Haya Mambo ya Viongozi wa Kisiasa Kwenda na Viti Vyao Kwenye Nyumba za Ibada Yasitishwe

Haya Mambo ya Viongozi wa Kisiasa Kwenda na Viti Vyao Kwenye Nyumba za Ibada Yasitishwe

View attachment 2976278
View attachment 2976279
View attachment 2976280
View attachment 2976281
Kumekuwa na picha zinazoenea kwenye mitandao zikimuonyesha rais samia akiwa katika ibada kanisani,sina uhakika ikiwa ni ibada ya pasaka au otherwise lakini kinachoonekana ni kwamba amekwenda na kiti chake cha ikulu kwenda kukalia kanisani,sawa na alivyofanya Makamo wake wa Rais.

Hili jambo kwa ujumla linapaswa kukemewa kwa sababu liko kinyume kabisa na maadili ya kiroho.

Inapaswa ieleweke kwamba kuna maeneo huwa binadamu tunapaswa tufanane katika safu moja ili utofauti abaki nao mwenyezimungu peke yake.

Ni wazi kwamba nyumba za ibada ni nyumba za mwenyezimungu,na ni mungu pekee anaepaswa kuenziwa katika nyumba hizo.

Bila kujalisha madaraka uliyonayo,unapofika katika nyumba ya mungu ni vyema kujidunisha na kukubali kuwa sawa na viumbe wengine.

SSH ni muislam na taratibu za kiislam anazifahamu.Anataka kutwambia hata anapokwenda msikitini huenda na kiti cha ikulu kukalia??

Au anataka kusema siku akienda kuhiji Makka atakwenda na kiti cha ikulu kukalia??

Au atakataa kuvaa mavazi ya hija kwa kuwa yeye ni rais??

Nafikiri ufike wakati,binadamu tupunguze kuwakweza binadamu wenzetukwa namna ya kumkufutu mwenyezimungu.

Nafasi ya urais haipo Tanzania tu.Pichani juu ni rais wa Zambia na Rais wa Marekani wakiwa katika nyumba za ibada na wamekalia bench.Huyu wa kwetu anashindwa nini kukalia bench,kwamba utakatifu wake umezidi marais wengine ama vp??

Mungu awabariki sana!!
na hili ni la kujadiliwa? tunakoelekea tutaomba kujua Rais ananunua nguo viwanda vya ndani au uturuki
 
Kwani shida ipo wapi hapo?.
Tatizo wabongo tunapenda ku- judge na kuhoji vitu visivyo na msingi. Hivi kuna madhara ama tatizo gani Kiongozi akiwekewa kiti Kanisani.
Kwa hiyo USA president angekuwa kawekewa kiti ndio ungeona sahihi kwako?.
Tusiwe watumwa wa kuiga vitu vya nje.

Inaonekana hujaelewa hoja ya mleta mada. Suala siyo kwa sababu kiongozi wa Marekani kafanya. Hoja ni kuwa kwenye nyumva za ibada, kwa msingi wa imani zote, uislam na ukristo, uingiapo ibadani hustahili kufanya kito chochote cha kujitofautisha na watu wengine kwa kuonesha kuwa wewe ni bora zaidi. Ni mahali pa kujishusha na kuonesha kuwa kwenye utukufu na ufalme wa Mungu, huna tofauti na mtu mwingine yeyote.

Mifano ya marais wengine ameitoa kuonesha tu jinsi hata marais wa nchi nyingine wanavyotii misingi hii ya kiimani. Ukiona wewe ni tofauti na wanadamu wengine, usiende. Fanya ibada yako kama yule mfarisayo aliyenena kuwa yeye siyo sawa na mtoza ushuru, lakini Mungu anasema unakuwa hujasali.
 
Hayo mabenchi ya mbao yanaumiza jaman..so wanaweka kiti chenye sponji ili awe comfortable

Kama ana tatizo la kiafya asiloweza kulivumilia, ni sahihi, anaweza kuwekewa kiti kinachoendana na afya yake, lakini si vema kuwa kiti cha ikulu. Kiti cha ikulu kina nembo. Ile nembo ni alama ya ufalme na mamlaka. Ndani ya nyumba ya ibada, ufalme ni wa Mungu pekee, hatustahili kupeleka ufalme mwingine ndani ya nyumba yake.
 
Kuwa sawa? Mbona mnavaa mavazi tofauti? Mbona mnavaa viatu tofauti? Mbona mnaishi nyumba tofauti? Mbona mna vipato tofauti?

Nyumba za Ibada ni kwa ajili ya kila mtu aingiaye humo kujifungamanisha na Mungu.

Masharti ya mkae wapi, mvae nini, na mseme nini ni ya kibinadamu tu.

Umekosea sana kusema eti kila mmoja kwenye nyumba ya ibada anasema anachokitaka. Kuna miongozo ya wazi kabisa, na imesisitizwa. Kunaweza kukawa na tofauti ya namna ya kunena na lugha inayotumika, lakini mantiki lazima iwe moja. Na hayo yamesemwa wazi kabisa kwenye vitabu vya neno la Mungu.

Kama ana tatizo la kiafya, anaweza kuwekewa kiti tofauti, lakini hakitakiwi kuwa na nembo yoyote inayoashiria mamlaka, maana kanisani mamlaka ni ya Mungu pekee yake.
 
View attachment 2976278
View attachment 2976279
View attachment 2976280
View attachment 2976281
Kumekuwa na picha zinazoenea kwenye mitandao zikimuonyesha rais samia akiwa katika ibada kanisani,sina uhakika ikiwa ni ibada ya pasaka au otherwise lakini kinachoonekana ni kwamba amekwenda na kiti chake cha ikulu kwenda kukalia kanisani,sawa na alivyofanya Makamo wake wa Rais.

Hili jambo kwa ujumla linapaswa kukemewa kwa sababu liko kinyume kabisa na maadili ya kiroho.

Inapaswa ieleweke kwamba kuna maeneo huwa binadamu tunapaswa tufanane katika safu moja ili utofauti abaki nao mwenyezimungu peke yake.

Ni wazi kwamba nyumba za ibada ni nyumba za mwenyezimungu,na ni mungu pekee anaepaswa kuenziwa katika nyumba hizo.

Bila kujalisha madaraka uliyonayo,unapofika katika nyumba ya mungu ni vyema kujidunisha na kukubali kuwa sawa na viumbe wengine.

SSH ni muislam na taratibu za kiislam anazifahamu.Anataka kutwambia hata anapokwenda msikitini huenda na kiti cha ikulu kukalia??

Au anataka kusema siku akienda kuhiji Makka atakwenda na kiti cha ikulu kukalia??

Au atakataa kuvaa mavazi ya hija kwa kuwa yeye ni rais??

Nafikiri ufike wakati,binadamu tupunguze kuwakweza binadamu wenzetukwa namna ya kumkufutu mwenyezimungu.

Nafasi ya urais haipo Tanzania tu.Pichani juu ni rais wa Zambia na Rais wa Marekani wakiwa katika nyumba za ibada na wamekalia bench.Huyu wa kwetu anashindwa nini kukalia bench,kwamba utakatifu wake umezidi marais wengine ama vp??

Mungu awabariki sana!!
Mbona viongozi wa kanisa wanakaa mbele na Wana viti vyao?
 
Sasa unatoa mfano wa marais wa marekani, kwanini hukutoa mfano wa marais wetu? JPM, Nyerere, Kikwete, Mkapa, Mwinyi walivyokuwa wanaenda makanisani walienda na viti vyao?
Tuige hata Kenya ambapo Rais hatembei na kiti maalum kila mahali.
 
Umekosea sana kusema eti kila mmoja kwenye nyumba ya ibada anasema anachokitaka. Kuna miongozo ya wazi kabisa, na imesisitizwa. Kunaweza kukawa na tofauti ya namna ya kunena na lugha inayotumika, lakini mantiki lazima iwe moja. Na hayo yamesemwa wazi kabisa kwenye vitabu vya neno la Mungu.

Kama ana tatizo la kiafya, anaweza kuwekewa kiti tofauti, lakini hakitakiwi kuwa na nembo yoyote inayoashiria mamlaka, maana kanisani mamlaka ni ya Mungu pekee yake.
Kwenye Urais wa kifalme hiyo ni muhimu.
 
Africa kuna mambo mengi ya ajabu, Museveni yeye hutembea na choo chake maalumu cha kutumia.
 
Mtu kukalia kiti Chake inaruhusiwa katika ibada hata msikitini. Wapo tele wanakalia viti vyao, tembelea tu misikitini utaona.
Msikitini waumini hawatumii viti
 
Isitoshe hata kwenye Biblia sidhani kama Wafalme waliingia mahekaluni na kwenye masinagogi na kukaa pamoja na commoners. Eti Mfalme Sulemani au babake Daudi wakalie mabenchi ya hekaluni. Aaaa wapi!
Usifananishe mambo ya Ufalme na Jamuhuri. Kwenye ufalme ndio kuna tofauti kati Royal blood na commoners.
 
Amewekewa msala wake wa kusalia !
Maana yake ni kwamba Rais ana ulinzi wa aina yake popote pale anapokuwepo !
Iwe ni Msikitini au Kanisani !
Na hata wale waumini watakaokaa karibu yake ni wale ambao wamekubalika na wanaosimamia ulinzi wa Rais ! Sio kila muumini ataruhusiwa kumsogelea Rais !

Watanzania tuna mahitaji muhimu sana kama Taifa,
Hii habari ya Viti au Misala ya kwenye nyumba za ibada tuwaachie walinzi wa Rais waamue wao atumie kiti au msala upi !
Sisi haituhusu hiyo maana sio kazi yetu !
Sisi tunataka Katiba mpya kwanza 🙏🙏🙏 !
Huwa inaanza viti inakuja misafara mirefu inayosimamisha shughuli za watu kwa masaa.
 
Ibada yako wewe Bw. Joseph inaathirika vipi na uendaji wa raisi na kiti chake mwenyewe???
 
Kama kanisa liko kwenye ujenzi bado, au halijajitosheleza kwa viti ni sawa waende na viti vyao. Lakini kama kuna viti vya kutosha, halafu wewe uende na kiti chako kwa kuona vile vya pale kanisani havina hadhi inayolingama na wewe, unamkufuru Mungu.
Kwa hiyo Bora usiende kabisa !??
 
Mbona viongozi wa kanisa wanakaa mbele na Wana viti vyao?

Kiongozi wa Kanisa awapo ibadani anakuwa kuhani, mchungaji na mwalimu. hufanya kazi ya ukuhani, kazi ya kufundisha na kazi ta kuwachunga kondoo wa Bwana. Yeye, tuwapo ibadani ndiye kiongozi mkuu, wengine wote ni kondoo aliopewa kuwaongoza. Huwezi kuwachunga kondoo, na wewe ukiwa umekaa katikati ya kondoo. Vile vilivyopo ndani ya hekalu, kanisa au pale madhabahuni, havipo kwaajili ya utukufu wa kiongozi wa ibada bali kwaajili ya utukufu wa kile anachokifanya. Na huwezi kusikia padre au mchungaji, baada ya ibada anachukua kiti au meza ya altareni kwenda kuitumia nyumbani kwake. Na pale atoleapo sadaka au amwombapo Mungu, hawezi kukaa kwenye kiti, husimama au kupiga magoti, kuonesha kuwa naye si chochote mbele ya ukuu wa Mungu. Wala hakuna kiongozi wa dini anayeingia kanisani na kiti au meza yake. Atatumia kile alichokikuta.
 
Kiongozi wa Kanisa awapo ibadani anakuwa kuhani, mchungaji na mwalimu. hufanya kazi ya ukuhani, kazi ya kufundisha na kazi ta kuwachunga kondoo wa Bwana. Yeye, tuwapo ibadani ndiye kiongozi mkuu, wengine wote ni kondoo aliopewa kuwaongoza. Huwezi kuwachunga kondoo, na wewe ukiwa umekaa katikati ya kondoo. Vile vilivyopo ndani ya hekalu, kanisa au pale madhabahuni, havipo kwaajili ya utukufu wa kiongozi wa ibada bali kwaajili ya utukufu wa kile anachokifanya. Na huwezi kusikia padre au mchungaji, baada ya ibada anachukua kiti au meza ya altareni kwenda kuitumia nyumbani kwake. Na pale atoleapo sadaka au amwombapo Mungu, hawezi kukaa kwenye kiti, husimama au kupiga magoti, kuonesha kuwa naye si chochote mbele ya ukuu wa Mungu. Wala hakuna kiongozi wa dini anayeingia kanisani na kiti au meza yake. Atatumia kile alichokikuta.
Kwaiyo Rais akiwa kanisani anakuwa sio Rais Tena na je huyo kuhani wako akitoka nje ya kanisa anakuwa sio kuhani Tena?
 
Kwahiyo kiroho unatakiwa kukalia benchi? Hebu acheni hekaya za kijima hizi.

Kiti cha rais au benchi la kanisani haviingiliani kwa vyovyote vile na mchakato wa maombi. Mtu anaweza hata akaja na godoro lake kanisani na wala hakuna shida. Msikariri.
Godoro labda msikitini
 
Back
Top Bottom