Kuna yule msanii mmoja wa kinondoni hivi ........anakuwaga na wasanii .........alilewa akaropoka jina lake limenitoka kidogoYameibukia wapi? Hata hivyo nimesema hii ni habari endelevu.
Chochote nitawajuza…
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna yule msanii mmoja wa kinondoni hivi ........anakuwaga na wasanii .........alilewa akaropoka jina lake limenitoka kidogoYameibukia wapi? Hata hivyo nimesema hii ni habari endelevu.
Chochote nitawajuza…
Sasa babu mengine nashindwa kukwambia ila nasikiaga Diamond kavua kofia kwa mtoto wa Bi Khadija, sio mchezo!Hapa ndiyo unatimia ule usemi kwamba mwonja asali huchonga mzinga.
Kuna sehemu Wanaume huwa tunaingia na kujisemea pale naonja na kupita hivi
Kumbe ndiyo unanaswa mazima
Unakuta jamaa wanajiuliza huyu Mwamba ameona nini Kwa kile kibinti, kumbe mambo unayopewa Kwa bed, hadi unajilaumu kwanini hatukujuana mapema 🏃🏃🏃🏃
mjomba ali muoa mkewe, ila mwanzoni ali ona mkewe ni mbwa mbea ila pisi.Hayo mambo ya kuonja onja hata yakitukuta sisi Wazee ndiyo mwanzo wa kumkabidhi Binti wa elfu 2 kadi na password ya Benki akajichotee Pension yote
Kuja kutahamaki unajikuta pension imeenda 🙌
Hiyo ni NDOA YA UJI, Baada ya Ramadhan inavunjika, ni aibu sana kwa Wasanii kuoana ili kukidhi matakwa ya RamadhanView attachment 3225842
Hatimaye!
Baada ya sarakasi nyingi, Msanii Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ amekata shauri la kumuoa mpenzi wake ambaye ni msanii ndani ya lebo yake ya muziki (WCB) Zuhura Othman Soud ‘Zuchu’
Uamuzi huo umekuja huku kukiwa na sintofahamu nyingi juu ya mahusiano yao ambapo mwishoni mwa mwaka jana Zuchu alitangaza kwa mara nyingine kuachana kwao japo amekuwa akifanya hivyo mara nyingi na baadaye kurudiana.
Safari hii mambo yamekuwa tofauti kidogo baada ya majuzi kuibuka ugomvi ndani ya kampuni upande wa redio kwa Zuchu kuwashutumu wafanyakazi wa Diamond kumvunjia heshima.
Zuchu ameonekana ‘kukaza’, hajacheka na yeyote akiwemo Diamond mwenyewe na pengine hili limesogeza karibu ndoa yao.
Zuchu ameshinda vita iliyowashinda wengi?…
The mother in law from hell, Mama Diamond amekuwa mwiba mchungu takribani kwa kila mwanamke aliyetoka kimapenzi na Diamond.
Amesemekana kikwazo kikuu kwa Diamond kuoa, hivyo posa hii kwa Zuchu inatuacha njia panda kwamba Mama Dangote kapata kiboko yake? Je posa hii ina baraka za mama yake Diamond?
Ndoa ni kabla ya Ramadhani…
Mwezi uliopita Diamond akiwa na msanii mwenzie Nandy katika mkutano mkuu wa CCM, alionekana akisema atamuoa Zuchu kabla ya Ramadhani ya mwaka huu ambayo inategemewa kuanza mapema mwezi Machi.
Diamond amekuwa akitoa ahadi nyingi hivyo wengi hatukuchukulia tamko lile kwa uzito, nimeshtuka baada ya kupewa taarifa za uhakika kuwa ni kweli na posa hiyo itapelekwa nyumbani kwa Bi Khadija Kopa Ijumaa ya keshokutwa tarehe 7.
Haya jamani, mambo ndio yako hivyo na hii ni habari endelevu nitakuwa hapa kuwajuza mapema kadiri nitakavyopokea taarifa.
Straight From The Horse’s Mouth,
Nifah.
Waswahili walisema ndege mjanja hunaswa na tundu bovu. Diamond kuoa Zuchu ni kichekesho ujueWataachana tu
Hakuna muoaji hapo😀Waswahili walisema ndege mjanja hunaswa na tundu bovu. Diamond kuoa Zuchu ni kichekesho ujue
Kweli bwana, imagine alisha lalamika kuwa alimla D2!Simba na kuruka na totozi kali kiasi kile anakuja kuoa Zuchu?
Mapenzi kitu cha ajabu..
Diamond anamuoa king’ang’anizi wake, huku Zuchu akiolewa na matatizo yake.
Siamini, Diamond kumwacha yule binti wa Kikenya akaoa Zuchu, au kwa vile umri wa Zuchu unambebaHakuna muoaji hapo😀
Anaitwa stan bakola.......ni juzi kati tu hapa eti bidada kasusaHiyo ni zamani Mkuu, chukua hii mpya na tusubiri kuona.
Maisha yangu yote nachukia sana ndoa kabla ya Ramadhani, huwa naona aibu sana.Hiyo ni NDOA YA UJI, Baada ya Ramadhan inavunjika, ni aibu sana kwa Wasanii kuoana ili kukidhi matakwa ya Ramadhan
Diamond hawezi akaoa mwanamke anayejitambua. Tanasha atakuwa anajitambua..Siamini, Diamond kumwacha yule binti wa Kikenya akaoa Zuchu, au kwa vile umri wa Zuchu unambeba