qh0mBdCkC_YbrD2OdbxudkJPaVfD1Z9e2frfb1i2hl4xfVTVN3pH-UiOr8PnRfR5iO6BmI8vtv0r73TMU8KSrTk1xOFHtEjJ9v3EkRnIVm8uXZIaD-70IrVEOgXBw40_4ASK5_-_BvYPfTaIQ6g1oFvccWhbXxUcDGgOWElMfKymmhfEDFKWitdxUTdcDV9af1-MwUB960GVxcucZjwpIrzrUJghCNC2lrHNE42wqJiQry9jK7PjhVLWs5Q7xOVFwRJRajd85QncwC-BSZBkzp07pu0lxWWKeCKc_lTyqkUO=w480-h360-no

Prof. James Giblin na mimi Chuo Kikuu Cha Iowa

Prof. Jonathon Glassman amenialika Northwestern University Evanston, Chicago na
nimetoa muhadhara hapo chuoni kwake.

Jz8eJae1OIk2GnIx4HOAL1r3eOqxlr7E7vwWM478W75gorY0waViRTej5bJqvT1MWXIFXsucS2q9s0SLRmKVyRz7EwsdEhQajMppLDtLVMDycvscOoEycHH-VHaF02nlQK1qn4_j4j0eOihL8jS28UJETVZ62rORB1-iHkGYMcA2SeAbnnzwmNmsGYTySRsEW62tSIfZVbiOBOlLpO_UcKhCrD45uCTWAOlUBKukm4c8zqFJ1axI5VFz_DT6fheCTaEk5GXh1GOuMdk49_5bJOWM851wYM2m8ScQ1IIx3GhpSMDOo3DxYsGIrdR0KsIG9yLJcwjJ6bwb1b5N-k9w0fJDXFtMUTxAbM3OuGJ4RpTowlr1Ruq7rkvE5CdDw3lACNEuudbpTrtrSd5qsx0vCi7TxH4YU8uF-5XLqSwBGv1t6Zy4-ChC7L0wmvgEifu6DCQcfL5bNquq_NbVYX469IHK5QEmTXZW_Wgtf4djt3QalEE00Eg5S67MJrksBdWZKIGmV8lc4wR_WJCFPdu_nmK_rdsJeX8jqTjZ5u57yPmsiH_hFSC0S3nfKz3AoZrmLqOoG28fD8Xw-b3TzmYJqjd3ksW0PZ5B=w480-h360-no


Dr. Kai Kresse wa Zentrum Moderner Orient (ZMO) alinialika kwenye taasisi yake ya
utafiti katika historia Berlin, Ujerumani nimeitika mwito na nimezungumza hapo.

8VC0IZYHk72VDPoMbixiQHstHp7AgmQhVmzOj-07j5YbxMvKvQO8YgazDnovgjDISvy5Bz__10_P-YLmvyHaIfBUlE4xgY8V8rIoOZE26bDWkOgTlHNWuNJ5qoO-I8xkoECZ6IT1dsXL5oa_Bz-kT6AYR3UZi__-pN9-60FByYmum6Dpt0O8HzJ9hdX51JuKktcFfC3XmFhMjwufvYCr6THGQR0VCBXNTXaUv6Vv7H1MGmoEARaSgzOH8aVyu7VyW4zjke6bJArsLY9KhkY4YmojiXS_q64jI506YS0mmfgLCO_-lC2QJBPx-fuPrlU0khAiC6DEL2fyoAt23pAAf3KBNYR_9beoiIEf_3pRvsbReiQ8BPtsRMVjHHU1avPU1KpSsqQLVEyTgKzVo151TWbkmLozmd4tIOA-SRU8idvdHT9ZvPMHQJdygTtpx03sVK9_taMApKG9BpUmywXMzBQsQFnFa3MZ1rdS7EKz1q8A8IdOPSIMQ6gPJUWSCedvPQZcPEgpdTbgtG7l-2qN-oQ2oke4vmQl-NrVphWxyfH-fHeNCZRSdHWgUZe4N31ZPcxenCqiulcj9dXCm7rDIzhU2sHfX-hy=w480-h360-no

Kai Kresse na mimi Berlin

Hata katika maswali na majibu katika mihadhara hii yote hakuna hata mtu mmoja
aliyezungumza kuhusu udini katika maandishi yangu.

Ikiwa wewe kwa ujuzi wako unaona kuwa mimi naandika udini hii itakuwa bahati mbaya
kwako.

Hii mosi.

Pili kuzungumza msikitini ndiko ninakoalikwa na Waislam na hata ikiwa nitaalikwa kanisani
In Shaallah nitakuja.

Labda nikukumbushe kuwa William Lukuvi alizungumza kanisani na aksema Zanzibar
lazima iwe chini ya uangalizi wa Bara ili Uislam usipate nguvu.

Unazungumza kuwa mimi, ''nataka muamini hii historia ndiyo ya kweli.''

Hapana kuamini au kutoamini kunategemea akili ya mtu anavyoliona jambo na kutafakari.

Mimi silazimishi mtu kuniamini ingawa napenda mtu asome historia hii kisha mwenyewe
ataamua nani anasema kweli.

Ni hii historia rasmi iliyodumu kwa miaka na miaka iliyowafuta wazee wangu au hii yangu
iliyochapwa London mwaka wa 1998.

Nyerere hakuombwa na wazee wowote kuja TAA.
Inaonyesha huijui historia ya Nyerere ambae unataka kumtetea katika maandishi yangu.

Nyerere alikuja na barua kutoka kwa Hamza Mwapachu aliyekuwa masomoni Chuo
Kikuu cha Wales, Cardiff kwenda kwa Abdul Sykes na aliyempeleka Nyerere kwa Abdul
nyumbani kwake alikuwa Joseph Kasella Bantu.

Hii ilikuwa mwaka wa 1952 na ni mwaka huo baba yangu alipomjua Nyerere hapo kwa
Abdul Sykes kwani kila mwisho wa juma Nyerere aifika kwa Abdul kumtembelea na
kuzungumza mustakbali wa nchi yao.

Hakika hakuna mtu anaeweza kufuta mchango mkubwa wa Nyerere katika TANU hili
haliwezekani hata kidogo.

Na hakuna mtu anaeweza kufuta mchango wa Mzee Klesit Sykes (1894 - 1949) katika
kuwaandaa Waafrika wa Tanganyika kuelekea kuwa na chama cha siasa.

Kwa msisitizo huu huu hakuna anaeweza kufuta mchango wa Abdul Sykes na mdogo
wake Ally katika kuiunda TANU na kupigani uhuru wa Tanganyika na haya ni majina
machache tu.

Labda hapa ndipo ilipo tofauti yetu kati mimi na wewe.
Wewe ungependa Nyerere aenziwe pweke.

Mimi nakueleza kuwa hakuwa peke yake.

Alikuwapo Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir,
John Rupia, Stephen Mhando, Zuberi Mtemvu, Ali Mwinyi Tambwe, Bi. Tatu biti
Mzee, Bi. Sharifa biti Mzee, Bi. Halima Selengia, Bi. Titi Mohamed, Mshume Kiyate,
Jumbe Tambaza, Idd Tulio, Idd Faiz Mafongo, Dr. Vedasto Kyaruzi, Kasella Bantu,
Said Chamwenyewe, Yusuf Chembera, Salum Mpunga, Saadan Abdu Kandoro
na
wengi wengi wengi sana ambao wote mimi najua michango yao na nimeiandika hapa siku
zilizopita na wengine nimekuwekeeni hadi picha zao wakiwa na Nyerere.

facebook_1425848560953%2B%25281%2529.jpg

Kushoto aliyesimama ni Ally Kleist Sykes, na kulia kwake ni
Abdulwahid Kleist Sykes, mbele kushoto ni Kleist Sykes
Mbuwane na
Abbas Kleist Sykes. Katika hawa aliye hai ni Abbas.
Ukoo huu umeacha kumbukumbu nyingi kwa maandishi katika harakati za
kuunda African Association 1929 na kuunda TANU 1954. Picha hii imepigwa
mwaka wa 1942 Abdul aliporudi Dar es Salaam kutoka Lower Kabete Kenya
alipokuwa akipata mafunzo ya kijeshi katika King's African Rifles kabla
hajakwenda Burma kujiunga na Burma Infantry. Angalia utaona Abdul amevaa
sare ya Jeshi la Mfalme wa Uingereza. Ilikuwa akiwa Burma Vita Vya Pili Vya Dunia
(1938 - 1945) ndipo alipoamua kuwa 6th Battalion iliyokuwa na askari kutoka
Tanganyika waunde TANU wakirudi Tanganyika kudai uhuru.
 
Pasco,
Unataka kupiga ala bila kujifunza chromatics.
Unataka kuizungumza historia ya Zanzibar bila kusoma historia yenyewe.

Lakini kubwa ni kuwa hata ''intellect,'' yako ni tatizo kidogo maana hata
mtu akikusoma hili linamtokea dhahiri kabisa.

Ataliona jinsi michango yako inavyokosa mantiki na matokeo yake ni haya
ya kuchanganya mambo.

Unachokijua wewe ni, ''mapinduzi matukufu,'' huna kingine.

Nikikuwekea mabandiko ya kukufikirisha unapotea kwa muda kisha unaibuka
na jambo lingine kabisa lile unalikimbia.

Ni kweli waliofungwa jela za Bara walinusurika kuuawa.
Lakini iweje umshukuru mtu aliyekukata mkono kwa kukurudishia kidole gumba?

Jana nilikuwa Zanzibar kutoa mada kuhusu Sheikh Hassan bin Amir.
Walionialika ni Mwinyi Baraka Foundation.

DSCN0876.JPG


Kongamano la Mwinyi Baraka Foundation 12 June 2016 Ukumbi wa Baytul Amiyn

Sheikh Hassan bin Amir ni Mzanzibari na alishiriki katika kuunda TANU na ni
mmoja wa wajumbe wa TAA Political Sub Committee 1950 wajunbe wengine
wakiwa, Dr. Kyaruzi, Abdul Sykes, Stephen Mhando, Hamza Mwapachu,
Said Chaurembo
na John Rupia.

Sheikh Hassan bin Amir ndiyo aliyiongoza TANU kuwa ''a nationalist secularist
party,'' baada ya kufanya mkutano wa siri Mtaa wa Pemba Dar es Salaam na
baadhi ya viongozi wa TANU mwaka wa 1955 wakiwamo Rajab Diwani, Sheikh
Abdallah Chaurembo, Sheikh Nurdin Hussein
na wengineo.

Sheikh Hassan bin Amir alikuwa Mufti wa Tanganyika hadi alipofukuzwa na
Nyerere mwaka wa 1968 na kurudishwa Zanzibar na kupigwa marufuku

kukanyagaTanganyika baada ya ''mgogoro,'' wa East African Muslim Welfare
Society (EAMWS) uliopelekea kuundwa BAKWATA.

Lakini baada ya Sheikh Hassan kufariki mwaka wa 1979 Nyerere alihudhuria
hitma yake Msikiti wa Mtoro alialikwa na Sheikh Abdallah Chaurembo na
Sheikh Kassim Juma.

Mimi nilikuwapo hapo msiktini siku hiyo.

Ikiwa huyajui haya kwa undani maisha utahangaika na historia ya Tanganyika
kwani huu ndiyo msingi unaosimamisha si historia ya Nyerere bali historia nzima
ya uhuru wa Tanganyika na baada yake.

Pasco,
Hebu jitulize na isome historia kwanza kabla hujataka kupambana na mimi.
Watoto wa mjini wana Kiswahili chao.

Wanasema, ''Mimi si saizi yako.''
Maana ukinivaa utapwaya.
Maalim sheikh wngu alhaji Mohamed Said hapo ndio unapo nikosha nafsi yngu pasco baada kutafuta Elimu toka kwako naona anaropoka kwa vitu asivyo vijua kikubwa usichoke kumpa Elimu ila hakika ujinga wake umma wote tumeuona hakika mungu akulinde akupe umri mrefu ili tuendelee kupata Elimu toka kwako
 
Mzee Mohammed Said, umesema huwezi kumpa sifa isiyositahiri Nyerere wala huwezi kumkosea adabu kwa kiasi anachokisema Pasco, lakini mtu akikaa akasoma mabandiko yako kwa utulivu na akili iliyowazi (open mind), atakuelewa kabisa mlengo wa maandishi yako. Mimi sina tatizo na maandishi yako kwa sababu kwanza kabisa najitambua na natumbua mnachokidai tangu siku nyingi sana. Pasco anasema maandishi yako yamejaa udini na kumdharau Nyerere kwa sababu mbili tu :kwanza, mihadhara mingi na hii historia unalotaka tuiamini kuwa ndo ya kweli inafanyika kwa asilimia kubwa misikitini (na wewe ni shahidi). Je, kizazi chenye uhalali wa kufahamu historia sahihi ya kupigania uhuru wa Tanganyika ni waislam pekee!? Pili :makongamano yenu mengi yanawalenga vijana wa kiislam na huko ndo mnaanza kuelezea negativite kuhusu Nyerere na uhuru wa Tanganyika, Je, hao wengine walioshiriki Jamii isiyokuwa ya Kiislam hawana haki ya kufahamu mchango wao!? Au kuelezea hiyo historia ya "kweli" kwa wengine mtakosa thawabu!? Kitu kingine unachotakiwa kusema kwa ukweli ambao naamini unakuuma kuusema na ndio maana hutaki kuusema ni kwamba NYERERE HAKUJIPELEKA TAA! ALITWA NA ALIOMBWA NA HAO WAZEE WALIOKUWA WANAFANYA HIZO HARAKATI ZA KUTAKA UHURU. SASA TWAMBIE, NI KOCHA GANI DUNIANI ANANUNUA MCHEZAJI ASIYEKUWA NA UWEZO WA ZIADA!? mchango mkubwa wa Nyerere upo, utaendelea kuwepo na wala hautaweza kuufuta kwani hata hao waliomuita hawakumbeza kama unavyojaribu kufanya wewe! Ingekuwa unachosema kina Afya katika Jamii usingekisemea kwenye majumba ya ibada na wanafamilia wa majumba hayo huku ukifahamu kabisa hao ni sehemu ndogo sana ya wanafamilia wanaohitaji kufahamu hao wapigania uhuru wengine na michango yao. Sio dhambi kwani sote tunafahamu uhuru haukupiganiwa na mtu mmoja, lakini hao wengine walikuwa na kiongozi wao! Na mwisho wa siku katika kikosi ukubali ukatae KIONGOZI ndio anayebeba kombe juu! Stop negativite towards Nyerere, be free to appreciate his work!
Lete ushahidi kuna kitabu kimeandika na maalim sheikh wngu alhaji Mohamed Said maisha na nyakati za abdulwahid sykes sina hakika km hicho kitabu kinauzwa misikitini tu km unavyotaka tuamini kuna kitabu kingine pia uamuzi wa ubasara wa tabora sina hakika na wala hamna ushahidi km kinauzwa misikitini tu km unavyotaka tuamini lete ushahidi wapi na lini mohamed said amemtukana au kumkashifu mwl nyerere kikubwa mnataka pia mwl apewe pia sifa zisizokuwa zake itakuwa ngumu hyo vitabu hvyo vinapatikana dukani ilala na wateja wngu ni dini zote na makabila yote
5d6f0a41b402acec3d69fa4faf5805ba.jpg
2118bc4e252e48a48a0566008876a993.jpg
419ff5aa2a723c60c7914e5c3282fd66.jpg
2ff6ae9bbb39f6785e9d5a1eb1dd7414.jpg
 
Lete ushahidi kuna kitabu kimeandika na maalim sheikh wngu alhaji Mohamed Said maisha na nyakati za abdulwahid sykes sina hakika km hicho kitabu kinauzwa misikitini tu km unavyotaka tuamini kuna kitabu kingine pia uamuzi wa ubasara wa tabora sina hakika na wala hamna ushahidi km kinauzwa misikitini tu km unavyotaka tuamini lete ushahidi wapi na lini mohamed said amemtukana au kumkashifu mwl nyerere kikubwa mnataka pia mwl apewe pia sifa zisizokuwa zake itakuwa ngumu hyo vitabu hvyo vinapatikana dukani ilala na wateja wngu ni dini zote na makabila yote
5d6f0a41b402acec3d69fa4faf5805ba.jpg
2118bc4e252e48a48a0566008876a993.jpg
419ff5aa2a723c60c7914e5c3282fd66.jpg
2ff6ae9bbb39f6785e9d5a1eb1dd7414.jpg

Rubawa,
Kuuza vitabu msikitini sidhani kama ni tatizo.

Kanisa Katoliki linauza vitabu kanisani pale Cathedral Bookshop
kwa miaka mingi sana.
 
Rubawa,
Kuuza vitabu msikitini sidhani kama ni tatizo.

Kanisa Katoliki linauza vitabu kanisani pale Cathedral Bookshop
kwa miaka mingi sana.

Na pia mueleze kuwa mimi sijasema kuhusu kuuza vitabu vyako, nimeongelea mihadhara, makongamano na hutuba nyingi zinazoelezea harakati za uhuru wa Tanganyika inayofanywa na mashehe wanaodhani wanaelewe sana kilichotokea hufanyika misikitini na /au makongamano yanayohusiana na waislam. Hicho ndo nilichosema, uuzwaji wa vitabu hutegemea sana na uhitaji na uwepo wawateja katika eneo husika Sina jambo na hilo Rubawa
 
Na pia mueleze kuwa mimi sijasema kuhusu kuuza vitabu vyako, nimeongelea mihadhara, makongamano na hutuba nyingi zinazoelezea harakati za uhuru wa Tanganyika inayofanywa na mashehe wanaodhani wanaelewe sana kilichotokea hufanyika misikitini na /au makongamano yanayohusiana na waislam. Hicho ndo nilichosema, uuzwaji wa vitabu hutegemea sana na uhitaji na uwepo wawateja katika eneo husika Sina jambo na hilo Rubawa
Uncle...
Haya ni mambo madogo sana.
Muhimu ni kwangu kuandika historia ya kweli ya TANU.
 
Kwenye historia ya Uhuru wa Tanganyika Nyerere,Ally Sykes,Abdul Sykes wana mchango mkubwa sana.
Zamani kwenye kitabu cha cha siasa cha darasa la nne majina ya Ally,Abdul,Nyerere na wenzao akina John Rupia na Dossa Aziz wametajwa kama wanachama wa mwanzo kujiunga na TANU.
Kila MTU ana mchango wake na ni lazima tuheshimu mchango wa mashujaa wetu hawa,nguvu yao ya pamoja na michango yao ndiyo iliyofanikisha Uhuru wa Tanganyika.
Tatizo wengi wetu tunaongozwa na mihemko ya kidini kuchambua/kuelezea historia ya Uhuru wa Tanganyika hapo ndio tunapokesea.
 
Hiyo picha inaonyesha huo ukoo wa kina Sykes ulikuwa na fedha sana mwaka 1942 Ally amevaa suti na tai!

Na ni watunzaji wazuri wa nyaraka na picha.
 
Hiyo picha inaonyesha huo ukoo wa kina Sykes ulikuwa na fedha sana mwaka 1942 Ally amevaa suti na tai!

Na ni watunzaji wazuri wa nyaraka na picha.
Kitulo,
Ngoja nikuchekeshe.

Mimi ''air condition,'' yangu ya kwanza niliona ofisini kwa Ally Sykes
katika miaka ya ya mwanzoni 1960s alipokuwa akifanya biashara na
Peter Colmore.

Vilevile hapo ndipo kwa mara ya kwanza niliona pia ''reel to real tape deck.''

Hivi vilikuwa vyombo vya hali ya juu vya kunasa sauti na kupiga muziki kwa
aina ya ''high fidelity.''

Iko siku nilimkumbusha Bwana Ally habari hii akacheka sana.

Ingia hapa utaweza kujifunza vipi watu hawa waliweza katika ukoloni
kufanyakazi na kunufaika na hali iliyokuwapo wakati ule:

Mohamed Said: THE BUSINESS GENIUS OF PETER HORACE COLMORE AND ALLY KLEIST SYKES
 
Na pia mueleze kuwa mimi sijasema kuhusu kuuza vitabu vyako, nimeongelea mihadhara, makongamano na hutuba nyingi zinazoelezea harakati za uhuru wa Tanganyika inayofanywa na mashehe wanaodhani wanaelewe sana kilichotokea hufanyika misikitini na /au makongamano yanayohusiana na waislam. Hicho ndo nilichosema, uuzwaji wa vitabu hutegemea sana na uhitaji na uwepo wawateja katika eneo husika Sina jambo na hilo Rubawa
Nlikuwa sijui kwamba ujerumani, USA, IRAN NK kote uko sheikh mohamed said alikokuwa anaitwa na kualikwa kumbe ilikuwa mihadhara ya misikitini hama kweli nmeamini mmejaa chuki na fitina za ajabu bila sababu na Alhaji Mohamed Said muwe mnajaribu kumsoma vzuri kwanza sio kila kitu muwe mnatanguliza chuki tu
77b3fa12d91f7cbb7e89ac5d9e3c2824.jpg
54d67c09ff2712be52c83ef365b6e6c7.jpg
 
Back
Top Bottom