Kuna jamaa aliokota nyumba.
Kuna kampuni ilikua ya ufugaji kwa msaada wa watu wa nje,badae shirika likafa,
Nyumba zilikua pembeni kidogo ya kijiji,zile nyumba kikapewa kijiji kiamue matumizi,
Ila kuna sehem walikua wanaoshea mifugo yao ni mbali kidogo na kijijini,kijiji kama cha nne hivi lakini zamana hapo ilo eneo lilikua mbali na kijiji.
Hivyo nyumba hiyo ilibaki tupu bila mtu,bahati nzuri mwaka 2006 ikajengwa shule ya kata karibu na eneo ilo,hivyo pakaanza kuwa na mahitaji.
Mwanzoni kuna kichaa alikua anakaa humo,wale machizi fresh yani sio kichaa jumla jumla,amekaa umo kwa muda kiasi akaondoka.
Kuna jamaa akaona isiwe tabu,akapasafisha,akaanza kuishi humo,badae kapiga rangi karekebisha mlimo bomoka ,basi maisha yanasonga.
Tokea 2007 mpaka saizi anaishi hiyo nyumba,historia hiyo alitupa yeye mwenyewe wakati wa sensa.
Na watu wengi wapya ilo eneo wanajua ni kwake na wenyeji wanahisi amenunua au kuna hatua alichukua