Hili suala la wanafunzi kubaki shule lina umuhimu mkubwa kwa maisha ya baadaye ya mtoto wako

Hili suala la wanafunzi kubaki shule lina umuhimu mkubwa kwa maisha ya baadaye ya mtoto wako

I don't get your point here!!

Yaani naamanisha kuwa, logic yako ni nini hasa hapa?

Je, una maana kuwa kusiwe na likizo za watoto/wanafunzi kupumzika, bali mwaka mzima wawe darasani wanafundishwaga na kusomaga tu?

Je, kwa akili na mtazamo wako unadhani kwa kufanya hivi ndo wataelimika (sio kufaulu tu), au siyo?

Vipi walimu? Nao wasipumzike? Wafundishe mwaka mzima?

Aaah aaah, you are very wrong my friend..!!

Au hujui kuwa mitaala iko designed in such away kwamba Ina specific time ya kukamilishwa?

Nikuambie tu kuwa, tatizo la elimu yetu hapa Tanzania halipo kwa watoto wawe na likizo ama wasiwe na likizo ya kupumzika...!!

Tatizo la elimu yetu lipo kwenye kwenye maeneo haya;

1. Uduni wa mazingira ya kujifunza na kujifunzia katika shule za umma karibu zote..

2. Uhaba wa vifaa kama vitabu, science labs ambazo ziko equiped na vifaa katika shule nyingi za umma..

3. Ubora wa walimu wetu, wengi wao wako chini ya kiwango ( most of them are incompetent)..?

4. Kwa upande wa walimu tena, ni kuwa, hata hao wachache waliopo ambao ni competent, wanakosa kitu kinachoitwa "motivation" Kwa sababu ya mazingira mabaya ya kazi, maslahi duni na changamoto zingine..

5. Changamoto ya lugha ya kufundishia na kujifunzia nalo ni tatizo kubwa...

6. Udogo wa budget ktk sekta ya elimu ni tatizo kuwa zaidi..

##Haya baadhi na mengine mengi ndiyo matatizo ya elimu ya nchi hii.

Hiki unachokijadili hapa ni matokeo tu ya matatizo ya msingi..

If we want to solve these problems permanently, let's go to the roots of the problem..!!

Moja ya solution ni kuhakikisha kuwa tuna invest heavily kwenye sekta ya elimu. Kutofanya hivi tutakuwa tunapiga kelele za "ufaulu" tu badala ya kutaka watoto wetu wapate "elimu bora" au "quality education!!"

Thank you.
Ni kweli kabisa walimu wengi wanadai stahili zao mfano malimbikizo ya mishahara ya tangu 2017 hayajalipwa kwa asilimia kubwa licha ya kupangiwa bajeti kila mwaka ila uidhinishaji wa malipo hayo kimekuwa kizungumkuti kwa mingi kilichoshuhudiwa ni propaganda za akina Lucas Mwashambwa za kusema serikali ya mh Samia imewafuta walimu sijui machozi kwa kuwalipa hizo arrears walimu wote.Walimu wapo wachache waliolipwa ila ni wale waliokuwa wanadai vilaki kadhaa wanaodai milioni 2 hadi 4 kwa sababu ya kuchelewa kubadilisha mishahara yao baada ya kupanda vyeo kwa zaidi ya miezi 15 hadi 20 plus hamna kitu kila mwezi.Lipeni hao walimu ili kuinua kiwango cha elimu kwa walimu kufanya kazi bila vinyongo mioyoni
 
Nashukuru kwa kunikosoa hapo juu.
Kwahiyo mkuu unataka kusema wanafunzi hao awapumziki?
Kuna mapumziko ya kila siku, kila juma,mwezi wa nne na baada ya mitihani.Mfano waliomaliza kidato cha nne mwaka jana mwezi wa Novemba mpaka leo wapo nyumbani takribani miezi nane.
Shule na wazazi waliokubali watoto wao kuendelea na masomo wako sawa in haki yao. Utafiti unaosema ninao uhakika wala ujui. Vijana waendelee na masomo tu ili waweze kufauru na kuendelea na masomo ya juu...
Wizara iachane kuangaika na vitu vidogo wakati kuna mambo makubwa kwenye in changamoto.
Nyumba za walimu,umeme,vyoo,usafiri,chakula,vitabu nk
Pengine hujui! Vipindi, mihula, masomo na livu zote zinapangwa na wataalam wa elimu! Narudia tena: masomo na likizo hupangwa na wataalam waliosomea. Iwapo inafuatwa kama inavyotakiwa, basi hakuna ulazima wowote wa kufundisha muda wa likizo. Ni kama unavyokwenda kwa daktari, yeye ndiye mtaalam na hukupangia muda na aina ya dawa utakazotumia. Pengine bado hujabahatika kutoka nje ya nchi na kuona elimu za nchi nyingine zinazoendeshwa. Likizo ni sehemu ya ratiba ya masomo na ni lazima ifuatwe. Wenzetu wamekwenda mbali zaidi mpaka wakati wa likizo kuna entertainment huwa wanafunzi wanapewa ili ku-refresh mind!
 
Pengine hujui! Vipindi, mihula, masomo na livu zote zinapangwa na wataalam wa elimu! Narudia tena: masomo na likizo hupangwa na wataalam waliosomea. Iwapo inafuatwa kama inavyotakiwa, basi hakuna ulazima wowote wa kufundisha muda wa likizo. Ni kama unavyokwenda kwa daktari, yeye ndiye mtaalam na hukupangia muda na aina ya dawa utakazotumia. Pengine bado hujabahatika kutoka nje ya nchi na kuona elimu za nchi nyingine zinazoendeshwa. Likizo ni sehemu ya ratiba ya masomo na ni lazima ifuatwe. Wenzetu wamekwenda mbali zaidi mpaka wakati wa likizo kuna entertainment huwa wanafunzi wanapewa ili ku-refresh mind!
Kwenda nje nakuelewa ni vitu tofauti ndugu.Ukisema kua wataalam wamefanya maamuzi sijui kama kweli unajua kua ata theories au principles mbalimbali mara zote ukutwa na mapungu basi ndiyo maana hamna utafiti au principle iliyo absolute. Mfano mimi shule yangu kuna upungufu wa walimu wa masomo ya Fizikia,Kemia na Hesabu na mara zote nimekua nikitumia walimu kwa kuazima shule za jirani. Ukifika muda wa likizo shuleni kwangu madarasa ya mitihani atufungi likizo ndefu asa ya mwezi wa sita ili kuweza kuwatumia walimu walioko likizo kuendelea kuwanoa wanafunzi wangu ili kumaliza sylabus. Je,hapo kuna shida gani?
Alafu nyie mnaojifanya kusoma au kwenda nje eti watoto wa huko muda huo ufanya refreshment nk kwahiyo nasisi iwe hivyo. Huu naweza kusema ni ujinga maana yake hamjui kua malengo ,sera,mazingira,mahitaji ya elimu ni tofauti kati ya nchi na nchi. Atuwezi kuendesha elimu yetu kama Finland au Marekani wakati mifumo na mahitaji yetu ni tofauti.
MKIPATA NAFASI YA KWENDA NJE KUSOMA AU KUTEMBEA ACHANE TABIA ZA COPY AND PASTE....Isitoshe ndiyo hayo hayo mnakuja kupigia chepuo ata ushoga kisa mmeona huko nchi za Ulaya au Marekani wanaona ni kawaida.
 
Mtu mwenye nia ya kufaulu atafaulu tu na asiye na nia ya kufaulu kitakachotokea lazima kitokee. Taratibu zote lazima zifuatwe. Serikali yenyewe badala ya kuwekeza kwenye vyanzo vya ajira, vitega uchumi na kurahisisha mazingira ya biashara kwa vijana badala yake inakwenda kutupa hela kwenye Mpira. Unadhani mwanafunzi atakuwa tena na nia ya kusoma zaidi ya kutegemea kuchzeza mpira?... Pumbavu kabisa!
 
Mtu mwenye nia ya kufaulu atafaulu tu na asiye na nia ya kufaulu kitakachotokea lazima kitokee. Taratibu zote lazima zifuatwe. Serikali yenyewe badala ya kuwekeza kwenye vyanzo vya ajira, vitega uchumi na kurahisisha mazingira ya biashara kwa vijana badala yake inakwenda kutupa hela kwenye Mpira. Unadhani mwanafunzi atakuwa tena na nia ya kusoma zaidi ya kutegemea kuchzeza mpira?... Pumbavu kabisa!
Punguza hasira
 
Kwenda nje nakuelewa ni vitu tofauti ndugu.Ukisema kua wataalam wamefanya maamuzi sijui kama kweli unajua kua ata theories au principles mbalimbali mara zote ukutwa na mapungu basi ndiyo maana hamna utafiti au principle iliyo absolute. Mfano mimi shule yangu kuna upungufu wa walimu wa masomo ya Fizikia,Kemia na Hesabu na mara zote nimekua nikitumia walimu kwa kuazima shule za jirani. Ukifika muda wa likizo shuleni kwangu madarasa ya mitihani atufungi likizo ndefu asa ya mwezi wa sita ili kuweza kuwatumia walimu walioko likizo kuendelea kuwanoa wanafunzi wangu ili kumaliza sylabus. Je,hapo kuna shida gani?
Alafu nyie mnaojifanya kusoma au kwenda nje eti watoto wa huko muda huo ufanya refreshment nk kwahiyo nasisi iwe hivyo. Huu naweza kusema ni ujinga maana yake hamjui kua malengo ,sera,mazingira,mahitaji ya elimu ni tofauti kati ya nchi na nchi. Atuwezi kuendesha elimu yetu kama Finland au Marekani wakati mifumo na mahitaji yetu ni tofauti.
MKIPATA NAFASI YA KWENDA NJE KUSOMA AU KUTEMBEA ACHANE TABIA ZA COPY AND PASTE....Isitoshe ndiyo hayo hayo mnakuja kupigia chepuo ata ushoga kisa mmeona huko nchi za Ulaya au Marekani wanaona ni kawaida.
Wewe ni mzinga wa countrybumpkin! Bado unaishi zile enzi za miaka ya 1960. Na huenda umesoma kwenye mazingira haya ya kusoteshwa kwenye kukariri na kutopata likizo za kutosha ndiyo maana hata kuandika maneno ya kiswahili rahisi kabisa hujui. Wewe ni mfano wa matokeo ya mfumo mbovu wa elimu unaodhani ndiyo unafaa. Kuhusu upungufu wa waalim hilo nalijua sana ila ni tatizo linalotakiwa kutatuliwa kwa kuongeza waalim na siyo kuongeza tatizo. Ukim-overwork mwanafunzi unatengeneza matatizo mengine na hutapata matokeo chanya.
 
Wewe ni mzinga wa countrybumpkin! Bado unaishi zile enzi za miaka ya 1960. Na huenda umesoma kwenye mazingira haya ya kusoteshwa kwenye kukariri na kutopata likizo za kutosha ndiyo maana hata kuandika maneno ya kiswahili rahisi kabisa hujui. Wewe ni mfano wa matokeo ya mfumo mbovu wa elimu unaodhani ndiyo unafaa. Kuhusu upungufu wa waalim hilo nalijua sana ila ni tatizo linalotakiwa kutatuliwa kwa kuongeza waalim na siyo kuongeza tatizo. Ukim-overwork mwanafunzi unatengeneza matatizo mengine na hutapata matokeo chanya.
Umeandika ujinga hakuna mwelevu wakusoma tena upupu kama huu
 
Wewe ni mzinga wa countrybumpkin! Bado unaishi zile enzi za miaka ya 1960. Na huenda umesoma kwenye mazingira haya ya kusoteshwa kwenye kukariri na kutopata likizo za kutosha ndiyo maana hata kuandika maneno ya kiswahili rahisi kabisa hujui. Wewe ni mfano wa matokeo ya mfumo mbovu wa elimu unaodhani ndiyo unafaa. Kuhusu upungufu wa waalim hilo nalijua sana ila ni tatizo linalotakiwa kutatuliwa kwa kuongeza waalim na siyo kuongeza tatizo. Ukim-overwork mwanafunzi unatengeneza matatizo mengine na hutapata matokeo chanya.
mzinga tena?Daah pole yako...waacheni vijana waendelee kunolewa baada ya siku watapumzika miezi takribani minane
 
Halafu wewe inawezekana ni mwalimu wakati kuandika maneno rahisi kabisa ya kiswahili huwezi . Hao wanafunzi unaofundisha watakuwa mazuzu zaidi yako!
Okay,sijaona maana ya andiko lako kuliko kujikita kwenye mada.Pia wanafunzi wangu walisha maliza masomo mwaka 1985 pale UDSM
 
Wazazi mwanao kama yupo form four, aendelee kusoma na kujisomea, haya matamko ya wanasiasa ni matamko ya kisiasa.

Wewe mwanao yupo shule ya kata, na unajua kuwa ili aweze kupata nafasi ya kwenda hata VETA au kuongeza ujuzi wowote basi cheti cha Form four lazima.

So akili kichwani, yaani mzazi unakaa na kusubiri future ya mwanao ambaye yupo shule ya kata iliandaliwe na waziri!

Mwanao akipata zero hata upolisi hawamchukui na huko mtaani ndio kizazi cha singeli hiki, pathetic.

Nimeandika maana nipo uswahilini De es Salaam, nimeona watoto wa kike na kiume wakikaa mtaani wanaishia kupoteza mwelekeo huku mtaani, hakuna mzazi makini wakumpa malezi bora mwanae.
Likizo iheshimiwe maana ndio muda wa watoto kupumzika
 
kama Mimi nilisoma saint kayumba na nikafaulu vizuri na Kila likizo nilikua naludi nyumbani sihitaji mtoto wangu abaki shule likizo. Hawa watoto wanaoshinda boarding tutajenga nao bond lini sisi wazazi. tumeweka ufaulu mbele sana. Kuna maisha baada ya A za darasani.
Mkuu maana watoto wako ni kama wewe?
 
Likizo muhimu ili mtoto apumzishe akili na mzazi uweze kumuelewa mtoto wako katika makuzi yake. Siyo unamuachia mwalimu na Matron ndiyo mlezi mwanao kuanzia Jan up to late June.
 
Back
Top Bottom