Tarehe kama ya leo mwaka 1959 alizaliwa Rais wetu mpendwa wa awamu ya tano Mhe. Dr. John Pombe Magufuli. Kimsingi,leo anatimiza miaka 60.
Kinachofanywa na Serikali anayoiongoza ya awamu ya tano kinaonekana. Kuna uimarikaji mkubwa wa nidhamu na uchapakazi kwenye utumishi wa umma; vita yenye mafanikio ya ufisadi na wizi wa Mali za umma.
Pia, tangu kuchaguliwa kwake ameimarisha nyanja za usaforishaji wa anga,reli na barabara; ameimarisha ulinzi na usalama wa nchi yetu na huduma za kijamii kama afya, elimu, maji,umeme na miundombinu mingine.
Anachokisimamia na kukifanya kinaonekana waziwazi. Mungu amlinde na kumpa maisha marefu zaidi na yenye baraka ili Tanzania yetu ifaidi matunda ya uongozi wake. Happy birthday Mr. President!