Hiki kidonda nateseka sana nikienda haja, mwenye kujua dawa ya kuharisha

Asante ndugu yangu, yaaani choo sio kama kigumu kwa sasa. Lakini ni kidonda tu. Maji kwa siku nakunywa lita 3. Yaaani natamani niwe naharisha tu yawe yanapita maji tu
Duh Pole sana aisee! Nenda ufanyiwe upasuaji.
 
Sishauri hili jambo
 
Anal fissures (vertical cuts kwenye anus)
Then umetaja na nyama imetoka nje hio ni hemorrhoids (bawasiri) stage 3 fanya matibabu utakua sawa
Mpendwa hiyo nyama sio ya Bawasiri, nilimuuliza dr ilo linyama ni nini ?? Alinijibu lakini nmesahau, sio vile vinyama vya bawasiri. Vile navijua
 
pole mkuu
 

Kwa mrindo huu acha madokta waendelee kulipwa mishahara mikubwa, hii kazi ngumu kweli kweli!!
 
Wakubwa ahsanteni kwa woote mlionishauri, jana jioni nilirudi tena hospital nikajieleza kama hapa. Nikaandikiwa dawa ya kulainisha choo inaitwa Osmolax, nikaanza kutumia jana ileile kwakweli nashukuru Mungu jana jioni na leo asubuhi nimepuu vizuuri sana, tena jana ndio kabla sijachuchumaa mzigo ukashuka wenyewe Alhamdulilah.. Japokuwa jana nilikunywa hii dawa, nikanywa na mafuta ya mnyonyo kijiko kimoja

Ko saiv nashukuru Mungu hata chooni situmii mda mrefu, yaaani mwanzo nilikuwa nikijisaidia kuna muda unaona kama mabonge mabonge yanatoka afu magumu balaa yaaani likipita maumivu yake ni makali sana, lakini saiv choo kinatoka soft
.
Pia nimeandikiwa nipake anusol cream, pamoja na ile ya kuchomeka kwa ndani
 
Na pia wengine woote naendelea kufanyia kazi ushauri wenu. Kama hapa nimetoka kununua mapapai. Ntakua najitahidi kila siku nile papai
 
Ila sijawahi kupata ugonjwa nikateseka kama hivi jamani tangu nizaliwe, yaaani nimeteseka jamani Kama ni mtihani Mungu kanipa jamani namuomba aniondoshee, au kama kuna sehem nimemkufuru ndio akaamua kuniadhibu basi Allah aniswamehe, yaaani sina raha na maisha, [emoji24]
 
Pole sana .
 
Kibaiolojia baadhi ya magonjwa hasa ya mtindo wa maisha huja kutuongoza turudi kwenye mstari.

Ushauri ni kutafuta kupata maarifa zaidi kuhusu healthy eating. Healthy drinking na mengineyo.

Wala Mungu hatuadhibu, ni vile tu tunapokea ishara na mirejesho ya kipi tunaendelea kufanya maishani. Polee.
 
Habari, Mimi nilikua nasumbuliwa Na constipation, Na kupata Choo kigumu Hadi nikachanika, Sasa kikawa Ni kidonda, Sasa kila nikijisaidia Choo kigumu panazidi kuchanika, nikaenda hospital wakaniambia Ni bawasiri wakanipa suppositories za anusol za kuingiza sehemu ya haja kubwa, lakini wapi, nikatumia vidonge vinaitwa Sitcom Na cream yake kupaka sehemu ya haja kubwa lakini wapi, nikawa nafanya research nikaona Sio bawasiri Bali Ni Anal fissure Sasa sijui nifanyaje? Please nisaidieni maana nikisikia kujisaidia naanza kusali Kwanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…