Hii ndiyo treni yenye spidi ya kasi sawa na ndege, nilidhani uongo kumbe kweli

Hii ndiyo treni yenye spidi ya kasi sawa na ndege, nilidhani uongo kumbe kweli

China imekamilisha jaribio la usafiri wa treni aina ya maglev yenye kasi ya juu (UHS), kuashiria hatua nyingine muhimu kwa aina hiyo ya usafiri inayoweza kusafiri kwa kasi ya hadi maili 621 kwa saa sawa na kilometer 1,000 kwa saa.

View attachment 3064287

Jaribio hilo lilifanyika katika mkoa wa Shanxi unaopatikana kaskazini mwa China.

Hili lilikuwa jaribio la kwanza na kubwa lililokamilika kwa mfumo wa usafirishaji kwa kutumia umeme wa bomba pana lililo wazi (utupu) UHS.

Mojawapo ya mafanikio makubwa yaliyopatikana wakati wa jaribio hilo ni kwamba ilithibitisha kuwa mazingira ya uwazi uliopo kwenye bomba hilo kwa umbali mrefu yanaweza kufanya spidi kuwa kubwa zaidi na kudumisha kwa kiwango kikubwa.

China ilianza kujenga mfumo wa usafiri wa UHS maglev katika Kaunti ya Yanggao mwaka wa 2022, mfumo huo unalenga kuunganisha teknolojia ya anga na mfumo wa usafiri wa reli kwa lengo la kuendesha treni kwa kasi ya maili 621 kwa saa.
Hapo MAREKANI atajinyonga kwa wivu!!
 
Mkuu hiyo kitu gharama za kuijenga ndio changamoto kwa uchumi wetu. Agalia gharama za kujengatu kwa mile 1 (km 1.6) tu ni USD 60 million (kama bilioni 150 za kitanzania). Hatuwezi leo wala kesho.
The Shanghai Maglev, which happens to be the fastest train in the world, cost a whopping $1.2 billion dollars to build. At only 20 miles long, that is an incredible amount of capital cost. At that cost, it is about $60 million dollars per mile of track.
😀 😀 😀 😀 dah kwa gharama hizo ni haiwezekani labda dunia ianze upya. Shida inakuja pale ambapo viongozi wetu ni kama wanatutambia wakiwa madarakani na v8 zao wakiwa wanapita vuu vuu speed kubwa wanaenda kuzindua mradi tuliojengewa na USAID
 
Nime fall in love na sayansi jamani🔥🔥, wanawezaje wezaje hawa?
Wanawekeza, serikali inaruhusu free tech kuzalisha huku yenyewe ikiwasupport na kuhakikisja hakuna mtu anabaki nyuma, pia kukiwa na tech mpya yenye faida kwa taifa serikali inatoa funds.

Angalia kile kigari cha Masoud Kipanya!.
 
Sana tu, JPM sifa ndio zilikuwa nyingi na umimi uliopitiliza. Hizo ndege tu zimetuacha na madeni, bado hasara kila mwaka na hazina ufanisi wowote. Alikuwa na uthubutu ila hakuwa strategic wala hakupenda kushauriwa, ilikuwa ni one man show.
alikua bwege tu. nchi yetu haijawahi pata kiongozi. hata nyerere alikua hovyo.
 
Kwa kasi hiyo, hivyo vyuma si vitawaka moto. Msuguano utakaokuwapo hapo si wa kitoto.
Maglev (magnetic levitation) trains huwa hazigusi chuma huwa zinaelea juu kwa juu zinatumia principle ya eddy current levitation kukamilisha hilo.

kwa mfano mrahisi ukichukua pande mbili za sumaku zinazofanana kisha ukajaribu kuzikutanisha zitakuwa zinakataana(principle of magnetism) sasa wakishakamilisha kule kukataana wanachofanya ni kutengeneza njia ya kupata msukumo (motion ) kupitia hizo hizo sumaku.

Japo eddy current levitation huwa zinazalisha pia joto (eddy current losses) ila nadhani huwa kuna mfumo wa kupooza kupitia maji , japan ,indonesia , malaysia na nchi nyenginezo baadhi za asia walikuwa nazo hizi treni muda tu. ila nadhani kwa spidi china ndiyo atachukua tuzo miaka ijayo.
 
Back
Top Bottom