Hili suala la wanafunzi kubaki shule lina umuhimu mkubwa kwa maisha ya baadaye ya mtoto wako

Hili suala la wanafunzi kubaki shule lina umuhimu mkubwa kwa maisha ya baadaye ya mtoto wako

Kusoma na kwrnda tour kuna fanana kumbe? Sema wazazi wana kwepa majukumu wanatamani hata watoto waishi shulieni milele wao wawe wanatuma tu Ada na Pokey money
Wakati nasoma miaka ya 90 nikiwa kidato Cha nne likizo nilikuwa naenda shule na mchana nikitoka naenda kufanya kibarua nipate ada na mahitaji mengine. Sasa huu ni mfumo wa tangu zamani kubakiza madarasa ya mitihani maana ndo fainali unalalaje? Yaani ni kama YANGA eti kipindi hiki wapo fainali wanasaka kombe mchezaji aombe likizo inawekana kweli? Hao watoto mwezi wa kumi na moja, kumi na mbili watakuwa nyumbani huko lakini watumie muda huu kuandaa form three na form five ya mwakani
 
Ujinga haya ni majukumu ya Wazazi, Watoto w Kihindi wao mbona hawapato Mimba? Wazazi wa Kibongo ni wapuuzi sana yaani wanakwepa majukumu ya kulea familia na wamekomaa kusakazia wati wengine,
Wazaz tuko busy kutafuta pesa, baba mhandisi, mama mhasibu, wote wanatoka asubuhi mtoto yupo likizo kaachiwa ps5 mpyaaa ili acheze games, jioni kuna tamthilia mwisho wa siku toto linarudi shule likiwa na ratiba zote za vipindi vya tamthilia za azam, muulize hata definition ya geography hajui
 
Ujinga haya ni majukumu ya Wazazi, Watoto w Kihindi wao mbona hawapato Mimba? Wazazi wa Kibongo ni wapuuzi sana yaani wanakwepa majukumu ya kulea familia na wamekomaa kusakazia wati wengine,
Unaweza ukaongea hapa kama mzazi Bora kumbe wewe ndo umetelekeza mtoto kule Arusha unakula maisha huko Mbeya hutaki kutoa hata mia kwa mtoto, analelewa na kusaidiwa na walimu. Hii kada ya elimu na malezi kama hujui Chochote Bora ukae kimya. Don't generalize parents. Kuna waliokwepa majukumu Yao wametelekeza watoto mashuleni wanalelewa na walimu, hivyo walimu wanawakazania ili angalau elimu iwakonboe wasipate machungu ya kutelekezwa
 
Mkuu sisi enzi zetu ikifika lilizo tulikuwa tunaruhusiwa kwenda nyumbani lakini tulifaulu masomo vizuri. Walimu hakikisheni mnakwenda na syllubus vizuri na kwa wakati! Lakini kwa habari ya Afya watoto waruhusiwe kupumuzika.
Elimu ya zamani ilikuwa inafaulisha mtoto 1 kati ya watoto 100 kutoka elimu ya msingi kwenda elimu ya secondari tofauti na Sasa idadi kubwa ya watoto wanaomaliza elimu ya msingi wanafaulu kwenda sekondari yani kati ya watoto 100 basi 5 watafeli na hao 95 watafaulu na
kuendelea na masomo ya sekondari hivo hapa tunapata picha ya kwamba mchujo uliokua ukifanyika zamani ulikuwa unachuja vilivyo Ili kuweza kumpata mwanafunzi aliye bora tofauti na hivi sasa.
 
Hao kidato cha nne hawapaswi kupumzika? wazazi wanakwepa majukunu ndio maana wanatamani kuwepo na Bording hata ya Watoto wachanga, Ingekuwepi ya Watoto wachanga tungewapeleka Bording kukwepa majukumu
Kijana wa form four mzazi anakwepa majukumu gani kwake??? zaidi akirudi kama ndo zile familia watoto wanajielewa wanakuwa wanasaidia shughuli za nyumbaniii...
 
Ujinga plus Ujinga plus Ujinga.

Wakati nasoma nakumbuka Mkuu wa Shule alikuwa amepiga kitabu Urusi, sasa Siku shule inafungwa alikuwa anatuambia kabisa nendeni mkapumzike, walio weka huu mfumo sio wajinga ndio maana hata Mfanyakazi anahitaji likizo akapumzike.

Hizi akili za kijinga tunaziyoa wapi?
Na ukifunga shule ukaenda likizo,unaporudi unaona shule na mazingira yake kama mapya kabisaa,yanakuvutia na kukupa hamasa ya kusoma..

Kwa sasa shule karibia zote wanawaza mitihani mitihani mitihani tu..ma group ya walimu wamebaki kutumiana mitihani ya kila mahali wakidhani ndiyo Elimu bora hiyo.

Ila nadhani shida imeletwa na wanafunzi wengi wasio na sifa ya kujiunga sekondari wako sekondari wanaigiza kusoma,na viongozi wanawatukana walimu kila kukicha kwa hao wanafunzi wasio na sifa wanapopata matokeo yao stahiki( kufeli).

Ila kwa kizazi kile cha mwanafunzi kujisomea mwenyewe kwa nguvu nyingi na msaada kidogo wa mwalimu,likizo zilifaa sana, ila kwa kizazi hiki cha mwalimu kutumia nguvu nyingi na nguvu kidogoo za mwanafunzi,kazi ipo.



Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Ahsante mkuu kwa kuleta hii mada. Isitoshe hao watu watoto wao wanasomea shule zenya kutoa au kua na mazingira bora ya kujisomea na kujifunzia.

Wanawadanganya wananchi walio hoi katika ili. Kwanza huyu Waziri na Kamishna ilibidi watumbuliwe
Walitakiwa Kukamatwa Haraka Sana Na Kutupwa Ndani Chap Chap
Maana Wanaupotosha Umma Wakati Wao Watoto Wao Full Connection
 
Wazazi wanakwepa majukunu hakuna cha zero wala Four, Sikiliza Mtoto kama kichwani ni zero ni zero tu atapata hoo four hata aishi Darasani
Sio kweli mtoto wa zero unaweza ukampeleka four ni swala la kutenga muda na utayari wa pande zote mbili
 
Hii ni sick and illest excuse..eti maxingira sijui walimu..

Acha kupotosha watu. Siku 194 za vipindi vya darasani hakuna topic inaacha guswa... Hakuna.. na kuna ample time ya revision ya kutosha. Hata huko vijijini.
Kuna uwezekano mkubwa watu wengine humu mnachangia hii maada hata shule za kata tunazozungumzia hamzijui.Shule za sekondari za kata zinaupungufu mkubwa wa walimu hasa sayansi.Haya hii hoja mfu ya mtoto akakae na wazazi wake ni sawa kwa boarding school lkn kwenye shule za kata mtoto ana kaa na wazazi wake anzia saa tisa jioni hadi saa 12.00 asubuhi kesho yake huyo mzazi halithiki tu kumuona huyo mtoto? Pili kipindi cha likizo walimu watafundisha mwisho saa sita na wiki mbili za mwisho watapumzika kabisa bado huo muda hautoshi mtoto kukaa nyumbani? Kama watoto hawalipishwI wala kuchangia chochote shida iko wapi?? Muhimu wanafunzi wasitozwe chochote wakati wa likizo.
Kupanga ni kuchagua kama tumeamua kumuelekeza namna daktari anavyopaswa kumhudumia mgonjwa wake tofauti na taaluma yake sawa "Yaani daktari anasema huyu mgonjwa anapaswa kupelekwa ICU sisi hatutaki basi sawa.
 
Unaweza ukaongea hapa kama mzazi Bora kumbe wewe ndo umetelekeza mtoto kule Arusha unakula maisha huko Mbeya hutaki kutoa hata mia kwa mtoto, analelewa na kusaidiwa na walimu. Hii kada ya elimu na malezi kama hujui Chochote Bora ukae kimya. Don't generalize parents. Kuna waliokwepa majukumu Yao wametelekeza watoto mashuleni wanalelewa na walimu, hivyo walimu wanawakazania ili angalau elimu iwakonboe wasipate machungu ya kutelekezwa
Malezi ni muhimu huenda kuliko Elimu, Googel Kisa kimoja cha Mdada wa Kenya alie kuwa anafanya Kenya Airways na yuko Busy na watoto wanatunzwa na Beki tatu, Ilibidi Mdada atoe notce ya Masaa 24 kuacha kazi
 
Na ukifunga shule ukaenda likizo,unaporudi unaona shule na mazingira yake kama mapya kabisaa,yanakuvutia na kukupa hamasa ya kusoma..

Kwa sasa shule karibia zote wanawaza mitihani mitihani mitihani tu..ma group ya walimu wamebaki kutumiana mitihani ya kila mahali wakidhani ndiyo Elimu bora hiyo.

Ila nadhani shida imeletwa na wanafunzi wengi wasio na sifa ya kujiunga sekondari wako sekondari wanaigiza kusoma,na viongozi wanawatukana walimu kila kukicha kwa hao wanafunzi wasio na sifa wanapopata matokeo yao stahiki( kufeli).

Ila kwa kizazi kile cha mwanafunzi kujisomea mwenyewe kwa nguvu nyingi na msaada kidogo wa mwalimu,likizo zilifaa sana, ila kwa kizazi hiki cha mwalimu kutumia nguvu nyingi na nguvu kidogoo za mwanafunzi,kazi ipo.



Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Ndio maana ya likizo
 
Sijakataa likizo wasiende bali vidato vya mitihani wabaki.
Wakati unasoma wewe ulienda likizo kwa vidato vya mitihani?? Kma ni ndio basi tunaanza kujenga taifa la vilaza
Hatukuwa na hicho mnachokiita siku hz eti madarasa ya mitihani.
Likizo tulienda shule nzima na bado kulikuwa na ufaulu mzuri tu
 
Hatukuwa na hicho mnachokiita siku hz eti madarasa ya mitihani.
Likizo tulienda shule nzima na bado kulikuwa na ufaulu mzuri tu
Kwani we ulisoma wapi?? Mwaka gani?? Au ulisomea Somalia nn???
 
Kuna uwezekano mkubwa watu wengine humu mnachangia hii maada hata shule za kata tunazozungumzia hamzijui.Shule za sekondari za kata zinaupungufu mkubwa wa walimu hasa sayansi.Haya hii hoja mfu ya mtoto akakae na wazazi wake ni sawa kwa boarding school lkn kwenye shule za kata mtoto ana kaa na wazazi wake anzia saa tisa jioni hadi saa 12.00 asubuhi kesho yake huyo mzazi halithiki tu kumuona huyo mtoto? Pili kipindi cha likizo walimu watafundisha mwisho saa sita na wiki mbili za mwisho watapumzika kabisa bado huo muda hautoshi mtoto kukaa nyumbani? Kama watoto hawalipishwI wala kuchangia chochote shida iko wapi?? Muhimu wanafunzi wasitozwe chochote wakati wa likizo.
Kupanga ni kuchagua kama tumeamua kumuelekeza namna daktari anavyopaswa kumhudumia mgonjwa wake tofauti na taaluma yake sawa "Yaani daktari anasema huyu mgonjwa anapaswa kupelekwa ICU sisi hatutaki basi sawa.
Umefunga mjadala kabisa, walioskia waskie na wasioskia waache. Walimu wana hela nyie asikwambie mtu
 
Elimu ya zamani ilikuwa inafaulisha mtoto 1 kati ya watoto 100 kutoka elimu ya msingi kwenda elimu ya secondari tofauti na Sasa idadi kubwa ya watoto wanaomaliza elimu ya msingi wanafaulu kwenda sekondari yani kati ya watoto 100 basi 5 watafeli na hao 95 watafaulu na
kuendelea na masomo ya sekondari hivo hapa tunapata picha ya kwamba mchujo uliokua ukifanyika zamani ulikuwa unachuja vilivyo Ili kuweza kumpata mwanafunzi aliye bora tofauti na hivi sasa.
Uyo uliemjibu kaishia la nne B kafeli so achana nae atakupotezea mda tu
 
Back
Top Bottom