Hawa ni watu maarufu duniani ambao viatu vyao vimekosa mvaaji

Hawa ni watu maarufu duniani ambao viatu vyao vimekosa mvaaji

Za asubuhi wakuu, leo nakuja na makala ya watu maarufu duniani, ambao wameacha alama kubwa katika tasnia zao na mpaka leo hakuna alietokea kuziba mapengo yao.

1) Mohammedi Ali
Huyu ni bingwa, mbabe na mtemi wa masumbwi ulimwenguni kote. Mohammed Ali ambae alizaliwa 17 January 1942, huko Louisville, Kentucky Marekani na kufariki 3 June 2016, huko Scottsdale, Arizona Marekani. Alikuwa ni bondia wa pekee kuufanya mchezo huo uwe na wapenzi na waangaliaji wengi ulimwenguni.

Licha ya kwamba mchezo huo ulikuwepo maelfu ya miaka kabla ya ujio wake Ali, lkn ni yeye ndio aliefanya watu waanze kuupenda zaidi mchezo huo na kuchukua nafasi ya pili kwa kupendwa duniani baada ya mchezo wa mpira wa miguu. Ali ambae alikuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki ulingo, kukwepa ngumi, na mwepesi wa kupiga ngumi za haraka haraka. Lakini pia alikuwa na mbinu nyingi za kuweza kumchosha na kummaliza kbs mpinzani wake wakati wowote alioutaka yeye ulingoni.

Ali alikuwa na uwezo wa kumsogezea mpinzani sura, lkn utashangaa hadi round nzima inaisha bila mpinzan wake kufanikiwa kumpiga ngumi hata 1 tu usoni (kama tuonavyo pichani) sometimes unakuta mpinzani wake anarusha ngumi (kota) na kuanguka mwenyewe, huku Ali akimtizama kwa dharau [emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787]

Pamoja na yote lkn kama ilivyo michezo mingine na yey kuna muda alikuwa anapoteza baadhi ya mapambano pia, aidha kwa kutokana na mchoko wa mazoezi makali anayokuwa amefanya kabla ya pambano nk. Toka Ali alipostaafu ngumi mpaka kifo chake, hakuna bondia ambae ashawahi kufikia rekodi ya upiganaji wake na vituko vyake awapo ulingoni na nje ya ulingo.

Mabondia wengi kama kina Mike Tyson, Evander, Lenox Lewis na wengineo walikuwa wanakwenda kumuona na kupata mbinu mbali mbali za kupigana ulingoni kupitia mfalme huyo wa ngumi ulimwenguni. Huyu ndio Mohammed Ali alieacha alama kubwa ktk mchezo huo maarufu wa ngumi duniani. Hakuna na hatotokea Mohammed Ali mungine, Never.
Mungu ailaze roho ya huyu Legend mahali pema peponi.

View attachment 2335340

2) Bob Marley
Bob Marley alizaliwa 6 Feb 1945, huko Nine Mile, Jamaica, na kufariki 11 May 1981, huko Florida Marekani.

Alipozaliwa aliukuta mzikiwa reggae ukiwa ulimwenguni miaka na miaka. Lkn kwa kipaji chake na uwezo wake akaanza kuleta mabadiliko makubwa katika mziki huo, hadi kufikia hatua ya kusikilizwa na viongozi wakubwa wa nchi mbali mbali. Japo kulikuwa na waimbaji wengine wakubwa kama kina Peter Tosh, Burn Spear nk, lkn ni yeye Bob Marley ndio aliefanya reggae ipendwe na walio wengi. Hadi anakufa Bob Marley aliacha muziki huo ukiwa na mamilioni ya wasikilizaji ulimwenguni.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

View attachment 2335341

3) Bruce Lee
Bruce Lee alizaliwa 27 Nov 1940, huko San Francisco, California Marekani na kufariki 20 July 1973 huko Kow loon Tong, Hong Kong.

Bruce alizaliwa na kuukuta mchezo wa kung fu au karate ulimwenguni. Lakini kwa kipaji alichozaliwa nacho, alianza kuleta mabadiliko makubwa kwenye mchezo huo hadi kushawishi mamilioni ya watu ulimwenguni kuupenda na kuanza kuufuatilia mchezo huu. Bruce alikuwa na uwezo mkubwa wa kucheza na hisia za adui na kujua ni wapi atapopiga lazima adui atakaa tu hata awe na mwili kama jumba.

Ikafika kipindi watu wakamshauri ajiunge kwenye tasnia ya uigizaji ili kuwavutia watu zaidi kuupenda mchezo huo, lkn pia kujifunza baadhi ya mbinu za upambanaji kupitia movie zake. Mpaka toka Bruce afariki mpaka leo bado anapewa heshima kubwa na magwiji wa mchezo huo wakiwemo wacheza sinema kama vile Jackie Chan, Jet Lee nk. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

View attachment 2335338

Wanaofuatia ni [emoji116]
4) Michael Jackson king wa Pop na mitelezo.

5) 2pac Shakur king wa Hip hop aliekuwa haiogopi serikali ktk kuwatetea wamarekani weusi wenzake na jamii nyingine zilizobaguliwa nchini Marekani, pia alipambana sana na polisi kuhusu unyanyasaji wowote uliofanywa na jeshi hilo kwa vijana mbali mbali hadi alipouwawa. Aliwahi kuwa na kesi ya kuwashambulia polisi wawili na bunduki, baada ya 2pac kupita sehem na gari aliwakuta polisi wakiwa wamemfunga pingu mtu mweusi huku wanampiga, kitendo kile kilimuuzi 2pac ndipo alipoamua kutoa bastola yake na kuwashambulia polisi, japo baadae polisi wale waliwahishwa hospital na kupona.
Katika kesi ile 2pac hakuhukumiwa baada ya kuonekana kuwa wale polisi walikuwa na makosa ya kiutendaji kwa mtuhumiwa waliekuwa wamemkamata.
Mungu awalaze roho zao mahali pema peponi.

6) Michael Jordan
Mzee wa kudumbukiza kikapuni. Huyu alikuwa na uwezo wa kuruka juu zaidi na kuonekana kama ameganda kwa sekunde kadhaa hewani kabla ya kutia mpira kapuni na kushuka chini. Toka astaafu bado hajapatikana Jordan mungine, japo bwana mdogo hayati Kobe Bryant alijitahidi kwa namna fulan, lkn bado hakufikia kule alipofikia mzee wa kazi.

View attachment 2335342

Hawa ni baadhi ya watu ambae mpaka leo viatu vyao viko wazi, havijapata wa kuvivaa vikawatosha.
Ndugu, Bob Marley ni level tofauti sana na hawa,ukivuta kumbukizi na kufatilia hata kama ni binadamu kama hawa lakini yeye alikua na kitu special zaidi, elewa ya kwamba Peter Tosh alikua mwamba wake sana ktk tunzi za muziki lakini Marley alitunukiwa kivingine kuleta ushawishi duniani

Ukimuondoa Yesu na Mohammed ni huyu Bob Marley anayefuata kwa kua na watu wengi zaidi duniani kama wafuasi na wwaliofatilia maisha yake, toka amefariki 1981,kuanzia hapo mpaka leo kaburi lake na makao yake ni eneo linalotembelewa na tu karibu kila siku ama kila wiki toka kipindi hicho mpaka leo hii

Hii inamfanya kua tofauti na hawa kina Alli, maana kidogo kidogo wanaanza kupotea lakini si Bob,fatilia utajua
 
Aliyevaa viatu vya Mohammedi Ali ni IRON MIKE TYSON


Aliyevaa viatu vya Bob Marley ni LEGEND LUCKY DUBE
Kwa umaarufu sawa. Kwa uwezo Tyson yuko overrated sana.

Kumfananisha Bob Marley na Lucky Dube ni sawa na kumfananisha Prince na Trey Songz.
 
Soma vizuri mkuu. Mohammed Ali nimemzungumzia kwa upande wake wa ngumi (boxer)
Bruce Lee nimemuweka kwenye kung fu au karate na..
Bob Marley amesimama kweny mziki wake mkuu.
Huyu alisoma kweli uzi kule juu????jaman jamani
 
Wewe jamaa acha kuongea bila takwimu mwenye ngumi hamna anayemfikia Mike tyson kaangalie talwimu zake na uwaaulize wataalamu katika hiyo fani.inawezekana kabisa Mohammed Ally anapenda lakini hamzidi Tyson katika fani.
Mkuu unaota ndoto za mchana. Tafuta rekodi zao, angalia kila mmoja alipigana na nani ndio uwafananishe.
 
Mkuu nakufananisha na The Icebreaker alietaka kusema kuwa Messi ndio awe king wa soka wa miaka yote.
Na wakati fact zinatamka kuwa king wa soka wa miaka yote ni mzee Pele.

Sasa na ww kama unataka kumjua king wa muda wote wa ngumi angalia hapo pichani.
Google sio reliable source,google ni search engine,hata wewe unaweza ukaandika chochote na kupost google.
 
Alejandro Pele wa Brazil naye Ni level nyingine kbsa.Naamini mpaka Dunia inaisha Hakuna mchezaji wa Sola atakaye kuja kufikia viwango vya Pele.

Duru zinasema katika kipindi chake Cha uchezaji jamaa alifunga mabao zaidi ya 1,500
 
Uzi wako umekosa maana kwa kukosa jina la mfalme wa Pop, Michael Jackson hapo ndipo ulichemka. Tena alitakiwa kuwa namba moja hapo. Hawa umewataja kuna watu wameweka rekodi za kuwafunika.

Mfano, Mohamed ali ukimuweka na Tyson, hivi nani katika ujana wake ameweka rekodi kali?!

Bruce lee ni mkali wa karate moves miaka hiyo ila ukitazama kuna mtu kama Don Yen,Jet Lee, ana moves kali balaa brucelee anasubiri.

Bob Marley raggae yake siwezi kusemea maana ni ya tofauti na reggae za sasa sababu yake ilikuwa politically motivated. Wenzake ni kama akina 2pac kwenye hip-hop hakuna wa kumlinganisha nae tokana na mistari yake na style ya delivery. So kwa bob Marley nitakupa pass.

Michael Jordan pia ukitazama League ya NBA kuna madogo wanapiga kikapu hadi unaogopa yeye mwenyewe Jordan ana appreciate uwezo wao na kukiri angekuwapo kwenye court miaka hii angetolewa jasho.

Ila nionyeshe msanii anayeweza match legacy ya Michael Jackson hadi leo hii tokea jamaa amefariki au hata alipokuwa hai! Huyo mtu hayupo.

Ntafutie mtu anayeweza kufunika legacy ya 2pac kwenye hip-hop?

Nitafutie mtu wa kufunika legacy ya Anold Schwarzenegger kwenye cyborg figure?

Nani anamfunika Kenny G katika uimbaji kwa kutumia tarumbeta?!




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Michael Tyson anaheshima yake ktk ngumi, lkn hawezi kufikia viwango vya Mohammed Ali mkuu. Ikumbukwe hata Tyson mwenyew ana mengi aliyojifunza kutoka kwa mtemi huyo wa ngumi ulimwenguni.
Sasa nikimuweka na Tyson itakuwa tasnia moja ina king wawili kitu ambacho kitasnia hakiwezekani mkuu.
So unataka kutuaminisha kuwa Mohammed Ali alikuwa anashinda mapambano yake ndani ya dakika 1,2 au 3?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu, Bob Marley ni level tofauti sana na hawa,ukivuta kumbukizi na kufatilia hata kama ni binadamu kama hawa lakini yeye alikua na kitu special zaidi, elewa ya kwamba Peter Tosh alikua mwamba wake sana ktk tunzi za muziki lakini Marley alitunukiwa kivingine kuleta ushawishi duniani

Ukimuondoa Yesu na Mohammed ni huyu Bob Marley anayefuata kwa kua na watu wengi zaidi duniani kama wafuasi na wwaliofatilia maisha yake, toka amefariki 1981,kuanzia hapo mpaka leo kaburi lake na makao yake ni eneo linalotembelewa na tu karibu kila siku ama kila wiki toka kipindi hicho mpaka leo hii

Hii inamfanya kua tofauti na hawa kina Alli, maana kidogo kidogo wanaanza kupotea lakini si Bob,fatilia utajua
Mkuu nakubaliana na ww kwamb Bob Marley ana heshima kubwa sana ukimlinganisha na hao wengine.
Lkn post yang haikuwa ya kumlinganisha na hao ma legendary wengine, bali ilikuwa inazungumzia wasanii na wanamichezo mbali mbali walioacha alama kubwa ktk tasnia zao, ndio nikagawa makundi kwa upande wa mziki na makundi kwa upande wa michezo.
Mfano kwenye michezo nimeweka makundi ma3 na wafalme wao hapo chini 👇
1) Boxer au masumbwi- Mohammad Ali.
2) Kung Fu au karate- Bruce Lee.
3)Basket ball- Michael Jordan.

Kwa upande wa mziki nimeweka makundi ma3 na wafalme wao hapo chini 👇
1) Reggae- Bob Marley.
2) Pop music- Michael Jackson.
3) Rap& Hip hop- 2Pac Shakur.

Nafikiri hapo utakuwa umeelewa mkuu!
 
So unataka kutuaminisha kuwa Mohammed Ali alikuwa anashinda mapambano yake ndani ya dakika 1,2 au 3?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu haya mambo nimeshayatolea ufafanuzi kwa baadhi ya post huko juu.
Iwe mpira, masumbwi, mziki nk tayari kuna wale ambao washapewa heshima ya ufalme na wahusika wa hiyo michezo. Haijalishi hawa vijana wa sasa au baadae wanaweza kufikia au kuzidisha rekord za hawa ma legends au not. Soma post namb 34 na 36 mkuu naambatanisha na picha hapo chini.

Kama chama cha ndondi duniani kimeamua kuwa Mohammad Ali ndio mfalme wa masumbwi wa miaka yote, mimi na ww ni kina nani mpaka tupingane na wajuzi hao.
Si waliwaona kina Lewis, Tyson na wengine wengi waliokuwepo kabla na baada ya Mohammad Ali?
 

Attachments

  • Screenshot_20220826-172228.jpg
    Screenshot_20220826-172228.jpg
    40.1 KB · Views: 18
  • Screenshot_20220826-160611.jpg
    Screenshot_20220826-160611.jpg
    36.6 KB · Views: 16
  • Screenshot_20220826-193449.jpg
    Screenshot_20220826-193449.jpg
    49.7 KB · Views: 15
1) Mohammad Ali
2) Bob Marley
3) Bruce Lee
4) Michael Jordan
5) Michael Jackson
6) 2pac Shakur
The Greatest of All Time- GOAT

Tukija Tanzania tuna hawa chini:
1) Julius Nyerere - Uhuru wa nchi yetu.
2) Marijani Rajabu - mziki
3) Madaraka Selemani - soka
4) Malkia Khadija Kopa - taarab
Hii list yako pia ni swadakta kabisa mkuu.
 
Ukimwacha magufuli sijakuelewa
Mkuu hawa niliowaandika hapo juu ni wasanii na wanamichezo tu.
Kwahiyo hata ukimuongeza sio mbaya, lkn nahisi Magufuli yeye alivaa viatu vya baba yetu wa taifa mw Nyerere.
 
Back
Top Bottom