Hatma ya Muslim University of Morogoro na Maono ya Aga Khan kuwasaidia Waislamu kujenga Chuo Kikuu

Hatma ya Muslim University of Morogoro na Maono ya Aga Khan kuwasaidia Waislamu kujenga Chuo Kikuu

City...
Hapana hilo ndilo jibu lake sijakwepa.
Ikiwa wewe hukulipenda jibu hili mimi sina jibu lingine.

Ikiwa hukupendezewa na huo waraka ni bahati mbaya kwako.

Muhimu ni kuwa waraka huo ni sehemu ya historia ya Waislam wa Tanzania.
Mzee Said, waraka nimeusoma na kuuelewa. Lakini, haujibu swali hilo uliloulizwa. Ukweli ni kwamba hakuna ubaguzi wowote wa kidini unaofanywa na NECTA. Hasa katika nyakati hizi.
Uwezo wa mwanafunzi ndiyo utampeleka mbele au la, safari yake itakoma.
 
Sawa. Sasa mzee, kwanini Bakwata haijajenga chuo chochote?
Au la, kwanini hamjaanzisha taasisi mbadala wa EAMWS ili mtimize mpango uliokuwepo. Kama shida ilikuwa Nyerere na serikali yake, alikoma kuwa rais miaka takribani 40 iliyopita.
City...
Inaelekea wewe ni mgeni katika historia hii.

Usipate tabu.

Bakia hapa hapa Jukwaa la Historia na usome post za nyuma.
 
Mzee Said, waraka nimeusoma na kuuelewa. Lakini, haujibu swali hilo uliloulizwa. Ukweli ni kwamba hakuna ubaguzi wowote wa kidini unaofanywa na NECTA. Hasa katika nyakati hizi.
Uwezo wa mwanafunzi ndiyo utampeleka mbele au la, safari yake itakoma.
City...
Ikiwa unaona hapakuwa na ubaguzi yote sawa.
 
Shida ya waislam wao main focus yao ni dini, kwa hio hata kwenye taasisi zao ni mwendo wa kufocus na dini tu
 
Kipindi cha Ali Hassan Mwinyi, Aga Khan alikuja nchini kwa mara ya kwanza baada ya kutokanyaga ardhi ya Tanzania kwa miaka 20. Kwa maneno ya Mohamed Said Aga Khan aliitisha mkutano wa Waislamu ambao una mchanganyiko wa BAKWATA na wawakilishi wa iliyokuwa EAMWS. Na kwenye mkutano huo HAKUKUWA na MKRISTU hata mmoja. Yasemekana Songambele alisema Waislamu hawahitaji Chuo Kikuu.

Mwaka 2000 wakati wa B W Mkapa, akaamua kuwapa jamii ya Waislamu kilichokuwa Chuo cha TANESCO pale Morogoro.

Je ni Waislamu wangapi wenye passmark za juu za A- Level wanadahiliwa pale Morogoro dhidi ya Waislamu wanaochagua kwenda vyuo visivyo na itikadi ya dini kama UDSM, Mzumbe, SUA, SAUT na MUHAS?


Mumeshindwa kujua mnchotaka, bado Mohamed Said unawalaumu JK Nyerere na WAKRISTU kuhusu elimu.
Tunataka tufundishwe kufuga majini na kuroga kwa albadili
 
Nyerere alitaifisha shule nyingi sana za kikiristu na kuzifanya za umma ili watu wote wasome bila kujali dini zao. Elimu ya Msingi hadi Chuo kikuu ilikuwa bure kwa wote, lakini watu waliofundishwa kulaumu watatafuta kila sababu kuwa waislamau walionewa wakati hali halisi ilikuwa kwamba mitihani yote kuanzia ule wa darsa la saba hadi wa Form 6 ulikuwa unatolewa kwa namba ili kuepuka bias ya majina, lakini bado watu walilalamika kuonewa tu. Nadhani watu wengine mafunzo ya dini wanayopata ni ya kuamini kuwa wanaonewa tu.
Haya ndiyo huyu mfiadini mjahidina Mohamed Said hataki kusikia. Ila ukweli ndiyo huwo
 
Nyerere alitaifisha shule nyingi sana za kikiristu na kuzifanya za umma ili watu wote wasome bila kujali dini zao. Elimu ya Msingi hadi Chuo kikuu ilikuwa bure kwa wote, lakini watu waliofundishwa kulaumu watatafuta kila sababu kuwa waislamau walionewa wakati hali halisi ilikuwa kwamba mitihani yote kuanzia ule wa darsa la saba hadi wa Form 6 ulikuwa unatolewa kwa namba ili kuepuka bias ya majina, lakini bado watu walilalamika kuonewa tu. Nadhani watu wengine mafunzo ya dini wanayopata ni ya kuamini kuwa wanaonewa tu.
Huyu mzee anapaswa awahimize wenzake kwamba:-

Wapeleke watoto wao shule Bora na vyuo Bora hio ndio harakati muhimu anayopaswa ifanya wakati huu.

Ili kupata jamii ya waislamu wasomi kutosha kwenye soko la Ajira.

Haya makelele yao ya sijui walionewa sijui wanaonewa Kilikwenda kilirudi ni time wasting campaign. At the same time wakristo wanapeleka watoto shule Bora na vyuo hadi nchi za nje kwa wingi.

Waache hizi mbanga zao hazitowasaidia.

Alhaj Ally Hassan Mwinyi aliwahi waambia hivi hivi pelekeni watoto wakamnasa kibao kwenye vikao vyao walivyomualika wenyewe.

Shida inaanzia kwao siku zote.
 
Mzee wangu unazunguka sana na hutaki kuukubali ukweli........hakuna ambae hajui kuwa waasisi wa harakati za kudai uhuru wa nchi walikuwa ni Waislamu tena walikuwa hawana DNA za utanganyika

Swali langu ni kuwa je,kwenye hao masheikh na Waislamu wote uliowataja nani alikuwa na uwezo Sawa na Nyerere kielimu au ata kimtazamo?? Ukinijibu hili swali nitajua kweli unachozungumza ni sahihi

Ata Zanzibar penyewe waasisi wa Mapinduzi ni Waislamu tena wengi wao masheikh ila bado Muikristo mmoja aliyeongoza Mapinduzi yale tukufu........kwahyo hii ni kusema kwamba Waislamu wapo vizuri kwenye kupiga mdomo ila inapotakiwa kuweka vitendo uwa inawashinda

Äta dola pindi inaposhikwa na Waislamu uwa haifanyi vyema na ufisadi uwa mwingi na akiingia Muikristo ndo huanza kusafisha machafu yote yale yaliyo achwa na Waislamu
Zanzibar ni shida.

Nina mchumba wangu aliwahi fundisha field huko anakuambia shuleni wakija hawafiki saa tisa jioni

Saa Tano washasepa

Ijumaa ndio hawaonekani kabisa.

Class ndio kabisa vilaza wa kutupwa.
 
Huyu mzee anapaswa awahimize wenzake kwamba:-

Wapeleke watoto wao shule Bora na vyuo Bora hio ndio harakati muhimu anayopaswa ifanya wakati huu.

Ili kupata jamii ya waislamu wasomi kutosha kwenye soko la Ajira.

Haya makelele yao ya sijui walionewa sijui wanaonewa Kilikwenda kilirudi ni time wasting campaign. At the same time wakristo wanapeleka watoto shule Bora na vyuo hadi nchi za nje kwa wingi.

Waache hizi mbanga zao hazitowasaidia.

Alhaj Ally Hassan Mwinyi aliwahi waambia hivi hivi pelekeni watoto wakamnasa kibao kwenye vikao vyao walivyomualika wenyewe.

Shida inaanzia kwao siku zote.
Mangungo II,
Naomba nikufunze uandishi na heshima katika mjadala.
Kwanza mjadala nia yake ni kuelimishana si kutoleana kejeli na jeuri.

Mathalani ungeweza kuandika hivi:
''Mzee angewahimiza Waislam kuwapeleka watoto shule.''

Hapo nimeondoa, ''Huyu Mzee.''

Sentensi ina maana ile ile iliyokusudiwa lakini kuna adabu na kuheshimiana.

Unasema, ''Haya makelele...''
Haipendezi si uungwana.

Mimi sipigi kelele na haiwezekani niwe napiga kelele kwa ilm ya somo hili ninavyoijua.

Nataka nikuambie kitu kuwa Waislam si kama unavyowaeleza.

Waislam wamepigania uhuru wa Tanganyika hadi umepatikana kwa salama.

Wameishi na Nyerere ndani ya majumba yao wakati Nyerere hana ndugu mjini Dar es Salaam.

Wametaka kujenga Chuo Kikuu 1968 serikali ikavunja taasisi yao.

Waislam si watu wa leo akasimama mtu ati anawaeleza umuhimu wa elimu na kuwapeleka watoto wao shule.

Hii ni kejeli kubwa.

Watu waliokuwa wanajenga Chuo Kikuu hawahitaji kuhimizwa kuhusu elimu.

Waislam tuna historia ya kutukuka na mimi nimeiandika na inasomwa kwingi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Nimeizungumza historia hii kwa mialiko katika Vyuo Vikuu na katika media ndani na nje ya Tanzania.

Nimeandika '' research papers'' kadhaa na zimechapwa katika academic journals.

Mimi niko hapa kazi niiyojipa ni kusomesha historia ya kweli ya nchi yetu ili watu waifahamu.

Hii ndiyo sababu nakuandikia maneno haya kutaka kukufanya ujaribu kusikiliza yale ambayo hukuwa unayajua.

Wewe unaandika uso wako umeuficha.
Mimi naandika jina langu linafahamika na uso na sauti yangu iko wazi.

Sijajificha.

Jiulize kwa nini sijajificha kisha jiulize wewe mwenyewe kwa nini unaogopa kutambulika unaficha uso wako na jina lako?
 
Nataka nikuambie kitu kuwa Waislam si kama unavyowaeleza.
Wametaka kujenga Chuo Kikuu 1968 serikali ikavunja taasisi yao.
Benjamin William Mkapa mwanzoni mwa miaka ya 2000, aliwapa kiluchokuwa Chuo cha TANESCO pale Morogoro,?je munakitumiaje kusomesha Waislamu?

Au mumeamua muwa watu wa kulalamika tu?
 
Tuanze hapa tulipo hivi sasa kisha nitaweka tulipotokea baada ya uhuru:

TUJIKUMBUSHE

Waislam wa Tanzania na Tatizo la Udini Katika Wizara ya Elimu.

Ndugu Waziri,
Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na maswali mengi wakijiuliza Waislamu, moja likiwa inakuwaje katika maeneo yenye Waislamu wengi ambapo idadi ya wanafunzi Waislamu inakuwa zaidi ya asilimia 70, lakini wanapochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya watoto wa Kiislamu huporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Swali na kitendawili hiki kimekuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa majibu.

Hata lilipofikishwa Bungeni mwaka 1999 na aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni, Mzee Kitwana Selemani Kondo, bado halikupatiwa jibu.

Akihoji juu hali hiyo, Mzee Kitwana Kondo alitoa mfano jinsi hali ilivyokuwa katika shule ya Pembamnazi iliyokuwa na Waislamu watupu na kwa miaka mingi mfululizo kulikuwa hakuna hata mtoto mmoja aliyekuwa akichaguliwa kwenda sekondari kutoka katika shule hiyo.

Aidha alisema kuwa, katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi ilikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini inapokuja kuchaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Waislamu iliporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Akizungumza Bungeni tarehe 2 Februari, 1999 alisema kuwa katika watoto waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1998, idadi ya Waislamu ilikuwa asilimia 71 na Wakristo 29%. Hata hivyo akasema, ilipotoka orodha ya waliochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Wakristo ikawa asilimia 79 (79%) na Waislamu 21%.

Je, hiyo ilikuwa na maana kuwa watoto wa Kiislamu kwa asili yao hawana akili?

Alitaka kujua Mzee Kitwana Kondo. Lakini hakuweza kupata jibu.

Mheshimiwa Waziri,
Ni wazi kuwa Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu ambaye ndiye msimamizi wa mambo ya serikali Bungeni asingeweza kutoa majibu ya uhakika kwa sababu swali lilihitaji kufanyika uchunguzi huru wa kina na makini kwanza.

Mheshimiwa Waziri,
Mwaka 1987 aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Kighoma Ali Malima, aliweka utaratibu mpya wa ufanyaji wa mtihani wa darasa la saba ambapo namba zilitumika toka kufanya mtihani, kusahihisha na kuchagua wanafunzi wa kwenda kidato cha kwanza.

Namba zilivishwa majina baada ya taratibu zote hizo kukamilika. Mwaka huo idadi ya watoto wa Kiislamu waliokwenda kidato cha kwanza iliongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, mara aliondolewa Waziri Malima katika wizara hiyo na utaratibu wa zamani ukarejeshwa ambapo yalikuwa yakichaguliwa majina na idadi ya Waislamu ikaporomoka na kurudi chini ya asilimia 20.

Mheshimiwa Waziri,
Hali kama hii hapana shaka inazua maswali mengi ambayo yanahitaji majibu na majibu hayo hayawezi kupatikana bila ya kufanyika uchunguzi.

Labda tuongeze mifano ili kuliweka wazi zaidi jambo hili.

Mwaka 1983 mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Kopa Abdallah akisoma katika shule ya msingi Kichangani, Kilosa, alikosa kuchaguliwa kwenda sekondari.

Yeye binafsi, wazazi wake na hata walimu wake hawakuamini matokeo yale kutokana na alivyokuwa akifanya vizuri kuliko wanafunzi wote.

Baadae ilikuja kugundulika kuwa nafasi yake alipewa mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Antoni Samirani ambaye alikuwa na uwezo mdogo sana ikilinganiswa na Abdallah.

Kilichofanyika ni kuwa jina la Abdallah lilifichwa na baadae Antoni akapewa jina hilo kimya kimya na kwenda kusoma sekondari akitumia jina Abdallah wakati yeye ni Antoni.

Taarifa zinasema kuwa Kopa Abdallah alipogundua hakuweza kufanya kitu akaishia kuwa dereva.

Hali kama hiyo ilimkuta pia Adam Ramadhani aliyekuwa akisoma shule ya msingi Rutihinda jijini Dar es Salaam na kumaliza darasa la saba mwaka 1999. Yalipotoka matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuonekana kuwa Adam hakuchaguliwa, baba yake hakuamini kuwa mtoto wake anaweza kufeli kutokana na uwezo aliokuwa nao na zaidi akitizama walivyochaguliwa watoto ambao Adam alikuwa mwalimu wao shuleni na mitaani.

Katika kufuatilia suala hilo wizarani, ilikuwa aibu kwa wizara baada ya kuonekana kuwa walichaguliwa watoto wa Kikristo wenye alama za chini kabisa huku akiachwa Adam Ramadhani aliyekuwa na alama za juu kuliko wote.

Mheshimiwa Waziri,
Mifano kama hii ni mingi mno na ipo katika ngazi zote kwa maana kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari, kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano na kutoka kidato cha sita kwenda Chuo Kikuu.

Kwamba hata kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano, wapo watu waliopata kushuhudia majina ya wanafunzi wa Kiislamu yakiwekwa pembeni japo walikuwa na sifa za kuchaguliwa.

Mheshimiwa Waziri,
Ukiacha hujuma katika kuwaacha wanafunzi Waislamu wenye sifa kuendelea na masomo, matatizo huanzia kwenye kuamua nani amefaulu na nani kafeli.

Tuhuma zilizopo ni kuwa wapo wanafunzi wanapewa madaraja ya juu wakati alama zao ni za chini na wapo wanaopewa madaraja ya chini wakati alama zao ni za juu.

Na hii ni kwa masomo yote.

Mheshimiwa Waziri,
Kumekuwa na utamaduni katika nchi hii wa kukataa ukweli.

Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Kamati za Bunge, tumeshuhudia wizi na ufisadi wa kutisha ukifichuliwa Bungeni hivi karibuni hali iliyopelekea mpaka Mheshimiwa Rais kubadili Baraza lake la Mawaziri.

Sasa baada ya kuyasema yote hayo, tunasema kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likilalamikiwa kwa zaidi ya miaka 30, lakini malalamiko hayo yamekuwa yakipokewa kwa sikio la uziwi.

Imefikia mahali tunasema kuwa hatuna tena imani na Baraza hilo.

Mheshimiwa Waziri,
Ili kupata ukweli wa malalamiko na shutuma hizi, na ili kujibu lile swali juu ya watoto wa Kiislamu ambalo halikupata jibu Bungeni, tunaitaka serikali kufanya yafuatayo:

1. Tume huru iundwe kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.

2. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaani na Baraza la Mitihani.

Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa Kumputa ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.

3. Hatua za kisheria na kibinadamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa Baraza la Mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.

4. Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha Makatibu Wakuu Watendaji na Manaibu Katibu Wakuu wamekuwa Wakristo na Wenyeviti wa Baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.

Mheshimiwa Waziri,
Tunaomba ieleweke kuwa tunachotaka ni kupatikana haki na kufanyika uadilifu kwa watu wote.

Hatudai wala hatutaki upendeleo kwa Waislamu na wala hatutaki kuona mtu yeyote anaonewa au kuporwa haki yake, awe Mwislamu au mtu wa dini nyingine.

Tunachoamini ni kuwa kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haina cha kuficha, basi itaunda Tume hiyo kwa haraka na kuhakikisha kuwa ni Tume ya kuaminika itakayofanya kazi yake kwa umakini, kwa kina na kwa uadilifu wa hali ya juu kabisa.

Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa.

Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Ni imani yetu kuwa utayapokea madai ya Waislamu na kuyafanyia kazi kwa umakini na kwa haraka ili kujenga mustakbali mwema wa nchi hii na watu wake.

Tunaomba kuwasilisha,

Mwenyekiti,
Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu

Sasa turudi nyuma wakati tumepata uhuru:


Ipyax,
Yametokea.
Serikali haiko tayari kutoa majibu.

Nina mengi naweza kukueleza muhimu ni wewe uwe tayari kusikiliza.

Marais Waislam hawakuchaguliwa kuchunguza watendaji Wakristo ndani ya serikali wana mchango gani katika matatizo haya yanayoelezwa na Waislam.

Endapo Rais Muislam ataingia madarakani na kuanza kuchunguza tatizo hili atakuwa anatengeneza tatizo kubwa zaidi linaloweza kuigawa nchi zaidi.

Hili la Waislam kuwekeza katika elimu hapa si mahali pake ila ningependa kukufahamisha kuwa baada ya kupatikana uhuru mwaka wa 1961 Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alijiuzulu siasa na kuanzisha taasisi yake, "Daawat Islamiyya," yeye akiwa Mwenyekiti na Katibu wake Schneider Abdillah Plantan.

Sheikh Hassan bin Ameir akasema sababu ya yeye kujiuzulu siasa ni kuwaongoza Waislam katika kutafuta elimu kama alivyowaongoza katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

(Naamini inawezekana historia hii ninayokueleza ikakupa tabu kwani hujapata kuisoma popote kuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mwanachama wa TANU na kapigania uhuru.

Schneider Plantan yeye ndiye aliyesimama mwaka wa 1950 kuutoa uongozi wa wazee katika TAA Rais ambae ni kaka yake, Thomas Plantan na Katibu Clement Mohamed Mtamila na kuingiza uongozi wa vijana Dr. Vedasto Kyaruzi kama President na Abdul Sykes Katibu).

Mwaka wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akishirikiana na EAMWS wakaitisha Muslim Congress agenda kuu ikiwa elimu.

Hii Muislam Congress ndiyo iliyoweka mpango wa kujenga shule Tanganyika nzima na Chuo Kikuu na kazi ilianza mara moja.

Mwaka wa 1968 Rais Julius Nyerere akaweka jiwe la msingi kujenga Chuo Kikuu.

Miezi miezi michache baadae Rais Nyerere akaivunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

Uwekezaji wa Waislam katika elimu na ujenzi wa Chuo Kikuu na shule ukakoma hapo.

Historia hii ni ndefu lakini naamini nimekujibu swali lako na umeelewa matatizo yanayowakabili Waislam.
Nimefanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 1985, Mzimuni P/s na tulitumia namba [sikumbuki Waziri wa elimu alikuwa nani], mwaka 1986 nilirudia tena shule ya msingi, na mwaka 1987 nikafanya tena mtihani wa darasa la 7 [tulitumia namba pia].

Mwaka niliorudia shule ya msingi tulikuwa wengi, watatu miongoni mwao walitumia majina ya Kiislamu na wawili [walikuwa na uwezo mzuri darasani] walifaulu. Nilipokuwa kidato cha kwanza, darasani kwetu waliorudia walikuwa 75% na walikuwa na majina ya Kiislamu.

Yawezekana madai yako yakawa na ukweli fulani lakini ukweli ni kuwa mwamko wa Waislamu kielimu hasa ngazi ya chini ni mdogo. Mimi kwetu ni Kigoma, Mwanga Vamia, na mama yangu alikuwa mwalimu shule ya msingi. Aliwahi kufundisha shule ya msingi Kipampa Ujiji. Aliwahi kutusimulia jinsi wazazi wa kule walivyokuwa wanakwenda shuleni saa 4 asubuhi na kuwachukua watoto wao na kuwapeleka chuoni huku masomo yakiendelea.

Ni siku hizi ndio angalau kuna mwamko wa Kielimu miongoni mwa Waislamu maana hata vyuo huanza kufundishwa alasiri.

Vv
 
We mzee mzushi na muongo mpotoshaji na mnafiki,ni aibu hata kijiita muislam na niaibu kwa dini ya kiisilam kuwa na muumini mpumbafu kama wewe,majina kuuzwa na ushuhuda wa ndugu yangu mkatoliki safi jina lake liliuzwa,ila wewe mnafiki unataka kuleta hoja za hovyo kabisa,unachokitafuta tunakijua.
Huyu mzee siku zote likitokea jambo, huliangalia kwa mlengo wa kidini pale muislamu anapokuwa muhanga. Hivi visa vya nafasi za waliofaulu darasa la saba kupewa watu wengine hata wenye 'majina' ya Kikristo nafasi zao walipewa wengine vilikuwepo vingi, tatizo ni pale mzee Mo anapogeuza na kuliweka kidini. Mimi nilisoma na wanafunzi wengi tu sekondari wenye majina ya Kiislamu ambao walifaulu. Darasani kwetu kulikuwa na 'Wakristo' watano wenye majina ya Kiislamu!

Vv
 
City...
Hapana hilo ndilo jibu lake sijakwepa.
Ikiwa wewe hukulipenda jibu hili mimi sina jibu lingine.

Ikiwa hukupendezewa na huo waraka ni bahati mbaya kwako.

Muhimu ni kuwa waraka huo ni sehemu ya historia ya Waislam wa Tanzania.
Ndio maana tynakuambu unaokoteza hoja..hakuna Mtoto wa Kisslam ambaye Leo hii ananaweza kudai kashindwa kusoma kimfumo! Acha uongo.na kuwapumbaza wachache!
 
Ndio maana tynakuambu unaokoteza hoja..hakuna Mtoto wa Kisslam ambaye Leo hii ananaweza kudai kashindwa kusoma kimfumo! Acha uongo.na kuwapumbaza wachache!
Maku...
Hakuna tatizo uzuri tumejadili.

Umesoma hoja zangu nami nimesoma zako.

Nimeeleza historia ya Waislam jinsi walivyozuiwa kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 kwa kupigwa marufuku EAMWS na kuunda BAKWATA na miaka ya 1970 kwa serikali kukataa OIC kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Nimeeleza matatizo ya ubaguzi katika Wizara ya Elimu na matatizo ndani ya Baraza la Mitihani.

Hii ni historia niliyotafiti na imechapwa katika kitabu na journals.

Vitabu na journals havichapi kazi za kuokoteza kwani huo ni uwanja wa wasomi.
 
Huyu mzee siku zote likitokea jambo, huliangalia kwa mlengo wa kidini pale muislamu anapokuwa muhanga. Hivi visa vya nafasi za waliofaulu darasa la saba kupewa watu wengine hata wenye 'majina' ya Kikristo nafasi zao walipewa wengine vilikuwepo vingi, tatizo ni pale mzee Mo anapogeuza na kuliweka kidini. Mimi nilisoma na wanafunzi wengi tu sekondari wenye majina ya Kiislamu ambao walifaulu. Darasani kwetu kulikuwa na 'Wakristo' watano wenye majina ya Kiislamu!

Vv
Vv,

Hili jibu langu nimempa Makulanga.
Nawe linakufaa pia:

"Hakuna tatizo uzuri tumejadili.

Umesoma hoja zangu nami nimesoma zako.

Nimeeleza historia ya Waislam jinsi walivyozuiwa kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 kwa kupigwa marufuku EAMWS na kuunda BAKWATA na miaka ya 1970 kwa serikali kukataa OIC kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Nimeeleza matatizo ya ubaguzi katika Wizara ya Elimu na matatizo ndani ya Baraza la Mitihani.

Hii ni historia niliyotafiti na imechapwa katika kitabu na journals.

Vitabu na journals havichapi kazi za kuokoteza kwani huo ni uwanja wa wasomi."
 
Benjamin William Mkapa mwanzoni mwa miaka ya 2000, aliwapa kiluchokuwa Chuo cha TANESCO pale Morogoro,?je munakitumiaje kusomesha Waislamu?

Au mumeamua muwa watu wa kulalamika tu?
Stux...

Hili jibu nimewapa pia wachangiaji wengine:

"Hakuna tatizo uzuri tumejadili.

Umesoma hoja zangu nami nimesoma zako.

Nimeeleza historia ya Waislam jinsi walivyozuiwa kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 kwa kupigwa marufuku EAMWS na kuunda BAKWATA na miaka ya 1970 kwa serikali kukataa OIC kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Nimeeleza matatizo ya ubaguzi katika Wizara ya Elimu na matatizo ndani ya Baraza la Mitihani.

Hii ni historia niliyotafiti na imechapwa katika kitabu na journals.

Vitabu na journals havichapi kazi za kuokoteza kwani huo ni uwanja wa wasomi."
 
Nimeeleza matatizo ya ubaguzi katika Wizara ya Elimu na matatizo ndani ya Baraza la Mitihani.
Wizra ya elimu haina ubaguzi wowote sema waislamu hawapendi kusoma. Kama kuna ubaguzi ni vipi wewe ulisoma, akina Kikwete, Prof Malima RIP, Prof Shivji na Waislamu wote kwa maelfu walio na degree!!

Acheni kuharibu nchi kwa ashiki zenu udini. Baada ya maisha hapa duniani huko ahera/peponi hakuna dini tena
 
Zanzibar ni shida.

Nina mchumba wangu aliwahi fundisha field huko anakuambia shuleni wakija hawafiki saa tisa jioni

Saa Tano washasepa

Ijumaa ndio hawaonekani kabisa.

Class ndio kabisa vilaza wa kutupwa.
Me kule nyumbani watu hawana uchungu kabisa na mambo ya skuli.........uwa natafakari siku tukijitenga na bara sijui nchi tutaiendesha aje
 
Back
Top Bottom