Pre GE2025 Hawa ‘Wakimbizi walioteuliwa kwenye nafasi za maamuzi’ ni kina nani?

Pre GE2025 Hawa ‘Wakimbizi walioteuliwa kwenye nafasi za maamuzi’ ni kina nani?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa mujibu wa mkuu wa majeshi Gen Jacob John Mkunda amemueleza Rais kuwa Kuna wakimbizi wapo Hadi Serikalini na wamepewa nafsi za juu kabisa za kimaamuzi

Hili inashangza na kufikirisha Sana inakuwaje Hadi mkuu wa majeshi anawajua wakimbizi na wameteuliwa na wala hajawasiliana na mamlaka za uteuzi kuzuia uteuzi wao yeye amekaa kimya Hadi leo ndio Kuja kumueleza Rais by suprise.

Mimi najiuliza hivi Rais leo atapata usingizi Kweli? Atakuwa anajiuliza ni Nani huyu nimemteua ambae Ni mkimbizi ?

Lazima Rais atapitia mafail yake kwa upya mnk kwa taarifa ya leo wa kamanda wake CDF kusema wasiwasi kuwa unawateua hadi wakimbizi inamaana kwamba wasaidizi wake wanamuingiza Chaka.

Anyway Kama Kuna kiongozi au afsa tunamuhisi siyo mtanzania mwenzetu Basi tumtaje hapa hajui kuwa siyo mwenzetu.





Pitieni huu uzi
Hiyo nchi kwa taarifa yako inaongozwa kutokea nje siku nyingi na sio kuanzia kwa uongoz huu tu. Sisi ni nyuki wa mashine hatuna madhara.
 
Asalaam aleykum wana Jf.
Leo Mkuu wa Majeshi, General Mkunda amegusia kuwa kuna baadhi ya wakimbizi wameshikilia nafasi nyeti serikalini kulingana na taarifa za kiintelijensia.
Sasa lengo la uzi huu ni kuwarahisishia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ili kuwabaini wakimbizi wote ambao wameteuliwa kwenye nafasi za maamuzi.

Hii itasaidia kudumisha ulinzi na usalama wa Taifa letu kwani ni hatari sana kukabidhi nafasi nyeti kwa wageni/wakimbizi kwa sababu kuna wale ambao hata kama wameishi miaka 1000 sehemu nyingine, huendelea kuwa wazalendo kwa Taifa lao la asili. Mfano hai ni Mh. PK, Rais wa nchi mojawapo jirani, ambaye ni kama tu alizaliwa na kukulia Uganda, lakini bado kilichotokea wote tunakifahamu.

Kwa wasiofahamu tu ni kwamba huyu Mh. PK alishikilia nafasi nyeti sana katika nchi ya Uganda ikiwemo Mkuu wa kitengo cha Intelijensia Jeshini, lakini bado tu roho yake na akili yake ilikuwa katika nchi yake ya asili!

Chonde chonde kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, siyo kwamba hawa watu hawajulikani, wanafahamika vyema ila kwa sababu ya rushwa na mambo mengine, basi kunakuwa na ile hali ya kufumbia macho.

Naomba kuwasilisha.

View attachment 2879699
Maandamano Hoyeee!
Kumbe basi ndio wanatakiwa kuwa wazalendo kwenye hili.la maandamano na watoboe siri hii nzito!
Maandamano ya Amani yanayodai haki hizo!.
Yaa CCM tuko na mauzauza Chama changu mnatu boa sana
 
Ako Mungai wakati furani ako na uwaziri wa mambo ya elimu hakuwa mbongo alikuwa raia wa nchi jirani
Wapo mbona wakat nipo kenya miaka hiyo alikuwepo mkuu wa polisi pwani. Somebody Mboya ulikuwa hunikamati
 
Leo nimepigiwq simu na kada mmoja wa ccm anataka nimsaidie kurekebisha profile zake na cv zake then kaniambia

Usiogope taja kiasi unachotaka nikitoka kwenye kikao cha chama nakupigia usiku.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa akipitia uzi huoni kama atajua!
Si umepita mafunzo mkuu mbona unajiachia hivo..
 
Lakini hili linapaswa kua jambo la kutekelezwa huko baada ya kuwagundua mamluki walio jiingiza kwenye mfumo sio kuja kutuambia sisi walala hoi tutafanya nini 🤔🤔

ukienda kigoma asilimia kama 70 ya wanao jiita waha ni warundi na wanyarwanda lakini pia hapo hapo kuna wakongo wengi wame jazana na wote hao wanajiita watanzania ukienda kagera nako hivyo hivyo pia wageni wengi Sana wamejaa kule

kama wanataka kutibu hilo tatizo waanze kuwazuia huku uraiani kabla hawajafika huko juu, huo ni uzembe mkubwa Sana kwa vyombo vya ulinzi na usalama
 
Kuna jamaa mmoja wa asili ya Congo DRC yupo uhamiaji cheo kubwa ni mwenyeji wa Bukavu. Alikuwa anawapa wacongo wenzie Work permit kishenz naishia hapo. Japo na Sisi tupo wa kutosha Lubumbashi
 
Tuanza na Upendo Peneza ni Mnyarwanda,pale Geita kuna wanyarwanda wengi sana,serekali kama wako serious waanze na ule mkoa,unafanya kazi na mdada pale GGM ghafla unashangaa unachangishwa mchango wa Harusi anaolewa Kigali kisha unaambiwa ni Mnyarwanda....waanze na Upendo Peneza na kaka yake Baraka
Hawa wanyarwanda Sasa inabidi kupitisha msako wa nyumba kwa nyumba huko Geita, mwanza , chato, bukoba, kigoma, simiyu,, hii phase ya kwanza
 
Watanzania tupo warahisi sana kuchezewa akili zenu. Lakini acha tu tuchezewe kwani huwa hatutaki kutafakari. Hivi jambo kama ni hili ni la utekelezaji au ni la kusemea kwenye majukwaa! Tuna idara za usalama, upelelezi na ulinzi. Kama wamegundua kuna watu wa aina hii kwa nini wasiondolewa kwanza? Rais kila siku ni lazima apewe briefing kuhusu masuala mbali mbali ya nchi, ina maana hawakumwambia huko kwenye vikao? Kwangu mimi hili ni suala la utekelezaji zaidi na siyo suala la kusemea jukwaani. Otherwise, kuna jambo fishy linataka kufanywa na huu ni mwanzo tu wa kulihalalisha.
Wewe na baadhi ndio mnawaza nje ya 📦
Kweli mpaka jeshi limekuwa siasa au kuna kitu?
Hata mimi siamini
 
Back
Top Bottom