Hii Taarifa ya NHIF kama ni ya kweli basi Tanzania tuna tatizo

Hii Taarifa ya NHIF kama ni ya kweli basi Tanzania tuna tatizo

NHIF ina ubaguzi katika utendaji wake. Inapendelea waajiriwa wanaokatwa kutoka mishahara. Wao ndiwo wanapata huduma kubwa.
Kama umejiunga mchangiaji binafsi, huduma zimegaiwa kwa daraja 3. Na hatà ukichangiya kifurushi wanaita TIMIZA, ambacho ndicho cha juu huduma nyengine hupati hata kama mchango wako ni mkubwa kuliko anavyokatwa muajiriwa.
Kuna vitu wanatakiwa kuboresha
 
Wamesema kwenye kituo kimoja ndani ya mwezi, wakati Kuna watu wanasafiri kila wiki. Na hata hivyo kwa nn mara 3?? Mimi najuaje kamaa nitaumwa mara 4 au 5??
Mleta mada kaleta wakati details hazijakamilika, tusubir mpaka ijumaa tutakuwa tumejua A to Z
 
Hapa ndio wa Tz tunatakiwa tuamke na kuingia barabarani kama ilivyokuwa Srilanka!
tatizo letu wa Tz tu manyangau sana na wazito kuhoji!
Wewe unaona hata akina Mbowe,Lissu,zitto viongozi wa dini na wengine waliojipambanua kuwa wapinzani wa serikali ya awamu ya tano wako busy kumung'unya asali tu hawasemi chochote harafu utegemee mabadiriko hapa nchini kweli?
 
... kero ni nyingi sana kwenye huu mfuko. Unakatwa mshahara wako kwa lazima kulipia NHIF ila kama huna mtoto wa kumzaa huruhusiwi kuweka ndugu (mfano unayemlea); nafasi zako 4 (kama ungekuwa na watoto) zinakuwa zimekwenda bure faida kwa mfuko. Ukiuguliwa na huyo ndugu itakubidi kuingia gharama za matibabu yake ilhali kwenye mfuko una nafasi ambazo hutakiwi kumsajili.

Pili, watoto wote uliokuwa umewasajili wameshavuka 18/21; kwanini mwanachama huyu asipate nafuu ya makato? Badala yake makato yake yanabaki yaleyale. Tatu, badhi ya huduma muhimu zimepunguzwa; ukosefu wa baadhi ya dawa hivyo mhusika kulazimika kuingia mfukoni, n.k.
Vipi kuhusu mzazi??
 
Yaani Mgonjwa Anapangiwa Sehemu Ya Kutibiwa Na Aende Mara Ngapi
Uhuni Ukomeshwe Haraka
 
Nawaunga mkono NHIF, maana Kuna wateja ambao ni wazururaji kwenye vituo vya afya, leo yuko huku, kesho kule , kesho kutwa kule, yaan daily yeye ni kuugua kweli?

Hawa wateja wa namna hii wanatia hasara Sana katika vituo vya afya kwa makosa ya double claiming!

Unakuta katoka kituo A Jana na shida ambayo kesho anakwenda nayo kituo B, na dawa anapewa zilezile, matokeo yake kituo B kinakatwa!

Kwenye hili halihusiani na Mama Samia!


NB: hata hiyo mara 3 kwa mwezi Ni offer nzuri naomba mlio katik utumishi wa umma mpokee hivyo hivyo, maana dawa so chakula, pengine wamefanya hivyo kudhibiti matumizi ya dawa hovyo

HONGERA NHIF KWA KULIONA HILI, hayo mengine simo
Anyway, Bima zibaki hiari.

Watu wachague sehemu ya kupeleka pesa zao.

Easy
 
Wafanyakazi sijui vyama vyenu huwa vinawasaidia nini.....!!?
Kama mazezeta vile.....!!
Haviwezi kuwahamasisha hata;
1) Migomo
2) Maandamano
3) Basi vitetee maslahi yenu...

Vyenyewe vipo kwa ajiri ya kuwakandamiza tu miaka inaenda vilio ni vile vile....
Ivi huwa mna matatizo gani...!!?

Kama ni mfumo au ni Uongozi si muwakatae hata kwa kuandamana....
 
Nimewapigia NHIF
Wamesema ni kweli yanayosemwa mitandaoni

Muda wa Jubilee, Strategies kuanza vuna watu
 
TAARIFA KUHUSU BIMA ZA WAGOJWA KUKATAA KUWA AUTHORISED KWENYE MFUMO

Utaratibu wa mfuko wa NHIF umebadilika ili kuzuia polyvisit za wagonjwa pamoja na polyservices zingine za wagonjwa wetu

Kuanzia sasa mteja atakua na nafasi ya VISIT 3 TU KWA MWEZI kwa kituo husika na mteja hawezi kujiamulia kuhama Kituo cha kutolea huduma(Hosp,H/na disp) moja kwenda nyingine kwa kujiamulia, mfano mgonjwa akianza kutibiwa Kituo X basi atakua wa X tu mpaka pale X tutakapo amua sisi mrefer mgonjwa kwenda sehemu nyingine la sivyo mgonjwa hataweza kwenda sehemu nyingine ,kama kuna emergency kutakua kuna utaratibu kwenye mfumo wa kuruhusu huduma ziendelee

Aidha mfuko utaweka pia utaratibu wa wale wagonjwa ambao ni wa refill ili kama amekuja kwa ajili ya refill asiweze kuchomekea kitu kingine cha kimatibabu

Kwa huduma za physio, meno kutawekwa utaratibu maalumu ili huduma kama hizo ziendelee

Mfuko unataka kubana wale wa watu wanaozunguka kila kituo kufanya vipimo, kuona madaktari na kulinganisha huduma za madaktari

Ni hayo tu ndugu zangu,muwe ka kazi njema.

Watu wa mapokezi mutakua munawaelekeza kwa upole wateja ambao kadi zao zimepata changamoto hizo.

NHIF.
Wafanyakazi ndo wenye pesa huwezi kumuamulia mwenye fedha kutibiwa anakotaka la sivyo serikali iruhusu mifuko mingine ili mchangiaji awe na uhuru wa kuchagua pa kwenda
 
TAARIFA KUHUSU BIMA ZA WAGOJWA KUKATAA KUWA AUTHORISED KWENYE MFUMO

Utaratibu wa mfuko wa NHIF umebadilika ili kuzuia polyvisit za wagonjwa pamoja na polyservices zingine za wagonjwa wetu

Kuanzia sasa mteja atakua na nafasi ya VISIT 3 TU KWA MWEZI kwa kituo husika na mteja hawezi kujiamulia kuhama Kituo cha kutolea huduma(Hosp,H/na disp) moja kwenda nyingine kwa kujiamulia, mfano mgonjwa akianza kutibiwa Kituo X basi atakua wa X tu mpaka pale X tutakapo amua sisi mrefer mgonjwa kwenda sehemu nyingine la sivyo mgonjwa hataweza kwenda sehemu nyingine ,kama kuna emergency kutakua kuna utaratibu kwenye mfumo wa kuruhusu huduma ziendelee

Aidha mfuko utaweka pia utaratibu wa wale wagonjwa ambao ni wa refill ili kama amekuja kwa ajili ya refill asiweze kuchomekea kitu kingine cha kimatibabu

Kwa huduma za physio, meno kutawekwa utaratibu maalumu ili huduma kama hizo ziendelee

Mfuko unataka kubana wale wa watu wanaozunguka kila kituo kufanya vipimo, kuona madaktari na kulinganisha huduma za madaktari

Ni hayo tu ndugu zangu,muwe ka kazi njema.

Watu wa mapokezi mutakua munawaelekeza kwa upole wateja ambao kadi zao zimepata changamoto hizo.

NHIF.
Wafanyakazi ndo wenye pesa huwezi kumuamulia mwenye fedha kutibiwa anakotaka la sivyo serikali iruhusu mifuko mingine ili mchangiaji awe na uhuru wa kuchagua pa kwenda
 
Nawaunga mkono NHIF, maana Kuna wateja ambao ni wazururaji kwenye vituo vya afya, leo yuko huku, kesho kule , kesho kutwa kule, yaan daily yeye ni kuugua kweli?

Hawa wateja wa namna hii wanatia hasara Sana katika vituo vya afya kwa makosa ya double claiming!

Unakuta katoka kituo A Jana na shida ambayo kesho anakwenda nayo kituo B, na dawa anapewa zilezile, matokeo yake kituo B kinakatwa!

Kwenye hili halihusiani na Mama Samia!


NB: hata hiyo mara 3 kwa mwezi Ni offer nzuri naomba mlio katik utumishi wa umma mpokee hivyo hivyo, maana dawa so chakula, pengine wamefanya hivyo kudhibiti matumizi ya dawa hovyo

HONGERA NHIF KWA KULIONA HILI, hayo mengine simo
Kutatua tatizo la mtu mmoja mmoja kwakuumiza wengi wenye huitaji ni ujinga.lakini pia hiyo yawatu kuzunguka kwenye vituo vya afya mbali mbali nikwasababu mtu haridhishwi na aina ya matibabu aliyoyapata kituo A.Mimi kuna mzee namfahamu yuko kwenye matibabu ya cancer ya tumbo sasa hivi na iligundulika baada ya kuhama hospital karibu 4 ya 5 ndo akaambiwa acheki CT scan ndo wakaona tumbo haliko poa.Uko nyuma kote alikopita walikua wanamwambia tu ana vidonda vya tumbo wanamlundika madawa.Kwahiyo angekua nimtu wakuridhika namatibabu aliyokua anayapata siajabu angekufa bila kujua kilichomuua.Watu wenhi magonjwa yao yanakua makubwa kwasababu ya kuridhika na matibabu anayopewa awali hata kama anaona hayaridhishi.Huo mfuko umekosa ubunifu ndo maana wanataka kuja na short cut badala yakufanya maboresho kwa watoa huduma wake.
 
AAR na STRATEGIES wateja wao huwa hawana tabia za kujirudia rudia kwenye vituo vya afya kupata huduma,, ila NHIF leo yupo hapa, kesho pale, kesho kutwa huku, ndyo maana wameamua kuwadhiti, hata wewe jiulize ndugu yangu, mtu hata dose hii hajamaliza kashahamia kwingine, huko nako hajamaliza dose aliyopewa kaenda kwingine, unakuta mtu mmoja kahudhuria mara 10 au zaidi vituo vya afya kwa mwezi!

NSSF wao huo utaratibu wa kutibiwa kituo kimoja tu na mara 3 wanao muda mrefu Sana, wateja wao hawasumbui washazoea.

Kwa Sasa kinachowafavour AAR na STRATEGIES, wao hawanalimit nyingi hasa upande wa dawa na vipimo, kwa hyo unaweza tibiwa vizur ukakaa Zaid ya miezi 3 hospital hupajui!

Ila Kuna viashiria nmeviona juzi juzi ndyo maana nasema Ni suala la muda huko kwao
Kumbe unajua kumbe hizo bima zingine zinatoa matibabu mazuri kwa wanachama wake todauti na Nhif.Tatizo ni aina ya huduma anayopata mgonjwa ndio itakayomfanya atulie.
 
Soma vizur maelezo ndgu, Kuna special Case zinazohitaji clinics , kama hiyo ya shda ya moyo unayozungumzia, kwa hyo utahitajika kahudhuria hapohapo JKCI unapofanyia clinic, lakin kwa mambo madogomadogo kama mafua, kikohozi, malaria, UTI tafuta kituo chako pendwa kimoja TU, in case hali yako Ni mbaya Sana unapewa rufaa, utaratibu sio mgum hata kidogo boss
Unaongea hivyo utafikiri watu wote wanaishi daresalam au watu wamepandwa sehemu moja.Ila pia pamoja na kuchagua unadhani ni vituo vingapi vitapata wagongwa.Kuna ambavyo vitakua na mlundikano wa wagonjwa huku vingine vikiwa vitupu.
 
Back
Top Bottom