Hawa ni watu waliomdhihaki Mungu na kupatwa na shida

Hawa ni watu waliomdhihaki Mungu na kupatwa na shida

Mtoa mada ndio unaofanya Mungu aonekane wa hovyo Mungu wetu hajui ubaya sasa haya yanatokea wapi huyo ni Mungu au shetani?
 


TAFSIRI YANGU ISIYO RASMI YA SIMULIZI HII KWA AJILI YA KUJIFUNZA

Kila dini inafundisha waamini wake kushika na kutii sheria zake..

Mungu anatuzuia kabisa binadamu kutilia shaka nguvu na mamlaka yake. Haijalishi mtu ni maarufu kiasi gani, tajiri kiasi gani au amefanikiwa kiasi gani, haya yote hayampi mtu yeyote kibali cha hata kudhania tu kuwa yuko au anaweza kuwa juu ya Mungu..

Katika Biblia, Mungu alimwadhibu mfalme Nebukadneza aliyejiinua na kujiona kuwa yeye ni Mungu kiasi cha kuamuru watu aliokuwa anaowaongoza wamwabudu yeye..

Ifuatayo ni orodha ya matukio maarufu ya watu duniani waliojaribu kufanya dhihaka dhidi ya Mungu kwa nia ya kushusha hadhi, nguvu na mamlaka yake, kilichowatokea ni historia ya kutufundisha sisi..

Hata hivyo, ikumbukwe kubwa, sisi wanadamu tunaweza kuja na nadharia tu, lakini ni Mungu yeye pekee yake ndiye ajuaye sababu halisi za kifo cha mtu...

1. TANCREDO NEVES.
Huyu alikuwa ni Rais wa Brazil.

Ilikuwa ni wakati wa kampeni za uchaguzi wa Urais na alidhihaki kwa kusema kuwa, iwapo angepata kura 500,000 toka chama chake na kushinda Urais, basi hata Mungu mwenyewe hataweza kumtoa katika Urais wake..!

Hakika alipata kura zote alizotaka na kushinda Urais. Bahati mbaya, aliugua vibaya na baadaye kufariki siku chache kabla ya kuapishwa...!

2. JOHN LENNON.
Huyu alikuwa mwanamziki wa kundi la muziki maarufu la Beatles miaka ya 1960s na 1970s

Lennon na wenzake katika kundi lao kina Paul McCartney, George Harrison na Ringo Star ⭐⭐ waliandika mamia ya nyimbo zilizopendwa na kuwapa umaarufu sana miaka hiyo..

Ikatokea siku moja na wakati fulani mwaka 1966 Lennon akihojiwa na jarida maarufu la Marekani alisema maneno haya;

"...ukristo utafika mwisho na utatoweka. Siwezi kujadili kuhusu hili hata kidogo kwa sababu nina uhakika na ninchosema..

Aliendelea kusema;

"...Yesu Kristo alikuwa mkamilifu. Lakini wafuasi wake walikuwa ni watu wa kawaida na rahisi tu. Leo hii, sisi BEATLES ni maarufu zaidi kuliko yeye (yaani Yesu Kristo)..."

Desemba 8, 1968 John Lennon alimiminiwa mvua ya risasi 6 kichwani na mpenzi wa mziki wake mbele ya nyumba yake na kufa hapohapo..!

3. CASUZA..
Huyu alikuwa Mbrazil mwenye jinsia mbili (bisexual), mwandishi wa nyimbo, mwimbaji na mshairi maarufu na mbobezi..

Ilitokea wakati mmoja wakati wa shoo yake huko Caneiro [Rio de Janeiro] akiwa stejini akivuta sigara yake, alibunda pafu ya moshi wa sigara hiyo na kuuachia juu angani huku akitamka maneno haya;

"...Mungu, hiyo ni kwa ajili yako...!"

Casuza alikufa katika umri wa miaka 32 tu kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ktk namna ya kutisha sana..

4. THOMAS ANDREWS..
Huyu ndiye mjenzi wa meli maarufu ya TITANIC iliyozama miaka kadha iliyopita nyuma...

Mara baada ya kumaliza kazi ya ujenzi wa meli hiyo, akihojiwa na ripota mmoja wa habari aliyemuuliza ni kwa kiwango gani anaamini meli ya TITANIC itakuwa salama..?

Katika namna ya dhihaka, alijibu swali hili la mwandishi kwa maneno haya;

"...Hata Mungu mwenyewe hawezi kuizamisha meli hiyo...!"

Hatima ya meli ya TITANIC wowote tunaijua...

5. MARYLYN MONROE
Huyu ni mwanamama tajiri na mwenye umaarufu mkuu ndani ya Hollywood nyakati hizo..

Mama huyu [celebrity] alikuwa na maisha kamilifu yanye utoshelevu kimwili ambayo kila mtu huota na kutamani kuyaishi..

Siku moja katika moja ya shoo zake, alitembelewa na mhubiri maarufu wa Injili, Billy Graham..

Billy Graham akamwambia Monroe kuwa, Roho wa Mungu amemtuma aje kwake ili amwambie habari njema za wokovu wa Yesu Kristo..

Hiki ndicho alichojibu Marylyn Monroe;

"...Simhitaji Yesu wako....!"

Wiki moja badaye alikutwa amekufa katika nyumba yake..

6. TUKIO LA CAMPINAS - BRAZIL MWAKA 2005
Kundi la marafiki huko Campinas, Brazil walikuwa wanakunywa na kulewa huku wakiendesha gari...

Wakaendesha gari lao hadi nyumbani kwa rafiki yao wa kike ili kumpitia waende walikokuwa wanataka kwenda...

Huyu rafiki (binti) alitoka ndani akisindikizwa na mama yake na kuelekea kwenye gari la rafiki zake...

Mama yake binti, aliingiwa na mashaka na wasiwasi baada ya kuwaona rafiki za binti yake wakiwa ktk hali ya kulewa chakari..

Akamshika mkono binti yake mkono ambaye tayari alishakaa kwenye kiti cha gari na kumwambia;

"...Binti yangu, tembea na Mungu na akulinde uwe salama..."

Sikiliza alichojibu binti;

"...Iwapo tu Mungu huyo atasafiri ndani ya sanduku, kwa sababu kama unavyoona ndani ya gari yetu, tumeshajaa...!"

Kama saa moja hivi baadaye, taarifa zikaenea kuwa, gari yao imepata ajali mbaya sana kiasi cha hata mtu asiweze kuitambua ni gari aina gani hilo kwa jinsi ambavyo lilivyokuwa limeharibika nyang'a nyang'a..

Wote waliokuwamo ndani ya gari ile walikufa palepale...!

Cha ajabu, ndani ya gari hilo nyuma kwenye buti, kulikuwa na sanduku (trunk) na ndani ya sanduku hilo kulikuwa na tray ya mayai ikiwa nzima bila hata na yai moja kuvunjika licha ya gari ile kuharibika nyang'a nyang'a..!

Polisi walishangaa sana kiasi cha kukiri kuwa, jambo hilo kwa hivihivi tu haliwezekani unless kuwe na nguvu fulani ya ziada iliyofanya mayai hayo yasivunjike..!

7. CHRISTINE HEWITT
Huyu alikuwa ni mwandishi wa habari, mburudishaji [entertainer] Mjamaika ambaye aliwahi kutamka maneno haya kuhusu Biblia - Kitabu cha Neno la Uzima kinachotumiwa na wakristo;

"...Biblia ndicho kitabu cha hovyo kabisa kilichiwahi kuandikwa...!"

Muda mchache baada ya marashi haya, Christine Hewitt aliokotwa akiwa amekufa kwa kuungua vibaya kiasi cha kutotambulikana kabisa akiwa ndani ya gari yake..!

NB: Binadamu hutumia nadharia zaidi juu ya kifo au matukio mabaya yawapatayo wanadamu. Lakini katika yote iwe kifo au tukio lolote lisilo pendeza, Mungu anabaki kuwa ndiye ajuaye sababu halisi ya kila jambo..

Asomaye na ajifunze..
 
Wasiomdhihaki Mungu hawafi?

Hawapati shida?
 
1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)
Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966. Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)
Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)
Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute" Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.

4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC
Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata Mungu hawezi kuizamisha" Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)
Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya "Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'. Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.

6.
Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa mtoto wake.
Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye boneti la gari". Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa. Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika.

7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)
Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia" Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)
Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simuhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu
hakuna kama Mungu.

Follow me on twiiter as LegalGentleman
Ungemalizia tu;
MAGUFULI JOHN POMBE
Aliitwa "mungu" na wahuni halafu yeye akanyamaza tu.Mwishowe akafa kibudu.
 
Kama Mungu yupo kweli hata kama ukimkebehi, ataona akili yako ni ndogo sana kwake na kukusamehe. Mungu halipizi. Waliosulubiwa huenda tu walikosea masharti katika ulimwengu wa roho.
 
Nakupa list ya wachungaji na masheikh ambao hawakumdhihaki Mungu na walipata shida na kufariki

1. TB JOSHUA
2. MAMA LWAKATALE
3. STEPHEN AKNOLA
4. ISSA TURAY
5. WILSON BADEJO

Sheikh nooren mohammed hakumdhihaki Mungu lakini alikufa kwa ajali mbaya sana.

Sheikh Saeed bin nahynan huyu kafa siku nne zilizopita naye kwa ajali mbaya sana na hakumdhihaki Allah

Rashid bin Mohammed naye alikufa kwa shambulio la moyo na hakuwahi mdhihaki Mungu.

Na sio tu hao wapo wengi sana wamekufa na wengine wakipata shida pasipo hata kumdhihaki Mungu.

Kinachokufanya uone hao watu uliowataja kua wamepatwa na shida kutokana na wao kumdhihaki Mungu ni kipi? Nani asiyepata tabu hapa ulimwenguni?

Huyo Mungu wako historia ya dini inaonesha yeye ndio alikua muanzilishi wa kupata tabu baada ya vita yake na shetani ambapo shetani alizua utata huko juu mpaka akafanikisha kusepa na robo tatu ya malaika unafikiri tabu aliyoipata huyo Mungu ilikua ndogo?

Kwa hiyo nayeye tuseme alimdhihaki nani mpaka ikamfika hiyo tabu?
Mama Lwakatre siyo, full stop. TB Joshua alisema nitakufa kabla ya birthday, baada ya muumini wake mmoja kumtakia HBD wiki mbili kabla na siku hiyo ndiyo aliyotabiri vita Urusi na kutengwa kwa Putin. Fuatilia vitu vizuri na ujue undani wa mtu kabla ya ku-judge kuwa yuko hivi au vile.
 
Unaamini unachoamini au umethibitisha?

Unaelewa kuwa kuamini si kuthibitisha?
Unataka Mungu awe kama wewe unavyotaka ndo ujue yupo ?unavyoonekana kuna kitu ulikua unamtegemea kikaenda tofauti ndo maana una vita nae .
 
Unataka Mungu awe kama wewe unavyotaka ndo ujue yupo ?unavyoonekana kuna kitu ulikua unamtegemea kikaenda tofauti ndo maana una vita nae .
Hapana,

Mungu mwenyewe dhana ya kuwepo kwake ina contradiction, kabla hata mimi sijazaliwa.

Na itaendelea kuwa hivyo. Hata baada ya mimi kufa.

Kwa sababu huyo Mungu hayupo.Katungwa na kuungwaungwa na watu tu, tena zama za ujinga ambako watu hawakuona hizo contradictions.

This has nothing to do with me.

Mimi ningekuwa mtu wa kuangalia nilichotegemea ili kuamini Mungu, nilitakiwa kumkubali sana Mungu.

Kwa sababu nimefanikiwa kuliko nilivyotegemea katika maisha haya.

Yani nimefanikiwa mpaka nimefikia kiwango cha kufikiria kuwafanikisha wengine tu kama changamoto yangu iliyobakia.
 
Kwani wasiomdhihaki Mungu hawapati shida?
Kamwe hawapatwi na shida!!! Mara nyingi kuliko zote wanatwaliwa tu!! km Musa hakuna kaburi lake hapa Duniani, alipanda Mlimani hakurudi ni wazi alitwaliwa!!

TB Joshua alilala hakuamka tena, hakuwa na tatizo kiafya NI wazi alitwaliwa na Mungu yule!! yeye Mungu hajaribiwi!

ktk Kiti cha enzi kuna wazee 24!! pale basi jua kuwa Joshua, Kareb na Musa ni miongoni mwao!!! inawezekana labda idadi iongezeke kwa siku hizi tulizo nazo lkn ndo ivo!!...uzima wa milele upo live!

ukimuamini unapata uzima wa milele! usipo muamini unakuwa km jiwe!
 
Aliyekuloga amekufa.Tutapata shida sana kukuagua kwa mitishamba.
Achana nae huyo Mzee hana jipya anaona ignore List ndo kitu cha maana!! hasa akisha shindwa hoja!!! hajui kwamba hata shetani alimuhasi Mungu lkn bado anaishi!

hilo zee bana likionaga hoja za nguvu linatishia ignore List!! na ma-bombastik yake ya kigiriki!! hajui kuwa anajiambia ma linguistic hawakufundishwa ivo!! wanaongea kitu kinachoeleweka kwa audience waziii!

kila mtu akiongea ma-bombastik words humu ujumbe hautafika! na hayo hayaishagi nilikuwaga naona hayo kwa wale waalimu vihiyo! wanaogopa maswali km Jamaa moja hivi aliitwa Dr Majaa!

huyo jamaa alitutesa sana tukiwa bado madenti na kiingereza chake cha kulazimisha kile .... huyo mzee muongo hata hajafanikiwa km mimi anajishaua tu!!...amepeleka misaada mingapi home kwani bana!! angalia...

Mimi nimejenga ward ya Ebola palee Hospital ya Temeke karibu na soko la wailes na vifaa vyote mle ndani nimetoa nje ya nchi na nikalipia kodi cash! japo TRA walisema nisilipe!

ile ni hela yangu tu pekee! na pameandikwa jina langu!! nendeni mkajiridhishe km haitoshi kila mwaka napeleka containers za Madawa Hospital teule ya wilaya Mugumu!

Sirari mpakani pale ule mjengo mweupe ni mimi nimeujenga na jiwe! Binafsi nayasema haya!! siyo kwa kujisheua kujidai/kuringa/ kujiskia nooo, ila nataka Diasporas wotee wenye viherehere vya bure humu mnajijua, mfikirie na

mpate uchungu wa kuchangia nchini kwao kadri Mungu anavyo wabariki... angalia sasa tunakuja kivingine!...Palee kirumi pale tumepewa Hekali kumi na kijiji ajili ya;

kutengeneza stop over five star Motel / na standby Air Emegency ambulances en' Classic Refferal Hospital....

hii ni kwa ajili ya wenyeji wa pale na watalii/safiri wooote wanao kwenda/ ingia Tanzania kutokea Kenya! na kupokea watalii wale woote wanao ingia serengeti kuelekea Kilimanjaro.

hata wale watalii wanao katiza safari zao ghafla ajili ya sababu mbali mbali!

kama vile; kuitwa kazini ghafla nchini mwao! kifo cha ghafla popote, ugonjwa, uchovu, Biashara, kuto taka /kujisikia tu kuendele na safari za kitalii, Mashaka binafsi. ujauzito, uzee nk!.... kwa sasa tumefikia pazuri!

Kifupi ni Destination ambayo ukifika pale kwa mtu yeyote unaweza kaa na kujisikia uko nyumbani na unapata kila aina ya huduma kikubwa ikiwa ni huduma ya afya! chakula na Malazi. na kwenda kokote unako taka!

Kwa mfano ukitaka kurudi nyumbani Ulaya faster tu unapanda ndege zetu dakika sifuri uko Kilimanjaro/Nyerere/jomo kenyata air port! km haitoshi tuna connection na Oliver Tambo I.A, Maseru one I.A!nk!

Na hizi ni tuna fanya gharama nafuu tu ili hata kwa wenyeji wapate huduma zinazo kidhi haja!
 
Back
Top Bottom