Hatma ya ndoa yangu leo usiku imekuwa hatari kwa maisha yangu

Hatma ya ndoa yangu leo usiku imekuwa hatari kwa maisha yangu

Nimeshangaa na mimi huku wanamshauri mtu avunje ndoa kisa dini. Aiseee. Kwani mke kuwa imani tofauti na mumewe kitapungua nini kwenye ndoa yao?
Kama ni waroman Catholic ndoa mseto zipo

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu jamaa ni mpuuzi tu kama wapuuzi wengine. Dini haijui wala ukwaju wala misingi yake na kwanini zimeletwa, thats very stupid of him. Huwezi acha mke kisa eti ameamua kuwa muislamu, ni utoto wa kiwango cha juu!
 
Yana ugumu gani ndugu? Infact mimi ndo ningekua wa kwanza kuafiki yeye kurudi kwenye dini ya wazazi wake ili sasa nipate wasaa wa kuchagua tubinti tubichiiii
Kuoa au kuolewa na mtu wa dini tofauti ni mtihani mkuu.
Na mwenzio anapokwambia nimekubali kubadili dini ili tuoane mara nyingi anaigiza tu mwisho wa siku anarudi kule kwao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani waafrika, msiwe wajinga kuendekeza imani za watu wengine....mnachezewa akili tu na kubaguana kisa dini. Angalieni ndugu zenu huko Afrika ya Kati wanavyouana wenyewe kwa wenyewe kisa dini za kuletewa na zisizo na tija yeyote kwetu waafrika. UWOGA=UMASKINI ukiona nafsi yako inakusuta juu ya maamuzi ya mkeo basi muache, achukue 50 zake nawe chukua zako muishi kwa amani!
Yaani ni shida kwelikweli, hivi wanaonshauri wanadhani mkiwa kwenye dini moja ndio hakuna changamoto? Walio wengi tuko kwenye hizi dini “ by default “ kila mmoja anaamini alichorithi kwa wazazi. Inatakiwa kutoka kwenye hili obwe la udini na kuishi kwa kukubaliana na utofauti ambao tunao. Mungu angelitaka angetufanya tuwe na dini moja. We need to embrace diversity and be tolerant to each other. Hapo ndio tutakuwa wamoja. Mbona familia nyingi zina ndugu wakristo na waislamu, je tumeshawahi kutengana kwa ajili ya dini? Mbona tunaishi nao kwa amani kabisa na kushirikiana. Jamaa afikirie mara mbili kabla ya maamuzi.
 
Labda kwa kuanza tu niwasalim wote na nawaomba muwe miongoni mwa mtakaookoa nafsi yangu iliyojaa MAUMIVU YASIYO NA KIFANI

NILIANZA KUISHI NA MKE WANGU HUYU 2008 KABLA YA NDOA NA TUKABAHATIKA KUPATA WATOTO WAWILI NA MWAKA 2018 JANUARY TUKAAMUA KUBARIKI NDOA

NA KILICHOKUWA KINACHELEWESHA NDOA ILIKUWA DINI TOFAUTI MIMI NI MKRISTO YEYE NI MWISLAM ILA MWISHO ALIAMUA KUBADILI DINI MWANZONI MWA MWAKA 2009 NA TUKAWA TUNAHUDHURIA IBADA PAMOJA NA WANETU MPAKA January HII NA TUPO MKOA MMOJA LAKINI WILAYA TOFAUTI

POINT YA USHAURI HII HAPA NAOHITAJI KWENU WAUNGWANA
LEO USIKU HUU KANIAMBIA ANARUDIA IMANI YAKE KWA KINA NA ANAHUDHURIA IBADA NA MAADILI YOTE YA IMANI YAKE (Islamic) NA HAKUNA WA KUMRUDISHA NYUMA TENA

ILA PIA ANAKIRI KURUDI KWENYE IMANI YAKE HANA MAANA KWAMBA HANIPENDI ANANIPENDA NA ATAENDELEA KUNIHESHIMU KAMA MUME WAKE NA PIA HATAACHANA NA MIMI LABDA MIMI NITAKAPOAMUA KUMUACHA

NA PIA NAENDELEA KUNIAMBIA AMESHAOMBA TOBA KWA MWENYEZI MUNGU AMSAMEHE MADHAMBI YAKE YOTE ALIYOTENDA KWA KIPINDI CHOTE ALICHIMCHANGANA NABII ISSA NA MUNGU

HAKUCHOKA WALA KUISHIA HAPO ALIENDELEA KUNIAMBIA NIMSAMEHE KWA MAAMUZI HAYO NA MAISHA YAENDELEA KAMA KAWAIDA NA PIA ALIFANYA NDOA KUWEZA KUTURIDHISHA MIMI NA NDUGU ZANGU

JAPO ANASEMA JAMBO HILO ANAAMINI HALIWEZI VUNJA UHUSIANO WETU NA HATA AKIBAKI KATIKA IMANI HII ATAENDELEA KUPRETEND AMBAVYO YEYE HATAKI KUPRITEND NA NILIOGOPA KUKUAMBIA MDA ILA LEO NIMEAMUA KUKUAMBIA TU

NA HAYA YOTE YANATOKEA BAADA YA KUMPELEKA KWENYE SHULE KURISIT MTIHANI WAKE WA KIDATO 4 KATIKA SHULE ZA KISLAM

SASA NAOMBA MNISHAURI NIFANYE NINI KWA KUWA NAONA KAMA MOYO UNATOBOKA SIJAPATA USINGIZI TOKA NILIVYOJARIBU KULALA SAA 2 YA LEO

PILI KIIMANI IKOJE TENA HII NDOA BAADA YA MWENZANGU KUAMUA HIVYO

Je kuna umuhimu wa kuendelea na mipango ya maisha ya pamoja mfano tulikuwa tumenunua viwanja vitatu na kimoja nimeandika jina langu viwili majina ya watoto na pia kiwanja kimojawapo tumeshaanza ujenzi na nilipanga kumalizia nyumba yetu mwezi Wa nne je kuna umuhimu wa kufanya hivyo ??

NB SIKUWEZA KUAMINI YALIYOTOKEA KWA KUWA YEYE ALIBADILI NA KUWA MKISTO BILA KUSHAWISHIWA NA MTU YEYOTE NA KWA KWELI TULIPENDANA NA NAWAPENDA SANA YEYE NA WANANGU
Wakorintho 7 kuachana ni kwasababu ya uasherati tuuu. Hapo sijui utafanyaje . Maanayake hakuna sababu ya kuachana except uzinzi ktk dini ya kikristo. Kubadili dini kwake ni mtihani kwako especially malezi ya watoto but kuachana biblical ilishakataa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo umezaa nae,kuzaa ni mkataba kama mkataba unavyojua kuna sehemu lazima mukae mujue kulea watoto.Kua nae lakini asije akakubadilisha na imani. Ukimwambia unamuacha kwa imani yake akakubali ujue ana mchumba huko shuleni

Sent using Jamii Forums mobile app
Atakuwa kapata baharia shuleni ana gonga ngozi huku anamuimbia kaswida
 
"Amepretend muda mrefu" inamaana alikudanganya for very long time. Anaweza ku pretend hata anakupenda kumbe yuko kwingine

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ameweza "kupretend" kwenye IMANI ....nini UPENDO .... ndoa eshaipata .... Imani yako haitaki... Na kuna uwezekano pia pendo kwako halipo.... Hakuna namna endelea kujifunika tu shuka moja na nyoka....
 
Elewa tu mkeo hana msimamo! hata huko mbeleni anaweza kumwambia tuachane kabisa kila mtu aishi maisha yake. Uamuzi utafanya mwenyewe sisi tunakushauri tu[ .QUOTE="UWOGA=UMASKINI, post: 30024278, member: 192780"]Nichukue maamuzi gani mwuungwana nipo na hali mbaya sana hapa[/QUOTE]
Nimeshangaa na mimi huku wanamshauri mtu avunje ndoa kisa dini. Aiseee. Kwani mke kuwa imani tofauti na mumewe kitapungua nini kwenye ndoa yao?
Kama ni waroman Catholic ndoa mseto zipo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkewe hana msimamo tatizo siyo hizo dini zao.
 
Elewa tu mkeo hana msimamo! hata huko mbeleni anaweza kumwambia tuachane kabisa kila mtu aishi maisha yake. Uamuzi utafanya mwenyewe sisi tunakushauri tu[ .QUOTE="UWOGA=UMASKINI, post: 30024278, member: 192780"]Nichukue maamuzi gani mwuungwana nipo na hali mbaya sana hapa
Mkewe hana msimamo tatizo siyo hizo dini zao.[/QUOTE]Msimamo upi? Aendelee kuabudu kwenye dini ambayo hana imani nayo? Na kasema alikubali kubadili dini Ili aolewe (aridhishe mume na ndugu zake)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani tatizo limetokea baada ya wewe kumpeleka kuristi mtihani katika shule ya Kiislam! Kule huenda amelishwa maneno na kupandikiziwa roho nyingine.
Lakini hata hivyo usimwache ni mkeo huyo.Dini siyo sababu ya kuvunja ndoa,kwani kila mtu atahukumiwa pekee yake siku ile ya mwisho.
 
mwanamke wa Kiislam kuolewa na mwanamme yeyote asiye Muislam
Hili swali liliwahi kuulinzwa kwenye muhadhara wa kiislamu, jibu likawa ndio Inawezekana kwa masharti huyo mwanaume asikuzuie kuabudu au kufata ibada zako, pia niliwahi kumuulizia Ostadhi wangu wa Madrasa akanijibu inawezekana 🤔🤔.
 
Nichukue maamuzi gani mwuungwana nipo na hali mbaya sana hapa
Endeleen na maisha mkuu unatakaiwa kuachana na mwanamke pale unapojua hakupendi tu ana haki ya kurudi kwenye imani inayomuweka huru kuliko kila siku afikirie kuwa anamkosea Mungu wake kwa ajiri yako wewe nawatakia maisha mema hakuna haja ya kuachana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama wewe kweli ni Mkristo tafakari maneno haya kutoka 1 Kor 7 : 1-16

Maagizo kuhusu Ndoa
1Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.

2Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.

3Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

4Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

5Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

6Lakini nasema hayo, kwa kutoa idhini yangu, si kwa amri.

7Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi.

8Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo.

9Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.

10 Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe;

11lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.

12Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.

13Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.


15Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.

16Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?
Nadhani kupitia mistari hii haitaji ushauri zaidi..
Mkuu usimwache mkeo.Nilitaka kusingizia dini yako lakini naona pia imekuruhusu.Endelea kumpenda mkeo na wanao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
...Muogope sana,mwanamke yoyote aliyetayar kubadili dini eti kwa ajili ya ndoa na si kwamapenzi.yke mwenyew,atakuyumbisha sana hasa ukiwa mwanaume unaamn dini yko ndio sahihi.

Ktk imani ytu ya kiislam kigezo kkubwa na cha kwanza ktk kuoa au kuolewa ni dini kwanza mamb mengne ndo yanafuata,ukikosea kwny dn umeumia.
 
Back
Top Bottom