Tatizo waswahili wanajua kusamehewa ni kuanza kupewa hela.Yeye kawasamehe ila hataki shobo nao.
Huwezii ila uwe makiniAs long as ni mama ntambeba tu... Unaanzaje kumtelekeza mama
Nimekuelewa mkuuWazazi hawalipizwi Kisasi ingawaje wanakosea, endelea kumsaidia Mama kulingana na moyo wako utakavyo.
Saudia pia na Ndugu zako Ila usiwaweke karibu yako. Saidia kulingana na uwezo wako lakini hakikisha hawawi karibu na wewe.
Nimeongelea power tiller wewe unaingelea trekta. Ama kweli, majungu yapo hadi mitandaoniHuu uzi ni feki kabisa...
dogo juzi tu kahitimu chuo 2021
kaanza kutuma maombi ya chuo mpaka 2022 hajapata Job..
hapa kaja na uzi kafukuzwa kazi katengwa na kila mtu mpaka chawa wamemkimbia😅
Nimefukuzwa kazi, nimetengwa na Ndugu, jamaa na marafiki!
Kazi Nilikuwa nafanyia kwenye moja ya taasisi kubwa za kimataifa. Wiki iliyopita kuna changamoto ilitokea ghafla Sasa kwa sababu Mimi ndiye nilikuwa team leader nikafukuzwa kazini! Taarifa zilienea kwa Kasi ya Moto wa msituni na Baada ya muda Mfupi nikatengwa na Ndugu jamaa na marafiki...www.jamiiforums.com
Halafu anatupanga kirahisi tu eti kanunua shamba heka 50, mara anunue trekta which is not less than 30mil dadek..
dogo hebu mrudishe mkeo shule mjenge familia mkiwa wote na akili mingi
Ushauri: Housegirl anataka nimuoe wakati aliishia Darasa la Tatu na miminatarajia mwakani nivae Joho la Degree
Wakuu Habari za muda huu! Tulianza kukutana bombani, kadri siku zilivyosonga tukazoeana na akataka kupajua ghetto kwangu nikamwonyesha. Juzi kati akaniletea zawadi ya vest! Niliipokea lakini sikuivaa. Sasa nashangaa sijawahi kumkaribia kimwili lakini nimeshtushwa na kauli yake ya kuniomba...www.jamiiforums.com
Sawa ahsantePomoja na hayo yote kutokea mkuu nakushauri usiache kumhudumia mama yako,siku zote yalipe mabaya kwa mema na Mungu atakubariki Sana.
😅😅😅😅Tatizo waswahili wanajua kusanehewa ni kuanza kupewa hela.
Mimi kuna ndugu zangu wala sina shida nao,tukikutana story tunapiga..ila mazoea sitaki na siwezi wapa hela yangu abadani.
Ushauri wangu mimi hao ndugu zako waache kama walivyo ila Mama yako Mzazi msaidie kwa kila hali hata kama alikulaumu kivipi? Wewe tekeleza wajibu wako kumuangalia Mama yako mzazi kwani umetoka nae mbali sana. Ukikosa kumsaidia mama yako mzazi ujuwe utaharibikia kila kitu chako ulicho kipanga huo ndio ushauri wangu ukiweza ufuate usipo weza uachilie mbali upite zake.Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo Hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi Ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.
Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.
Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na Sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.
Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!
Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.
Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.
Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.
Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Ahsante mkuuUshauri wangu mimi hao ndugu zako waache kama walivyo ila Mama yako Mzazi msaidie kwa kila hali hata kama alikulaumu kivipi? Wewe tekeleza wajibu wako kumuangalia Mama yako mzazi kwani umetoka nae mbali sana. Ukikosa kumsaidia mama yako mzazi ujuwe utaharibikia kila kitu chako ulicho kipanga huo ndio ushauri wangu ukiweza ufuate usipo weza uachilie mbali upite zake.
Interesting 😅Ndugu wa Tanzania wanakusubiria ufike juu waanze kusema una roho mbaya na unaringa
Ilikuwaje mkuuMmmh ndugu Sina hamu Mimi. Nilifirisiwa kwa siku 1. Sikuyaamini macho yangu. Nimesamehe Ila ukaribu noo.
hakika ni fumbo kubwa sana na anaeweza kufumbua hili fumbo ni MUDA peke yake.Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Surelyhakika ni fumbo kubwa sana na anaeweza kufumbua hili fumbo ni MUDA peke yake.
Kuna kitu hakipo Sawa kwenye hii Hadithi yako maan Hadithi ya kuanzia utotoni haiwezi kuisha Kwa mistari michache ulioiandika,Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.
Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.
Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.
Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!
Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.
Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.
Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.
Maisha ya hapa Duniani ni fumbo