Hii hapa mikoa 12 inayoendesha uchumi wa nchi, inamiliki na kushikilia asilimia 70% ya uchumi wa Tanzania

Hii hapa mikoa 12 inayoendesha uchumi wa nchi, inamiliki na kushikilia asilimia 70% ya uchumi wa Tanzania

Dhahabu hazichimbwi Mwanza,mgodi wanaoutegemea Kama ukianza ni ule wa Nyanzaga but ligtime yake itakuwa chini ya miaka 15.

Mwanza inategemea service industry,uvuvi na Mikoa inayoizunguka.

Nyie Tanga hakikisheni mnawashusha Wabishi Mbeya ndio nitajua mko seriously otherwise Viongozi wenu eti Wana Mpango wa kugawanya huo Mkoa so mtazidi kudidimia 😁😁

Tanga
Tanga haiwezi kuishusha Mbeya, tuache ubishi wa mwanza na mbeya, ile ni zone kubwa Kwa Tanzania lile ni lango, utake kutoka mbeya, south, zimland, zambia, tswanaland, malawi, halafu kilimo, mpunga, mahindi, uchimbaji wa dhahabu japo chunya yote imejaa wasukuma ndio wanaofaidi dhahabu ile, kitu pekee cha ajabu ni serikali kutowekeza miundombinu bora, mfano uyole na mafiati panakosaje bypass au hata vivuko vya juu Kwa watembea Kwa miguu, haya cocoa ujue kyela ndio ina bei nzuri kuliko Tanga na Moro japo nao wana kokoa, Kwa kesi ya moro ngoja waanze kuexport karafuu tutawasikilizia mbali sana
 
Mikoa isiyo na rasilimali kwa wingi itakuwaje ?
Hakuna Mkoa usio na Rasilimali Kwa Wingi hapa ila mfumo wa Utawala hautoa nafasi ya ufanisi mzuri na ushindani na pia Serikali ndio inaamua kipaombele.

Unadhani kungekuwa Kuna kujisimamia ,Hali ya Maendeleo ingekuwa duni kama ilivyo?

Mwisho nitajie Mkoa ambao unadhani hauna Rasilimali lakini pia Kuna kanuni za mgawanyo ambazo Huwa Zina consider factors zote ikiwemo hiyo unayoisemea wewe.
 
Kwa Kigoma ni Suala la mda tuu itafunguka,hata kilichowasaidia Tabora ni kuimarika Kwa Barabara zote kuu zinazoingia na kutoka ndio maana imeanza kujitokeza maana ni Kwa mara ya kwanza Tabora inatokea kwenye list.

Miradi inayoendelea Kigoma ni Mingi sana ila poleni watu wa Tabora mnaenda kugawanywa so mtazidi kurudi kule kule kwenye level zenu za umaskini 🤣🤣
Tabora itaimarika zaidi, kigoma nakubali miradi yao ya barabara ikiisha, watatisha sana , nilifika kasulu miaka mitatu nyuma wale waha biashara wanafanya sana, ni wilaya ambayo niliona wacongo, warundi wanafunga mzigo wa duka pale na magorofa yanajengwa Kwa kasi kubwa hadi unapata hamasa watu wanavopambana
 
Tanga haiwezi kuishusha Mbeya, tuache ubishi wa mwanza na mbeya, ile ni zone kubwa Kwa Tanzania lile ni lango, utake kutoka mbeya, south, zimland, zambia, tswanaland, malawi, halafu kilimo, mpunga, mahindi, uchimbaji wa dhahabu japo chunya yote imejaa wasukuma ndio wanaofaidi dhahabu ile, kitu pekee cha ajabu ni serikali kutowekeza miundombinu bora, mfano uyole na mafiati panakosaje bypass au hata vivuko vya juu Kwa watembea Kwa miguu, haya cocoa ujue kyela ndio ina bei nzuri kuliko Tanga na Moro japo nao wana kokoa, Kwa kesi ya moro ngoja waanze kuexport karafuu tutawasikilizia mbali sana
Pamoja na kwamba wewe unasema Mbeya ni rangi ila Mbeya inapakana na Malawi tuu,Rango la Sadc ni Mkoa wa Songwe,Tunduma huko ambao ulimegwa Kwa Mbeya.

Mbeya Ina watu aggressive sema nini ,hata kama Walimega Songwe Ile distance ya Tunduma Hadi Mbeya ni fupi so Bado Mbeya ndio Ina influence kote huko na kufaidika na Ile establishment yake Toka Mwanzo.
 
Tanga sio ya kuona, Tanga iliwahi kua na viwanda vingi nyuma huko kuliko hata Dar, ona bandari ikiboreshwa, bomba la mafuta ya uganda likamilike, ile ni strategic zone toka enzi ya mkoloni
Kuna kitu kikiuliwa pale Tanga basi ikuwa na maendeleo sana
 
Ruvuma kuna uvunaji mkubwa sana wa Makaa ya mawe unaendelea. Huu uvunaji hauna impact ya moja kwa moja kwa mwananchi wa kawaida wa Ruvuma zaidi ya kuongeza mapato ya Mkoa na Taifa. Maisha ya wanaruvuma bado ni duni sana kusema kweli.

Kila mara nasema itungwe sheria kulazimisha sehemu ya mapato yatokanayo na rasilimali ibaki eneo husika ili kusaidia maeneo hayo kiinuka kiuchumi. Kwa sasa wanaruvuma wanashangaa tu malori maelfu kwa maelfu yanasomba mkaa kila uchao bila faida yoyote kwao
Kila nikipita Nyakanazi ninakutana na malori yenye plate number zinazoanzia na RA, naambiwa ni malori ya Rwanda yanayopeleka Rwanda makaa ya mawe kutoka huko ulikotaja.
 
Tujenge kituo Cha uwekezaji Kigoma au Tabora kutarget soko la DRC, RWANDA, BURUNDI na Zambia, badala ya nchi hizo kufuata mizigo China ziichukulie Tabora au Kigoma.
Ushauri utazingatiwa.Tungekuwa na kanuni za Utawala zinazoruhusu ushindani hili lingefanyika ila Sasa inategemea Huduma za Wanasiasa wa Chama Tawala 🤣🤣

Ndio maana napinga mfumo wa Utawala huu wa centralization sio mzuri
 
Kila nikipita Nyakanazi ninakutana na malori yenye plate number zinazoanzia na RA, naambiwa ni malori ya Rwanda yanayopeleka Rwanda makaa ya mawe kutoka huko ulikotaja.
Ni hatari. Hayo umeona ya Rwanda ukienda Namanga mpakani au Bandari ya Mtwara ndiyo utazimia kwa wingi wa hayo malori. Lakini ukienda Songea au Mbinga yanakotoka hayo makaa yenyewe wamechoka hadi wanatia huruma.
 
Pamoja na kwamba wewe unasema Mbeya ni rangi ila Mbeya inapakana na Malawi tuu,Rango la Sadc ni Mkoa wa Songwe,Tunduma huko ambao ulimegwa Kwa Mbeya.

Mbeya Ina watu aggressive sema nini ,hata kama Walimega Songwe Ile distance ya Tunduma Hadi Mbeya ni fupi so Bado Mbeya ndio Ina influence kote huko na kufaidika na Ile establishment yake Toka Mwanzo.
Songwe ukitoa mlowo, tunduma na kiasi isongole, mkwajuni, uende hadi mbalanga huko, mbeya bado ni baba yake sawa na mwanza ilivozaa geita, geita haitokuja kuipita mwanza
 
Hiyo mikoa yote iliyotajwa Kuna key factor moja ambayo mikoa ya Njombe haina.
Idadi ya Watu.
Kuna wenye watu wengi ila wako hovyo eg Kagera,Simiyu,Rukwa nk.

Sema hivi miundombinu ya uchumi ilichelewa na huo ni Mkoa Mpya huwezi linganisha na Mikoa mikubwa but with time itafunguka na itarealise their potential
 
Umejipinda kweli kweli ila inakuaje Mkoa wenye wasomi udai kwamba unatengwa? Si Kila Idara ya serikali mumejaa? Why msijipakulie minyama?

Visingizio fc 🤪🤪🤪🤪
Nadhani wewe ni wale wanaosoma bila kuelewa kilichoandikwa na ni miongoni mwa niliowaongelea kwenye aya ya kwanza. Sasa unasema tumejaa kila idara na unasema tujipakulie ni wapi nimekwambia natokea huko?
Hata hivyo fikiria nje ya box.

Nilipata kusoma sehemu kuna yule mzee wa miaka hiyo aliyesema wajitenge kama serikali inavyowatenga wawe na nchi yao hakukosea kwa nilichokiona na kukipitia. Ndiyo maana nimesema kinachoendelea huko hakiwezi kueleweka kwa wale wasio wafuatiliaji na wapambanuzi wa mambo.J

Juzi juzi hapa tulimsikia Mbowe akisimama na kuongelea masuala ya biashara na uwekezaji. Kuna wakati alitamka neno "wachaga tulitengwa", wengi walimshambulia nikiwemi mimi kwa kuwa alitumia hilo neno la wachaga na ikaonekana ni mkabila lakini baada ya tafakari ya kina na kuzungumza na walioko katika hayo maeneo nilielewa ni kwanini alisema hivyo. Sasa ndiyo sawa na wewe unayesema "mmejaa kwenye kila idara"
 
Nadhani wewe ni wale wanaosoma bila kuelewa kilichoandikwa na ni miongoni mwa niliowaongelea kwenye aya ya kwanza. Sasa unasema tumejaa kila idara na unasema tujipakulie ni wapi nimekwambia natokea huko?
Hata hivyo fikiria nje ya box.

Nilipata kusoma sehemu kuna yule mzee wa miaka hiyo aliyesema wajitenge kama serikali inavyowatenga wawe na nchi yao hakukosea kwa nilichokiona na kukipitia. Ndiyo maana nimesema kinachoendelea huko hakiwezi kueleweka kwa wale wasio wafuatiliaji na wapambanuzi wa mambo
Sasa usitete watu wavivu
 
Kigoma inafunguka, point hapo ni miundombinu ijengwe kigoma, Tabora tayari ina shughuli nyingi za kiuchumi, kigoma ilikua sawa na kagera lakini naona kagera inaachwa hadi na kigoma sijui ule mkoa una laana gani maana wanakila kitu cha kufanya waendelee
Hakuna laana yoyote. Ungejua miradi inayotekelezwa Kagera. Ungekaa kimya tu...
Zaidi ya Km 150 za lami zinajengwa kagera, km 5 za njia nne Bukoba mjini, upanuzi wa bandari za Bukoba na kemondo, kuna meli mpya ya Mv mwanza inaanza safari za Mwanza Bukoba soon...uwanja wa Bukoba unawekewa taa za kuongoza ndege ( kigoma ule uwanja acha tu)...
Kuna miradi ya maji kibao tu ya kusambaza maji vijijini huko kama mradi wa maji kutoa ziwa victoria ( vijiji kibao Bukoba vijijini karibu na kwa kina bashiru ally kemondo vinawekewa maji ya bomba) kuna mradi wa maji wa kyaka... vijiji kibao vina maji ya bomba

Kuna campus mpya ya chuo cha UDSM inajengwa km chache kutoka Bukoba mjini...kwenye mashule na hospital huko usiongee kabisa

Hizo takwimu za makaratasi zisikupumbaze. Kigoma bado sana kulinganisha na kagera. Huo ndo uhalisia...sio kigoma tu mikoa mingi bado sana kulinganisha na kagera...

Siku hiz hadi barabara za vijijini mfano ile ya muhutwe, kamachumu nshamba...na ile ya muleba Rubya zina lami!
 
Inaumiza sana sana mkoa kama shinyanga, Geita, Mara penye madini mengi ya dhaabu lakin ndiyo kwenye amaskini mkubwa maji tu na shule ni shida hadi huruma na wananchi wanaona kawaida tu alafu tunawasingizia wawekezaji ila jukumu ambalo serikali ilitakiwa kulitekeleza kutoa at a asilimia 10 ya mapato ya madini kuendeleza maeneo ayoo ila imekuwa kama kiini macho tu
Nasikia kuna Mzungu alishawahi kufunga safari hadi Geita kwa lengo la kwenda kushuhudia hali ya huo "mji"unaosifika kwa kutoa dhahabu! Alipofika alistaajabu! Badala ya kukuta jiji lililojengwa na kujengeka, alikutana na mkoa uliogubikwa na harufu ya umaskini kuanzia mwonekano wake mpaka watu wake.
 
Ni sahihi kabisa lakini hao watu walishaachana na masuala ya takwimu za NBS kwa maana hata wanaozijadili wamejikita katika kuongelea umasikini kwa kuangalia GDP ambayo hata hawajui inatafutwa namna gani na inachangiwa na nini na kuacha nini. Wengine wanajadili kwa kuongozwa na ukabila.

Kuna kitu wengi hawakielewi kuhusu kutengwa kwa makusudi kwa huo mkoa na ukiwa mfuatiliaji kwa kina utalijua hili. Achana na masuala ya kupelekewa meli inayobeba mizigo ambayo serikali haijui inazalishwaje kwa maana sehemu zingine utasikia Serikali imepeleka pembejeo za kilimo kwa wakulima lakini hutasikia kitu cha namna hiyo kwa mkulima wa eneo hilo.

Juzi bungeni kuna mbunge wa huko aliongelea masuala ya NIDA na uhamiaji na akaomba serikali ipeleke maafisa wanaofahamu kwa undani kuhusu hayo maeneo na wale ambao ni eneo geni kwao basi wawe informed na trained ipasavyo kuhusu hilo eneo. Ukiliangalia hili kwa macho ya juu utaona halina maana kwamba mbona maeneo mengine wanaenda tu lakini kwa upande wa mfanyabiashara au mwekezaji ataelewa ni kwanini huyo mbunge aliomba hilo. Nillilima huko miaka kadhaa najua ni kipi wanakumbana nacho sababu nilikumbana nacho mimi nikiwa nimepokelewa vyema na wenyeji.

Ni wazalishaji hodari wa Kahawa lakini jiulize serikali inaweka nini zaidi ya hapa juzi kuja na habari za kupunguza kodi sijui 15 na wakati huo huo unamzuia mtu asiuze kahawa yake sehemu nyingine ambako anapata bei kubwa zaidi kuliko anayoipata hata baada ya kuondoa hizo kodi 15. Ukiuza kwa aliyekuja kutoka nje ya nchi unaambiwa umeuza magendo wakati huo huo yapo maeneo mnunuzi kutoka kenya anaingia mpaka shambani ndani ndani huko bila shida yoyote. Je, hiyo GDP itapandishwaje?

Nilipata mashamba huko maeneo ya Karagwe kama unaenda eneo wanaita chabalisa na mpaka sasa niliyatelekeza yapata miaka 6 na kurudi kwetu kufanya mambo mengine. Sababu ya kuyaacha ni kile kinachoendelea kimya kimya kuhusu hilo eneo. Hivyo hali ya huko naijua vyema hasa katika suala zima la uzalishaji. Achana na ngonjera za mitandaoni sijui wenyeji hawapendi wageni, sijui hawapendi kazi ngumu na blaa blaa nyingi na hizo takwimu za NBS ambazo mtu anayepata mahitaji yake ya chakula cha kila siku kutoka shambani kwake moja kwa moja huku akihitajika kununua vitu vichache sana ambavyo hapati shambani anahesabiwa sawa na yule anayefanya spending ya kila kitu kwa kununua tena kila siku.

Ukiuliza kuhusu viwanda vya samaki vilivyokuwepo utakachojibiwa utaelewa. Kuna kiwanda cha kinaprocess kuuza kahawa ya kopo ya TANICA kama ilivyo AfriCafe. Ukiuliza kuhusu mikakakati ya serikali kukiwezesha zaidi ili kiprocess kwa wingi kahawa inayozalishwa huko utabaki unashangaa.

Achana na masuala ya kupanua bandari, kujenga barabara ya njia nne mjini ilhali bidhaa zinakotoka hakuna lolote linalofanyika. Watafute wenyeji na walioko kwenye mifumo ya serikali watakufumbua macho. Wewe hujawahi kujiuliza ni kwa nini Mkoa wa Kagera huwa hautajwi sehemu yoyote kila ikitamkwa mipango na mikakati kwenye mikoa ya kanda ya ziwa? Zaidi utasikia ukitajwa pale kunapolipuka magonjwa yanayoanzia nchi jirani na kebehi kadha wa kadha.

Kuna kipindi Rais Samia alifanya ziara huko na kuelezea mikakati kadhaa lakini jiulize ni kwanini katika kutembelea na kuzindua miradi mikubwa ya kiserikali inayotekelezwa Mkoani humo aliishia kutembelea kiwanda cha Kagera Sugar ambacho kila kiongozi akienda huko akiwemo PM wote wanatembelea hapo tu?

Ulishawahi jiuliza ni kwanini vyuo tuite colleges zilizofunguliwa huko miaka utawala wa JK zilifungwa miaka ya utawala wa JPM na mpaka sasa hazijafunguliwa wakati colleges zenye hadhi sawa na hizo zinaendelea kushamiri kwenye mikoa mingine? Kipindi cha JK alianza taratibu jitihada za kufufua fua baadhi ya sekta lakini alivyoondoka zikaanza kurudishwa na kupotezewa.

Uliwahi kujiuliza kwamba ni kwanini hata zikiwa zinasomwa taarifa kuhusu eneo la kanda ya ziwa itatajwa Mwanza, Mara, Geita na utaambiwa imepakana na Kigoma au Simiyu lakini hutasikia Mkoa wa Kagera ukitajwa?

Hao watu wanapambana wao kama wao na ndiyo maana kwa kiasi kikubwa wanatudharau sisi watu tulio katika maeneo mengine ambao tunapata support kubwa sana ya serikali lakini bado tunalia wakati wao wanapambana wenyewe kama wenyewe na wanasonga.
Hilo swala vyuo sijawahi elewa kwa nini havifunguliwi aisee....wawekezaji walijitahidi wakajenga majengo na wanafunzi walikuwa wanasoma vzr. Serikali ikavifunga mpaka leo. Wamiliki wameomba sana TCU lakini wapi. Huenda leo vingekuwa vyuo kamili vinavyojitegemea...wanasahau watu waliokuwa wamejenga hostels, clubs nk karibu na vyuo hivyo biashara zilivyoharibika...

Hata hiki chuo kipya cha UDSM kinachojengwa hapo Bukoba ni baada ya maprofessor wa kihaya wakina Rutinwa UDSM kuomba sana serikali hadi kushawishi wanakijiji watoe ardhi bure ili chuo kijengwe ( mikoa mingine serikali inanunua viwanja yenyew na kujengwa vyuo)
Chuo kinajengwa sasa....lakin viwanja vyote karibu na chuo vishanunuliwa...na mji wa Bukoba unapanuka kuelekea huko..

Kagera watu wanapambana wenyew
 
Back
Top Bottom