Heshima kitu cha bure! Kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote lakini ni lazima aheshimiwe na wote? Akosolewe kwa staha na asitukanwe!

Heshima kitu cha bure! Kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote lakini ni lazima aheshimiwe na wote? Akosolewe kwa staha na asitukanwe!

Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.

Hoja hii ni kufuatia mjadala mingi kwenye mitandao ya jamii kwenye issue ya Bandari yetu na DPW, kuna watu wamevuka mipaka na kumkosea heshima Rais Samia na kumkosoa kwa lugha kali, kumtweza, kumkashifu na wengine kuvuka mipaka kwa kumtukana hadi matusi ya nguoni!, this is not right!.

Angalizo la Uzalendo Uchawa Vs Uzalendo Halisi!.

Kufuatia kuibuka kwa dhana ya uchawa, kuna watu wanajiita kabisa chawa wa Mama, hivyo mtu kama mimi nikijitokeza kutaka Rais Samia aheshimiwe wote, watu wenye akili fupi hawachelewi kuniona chawa!. Mimi sio chawa na hili sio bandiko la uchawa! ni bandiko la kukumbushana heshima ya kiasili ya Kiafrika ya heshima kitu cha bure, mkubwa kumheshimu mdogo, na mdogo kumheshimu mkubwa, heshima kwa wote.

Declaration ya Kutosaka Uteuzi.
Kumezuka mtindo wa sisi waandishi wa habari na watu wa media, tukiusifu utawala kwa mazuri au tukisifu viongozi, tunaonekana kuwa tunasaka uteuzi, naomba niwahakikishie tena Paskali hasaki uteuzi wowote na hili Paskali aliisha mueleza mteuzi mwenyewe face to face Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!

The Duality of President. heshima ya lazima ya kimamlaka!, Akosolewe kwa Staha na Asitukanwe!.
Duality ni kanuni ya mtu mmoja ku na personalities mbili kwa wakati mmoja.
Rais wa nchi ni dual personality ana personalities mbili ambazo ni duality but they exist in one!. Yaani ni mtu mmoja mwenye two personalities ambazo zina exist in one and at the same time.

Kanuni hii ya double personalities au dual personality imezungumzwa vizuri na Mwana Saikolojia mahiri wa Marekani, Dr. Segmund Freud katika kukichambua kitabu cha Dr. Jekyll and Mr. Hyde, kilichoandikwa na Dr. Robert Luis Stevenson aliyeandika pia kitabu cha Kisiwa chenye Hazina, Treasure Island, ambapo mtu mmoja mwenye double personality mchana yuko vingine na usiku yuko vingine kama watu wawili tofauti.

Hii duality ipo sana katika jamii zetu mfano mzuri ni wanga, wachawi na washirikina, ukiwaona mchana ni watu wa kawaida, lakini usiku ni watu wengine kabisa!.

Persnality ya kwanza ya Rais wa nchi ni human personality, yaani rais ni binadamu, a human being kama binadamu mwingine yoyote wa kawaida anayestahili mahitaji tote ya kibinadamu, hivyo rais wetu Samia ni mtu anayeitwa Samia Suluhu Hassan, Huyu ni human being, she has all human needs including feelings, love and compassion na ana mahitaji mengine yote ya kibinaadamu ikiwemo kupenda, kupendwa na heshima, love and dignity and can make mistakes just like any other human beings. Hivyo huyu Samia ambaye she is only a human, unaweza kumpenda au usimpende, unaweza usimkubali, unaweza kumbeza, unaweza kumtukana na kumdhalilisha au kusema chochote kumhusu mtu anayeitwa Samia Suluhu Hassan na hakuna tatizo!. Mfano mzuri wa hili ni huyu mtu niliyemzungumzia hapa Ikitokea kuna Kiongozi ana Macho mazuri, na umeyapenda, je, kuna ubaya kumsifia macho yake? Ni ukosefu wa heshima na adabu? bandiko kama hili liliwezekana kupandishwa kwasababu she is just a human na enzi hizo alikuwa na single personality, sasa with dual personality bandiko kama hili haliwezi kupanda.

Jee ni lazima kumpenda Rais?.
Kumpenda mtu yoyote ni person preferences, mtu yoyote anaweza kumpenda mtu mwingine yeyote, kwa sababu zozote au bila sababu, au unaweza usimpende kwa sababu zozote, au bila sababu, na hakuna kosa lolote kutompenda yeyote lakini hata ikitokea mtu fulani humpendi, bado una wajibu wa kumheshimu na kuulinda utu wake.

Hivyo watu wako huru kumpenda Rais Samia ama kutompenda ila kumheshimu ni wajibu ndio maana kumtukana mtu ni kosa.

Personality ya pili ya Rais Samia, ni rais wa nchi, hivyo huyu binadamu anaitwa Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwa ni rais wa nchi, assume kitu kinachoitwa presidential personality, huyu sasa sio mtu binadamu, ni mtu taasisi yenye mamlaka ya juu kabisa ndani ya JMT, hivyo rais wa nchi kwa personality yake ya urais, ni lazima aheshimiwe, utii kwa mamlaka, huwezi kumtukana, huwezi kumdhalilisha, itakuwa ni kuitukana taasisi ya urais.

Rais Samia kama taasisi ya urais, huhitaji kumpenda lakini ni lazima kumheshimu. Rais Samia kama taasisi ya urais, she is not human, hawezi kufanya makosa ndio maana hawezi kushitakiwa!.

Wito kama huu niliwahi kuutoa enzi za utawala wa JK, Mapungufu ya Kikwete: Constructive Criticisim! na wakati wa Magufuli pia nilishauri Wito Kwa wana JamiiForums kuhusu ukosoaji wa Rais Magufuli
Hivyo sasa tuko na Samia, tunaweza tusimpende lakini lazima tumuheshimu na ukitokea ukosoaji, tumkosoe kwa lugha ya staha na sio kumtukana na kumdhalilisha.

Niliwahi kushauri humu kuwa Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda unaweza usimpende lakini ni lazima kumheshimu.

Hitimisho
Rais Samia ni rais wetu, tumpende, tumheshimu, tumsuport, na hata ikitokea, kuna sehemu anakosea tumkosoe kwa heshima na staha.
Kwa sisi wengine ambao tunamkubali Samia kama Mama, mzazi wako, hata akukosee vipi, kamwe huwezi kumtukana!. Samia ni Mama wa Taifa, tumheshimu, namalizia kwa msisitizo huu

Heshima Kitu cha Bure, Rais Samia, ni lazima aheshimiwe na wote, akosolewe kwa staha na asitukanwe!.​

Paskali
Kwanzia Leo na kuendelea uitwe paschalojo nguruwe lenye njaa
 
Kuwa serious Pascal. Ni kwa namna gani tunaweza kumheshimu Rais ambaye amesaini mkataba unao ziweka sheria zote za nchi yake kuwa chini ya Mkataba wa DP World? Kuna masuala sensitive sana yamekubaliwa kwenye ule mkataba na ndiyo maana werevu wanatoa machozi. Toka nianze kuijua mikataba ya kimataifa sijawahi ona mkataba wa kipumbavu kama huu, kwamba ikitokea mkataba ku-conflict na sheria yoyote ya nchi basi mkataba utakuwa juu ya sheria ama kanuni hizo. Kwa mkataba ulio sainiwa DP World watakuwa na uwezo hata wa kuua na wasiwajibike kwa sheria yoyote
 
Pasko! Umeanza tena! Unajua mtu akikwambia kwa maneno ya upole kuwa hapa umenikosea na ukakaa kimya kama hakijatokea chochote, mpige tusi au kuwa mkali, lazima atakujibu tu, hivyo hii ilikuwa ni njia ya watu kupata majibu wala siyo matusi.
Technic hii inaitwa agent provocateur, sisi waandishi tunaitumia sana, kanuni na maadili ya habari, yanasisitiza ku balance story, lakini kwenye stories za madudu, wahusika wana kwepa the media, hivyo sometimes you have to provoke them to come out, lakini ndio utukane?
P
 
Nimenukuu maneno haya sehemu na yako kwenye kiingereza...

"respect must be earned. It may be demanded"...., in this case as a president, " ....but it can never be imposed. Fear may be coerced, and obedience may be enforced; but respect flows freely from a heart full of appreciation for admirable qualities and behavior..."

......Mwishi wa kunukuu
===================


Kwa kusikitisha, mitazamo yetu wa kuwa na uwezo wa kuchambua na kudadavua mkataba huu ili kujaribu kuivusha na kufikia malengo fulani kwa Nchi yetu tumepigwa(haujazingatiwa kwa mapana yake) na kudharauliwa au kubezwa yaani tunajisikia tunaachwa bila kupewa maanani. (Hatusikilizwi) wameziba masikio!

Hakika wadau hawajapendezwa(binafsi sijapendezwa)na tabia zilizoonyeshwa.

Inaweza kuwa ukweli ni mchungu na ni mgumu kuukumbatia, na kidonge kichungu kumeza. Lakini mwisho wa siku,uwepo angalau, ufahamu kuwa wananchi hawajapenda kudharauliwa!
Uongozi wa CCM na Serikali Wasijiondoe ufahamu.

Mpaka kieleweke.
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.

Hoja hii ni kufuatia mjadala mingi kwenye mitandao ya jamii kwenye issue ya Bandari yetu na DPW, kuna watu wamevuka mipaka na kumkosea heshima Rais Samia na kumkosoa kwa lugha kali, kumtweza, kumkashifu na wengine kuvuka mipaka kwa kumtukana hadi matusi ya nguoni!, this is not right!.

Angalizo la Uzalendo Uchawa Vs Uzalendo Halisi!.

Kufuatia kuibuka kwa dhana ya uchawa, kuna watu wanajiita kabisa chawa wa Mama, hivyo mtu kama mimi nikijitokeza kutaka Rais Samia aheshimiwe wote, watu wenye akili fupi hawachelewi kuniona chawa!. Mimi sio chawa na hili sio bandiko la uchawa! ni bandiko la kukumbushana heshima ya kiasili ya Kiafrika ya heshima kitu cha bure, mkubwa kumheshimu mdogo, na mdogo kumheshimu mkubwa, heshima kwa wote.

Declaration ya Kutosaka Uteuzi.
Kumezuka mtindo wa sisi waandishi wa habari na watu wa media, tukiusifu utawala kwa mazuri au tukisifu viongozi, tunaonekana kuwa tunasaka uteuzi, naomba niwahakikishie tena Paskali hasaki uteuzi wowote na hili Paskali aliisha mueleza mteuzi mwenyewe face to face Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!

The Duality of President. heshima ya lazima ya kimamlaka!, Akosolewe kwa Staha na Asitukanwe!.
Duality ni kanuni ya mtu mmoja ku na personalities mbili kwa wakati mmoja.
Rais wa nchi ni dual personality ana personalities mbili ambazo ni duality but they exist in one!. Yaani ni mtu mmoja mwenye two personalities ambazo zina exist in one and at the same time.

Kanuni hii ya double personalities au dual personality imezungumzwa vizuri na Mwana Saikolojia mahiri wa Marekani, Dr. Segmund Freud katika kukichambua kitabu cha Dr. Jekyll and Mr. Hyde, kilichoandikwa na Dr. Robert Luis Stevenson aliyeandika pia kitabu cha Kisiwa chenye Hazina, Treasure Island, ambapo mtu mmoja mwenye double personality mchana yuko vingine na usiku yuko vingine kama watu wawili tofauti.

Hii duality ipo sana kwa binadamu wote, yaani nafsi na roho, au me & I. mambo kama ya de javu, third eye, physical body na astra body, mambo ya ying na yang, vyote hivi vinatumia kanuni ya duality.

Wanawake wengi wanalelewa kwa kuandaliwa kuwa wife materials, ili kupata mchumba hivyo katika kusaka ndoa anakuwa na one personality na akiisha pata ndoa na kuolewa, ana change na ku show her true colours!.

Jamii zetu nyingi za kiasili za Kiafrika kina watu wanaishi double life mfano mzuri ni wanga, wachawi na washirikina, ukiwaona mchana ni watu wa kawaida, lakini usiku ni watu wengine kabisa!.

Na kwenye siasa ndio usiseme!.

Persnality ya kwanza ya Rais wa nchi ni human personality, yaani rais ni binadamu, a human being kama binadamu mwingine yoyote wa kawaida anayestahili mahitaji tote ya kibinadamu, hivyo rais wetu Samia ni mtu anayeitwa Samia Suluhu Hassan, Huyu ni human being, she has all human needs including feelings, love and compassion na ana mahitaji mengine yote ya kibinaadamu ikiwemo kupenda, kupendwa na heshima, love and dignity and can make mistakes just like any other human beings. Hivyo huyu Samia ambaye she is only a human, unaweza kumpenda au usimpende, unaweza usimkubali, unaweza kumbeza, unaweza kumtukana na kumdhalilisha au kusema chochote kumhusu mtu anayeitwa Samia Suluhu Hassan na hakuna tatizo!. Mfano mzuri wa hili ni huyu mtu niliyemzungumzia hapa Ikitokea kuna Kiongozi ana Macho mazuri, na umeyapenda, je, kuna ubaya kumsifia macho yake? Ni ukosefu wa heshima na adabu? bandiko kama hili liliwezekana kupandishwa kwasababu she is just a human na enzi hizo alikuwa na single personality, sasa with dual personality bandiko kama hili haliwezi kupanda.

Jee ni lazima kumpenda Rais?.
Kumpenda mtu yoyote ni person preferences, mtu yoyote anaweza kumpenda mtu mwingine yeyote, kwa sababu zozote au bila sababu, au unaweza usimpende kwa sababu zozote, au bila sababu, na hakuna kosa lolote kutompenda yeyote lakini hata ikitokea mtu fulani humpendi, bado una wajibu wa kumheshimu na kuulinda utu wake.

Hivyo watu wako huru kumpenda Rais Samia ama kutompenda, it's an option lakini kumheshimu is not an option ni wajibu ndio maana kumtukana mtu ni kosa.

Personality ya pili ya Rais Samia, ni rais wa nchi, hivyo huyu binadamu anaitwa Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwa ni rais wa nchi ana, assume kitu kinachoitwa presidential personality, huyu sasa sio mtu binadamu, ni mtu taasisi yenye mamlaka ya juu kabisa ndani ya JMT, hivyo rais wa nchi kwa personality yake ya urais, ni lazima aheshimiwe, utii kwa mamlaka, huwezi kumtukana, huwezi kumdhalilisha, itakuwa ni kuitukana taasisi ya urais. Dini zote zinafundisha utii kwa mamlaka, iwe ni mamlaka halali au haramu, una wajibu wa kutii mamlaka, ndio maana hata enzi za yule Blaza wangu, kabla hajagombea urais, toka ile 2014 nilipoambiwa ni yeye, nilileta angalizo humu Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli baada tuu ya kushinda nikatoa ushauri huu Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him! na pia nikatoa angalizo hili Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!
Hivyo despite all the odds heshima na utii kwa mamlaka ni jambo la wajibu!.

Rais Samia kama taasisi ya urais, huhitaji kumpenda lakini ni lazima kumheshimu!. Rais Samia kama taasisi ya urais, she is not human, hawezi kufanya makosa ndio maana hawezi kushitakiwa!.

Wito kama huu niliwahi kuutoa enzi za utawala wa JK, Mapungufu ya Kikwete: Constructive Criticisim! na wakati wa Magufuli pia nilishauri Wito Kwa wana JamiiForums kuhusu ukosoaji wa Rais Magufuli
Hivyo sasa tuko na Samia, tunaweza tusimpende lakini lazima tumuheshimu na ukitokea ukosoaji, tumkosoe kwa lugha ya staha na sio kumtukana na kumdhalilisha.

Niliwahi kushauri humu kuwa Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda unaweza usimpende lakini ni lazima kumheshimu.

Hitimisho
Rais Samia ni rais wetu, tumpende, tumheshimu, tumsuport, na hata ikitokea, kuna sehemu anakosea tumkosoe kwa heshima na staha.
Kwa sisi wengine ambao tunamkubali Samia kama Mama, mzazi wako, hata akukosee vipi, kamwe huwezi kumtukana!. Samia ni Mama wa Taifa, tumheshimu.

Namalizia kwa msisitizo huu

Heshima Kitu cha Bure, Rais Samia, ni lazima aheshimiwe na wote, akosolewe kwa staha na asitukanwe!.​

Paskali
Paschal, siyo lazima kumpenda Rais. Lakini mtu anaweza kuibomoa heshima yake mwenyewe. Kwenye maisha unaweza ukaheshimiwa kweli lakini ukija ukawadharau wale wanakuheahimu pia wao watakudharau na kukupuuza kabisa.
Jiheshimu utaheshimiwa,thamini wengine watakuthamini,wapende wengine watakupenda pia.
Kiongozi huyu ametukosea Sana Watanzania kwa MOU Ile. Paschal haifai na mtu mwenye akili timamu Tena aliyepewa mamlaka ya kuongoza nchi akakubali kusaini mkataba kama ule ni maajabu.
Zaidi ni alituona sisi hatufai, ni wajinga, ametupuuza na hatupendi Toka moyoni.
Bro,kaka. Ni aibu,ni aibu kubwa. Wengi hatukutegemea kuona hilo likifanyika lakini mwenzetu kafanya Tena tukikumbuka tumetoka kupigwa kwenye madini na gesi.
Yeye ni Binadamu na atapita lakini aitendee haki nchi yake kwani hata udongo wake ndiyo utamzika hata zikwa na udongo toka Uarabuni..
Atupende tutampenda,atuthamini tutamthamini, atujali tutamjali
Tanzania ndiyo nchi yetu ya furaha.🇹🇿
 
Pascal Mayalla hoja yako ni nzuri na ni ya msingi sana tena sana. Bahati mbaya sana maji yalishamwagika
No hayajamwagika ni paa letu tuu linavuja na ukuta wa nyumba yetu umepata ufa, mvua zikinyesha tutaangazia panapovuja na kupaziba, na huu ufa tutauziba bila ya kusubiria kujenga ukuta.
kudhihaki/kukebehi/kudharau/kubeza/kukaaa kimya pale kauli tata za kutweza utu wa Dkt Magufuli na yeye mwenyewe pia kutoa kauli tata kipindi cha maombolezo.
Sikumbuki Viongozi kumtweza JPM, kila kinachosemwa kumhusu ni ukweli mtupu!. Mfano kumuita Mwanamke "we malay... " ni kumtweza na kumtukana, lakini kama Mwanamke huyo kweli ni malay. na anaendesha maisha yake kwa shughuli hiyo, kumuita malay. sio kumtukana au kumtweza bali ni kumwambia ukweli!.
Tena tuliandika hata wewe ni shahidi, tena tulimuomba mara kibao hata Maxence Melo waangalie utaratibu wa kufunga na kuzui posti zote zinazotweza utu wa aliyetumikia taifa kwa uzalendo ila hatukusikilizwa.
Hii ndio jf advantage, maximum freedom of expression. Afadhali Max alikataa maana huo pia ni udikiteta
 
Kiukweli kabisa vitu vingine ni ujinga tuu wa watu kutokujua, Bandari zetu ni zetu milele, Mwarabu wa Dubai hapewi Bandari zetu bali sisi hatuna uwezo kuzi operates kwa faida hivyo tumewaomba watusaidie kutuendeshea kwa ufanisi, baadhi tuu ya magati. Bandari haijauzwa hata milimita moja!. Watanzania tujifunze kukubali kuna vitu hatuwezi, tunaposhindwa tukubali kusaidiwa au tukomae? Baada ya Bandari ni ATCL na SGR au Tusubirie?
p
Kwa hiyo kaka, akina tibaijuka,warioba,shivji,Adam Malima, Lisu,mbowe,Butiku,mawakili mbalimbali,Diaspora na wengine wengi, wameongea/wanaongea kwa kupotosha???? Ni kichaa tu anayeweza kusaini masharti yale
 
Kwa hiyo kaka, akina tibaijuka,warioba,shivji,Adam Malima, Lisu,mbowe,Butiku,mawakili mbalimbali,Diaspora na wengine wengi, wameongea/wanaongea kwa kupotosha????
Hakuna mtu yoyote anajejua kila kitu, hivyo pia inawezekana they are all wrong. Mimi ni miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa kukosoa makubaliano hayo Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! ile mambo yanarekebishika.
Ni kichaa tu anayeweza kusaini masharti yale
Huku pia ni kumtukana kwa matusi ya reja reja!, unamuita kichaa!. Heshima ni kitu cha bure!. Mama yako aliyekuzaa, akifanya jambo usilopendezwa nalo, unaweza kumuita kichaa?.
P
 
Kiukweli kabisa vitu vingine ni ujinga tuu wa watu kutokujua, Bandari zetu ni zetu milele, Mwarabu wa Dubai hapewi Bandari zetu bali sisi hatuna uwezo kuzi operates kwa faida hivyo tumewaomba watusaidie kutuendeshea kwa ufanisi, baadhi tuu ya magati. Bandari haijauzwa hata milimita moja!. Watanzania tujifunze kukubali kuna vitu hatuwezi, tunaposhindwa tukubali kusaidiwa au tukomae? Baada ya Bandari ni ATCL na SGR au Tusubirie?
p
Hebu tuoneshe kwenye ile IGA ni wapi pameandikwa waarabu wataendesha baadhi ya magati, halafu mimi nikuoneshe wapi pameandikwa wataendesha bandari zetu zote Tanganyika milele..

Mayalla hii kazi unayoifanya, kupigia debe rasilimali.za taifa kutolewa bure kwa wageni, hata kama unajipendekeza kwa mtawala ili upate chochote, mimi nakuona kabisa unajitafutia laana ya uzeeni, laana utakayokwenda kufa nayo usipotubu mapema.
 
Sikumbuki Viongozi kumtweza JPM, kila kinachosemwa kumhusu ni ukweli mtupu!. Mfano kumuita Mwanamke "we malay... " ni kumtweza na kumtukana, lakini kama Mwanamke huyo kweli ni malay. na anaendesha maisha yake kwa shughuli hiyo, kumuita malay. sio kumtukana au kumtweza

Kwa manitki hiyo hapo juu, ni sawa kabisa SSH aitwe na kuzodolewa kama alivyofanywa na hao wanaomtukana au lah!

Yaani kuwa kinachosemwa kipo! kweli haiingii akilini kudai wanaosema kuna kasoro lukuki huko halafu ionekane wote wakawa wanakosea
Kwa hiyo kaka, akina tibaijuka,warioba,shivji,Adam Malima, Lisu,mbowe,Butiku,mawakili mbalimbali,Diaspora na wengine wengi, wameongea/wanaongea kwa kupotosha????
...Suala zima limekuwa mishandled from the beginning...mnafunika funika vifuu vya moshi. It is sad to imagine wanatoa kifuu kimoja kimoja chenye moto na kinachofuka moshi kutoka kwenye rundo la vifuu vinavyowaka moto. The buck stops with her...as a President she needs to pay attention and do something period.
 
Back
Top Bottom