Hii chapati niliyotengeneza, usipokua makini utajing'ata Vidole

Hii chapati niliyotengeneza, usipokua makini utajing'ata Vidole

[emoji23] [emoji23] [emoji23] nataman nikuone unavokuna nazi

Unaona sasa...itabidi nikukague kwanza usijekuwa na kifaa cha kurekodia picha! Huwezi amini hakuna mtu amewahi kuniona nikikuna nazi....


[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] namuelekeza jamani anogeshe chakula chake

Ila akikuelekeza mumeo itakuwa shida hah
 
Uwe unakuna nazi ya kutosha unaweka kwenye fridge. Ukikata kupika unapasha tu maji unachuja zako tui. Mi nazi ya azam siwezi kuila tena. Nazi ya kawaida ina ladha kwenye msosi. Ile ya azam unasikia harufu tu ila ladha hamna. Kama dada anakujaga kwako mwambie awe anakukunia aweke kwa fridge uachane na nazi za azam

Aisee hili ni bonge la idea....nimelipokea kwa mikono miwili. Nitakuwa nafanya hivi.

Nakumbuka enzi hizo za kuishi nyumba za kupanga (isomeke 'chumba') Kigamboni sasa jirani akaniona narudi nyumbani na nazi kadhaa na anajua sijaoa...aliniangalia weee nikamuona kabisa anatamani kuniuliza ila akashindwa!

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwamba unahisi atakua anakuna kama wanavyofunzwa kina dada jinsi ya kukuna nazi na makungwi wao?

Mnaona sasa...

Hebu rudini kwenye topic ya chapati za figganigga bana.

Cc: Jolie Jolie
 
Aisee hili ni bonge la idea....nimelipokea kwa mikono miwili. Nitakuwa nafanya hivi.

Nakumbuka enzi hizo za kuishi nyumba za kupanga (isomeke 'chumba') Kigamboni sasa jirani akaniona narudi nyumbani na nazi kadhaa na anajua sijaoa...aliniangalia weee nikamuona kabisa anatamani kuniuliza ila akashindwa!



Mnaona sasa...

Hebu rudini kwenye topic ya chapati za figganigga bana.

Cc: Jolie Jolie
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] itakua aliwaza umeanza ushirikina sasa unaandaa vitendea kazi vya kwenda kupasua njia panda usiku kumbe mwenzie unajipikia.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] itakua aliwaza umeanza ushirikina sasa unaandaa vitendea kazi vya kwenda kupasua njia panda usiku kumbe mwenzie unajipikia.


Ayaaaaa halafu sikufikiria hili aisee...huenda!


Ila enzi zile za nyumba za kupanga ilikuwa raha jamani ukiwa na majirani wakarimu. Mimi nilikuwa nikisafiri lazima nirudi na zawadi za majirani (matunda, nazi, ndizi, ...) basi nawagawia hata kidogo kidogo tu. Sitosahau ule mfungo wa Ramadhani kipindi kile. Nilikirimiwa sikupika mwezi mzima...jirani huyu anakuletea daku asubuhi (ila ilikuwa adhabu kuamshana saa kumi sijui ile) na nikirudi jioni nakuta msosi unanisubiria. Wale wadada (mashemeji zangu) walikuwa wataalamu hasa. Huko nadhani ndipo nilijifunzia mapishi ya chapati za maji na mkate wa kumimina. Good old days aisee..ukiishi na watu vyema utavuna mengi mema!

Dah umenifanya nipamiss Kigamboni aisee... [HASHTAG]#nimekumbukaZamani[/HASHTAG]
 
Ayaaaaa halafu sikufikiria hili aisee...huenda!


Ila enzi zile za nyumba za kupanga ilikuwa raha jamani ukiwa na majirani wakarimu. Mimi nilikuwa nikisafiri lazima nirudi na zawadi za majirani (matunda, nazi, ndizi, ...) basi nawagawia hata kidogo kidogo tu. Sitosahau ule mfungo wa Ramadhani kipindi kile. Nilikirimiwa sikupika mwezi mzima...jirani huyu anakuletea daku asubuhi (ila ilikuwa adhabu kuamshana saa kumi sijui ile) na nikirudi jioni nakuta msosi unanisubiria. Wale wadada (mashemeji zangu) walikuwa wataalamu hasa. Huko nadhani ndipo nilijifunzia mapishi ya chapati za maji na mkate wa kumimina. Good old days aisee..ukiishi na watu vyema utavuma mengi mema!

Dah umenifanya nipamiss Kigamboni aisee... [HASHTAG]#nimekumbukaZamani[/HASHTAG]
Mpaka mkate wa kumimima unapika? HESHIMA YAKO.
 
Mpaka mkate wa kumimima unapika? HESHIMA YAKO.


Walaumu wale wadada wa Kipemba. Hilo lilikuwa pishi lao la wikiendi. Walinifundisha mapishi mengi hadi vitumbua ingawa nahisi nimesahau kidogo. Yani Jumamosi asubuhi utadhani kuna sherehe...huyu yuapika vitumbua na mwenzake anapika mkate...kitu cha jiko la mkaa peke yake.

Ilipofikia mapishi ya urojo sasa nikahama...hahah
 
Back
Top Bottom