Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Nipo Direct sipendi unafiki. Hutaki amua. Nimeshasema sitaki wageni wa ghafla ambao sikujipanga nao. Nina watoto wadogo wananitegemea. Period.

A direct person doesn't switch off his phone, coward is the right name! Direct person respectful says:

  • I apologize, I can't help.
  • Not this time, may be next time.
  • ningejua mapema ningejiandaa
  • Nyumba yangu haitoshi.
  • Naweza kukusiriri siku moja.
  • Nitakusaidia hela ya lodge 1 night.

Huwezi telekeza mtu unayemfaham stand, na ukazima simu halafu uje hapa kungoja tu support ujinga huo sisi.
 
Kinachosikitisha zaidi, ndugu wa mke, wakija haina shida, Ila ndugu wa mume ndo wanalalamikiwa sana, hauwezi kumzimia simu ndugu yako huo ni upumbavu
Ukweli kabisaa, ndugu wa mke huwa hawapatagii tabuuu.

Sitasahau mie nilichofanyiwa, niliondoka mie mdogo wa mke wa Kaka alibakiii. Baadae nilijua kuwa yule ndo ubavu wa Kaka na pale ni kwake ana mamlaka ya nani akae nani asikae.

Mwaka wa 11 huu sijawahi kanyaga tena kwao.
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingia simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.




Mimi walienda kusema nafuja sana pesa badala ya kuwasomesha watoto wao. Mtu kazaa watoto 13 anataka nimsomeshee... Mimi nina 3 tu. Bado wanaenda kusema nakuaje na watoto wachache ... Mwanaume gani. Mke amenikalia kichwani anarudi jioni kama mwanamke. Wanataka wife awafulie nguo zao. Na wanakuwa wakali akirudi awapatie chakula n.k sina hamu na ndugu kabisa.

Mmoja tumekaa naye mwaka mmoja amekuja nimsomeshe diploma. Akirudi toka chuo anaangalia TV mpaka saa 4 akipewa kazi basi za home siku yupo asaidie... Anasema anateswa sana hawezi soma. Nikasubiri likizo. Akaenda kwao kusalimi. Nikamwambia atafute chuo aendelee kusoma huko nitamlipia ada.

Alilia sana anataka arudi Dar. Nlimwambia huku wifi yako atakutesa hutapata muda wa kusoma. Akabembeleza sana nilimkatalia coz alishanipakaza sana kijijini na kumchafua sana wife. Na mtu mwenyewe ni ndugu wa mbali k
# Hata dar mbn ni mikoani
# Wewe una asili ya roho mbaya - wewe mbn ukienda kijijini huwa unafika kwa kila ndugu?
 
Ukweli kabisaa, ndugu wa mke huwa hawapatagii tabuuu.

Sitasahau mie nilichofanyiwa, niliondoka mie mdogo wa mke wa Kaka alibakiii. Baadae nilijua kuwa yule ndo ubavu wa Kaka na pale ni kwake ana mamlaka ya nani akae nani asikae.

Mwaka wa 11 huu sijawahi kanyaga tena kwao.
Unawangojea kwenye kona
 
Soma hapo mwanzo nimesema mara nyingi.
Hata wanaonyang"anya mali za mjane na watoto ni ndugu wa mume sio wa mke.

Mawifi na mama wakwe upande wa mume ndo huwa wakorofi zaidi.
Nakubaliana nawewe, lakini ni rahisi zaidi mwanamke kuwavumili ndugu zake mapungufu Yao kuliko ya ndugu wa mume, ingawa Mara nyingi wanawake waliotoka kwenye maisha ya shida ndo wanakuwaga na roho mbaya sana kwa ndugu wa mume kwasababu ya roho y kimaskini tuu.
 
Umeandika yote kwa usahihi lakini chanzo cha yote ni UMASIKINI NA BAJETI ULIYO NAYO ISIYONYUMBULIKA.

Mtu kuja kwako lazima atoe taarifa hili naunga hoja kwa 100% ndiyo mfumo wa maisha.

Lakini mtu anapokuja bila taarifa ameshakuja tayari, hatuangalii madhaifu ya kuja bila taarifa muda huo tunakabiliana na shida ya kuja kwake bila taarifa.

Mtu msitaarabu na mwenye uwezo na bajeti ya ziada ambaye hayana dhiki na umasikini, atamkaribisha mgeni atampeleka nyumbani, atampa maji,chakula na mengineyo, haijalishi utamlaza sebuleni, kwenye ukumbi wa nyumba, jikoni kwenye korido siku kwanza ipite.

Kukicha au ucku ule ule unamwambia nashukru umekuja lakini ulijisahau kuja bila kuniambia.

Kwangu hakuna nafasi kwa sasa ya kutunza mgeni hatakama nafasi ipo utatumia lugha ya kiutu.

Hivo utakaa hizi cku 3 kwa shida ili tutafute nauli urudi au kama una nauli ya kurudi itabidi urudi siku fulani.

Kama wote hamna nauli hilo sasa ni tatizo ambalo mtajadili kama familia wewe na ndugu zako huko alikotoka kuwa huku hakuna nafasi ya yeye kukaa na wote maisha ni magumu, uzeni mbuzi huko, kuku, bata, njiwa au gunia la mahindi mtume nauli arudi nyumbani.

KUMZIMIA MTU SIMU, KUMKIMBIA STAND NI DALILI ZA UBABAISHAJI, UJANJA UJANJA, UELEWA MDOGO NA UPUUZI.

Pokea simu mwambie ukweli bila kupepesa macho full stop.

Mwisho.

Umasikini ni kitu kibaya sana unaweza kuongozwa na umasikini huo ukahisi uko sahihi maamuzi yako kumbe tu ni umasikini.
Na huu ndio ustaarabu [emoji4]
 
Back
Top Bottom