Hasara zipi unazipitia kwa kuwa na tabia za introvert?

Hasara zipi unazipitia kwa kuwa na tabia za introvert?

Mimi sijswahi kuwa na hasira hizo.

Ila nina mshkaji wangu yuko kenya ni mshkaji kishenzi,nikipata jambo gumu la stress nalipunguzia kwake nyongo inapungua kidogo mambo yanaenda,mana kuna mambo huwezi kumuambia wife unayamaliza juu kwaju
Kiutu uzima nakubali.
 
Introvert = Online Businessman
Introvert = Books Reader
Introvert = Gamer
Introvert = Movies Addicted
Introvert = Workout/Yoga

Bana kama wewe introvert na hau engage kwenye kitu hata kimoja hapo juu toka tu humo ndani kapige story kijiweni usije kuwaza kujiua bure.

NB: Raha ya kuwa Introvert especially Dunia ya sasa uwe na pesa/kipato bila ya hivi tatizo sana, kuna material things zinasaport hali ya Introvert most of them ni Expensive kuwa navyo, pia Introvert hatakiwi kuwaza pesa ya kula anatakiwa kuwa na kipato ili awe Mind Free kuwaza makubwa.

Mimi Introvert sana ila kwasababu za uchumi inabidi niuvute u-extrovert kidogo kwa muda kuna mshikaji wangu anakuja DSM tutaishi wote geto kuna mitikasi yakufanya, So kuna uhusiano mkubwa au mvutano wa Uchumi na U-introvert kuna watu wamekuwa Introvert baada ya kuwa na uchumi/kipato.
 
Introvert = Online Businessman
Introvert = Books Reader
Introvert = Gamer
Introvert = Movies Addicted
Introvert = Workout/Yoga

Bana kama wewe introvert na hau engage kwenye kitu hata kimoja hapo juu toka tu humo ndani kapige story kijiweni usije kuwaza kujiua bure.

NB: Raha ya kuwa Introvert especially Dunia ya sasa uwe na pesa/kipato bila ya hivi tatizo sana, kuna material things zinasaport hali ya Introvert most of them ni Expensive kuwa navyo, pia Introvert hatakiwi kuwaza pesa ya kula anatakiwa kuwa na kipato ili awe Mind Free kuwaza makubwa.

Mimi Introvert sana ila kwasababu za uchumi inabidi niuvute u-extrovert kidogo kwa muda kuna mshikaji wangu anakuja DSM tutaishi wote geto kuna mitikasi yakufanya, So kuna uhusiano mkubwa au mvutano wa Uchumi na U-introvert kuna watu wamekuwa Introvert baada ya kuwa na uchumi/kipato.
Mkuu ukiwa na pesa ndo tabia yako inafahamika.

Kama unazo pesa alafu hunywi pombe wewe sio mlevi kwa sababu uwezo wa kupata pombe unayo.

Kama una pesa na sio jeuri basi wewe huna tabia ya jeuri kwa sababu unazo sababu za kuwa jeuri.

Kama una pesa na sio malaya basi wewe sio malaya kwa sababu uwwezo wa kuwa malaya unao ila hujataka kwa sababu mbalimbali.

Na kama unazo pesa alafu bado ni mtu wa kujitenga na sio mtu wa viwanja na kutanua basi hapo ujue wewe una tabia za hao introvert kwa sababu sababu ya kutoka unayo kwa kuwa una pesa,sehemu za kwenda kutumia zipo lakini husukumwi na pesa zako kutoka nje.

Kwa hyo pia mtu anaweza kuwa introvert lakini akawa anatoka anapiga misele kutafuta pesa lakinni asili yake sio mtu wa misele lakini ndo maisha anatafuta.
 
Kushindwa kujichanganya na watu ambao kwa namna moja au nyingine khna faida kufahamiana nao na pia kushindwa kutoa hisia zangu kwa mtu nnayempenda.

Changamoto nyingine ni kushindwa kuja ma majibu ya haraka katika muda ambayo yanahitajika kwani nachukua muda mrefu kuprocess taarifa na kuja na mjibu sahihi, kitu ambacho huwa kinawakwaza wakati wengine nnaofanya nao kazi
Kweli hii inanihusu hata mimi.
 
Tabia ya kupenda kukaa peke yangu bila kuwa na mazoea sana na washakaji ama majirani, kuna siku niliumwa wakuu nikakaa ndani siku nzima nakunywa maji tu hakuna anayejua kama naumwa.

Homa ilinikamata vibaya nje sionekani washakaji na majirani wakajua ndio kawaida yangu kuwa ndani kumbe mwenzao maji ya shingo, niko mbali na familia, wife hayupo.

Nikapiga simu kwa wife, wife akasema huyu jamaa atakufa kwa sababu ananijua sina kampani, wife akasafiri kesho yake akaja ndio ikawa afadhali yangu maana ugonjwa ukiwa peke yako unazidi.

Nikasema nikipona mimi jamani ntatafuta washkaji wa kutembeleana ili nikipata matatizo nisaidiwe, baada ya wiki kupona ndio kwanza nikazidi kujichimbia ndani na vitabu vyangu uchwara[emoji3][emoji3][emoji3]

Nashauri wakuu tujitahidini kuwa na watu wa karibu washkaji ama majirani, mimi imenishinda kidogo.
Nikasema nikipona mimi jamani ntatafuta washkaji wa kutembeleana ili nikipata matatizo nisaidiwe, baada ya wiki kupona ndio kwanza nikazidi kujichimbia ndani na vitabu vyangu uchwara[emoji3][emoji3][emoji3]

Hahahhaha
 
Kuchoka kuwa introvert ni Sawa na kuuchoka uasilia wako,unaweza jaribu kujibadili ila mwisho wa siku unajikuta peke yako pasipo kupenda
Me mpaka Leo zaidi ya mika 24 cjawai kuwa na mpenzi/demu nikijaribu kutafuta mpenzi kunamaswali huwa najiuliza na kujijibu mwisho Siku zinaenda hvhv
Hahaha inafurahisha mno
 
Mimi sipendi kelele ya aina yoyote. Connection niliyonayo ni ya watu ninaofanya nao kazi. Sikuwa mzungumzaji tangu nilivyokuwa shule. Wengine waliniita mkimya, wengine waliniita kauzu. Wengine wakasema huyu wakishua hapendi bughudha na watu.

Starehe yangu muvi, kucheza game, kula na sasa hivi nina plan ya kujifunza kutembelea mbuga na hata mikoa tofauti kwa kutumia likizo zangu ili nijifunze zaidi kuhusu mazingira na maisha kwa ujumla. Imenifanya muda wangu mwingi nimekuwa najifunza mambo tofauti na kusoma vitabu tofauti vya dini vya maarifa na kuhusu mambo mbalimbali.

Vipindi ninavyovipenda unaweza ukaniita dingi! Taarifa ya habari, channel inayoitwa Investigation Discovery, National Geographic, Beyond Belief: Fact or Fiction tangu 2008 nilikuwa naitizama, mpenzi wa You Tube channel zinazohusu watu wanaofanya kilimo na ufugaji wa kuku. Vipindi vinavyohusu ujenzi wa nyumba. Napenda science pia! Imenifanya nawaza tofauti.

Kingine nipo real tu sifeki maisha. Na imenifanya mambo ya ujana mengi siyajui. Sisikilizi radio naona wanachokizungumza si ninachokitaka. Nimeacha kusikiliza tangu 2012 au 2013! Naona wanazungumza ujinga tu na mimi nahitaji vitu vitakavyonijenga.

Kingine imenifanya nafocus kwenye kujenga maisha na kuyafanya yawe bora zaidi. Sipendi ujinga! Sifuatilii mtu labda awe kafanya kitu kinachoigusa jamii ndiyo nitachungulia. Sishoboki na mtu. Hata nikijihisi mpweke kinachonitoa upweke ni kwenda mahali kukaa peke yangu sihitaji bughdha na mtu.

Kingine naamini Mungu yupo. Inanipa amani na furaha ndani ya moyo kwa sababu napenda kumkumbuka.
Hongera sana mkuu
 
Sahihi mkuu.

Na mimi nina machache ya kuelezea lakini naona inatosha kuyasoma ya wadau.


Muhimu naona kuwa watu sisi wenye tabia hizi tutumie muda wetu kujinufaisha zaidi kuliko mtu anakaa peke yake huku akifanya ujinga.


Tabia ya kukaa peke yangu imenifanya niwe mtu wa kuwaza tofauti sana,na hili nalishuhudia kwa watu wangu ambao wamekuwa wakinitegemea katika mawazo wakati wao ni watu wazima.

Kwa kweli hii tabia ni nzuri sana,japokuwa mimi nina rafiki angu
Ni kama hujamalizia mkuu, japokuwa kuwa una rafiki yako ....
 
Back
Top Bottom