Hiki ni kiwango kilichopitiliza cha Ukatili kwa watoto

Hiki ni kiwango kilichopitiliza cha Ukatili kwa watoto

Bila kujali kosa la hao watoto hiyo adhabu ni kubwa kwao.

Nawashangaa sana ninyi mnaofananisha dunia ya sasa na hiyo ya miaka ya tisini.

Mfano kosa la uchelewaji, hilo kosa kwa miaka yetu ya giza utakumbushwa kwa viboko, ila siku hizi kuna means nyingi unaweza kuelekezwa zikakufanya ukawahi kuamka/kuwahi jambo fulani.

Hao madogo wamechelewa, mtoto kama huyo kuchelewa madrasa mara nyingi huwa sio kosa lake, kuna mwingine hapo kabeba kapu kabisa ikiwa na maana aidha akitoka hapo au alikotoka huko kahemea ndio kaenda madrasa.

Hivi kweli unashindwa kuicontrol akili ya mtoto hadi umpige, mbona akili yake unaisoma chap tu na kupredict his/her next move.
Wewe baby boomer acha kujifanya Gen Z huyo mtoto wa miaka 9 mpaka 11 kumuelewesha kwa maneno ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.

Mkiwa mnaiga maisha igeni vile vyenye manufaa.Sio kila jambo linalowezekana ULAYA na huku mavumbini lawezekana.

Wenzetu wameandaa mifumo waalimu wamesoma ualimu tena kuna nchi nyingine waalimu wa awali(chekechea) wanamasters sasa huwezi kumfananisha huyo mbobevu na mwalimu ambaye kwanza ameenda kusomea ualimu kama last option.

Pili hana intrest wala hajui makuzi ya watoto yanataka nini na approach zake.Kiuhalisia mnachokitetea kitawezekana kama mtawekeza kwa hao walimu.
 
Tatizo si adhabu bali ni aina, uzito/ukali wa adhabu inayotolewa na umri, afya na uzima wa anayepewa adhabu na uwezo wake wa kuhimili/kupokea adhabu hiyo anayopewa. Lengo liwe kujenga na kurekebisha na sio kumjengea hofu na kumuumiza mpewa adhabu kisaikolojia. Kwa mujibu wa video adhabu inayotolewa ni kali na ni ya nguvu zaidi (Intense) kulinganisha na umri wa watoto wanaonekana wazi kwamba ni wadogo. Hoja ya kwamba kwa kuwa fulani alipigwa sana alipokuwa mtoto hivyo inafaa pia watoto hawa nao wapigwe haina mashiko, hatuwezi kuhalalisha jambo baya leo kwakuwa liliwahi kufanyika huko zamani. Kuna tafiti na shuhuda nyingi mbalimbali zinathibitisha kwamba kuna watoto na watu wazima wengi ambao hawakuwahi kupigwa viboko au adhabu kama hizo, na bado wamekuja kuwa raia wema wenye tija kubwa kwenye jamii. Hivyo mtoto kupewa sana au kupewa adhabu kali, sio halalisho la kwamba eti atakuwa mtu mwema huko baadaye, sana sana atakuwa anajengewa hofu na kuumizwa kiakili badala ya kumrekebisha.
 
Mtu wa bikira 72.............anagawa dozi bila kujali utadhani yeye huwa akosei...........shame on kobazz unapata wapi ujasiri wa kupiga mtoto wa mtu hivyo?? Je ndio maelekezo ya dini ?? Mwanangu ukimpiga hivyo naweza kupata kesi ya kudhuru bila kuua maana utachezea ambakati mpaka kanzu igeuke dela...........
 
Wewe acha kujifanya Gen Z wakati ni millenia au baby boomer😀😀😀

Enzi zetu unachapwa mbaya mbovu na hakuna mahali utashtaki.

Huu mmomonyoko wa maadili umeletwa na vilaza wanaofake maisha ya ulaya wakati mifumo yenu ni ya kimbwambwa.Acheni kutetea ujinga hauwafanyi kuonekana mnaakili ila mapunguani.
Hakuna anaejifanya gen Z, zuia ukatili kwa watoto. ( hizo Gen Z sijui baby boomers ni za wamarekani kijana, hatuna hizo hapa kwetu, unawaiga huku hutaki kuwaiga)

Hao machalii hamna unalowafunza kwa viboko zaidi ya kuwatia hofu tu.
Na ndio maana wakifika umri fulani huwa wanakimbia madrasa. Hao madogo wakiacha kufatiliwa kidogo tu basi hawaendi tena.

Dogo chini ya miaka 10 unamlamba mboko za kiutu uzima hizo, sio sawa.

Kama kwenu mlikua mnadundwa namna hiyo, mkuu pole sana.
 
Hakuna anaejifanya gen Z, zuia ukatili kwa watoto. ( hizo Gen Z sijui baby boomers ni za wamarekani kijana, hatuna hizo hapa kwetu, unawaiga huku hutaki kuwaiga)

Hao machalii hamna unalowafunza kwa viboko zaidi ya kuwatia hofu tu.
Na ndio maana wakifika umri fulani huwa wanakimbia madrasa. Hao madogo wakiacha kufatiliwa kidogo tu basi hawaendi tena.

Dogo chini ya miaka 10 unamlamba mboko za kiutu uzima hizo, sio sawa.

Kama kwenu mlikua mnadundwa namna hiyo, mkuu pole sana.
hapo ukatili upo wapi???

Onyesha ukatili kwanza acha mbambamba.
 
Hakuna anaejifanya gen Z, zuia ukatili kwa watoto. ( hizo Gen Z sijui baby boomers ni za wamarekani kijana, hatuna hizo hapa kwetu, unawaiga huku hutaki kuwaiga)

Hao machalii hamna unalowafunza kwa viboko zaidi ya kuwatia hofu tu.
Na ndio maana wakifika umri fulani huwa wanakimbia madrasa. Hao madogo wakiacha kufatiliwa kidogo tu basi hawaendi tena.

Dogo chini ya miaka 10 unamlamba mboko za kiutu uzima hizo, sio sawa.

Kama kwenu mlikua mnadundwa namna hiyo, mkuu pole sana.
Sasa hapo wakiachwa kuchapwa kesho yake madrsa wataenda muda wa kutoka.Ustadhi umlipe miamia na mtoto akufundishie sawa na bure bado unachonga mdomo kwa matatizo ya ukosefu wa adabu na malezi ya mitoto yenu.

📌📌📌Ifike mahali maustadhi waanze kutoza mpaka 50k kwa kichwa kwa mwezi ili kupata watoto sahihi hao watoto wenu mnaowaabudu mkawafundishe wenyewe majumbani mwenu.
 
hapo ukatili upo wapi???

Onyesha ukatili kwanza acha mbambamba.
Aina ya adhabu Vs umri wa watoto bila kujali kosa lao.

Hao ukiwalamba mbilimbili tu za fasta fasta na onyo kali kesho anawahi, sio bakora 5 mpaka dogo anapiga kelele ka anauawa vile.

Kipindi hiki cha utandawazi fimbo sio suluhu kama zamani, unaweza kuchapa kama hivyo ukatengenezewa zengwe ukatupwa lupango, nenda na wakati kijana, haukusubiri.
 
Kuna shule ya ipo karibu yangu hapa madogo wanakula sana mboko, sasa imagine dogo kala mboko skuli, kafika home msosi hakuna, anawahi madrasa huko nako anakutana na bakora 5 za moto.

Huyu akija kua kibaka kukutia bisu hataona kazi dadeki.
Ni ukatili ambao unamjengea mtoto effect atakuja kuona baadae akikua fimbo sio sawa
 
Mbona hapo hamna ukatili mnataka kila mtu alee mtoto kama mnavyolea mitoto yenu inaishia kuwa mishoga na mi malaya inayozalia nyumbani.

📌Samaki anakunjwa akiwa mbichi.!
Mbona hapo ndo wanapozalishwaga mashoga
 
Ushauri kwa maostadhi wafukuzie mbali mitoto isiyotaka kufata taratibu za kusoma.Ili kujiepusha na kero za wazazi wanaoabudu watoto wao.Fukuza tu kama seminari.Wengine lazima wawe kafari hatuwezi kufika wote.

Waongeze kiwango cha ada ili kuchuja mchele na mashudu.Kukiwa na kiwango cha maana wanacholipia wazazi itasaidia watoto na wazazi wao waelewe umuhimu wa elimu hiyo tofauti na sasa madrasa imegeuzwa kama sehemu ya kwenda kupotezea muda na kukua.

Watoto wazito na wenye vichwa vigumu fukuzia mbali maana hawa ndo huwa bila mboko hawaelewi.Hii itasaidia kujiepusha na kelele na matatizo yasiyo na msingi.
 
Sasa hapo wakiachwa kuchapwa kesho yake madrsa wataenda muda wa kutoka.Ustadhi umlipe miamia na mtoto akufundishie sawa na bure bado unachonga mdomo kwa matatizo ya ukosefu wa adabu na malezi ya mitoto yenu.

📌📌📌Ifike mahali maustadhi waanze kutoza mpaka 50k kwa kichwa kwa mwezi ili kupata watoto sahihi hao watoto wenu mnaowaabudu mkawafundishe wenyewe majumbani mwenu.
Ishu sio kutochapwa au kutopewa adhabu, hata huko ulaya unakosema tunaiga hata wao wanatoa adhabu japo sio viboko kama huku kwetu.

Sasa kwenye hizo adhabu angalia na hali ya mwanao sio kila mmoja anazimudu, hapo ukimchana kiganja mtoto utawaambia nini waja wakuelewe, hata kama ulikua unafanya jema kumnyoosha hamna ataekuelewa.

Uliona clip ya yule binti aliekua anamkung'uta mwanae?? Nae alirekodiwa akatiwa lupango, uliona clip ya walimu wa shule ya Mbeya wakimpa kipigo yule dogo mtukutu, nao walipoteza kazi zao.

Sasa kama hujifunzi kwayo, ulimwengu utakupa somo na kukuelekeza ni adhabu gani unapaswa kumpa mwanao na zipi unapaswa kupewa wewe na sio mwanao.
 
Tulichambue Jambo Hili Bila kudhihirisha chuki au Mapenzi Yetu katika Dini Zetu.

Ukatili Ni nini?? Unaweza Kutafsiri ukatili kuwa ni kila Adhabu ya Viboko anayopewa Mtoto??
Au ukatili unapimwa kwa reaction ya mfanyiwaji bila kuangalia aina ya adhabu na Ukubwa wake??


Basi sisi kama wazazi wote ni wakatili Sisi Tunawaadhibu watoto wetu Kwa bakora zaidi ya Hivyo.

Huyo mwalimu Ametoa Adhabu ya Bakora za Mikononi ##Tano hadi Sita kwa Kila mwanafunzi (Hatujui kosa ni Nini labda tungejua kosa gani wamefanya Hao watoto labda tungeiona hiyo adhabu kuwa ni Ya kawaida tuu.

Shule za Serikali na binafsi adhabu ya Viboko bado ipo tena wanafunzi wanapigwa kwelikweli.

Nakumbuka nikiwa Shule Mwalimu alikuwa anaweza kumuadhibu mwanafunzi hadi bakora 20 yes 20 na ni kawaida tuu kwa walimu wa shule za Serikali sisemi ni sawa lakini Ni namna ya njia ya Kuwanyoosha Vijana iliyochaguliwa na Wahusika.

Ikiwa ni Hivyo jee Suala ya Bakora 5 au sita tena za Mkononi sehemu Salama kabisa itafsiriwe ni Ukatili!!! Labda kama tunataka kuwalea Watoto wetu kizungu alafu baade waje watushitaki ukimkalipia au ukimfokea kama walivyo watoto wa kizungu nowdays.

Jee tunataka tufike huko???
Ukatili ni kitendo anacho fanyiwa mtu bila lidhaa yake na kumletea sonona au mfadhaiko

Adhabu zinategemeana na umri wa mtoto uyo mtoto na fimbo anayo mpigia unaona nisawa?

Kuna namna ya kumuadhibu mtoto pindi anapokesea mkuu na sio ivyo anavyo fanya uyo mwalimu
 
Back
Top Bottom