Hili la wamachinga kurudi kwenye maeneo waliyoondolewa, wasaidizi wa Rais Samia wajitafakari sana

Hili la wamachinga kurudi kwenye maeneo waliyoondolewa, wasaidizi wa Rais Samia wajitafakari sana

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Ni muda kidogo sasa tangu kutekelezwa kwa agizo la kuwaondoa Wamachinga maeneo ya katikati mwa majiji na miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Arusha kwa lengo la kuwapanga vizuri lakini pia kuyaweka maeneo hayo katika hali ya usafi.

Habari mbaya ni kwamba katika maeneo mengi wafanyabiashara hao wamesharejea na wanafanya biashara kama zamani tu. Maeneo ya stendi, chini ya mti, Kilombero n.k jijini Arusha, Dar maeneo karibu yote kuanzia Mwenge hadi Kariakoo, Mwanza nako maeneo ya katikati ya Jiji hali ni kama zamani tu.

Maeneo yote haya yana viongozi lakini kama kawaidia wanafanya kazi kwa mazoea, wanasubiri kufanya kazi kwa zimamoto, wanasubiri ziara ya Rais ikaribie ndipo wafanye majukumu yao.

Hawa ni viongozi mzigo, wanaopaswa kujitafakari na kujipima.

wamachinga-pic-data.jpeg
 
Magufuli angepata muda zaidi ndiyo angeweza kudeal na hii biashara maana alikuwa na roho ngumu inayohitajika kutatua suala hili. Alikuwa anawalia timing tu ingawa ulikuwa mtaji wake wa kisiasa.
 
Amos Makala kesho utamuona na miwani zake zile nyeusi. Jamaa huwa anapiga miwani ya jua hata akiwa kwenye mwanga hafifu. Kifupi Jiji limemzidi uwezo kabaki kuwa propagandist hata usafi tuu umemshinda. Nimepita juzi juzi mitaa ya mabibo sokoni. Hopeless
 
Wengine tulijua ilikuwa propaganda tu wamachinga kuondoka kwa HIARI wakati miaka yote huondolewa kwa mabomu.
 
Mtoa mada unaweza ukaongea kwa nafsi yako ni sawa, lakini kiuhalisia hali ya machinga nje ya maeneo yao waliyoyaanzisha wenyewe ni ngumu sawa na watu wamekata mitaji balaa, ndoa zimevunjika na mambo mengine mengi. ila kwa sababu tunatofautiana utafutaji unaweza walaumu machinga na kuona ni uchafu mjini... lakini nakuhakikishia, ingawa wanaonekana kpata shida ni machinga ila hata watu wenye uwezo mdogo wa manunuzi nao wamepata shoida sana ni kwa vile hakua umoja wa wateja wa wamachinga ndio ungesikia shida wanazopata waniunuzi pia.

Unaweza ukawa unajua iala natka nikukumbushe, biashara ni location na sio kila sehemu au location ni rafiki kwa kil biashara, machinga wengi kwenye yale maeneo walikuwa wamepatia location ndio maana ulikuwa ukiwaona wanatoboa na kushusha marobota kila siku.. sasa hivi niambie ni nani anashusha robota kama zamani.
kwa wale wanaoishi kisesa mwanza ndio wanajua...

Toka watu waondolewe pale jiwe la mkapa na kupelekwa kona ya kayenze watu wamekata mitaji na kule kona biashara mwisho saa tatu asubuhu kama hadi mda huo haujauza mzunguko unakata we tafuta sehemu ukalale tu. ndio maana wanalazimisha kuja stand ya magu huku juu.
 
Ni muda kidogo sasa tangu kutekelezwa kwa agizo la kuwaondoa Wamachinga maeneo ya katikati mwa majiji na miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Arusha kwa lengo la kuwapanga vizuri lakini pia kuyaweka maeneo hayo katika hali ya usafi.

Habari mbaya ni kwamba katika maeneo mengi wafanyabiashara hao wamesharejea na wanafanya biashara kama zamani tu. Maeneo ya stendi, chini ya mti, Kilombero n.k jijini Arusha, Dar maeneo karibu yote kuanzia Mwenge hadi Kariakoo, Mwanza nako maeneo ya katikati ya Jiji hali ni kama zamani tu.

Maeneo yote haya yana viongozi lakini kama kawaidia wanafanya kazi kwa mazoea, wanasubiri kufanya kazi kwa zimamoto, wanasubiri ziara ya Rais ikaribie ndipo wafanye majukumu yao.

Hawa ni viongozi mzigo, wanaopaswa kujitafakari na kujipimaView attachment 2337449
Ukweli ni kwamba machinga hufuata wateja,njia pekee ya kukabiliana na machinga ni kujenga miundombinu ambayo ita accommodate biashara zao na hapa lazima watu wa mipango miji na wajenzi wa Barabara lazima waanze kufanya hili..

Swala la kuwapeleka sijui wapi wakati wao wanafuata wateja ni uongo.
 
Back
Top Bottom