Hili la kuweka vibao viwili Kwa Nchi Moja Tanzania na Zanzibar limekaaje?

Mwakani ataondoka msiwe na shaka yote yataisha CCM ni chama makini sana, haya hayajawahi kutokea hapo kabla
 
Nilipo sema Samia amekuja kuimaliza Tanzania, sikukosea hata neno moja.
Lililobaki sasa akamilishe kazi ya kuiua CCM, hapo atakuwa amejijengea 'legacy' ya kipekee kabisa.
 
Labda umaarufu wa urojo! Ka nchi maskini kuliko hata mkoa wa Lindi! Nje ya muungano Zanzibar watakufa njaa!
Inawezekana pia, ila swali dogo tu,

zenji wanataka kuvunja muungano, sasa kwanini bara wanaulazimisha? Hapo tu,
Nikieleweshwa hapa tu basi kweli nitaamini zenji wanaenda kufa njaa
 
Inawezekana pia, ila swali dogo tu,

zenji wanataka kuvunja muungano, sasa kwanini bara wanaulazimisha? Hapo tu,
Nikieleweshwa hapa tu basi kweli nitaamini zenji wanaenda kufa njaa
Viongozi ndio watuambie wana maslahinganinna Zanzibar! Hakuna mwananchi wa kawaida anautaka huo muungano.
 
Pascal Mayalla unasemaje hapa?
 
Huyu bibie (Mama Samia Suluhu Hassan), Mzanzibari na Kaimu Rais wa Tanganyika, anashindwa nini kutumia mamlaka yake ya U - Rais kuamuru mchakato wa kukamilisha uandaaji wa katiba mpya kuendelea...?

Iweje anataka kusababisha sintofahamu isiyo na sababu kwa kukiuka na kuvunja katiba kwa kuipa Zanzibar vitu na mambo yasiyokuwepo ktk makubaliano ya muungano kwa kupitia mlango wa nyuma wakati ana fursa ya kuyafanya kuwa halali kikatiba...?

Awape Zanzibar mamlaka kamili. Na sisi Watanganganyika tunataka Tanganyika yetu irudi haraka sana kutoka huko ambako CCM imeificha....!!
 
Sasa ni wakati mzuri WA kutekeleza riporti ya Nyalali, Kisanga na ya Warioba juu ya Muungano, WA Sirikali,3 , Mbili za Wanaoungana yaani ya Tanganyika (Tanzania Bara) ya Tanzania Visiwani (Zanzibar) na ya Muungano.
 
Hivi ni vitu vidogo, kuna nchi nyingi kabla ya Muungano zilikuwa na ubalozi Tanganyika na ubalozi Zanzibar, baada ya Muungano, nyingi zilifunga balòzi zake za Zanzibar na kubaki za Tanganyika zilizogeuka za Tanzania, miongoni mwa nchi ambazo hazikufunga ubalozi wake Zanzibar ni pamoja na yale mataifa makubwa matano yenye veto UN, Marekani, Urusi, Uingereza, Ufaransa na China, India pia haikufunga, bali walizigeuza balozi hizo kuwa balozi ndogo. Nchi hizi zinai treat Zanzibar with a special treatment of autonomous, hivyo wakitoa mualiko Tanzania inàalikwa kama nchi Tanzania na Zanzibar inaalikwa kama autonomous part of Tanzania hivyo kila mtu na mwaliko wake na kibao chake, bali Tanzania kama nchi ni nchi moja tuu, JMT!.
P
 
Ni suala la muda tu Zanzibar itakuja kujitenga, Unajua why SSH anamkubali lissu sababu lissu haungi muungano wa kitapeli huu hata mama yenu pia hakubali huu muungano coz upo kihuni kihuni.
 
Sawa nchi ni moja kaka, heshima kwako.
Kwa maoni yako kwa nini chetu ni chao na chao ni chao, mfano ajira na kumiliki Ardhi.
 









US au UK wanaye balozi kamili anayewakilisha nchi yao huko zanzibar?
 
Sawa nchi ni moja kaka, heshima kwako.
Kwa maoni yako kwa nini chetu ni chao na chao ni chao, mfano ajira na kumiliki Ardhi.
Sababu ni moja tuu, they are the minority!. Muungano ni wa nchi mbili zenye equal status, kuungana na kuunda nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa Tanzania, kwa vile Tanganyika ni giant na Zanzibar ni minutes, itaonekana kama Zanzibar imemezwa na Tanganyika, Tanganyika ni the majority na Zanzibar ni the minority, Mwalimu Nyerere akaamua Tanganyika ndio ife, Zanzibar ibaki with its internal autonomous.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…