Hatma ya ndoa yangu leo usiku imekuwa hatari kwa maisha yangu

Hatma ya ndoa yangu leo usiku imekuwa hatari kwa maisha yangu

Kupendana kwenu hakuna uhusiano na dini, watu wengi tu wameoana na wanasali dini tofauti. Sema tu changamoto ipo kwa watoto, watafuata dini gani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda kwa kuanza tu niwasalim wote na nawaomba muwe miongoni mwa mtakaookoa nafsi yangu iliyojaa MAUMIVU YASIYO NA KIFANI

NILIANZA KUISHI NA MKE WANGU HUYU 2008 KABLA YA NDOA NA TUKABAHATIKA KUPATA WATOTO WAWILI NA MWAKA 2018 JANUARY TUKAAMUA KUBARIKI NDOA

NA KILICHOKUWA KINACHELEWESHA NDOA ILIKUWA DINI TOFAUTI MIMI NI MKRISTO YEYE NI MWISLAM ILA MWISHO ALIAMUA KUBADILI DINI MWANZONI MWA MWAKA 2009 NA TUKAWA TUNAHUDHURIA IBADA PAMOJA NA WANETU MPAKA January HII NA TUPO MKOA MMOJA LAKINI WILAYA TOFAUTI

POINT YA USHAURI HII HAPA NAOHITAJI KWENU WAUNGWANA
LEO USIKU HUU KANIAMBIA ANARUDIA IMANI YAKE KWA KINA NA ANAHUDHURIA IBADA NA MAADILI YOTE YA IMANI YAKE (Islamic) NA HAKUNA WA KUMRUDISHA NYUMA TENA

ILA PIA ANAKIRI KURUDI KWENYE IMANI YAKE HANA MAANA KWAMBA HANIPENDI ANANIPENDA NA ATAENDELEA KUNIHESHIMU KAMA MUME WAKE NA PIA HATAACHANA NA MIMI LABDA MIMI NITAKAPOAMUA KUMUACHA

NA PIA NAENDELEA KUNIAMBIA AMESHAOMBA TOBA KWA MWENYEZI MUNGU AMSAMEHE MADHAMBI YAKE YOTE ALIYOTENDA KWA KIPINDI CHOTE ALICHIMCHANGANA NABII ISSA NA MUNGU

HAKUCHOKA WALA KUISHIA HAPO ALIENDELEA KUNIAMBIA NIMSAMEHE KWA MAAMUZI HAYO NA MAISHA YAENDELEA KAMA KAWAIDA NA PIA ALIFANYA NDOA KUWEZA KUTURIDHISHA MIMI NA NDUGU ZANGU

JAPO ANASEMA JAMBO HILO ANAAMINI HALIWEZI VUNJA UHUSIANO WETU NA HATA AKIBAKI KATIKA IMANI HII ATAENDELEA KUPRETEND AMBAVYO YEYE HATAKI KUPRITEND NA NILIOGOPA KUKUAMBIA MDA ILA LEO NIMEAMUA KUKUAMBIA TU

NA HAYA YOTE YANATOKEA BAADA YA KUMPELEKA KWENYE SHULE KURISIT MTIHANI WAKE WA KIDATO 4 KATIKA SHULE ZA KISLAM

SASA NAOMBA MNISHAURI NIFANYE NINI KWA KUWA NAONA KAMA MOYO UNATOBOKA SIJAPATA USINGIZI TOKA NILIVYOJARIBU KULALA SAA 2 YA LEO

PILI KIIMANI IKOJE TENA HII NDOA BAADA YA MWENZANGU KUAMUA HIVYO

Je kuna umuhimu wa kuendelea na mipango ya maisha ya pamoja mfano tulikuwa tumenunua viwanja vitatu na kimoja nimeandika jina langu viwili majina ya watoto na pia kiwanja kimojawapo tumeshaanza ujenzi na nilipanga kumalizia nyumba yetu mwezi Wa nne je kuna umuhimu wa kufanya hivyo ??

NB SIKUWEZA KUAMINI YALIYOTOKEA KWA KUWA YEYE ALIBADILI NA KUWA MKISTO BILA KUSHAWISHIWA NA MTU YEYOTE NA KWA KWELI TULIPENDANA NA NAWAPENDA SANA YEYE NA WANANGU
Wewe fala au ni ubaguzi wa dini. Umeoa dini au mwanamke

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Elewa tu mkeo hana msimamo! hata huko mbeleni anaweza kumwambia tuachane kabisa kila mtu aishi maisha yake. Uamuzi utafanya mwenyewe sisi tunakushauri tu[ .QUOTE="UWOGA=UMASKINI, post: 30024278, member: 192780"]Nichukue maamuzi gani mwuungwana nipo na hali mbaya sana hapa[/QUOTE]
!
 
Nakuambia amehudhuria kanisani miaka kumi na kubatizwa kabatizwa sasa nashindwa elewa na nimemwuliza uko serious akaniambia hawazi kurudi nyuma coz amepretendi mda mrefu dini ya kweli in uislam pekee hakuna nyinginee
Hata mashoga wasagaji wazinifu kama wewe na huyo mkeo mulio zini mkapata "illegitimate kids" pia msimlikuwa mnahudhuria kanisa ni nyumba ya matembezi na unafiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakuambia amehudhuria kanisani miaka kumi na kubatizwa kabatizwa sasa nashindwa elewa na nimemwuliza uko serious akaniambia hawazi kurudi nyuma coz amepretendi mda mrefu dini ya kweli in uislam pekee hakuna nyinginee
Huyo alitaka ndoa tu, kaipata. Sasa mwambie unaongeza Mke wa pili, dini yake si inaruhusu????😂🤣😂🤣
 
Mkuu hao watu wanaumiza sana na kuturudisha nyuma ww cha kufanya kaa nae mwelekeze misimamo yako km hataifata ww ndo wa kuamua..Ila najua mapenzi yanauma sana tena sana ila ndo hivo kuna watu wamemvuta masikio huyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo kwa kuendelea kuishi na wewe kama mke na mume hana Uislam kwani Uislam hauruhusu mwanamke wa Kiislam kuolewa na mwanamme yeyote asiye Muislam.

Hivi shule ya Kiislam ni ipi? Mimi nafahamu shule za Kiislam ni madrasa tu Tanzania hii.

Labda uliposema shule ya Kiislam ulimaanisha shule ya Waislam?
Takbiiirii
 
Mkuuu unahangaika na nini mwambie ni sawa umeuelewa msimamo wake kwa vile dini ya kiislam inakubadili mke zaidi ya mmoja mwambie unamletea mke mdogo kulingana na mafundisho ya dini yake kingine mkuu JINGA SANA WEWE MKE HASOMESHWI

Sent from Tapatalk
 
Tatizo lilianzia tangu mlipoanza mahusiano wakati nyote mnatambua kwamba mna imani tofauti, mkaendelea na hadi mkaamua kuzaa na kuoana, mlitegemea nini? Kinachotokea sasa ni matokeo ya makosa mliyoyafanya tangu mwanzoni - kuanza mahusiano bila kutafakari tofauti ya imani zenu. Kuwa kwenye ndoa au mahusiano yoyote ya kimapenzi mkiwa na imani tofauti ni changamoto kubwa sana. Na changamoto hizo zitaendelea kujitokeza zaidi na zaidi kwasababu msingi wa matatizo ni MTAZAMO wako juu ya imani zenu. Utambue kwamba SIO RAHISI kwa mtu aliye na imani yake tangu utoto halafu aje abadilishe imani yake akiwa mtu mzima kwa sababu tu ya kuolewa au kuoa!!! Ni Ngumu sana. Hekima na busara inahitajika ili maisha yaendelee. Huyu ni mkeo tena yaonekana mnapendana na mmeshabarikiwa watoto, haijalishi ana imani gani bado ni yule yule tena amekuahidi kwamba ataendelea kukupenda kama kawaida. Kinachotokea hapa ni kwamba mkeo pamoja na kukupenda anaelemewa na imani yake aliyozaliwa nayo, nafsi inamsuta. Nadhani badala ya kumlaumu au kulalamika muunge mkono, muoneshe kwamba unaelewa ni kwa kiasi gani anapata na anapitia wakati mgumu hadi anababaika kurudi kwenye imani yake. Kama kweli unampenda mkeo, basi heshimu maamuzi yake na endeleeni kujadili kwa hekima na upendo badala kumlaumu kwamba ameingia kwenye imani yako miaka kumi au zaidi..... anahitaji kuungwa mkono na wewe kuliko mwingine yoyote wakati huu. Kwenye mahusiano yenye changamoto za kiimani kama haya unahitaji 'sacrifice' - yaani ukubali kupata hiki na kupoteza kile, hicho kaa chini na utafakari kipi uko tayari kupoteza na kipi hauko tayari kupoteza, na kisha maamuzi yako yajikite kwa mukhtadha huo. Je uko tayari kumpoteza mkeo? Watoto wako? Ndoa yako? Furaha yako? Au Sifa kutoka kwa ndugu na rafiki zako? Tafakari na kisha amua
 
Anarudia mapepo. Ukitaka umkomoe, kila siku sali, piga pambio, ktk Jina la Yesu Kristu kila siku, asubuhi mchana na usiku, lazima atakukimbia kwa sababu mapepo ya hiyo dini yanamfahamu Yesu Kristu, ila inabidi uwe msafi, no pombe, no mchepuko, otherwise utakufa maana mapepo yanajua usafi wa mhusika
Kama ulijua kabla hajabatizwa na kuokoka alikuwa anasumbuliwa na mapepo sana Ila yalikoma soon baada ya yeye mwenyewe kuniambia nimpeleke kanisani
 
hapo umestuck,ila kila jambo Lina namna ya utatuzi wake...utoke kwa reverse ama uvutwe kwa mbele

~chanzo cha yote in ile kumpeleka shule;kama bado anasoma hapo mhamishe tena Mara moja na kwa haraka:hapo analishwa sumu itakayowadhuru nyote

~Sikushauri kamwe muachane,HAWA akina HAWA inabidi kuishi nao kwa maarifa.Dini isikuvuruge,kwanza zimeletwa na meli..

*umemgusia kuachana na akakujibuje
Anadai hataki tuachane na bado ananipenda ila kama Mimi nitaamua
 
Kama ulijua kabla hajabatizwa na kuokoka alikuwa anasumbuliwa na mapepo sana Ila yalikoma soon baada ya yeye mwenyewe kuniambia nimpeleke kanisani
Tuseme amerudi kule kule kwenye mapepo. Aisee pole
 
Mkuu unakuja huku kuomba msaada... Nenda kwa mlezi wako Wa kiroho kamwambie habari hizi yeye ndiye atakayekwambia kama ndoa ipo au haipo....

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaisi mlezi wa kiroho atamwambia nn zaidi ya kumwambia atafute wa dini yake bora atafute mtu mzm mwenye busara viongozi wa dini wote wanafki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom