Haya ndio maumivu au uchungu wa kifo unaompata mtu anayekufa 'Sakaratul-Mauti'

Haya ndio maumivu au uchungu wa kifo unaompata mtu anayekufa 'Sakaratul-Mauti'

Jina lingine huitwa ''Ulevi wa kifo'' haya ni 'maumivu ya kifo' au mafuriko ya mauti. Hakika Kila nafsi itataabika wakati wa mauti yake. Kwetu sisi waislamu tunazo dalili ambazo humpata mtu siku 40 kabla ya kufa kwake.

Nafsi zetu ipo siku zitalipwa adhabu ya udhalili kwa sababu zilikuwa zikisema uwongo juu ya Mwenyezi Mungu, na kuzifanyia kiburi Ishara zake.

Sakaratul Mauti ni Uchungu wa kifo, ni magumu ya pekee ambayo mtu anayekufa hupata kabla ya kifo chake na wakati nafsi inatoka kwenye mwili wake. Ni ngumu sana mwanaadamu kupata nafasi ya kutoa Wosia kwa jamaa zake akiwa katika kipindi hiki.

Ulevi wa mauti' ni hali maalum inayoambatana na ukali na ina athari kubwa katika nafsi na mwili wa mwanadamu, na miongoni mwa athari zake ni kutokea hali mbaya ya usingizi na ulevi kwa mtu anayekufa, na hali hii inamshinda, kubadilika. ufahamu wake na akili yake, hivyo kwamba mtu anayekufa katika hali hiyo anakuwa kama mlevi, na ndiyo sababu ikasemwa kwamba 'Kifo ni kichaa''. Siku zote anayekufa lazima ajisaidie haja kubwa na ndogo.

Na ulevi wa mauti kwa mtu anayekufa huwa ni mkali sana, yaani ukali wake unaoushinda na kuubadilisha ufahamu wake na akili yake ni kama ulevi kutokana na kinywaji.

Viwango vya ukali wa kifo

Ulevi wa kifo ni moja ya hali ngumu sana ambayo mtu hupitia mwisho wa maisha yake ya dunia wakati anakufa na roho inapotoka kwenye mwili wake, kifo na ukali wake, lakini wakati wa kufa kwake ni mwanzo wa faraja yake, na kuokoka kwake na matatizo ya dunia, hivyo anajikuta katika hatua nyingine ya maisha.

Ukali wa kifo “Kwa Muumini ni kama harufu nzuri anayoisikia, kisha analala usingizi kwa sababu ya wema wake, na uchovu wake wote na maumivu huondolewa kwake, na kwa mtu mwenye kiburi aliyepuuza matakwa ya MUNGU ni kama kuumwa kwa nafsi. Michomo ya nyoka na n'ge, ukali wake huwa ni mbaya zaidi.

Katika Hospitali nyingi kumeshuhudiwa watu wakitapa na kuhangaika wakati wa kukata roho, mwingine roho inatoka akiparamia ukuta kwa machungu.

Maumivu ya kifo ni kama chujio kwa watu wengi, ni lazima kila mwanaadamu kupitia hatua hizi, hata wanyama hupitia hatua hizi wakati wa kuchinjwa kwao, hupaparuka na kwenda hovyo. Uchungu wa kifo wakati mwingine umefananishwa na machungu anayopata mbuzi akichunwa ngozi yake akiwa mzima.

“Mauti ni msafishaji, huwachuja Waumini na dhambi zao, na ni uchungu wa mwisho unaowasibu, ni fidia ya dhambi iliyobakia.” Kwa ajili yao, na Atawatakasa walioamini na matendo yao mema. , ili iwe ni raha au faraja ya mwisho itakayowafuata, na iwe ni malipo mema ya mwisho watakayopata.

Uchungu wa mauti na ukali wake ni lazima kwa kila nafsi, na ni makali sana kwa watu wasiomjua MUNGU, na inaweza kuwa kali kwa baadhi ya waumini ili wanyanyue safu zao na kuwaondolea madhambi yao, kwa kuwa inaweza kuwa nyepesi. kwa wengi wao:

View attachment 2700348
Point yako ni nini hapa? Maana najaribu kusoma lakini nikionacho ni abunuwasi akijaribu kusimulia abracadabra zake.
 
Acha uwongo, upingaji wako usivuke mipaka na kuanza kuongopa. Pinga kwa hoja, jicho lako halina uwezo wa kuona Km million 50
Mnafundishwa ujinga huko Bakiif naona.
Mars inaonekana kwa macho kila baada ya miaka kadhaa inapokuwa karibu na dunia

Screenshot_20230727_120557_Chrome.jpg
 
Sijakupongeza, nimeuliza swali. Point yako ni nini? Bado haujajibu swali.
Swali si umeshajijibu mkuu: Kwamba ''Maana najaribu kusoma lakini nikionacho ni abunuwasi akijaribu kusimulia abracadabra zake.'' Sasa nikupe jibu gani hapo tena?
 
Mwenye kukanusha maisha baada ya kifo ni mpingaj wa MUNGU, Kukataa imani ya Akhera ni kukataa aina yoyote ya uwajibikaji. Watu kama hao hawaamini malipo au adhabu kwa matendo. Hapa hapa ulimwenguni tu, ukivunja sheria za jamii uanchukulia hatua. Iweje kuvunja sheria za aliyekuumba akuache hivihivi?
Acha fix wewe. Huyo alikuumba wewe ulimuona wapi? Wadangaje wajinga wenzako mimi nishushe nimefika.
 
Hata mwanao wa kumzaa kamwe huwezi kumuacha aishi anavyoona yeye, utatumia gharama nyingi kumlinda, kumfundisha, kumtunza na kumuongoza kwa namna unavyoona wewe inafaa, tena utamfungia ndani ya geti kuepuka madhila ya binaadamu. Iweje MUNGU akuumbe halafu akuache hivi hivi ufanye unavyoona wewe ilihali anajua nje kuna shetani wa kukupoteza?
Kama Mungu anatupenda kweli angepambana na shetani yeye mwenyewe kuliko kutuachia msala sisi. alafu yeye akaenda kujificha
 
Fikiria kwanza michakato iliyopitika hadi kupatikana huo ubongo, fikiria huyo mtu ametokea wapi? miezi 9 katika tumbo. Kabla ya hapo alikua wapi? miaka mingapi katika korodani? kabla ya hapo alikua wapi? alikua ni chakula na nafaka? au alikua wapi? nani kamleta hapa? je huyo aliyemtoa huko alikotoka hadi akamfisha anashindwa vipi kumrejesha? na kumpitisha katika hatua hizi za sakaratul-mauti? Ikiwa tu mwanaadamu mwenzako anaweza kukupa sindano ya usingizi na akakufanya atakavyo iweje MUNGU ashindwe kukupitisha atakapo?
Ulivyo kua kabla hujazaliwa ndivyo utakua baada ya kifo. Achana na ngonjera nyiingi zisizo na kichwa Wala miguu
 
Ukiachana na Imani kifo si mchezo nmeshuhudia vifo vingi ndo kitu pekee kinachofanya niamini kuna vitu vipo hatuvijui
SAKARATUL MAUTI naweza kusema ni pale ambapo brain inaanza kua deprived na oxygen hivo mtu anapata neurological deficits anaanza kuona watu wanaomtisha na ni kweli utaona mtu anaogopa anajificha
Kutoa haja si lazima ila ni common sababu bladder na njia ya nyuma ukiwa unakata roho kunakua hakuna innervation ya sphincter muscles zinazoshikilia
Ila kama marehem ataempty bladder punde kabla ajakata roho ni uncommon kujiokojolea
ALLAHU AALAM
 
Acha uwongo, upingaji wako usivuke mipaka na kuanza kuongopa. Pinga kwa hoja, jicho lako halina uwezo wa kuona Km million 50
Hongera,naona umetayarisha fimbo za kutosha,Kila anayenyanyuka unae.

Ndani ya hizo siku arobaini atatokewa na malaika mara tatu,,,nifunulie hapa.
 
Back
Top Bottom