Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Nimejaribu sana kupata majibu ya maswali myepesi sana kwa Mag3 au wanaomuunga mkono, lakini mpaka sasa sikuambulia kitu. Hivi kuna msomi akajificha asijulikane halafu anakuja kupingana na mwana historia aliojiweka wazi kabisa?

Maswali yangu yalikuwa haya:

FaizaFoxy https://www.jamiiforums.com/members/faizafoxy.html Yesterday 17:44 #30

Mohamed Said anapotaja wazee wake anaonesha na nini walikifanya na dalili anaziweka wazi, sasa huyo aliyeambiwa na wazee wake bila kutupa dalili za hao wazee walikuwa kina nani walikuwa na harakati zipi, tumuamini vipi?

FaizaFoxy Yesterday 17:55 #33

Tumeona Mohamed Said akitubwagia kinaga ubaga vitabu alivyoandika na "papers" alizoandika, mihadhara aliyoitowa / hudhuria vyuo mbali mbali duniani, Jee, na wewe upo tayari kutuwekea hapa ili tujuwe "credibility" yako katika historia? au ndio wakudonyoa donyoa mtandaoni? na ya kuhadithiwa na wazee wako ambao hata dalili hautupi walikuwa na harakati zipi katika siasa au jamii wakati huo? Tuwekee wazi ili tusikuone kama ni mpiga porojo tu.

FaizaFoxy Yesterday 23:59 #48

Mohamed Said kaelezea vitabu alivyokwishaandika, papers zake, vyuo na makongamano tofauti duniani alivyohudhuria.

Kawataja wazee wake ni kina nani na walikuwa wanafanya nini.

Huyo Mag3 hakuna kimoja katika haya aliyotuwekea wazi hata jina lake na nasaba yake hajaiweka wazi.

Hatuna reference yake hata moja ya amma kwa kitabu au paper ya history. Isitoshe, ameanza kwa kejeli na matusi, jee hapo kuna "credibility" yoyote ambayo kwa ujasusi wako unaweza kuitetea?

FaizaFoxy Today 08:35 #70
Hicho ulichonibandikia, huyo ni Mag3? nilichoulizia ni credibility ya Mag3 na atueleze hapa yeye ni nani hao wazee wake anawanukuu ni kina nani? walifanya nini katika harakati za kudai madaraka / nyadhifa za kijamii / siasa wakati huo? Yeye kishaandika au hajaandika kitabu chochote? kama kaandika ni kitabu kipi? au "paper" zipi za usomi kishaandika? vyuo alivyohudhuria, makongamano au kualikwa kuongea, kutetea maandiko yake?

Kwa ufupi ni nani?

Naona mpaka sasa bado anatafuta "data" zake kwa haya maswali.

Msomi yoyote mwema, hujitambulisha au hutambulishwa na amma usomi wake, amma kazi zake, amma utu wake (kwa wamjuao). sasa msomi Mag3 sijayaona yote hayo. Mnaweza mkamsaidia mumjuwae.

Msomi alioweka post kwa mbwembwe eti anaeweza kuelezea history ya Tanganyika anashindwa kujieleza yeye ni nani? Hapa panaleta raha sana.
 
Mohamed Said msalie mtume,yaani Waikela kamnyoshea kidole Nyerere.Huyu ni Nyerere tunaemjua au mwingine??????
 
Nimejaribu sana kupata majibu ya maswali myepesi sana kwa Mag3 au wanaomuunga mkono, lakini mpaka sasa sikuambulia kitu. Hivi kuna msomi akajificha asijulikane halafu anakuja kupingana na mwana historia aliojiweka wazi kabisa?

Maswali yangu yalikuwa haya:









Msomi alioweka post kwa mbwembwe eti anaeweza kuelezea history ya Tanganyika anashindwa kujieleza yeye ni nani? Hapa panaleta raha sana.

Mbona wewe hujataja majina yako? Hata kama hajakutajia jina lake halisi haiondoi ukweli kwamba historia anayoisema ni ya kweli.
 
Mbona wewe hujataja majina yako? Hata kama hajakutajia jina lake halisi haiondoi ukweli kwamba historia anayoisema ni ya kweli.

Mimi amma nauliza nisilolielewa amma najibu shutuma amma nikiweka bandiko naweka na ushahidi. Kama hunijui na hutonijuwa nimeshasema mara nyingi humu JF mimi Jina langu Faiza, umaarufu wangu Foxy kwetu ni Udoe na Lumumba (New Street), Kariakoo. Ofisi za Tanu ni ubavu kwa ubavu na nyumbani kwetu. Wengi wa Kariakoo waliomo JF tunajuwana.

Hiyo avatar si picha yangu, huyo ni mwanamke shujaa wa Kiislaam aliyegoma kuvuwa Hijab yake Mahakamani Merekani na ni "role model" wangu. Hajatetereshwa hata na Jaji wa Kimerekani na kakubali afungwe kuliko kuvuwa Hijab.

Sijaandika kitabu wala paper yoyote ya historia lakini historia ni moja katika hobby zangu na nnapenda sana kuisoma.

Wazee wengi wanaotajwa na Mohamed Said amma nnawajuwa wao amma nnawajuwa watoto zao tuliokuwa pamoja Kariakoo.

Nadhani nimejieleza kwa ufupi na inatosha ili nisiharibu mada. Ukitaka kunijuwa zaidi, tumia google ubofye FaizaFoxy utapata habari zangu nyingi tu. Ooooopsss pia ni selebriti namba moja wa JF, nyuzi nyingi zimeshafunguliwa kwa jina langu na hujaza posts.
 
Alexism,
Wazee wetu walikuwa "nationalists" na ideology waliyoitaka kwa TANU ni "nationalist secularist"
waliamini katika hilo hadi walipojua kuwa mategemeo yao yamegonga mwamba pale vita
vilipoanza dhidi ya ya Uislam. Nakuwekea hapa chini mambo yalivyokuwa wakati ule:

"Huu ndiyo ukuwa mwanzo wa upinzani (Baada ya Kura Tatu mwaka 1958) wa chini chini dhidi ya TANU. Mwaka 1959, Ramadhani Mashado Plantan, mhariri hodari wa gazeti la Zuhra wakati mmoja gazeti hili likiwa ndiyo sauti ya TANU na wananchi wa TAnganyika, pamoja na kikundi kidogo cha Waislam akiwemo Saleh Muhsin walijiuzulu kutoka TANU na kuunda chama chao cha upinzani, All Muslim National Union of Tanganyika (AMNUT).[1]Wanachama wengine waasisi walikuwa Abdallah Mohammed ambaye alichaguliwa kuwa rais na Plantan akiwa katibu. Plantan alijitolea chumba kimoja nyumbani kwake Kirk Street, Gerezani kama ofisi ya kwanza ya AMNUT. Mara tu baada ya kuundwa kwa AMNUT, ulizuka mgogoro katika uongozi na ofisi hiyo ilibidi ihamishwe kutoka nyumbani kwa Plantan hadi Libya Street, eneo lenye Wahindi wengi katikati ya mji. Uongozi mpya ulikuja madarakani na katibu mpya Abduwahid Abdulkarim. Abduwahid Abdulkarim, kijana mwenye umri wa miaka 25 alichaguliwa kuchukua nafasi ya Plantan. Abdallah Mohamed alibakia na cheo chake kama rais. AMNUT haikuweza kumudu kodi ya nyumba katika eneo lile la matajiri wa Kihindi. AMNUT ikaihamisha ofisi yake na kwenda Kariakoo, Narungíombe Street, karibu na msikiti wa Sheikh Idris bin Saad.
Lengo kuu la AMNUT lilikuwa ni kulinda haki na maslahi ya Waislam ambayo ilikuwa ikihisi yalikuwa hatarini katika serikali iliyoshikiliwa na Wakristo. Abdulkarim alikwenda Tabora kujaribu kutafuta kuungwa mkono AMNUT lakini matokeo yalikuwa ya kukatisha tamaa. Abdulkarim alichagua Tabora kwa sababu ilikuwa mahali penye athari kubwa ya Uislamu. Hata hivyo Abdulkarim alifanikiwa kupokea mwaliko kutoka kwa Ali Muhsin Al Barwani kiongozi wa Zanzibar Nationality Party (ZNP) ahudhurie mkutano wa kamati kuu na awakilishe suala la AMNUT. Mkutano huu ulifanyika katika ofisi ya ZNP Darajani huko Zanzibar. Ali Muhsin alimwambia Abdulkarim kwamba ZNP haiwezi kujifungamanisha na tatizo la Uislam kwa sababu ZNP haikuwa inaamini kama Ukristo una uwezo wa kuhatarisha Uislam hasa ukichukulia kuwa Waislam ni wengi nchini Tanganyika. Waislam wa Tanganyika walikataa kuiunga mkono AMNUT wakihisi sera zake zilikuwa za kuwagawa watu kwa misingi ya dini. Kwa ajili hii basi AMNUT haikuwa na maslahi ya wananchi.
Lakini pigo kubwa kwa AMNUT lilikuja kutoka kwa masheikh wa Tanga. Masheikh na waalimu wa Qurían mjini Tanga walitia sahihi azimio la pamoja kuipinga AMNUT. Azimio hilo lilisema kuwa AMNUT ingezua janga. Masheikh walisisitiza kwamba wataiunga mkono TANU mpaka uhuru upatikane kwa sababu wana imani na malengo yake.[1]AMNUT ikikabiliwa na mashambulio kama hayo kutoka tabaka ambayo ilidai inawakilisha maslahi yao, chama hicho hakikuweza kustawi. Haukupita muda mrefu AMNUT ikafa. Mwaka 1960, Plantan sasa akiwa nje ya AMNUT na siasa, alitoa kauli moja iliyokuwa kama anatoa buriani kuteremsha pazia na kuaga jukwaa la siasa. Plantan aliwaambia Waislam kwamba hata kwa miaka mia moja hawataweza kuwafikia Wakristo. Baada ya kauli hiii hakuna kilichosikika kuhusu Ramadhani Mashado Plantan. Aliishi miaka ya mwisho ya maisha yake hapo Gerezani, akitumia wakati wake baina ya nyumba yake na msikiti wa jirani ambao alikuwa akiufagia kuuweka safi akisubiri mauti yaje akasimame mbele ya haki.Nyerere alikubali ukweli kuwa kulikuwa na upogo baina ya Waislam na Wakristo hususan katika elimu ambayo itawazuia Waislam kushika nafasi za uongozi katika serikali ya wananchi. Nyerere aliwaomba Waislam waweke matumaini yao kwa TANU ambayo itaanzisha mabadiliko ya lazima kuwainua Waislam kwenye nafasi za usawa pamoja na Wakristo mara tu uhuru utakapopatikana. Lakini hili, Nyerere aliwakumbusha Waislam mara kwa mara kuwa linaweza kufanyika tu kwenye Tanganyika huru na siyo chini ya utawala wa Kiingereza. Waislam katika TANU, kwa upande wao, waliamini kwamba ilikuwa kinyume kwao kuanzisha chama cha kisiasa chini ya maslahi ya kikundi kimoja kama ndiyo lengo la kudai uhuru. Hili, wengi waliamini, lingesaidia kuunda vikundi vingi na kusababisha mfarakano. Kwa kweli madai yaliyokuwa yakitolewa na AMNUT hayakuwa madai ambayo yangetolewa kwa TANU katika wakati ule. Vita vya mwaka 1947 kati ya India na Pakistan vilivyosababisha kupoteza maisha ya watu wengi, vilikuwa bado vinakumbukwa na watu wengi. Chanzo cha ugomvi huo kilikuwa ushindani baina ya Waislam na Wahindu. Kabla ya mwaka 1947 India na Pakistan zilikuwa nchi moja chini ya ukoloni wa Mwingereza. Waislam na Wahindu walipigania uhuru pamoja na walifarakana mara tu ilipokuwa wazi kuwa Uingereza ingetoa uhuru kwa India. Watu wengi nchini Tanganyika walihofia kwamba kuruhusu fikra kama zile zilizotolewa na Sheikh Takadir kuota mizizi kulikuwa kukaribisha ile hali ya India na Pakistan Tanganyika. Nyerere alionya kuwa hakutaka hali kama ile ije kuisibu Tanganyika."

Mohamed
 
Mimi amma nauliza nisilolielewa amma najibu shutuma amma nikiweka bandiko naweka na ushahidi. Kama hunijui na hutonijuwa nimeshasema mara nyingi humu JF mimi Jina langu Faiza, umaarufu wangu Foxy kwetu ni Udoe na Lumumba (New Street), Kariakoo. Ofisi za Tanu ni ubavu kwa ubavu na nyumbani kwetu. Wengi wa Kariakoo waliomo JF tunajuwana.

Hiyo avatar si picha yangu, huyo ni mwanamke shujaa wa Kiislaam aliyegoma kuvuwa Hijab yake Mahakamani Merekani na ni "role model" wangu. Hajatetereshwa hata na Jaji wa Kimerekani na kakubali afungwe kuliko kuvuwa Hijab.

Sijaandika kitabu wala paper yoyote ya historia lakini historia ni moja katika hobby zangu na nnapenda sana kuisoma.

Wazee wengi wanaotajwa na Mohamed Said amma nnawajuwa wao amma nnawajuwa watoto zao tuliokuwa pamoja Kariakoo.

Nadhani nimejieleza kwa ufupi na inatosha ili nisiharibu mada. Ukitaka kunijuwa zaidi, tumia google ubofye FaizaFoxy utapata habari zangu nyingi tu. Ooooopsss pia ni selebriti namba moja wa JF, nyuzi nyingi zimeshafunguliwa kwa jina langu na hujaza posts.

Mimi binafsi nawaheshimu sana waislamu si kwa sababu ya dini yao bali ni kwa sababu ni binadamu wenzangu wanaostahili kuheshimiwa utu wao. Katika familia na koo zinazozaa familia yetu kuna mchanganyiko wa hizi dini mbili, Uislam na Ukristo. kuna ndugu zangu wa dini zote mbili kwenye ngazi zote mbili yaani kwenye familia yetu na kwenye ukoo wetu pia.

Wakati fulani huwa nastushwa na falsafa kama yako Faizafoxy kwamba "ndugu" zako ni waislamu wenzako. Kama dini inaua undugu si dini ya mwenyezimungu bali ina chanzo kingine kabisa. Mmoja wa babu zangu alikuwa ni Muislamu na hadi kifo chake kinatokea sikuona hata siku mmoja akiwabagua watoto wake ambao ni wakristo. Kama mungu alitaka waja wake wote wawe na dini moja basi angefanya hivyo na wala mungu wa kweli haitaji "msaada" wa mwanadamu ambaye amemuumba yeye mwenyewe kumsaidia kuieneza dini yake kwa mabavu.

Turudi kwenye mada. Hoja kubwa hapa ni kama ni kweli Nyerere yeye mwenyewe ama mtu mwingine alihusika kwenye "kuzuia" hao wazee wa Mohamed Said kuingizwa kwenye Historia ya kupigania Uhuru wa nchi hii kwa sababu ya dini zao. Babu zangu wote wawili walikuwa ni wapigania Uhuru kutoka kwenye mikoa miwili (siyo ya pwani) tofauti na Majimbo toafauti ambao siku ya kupatikana Uhuru walikesha kusheherekea. Lakini wote wawili hakuna mahali popote majina yao yametajwa kama walikuwa ni wapigania uhuru wa nchi hii.

Hata kwetu pia tunayo picha ambayo Babu yetu alipiga pamoja na Nyerere na wanakijiji wa kijiji chake wanaikumbuka siku ambayo Nyerere alifika kijijini kwao kuwaelezea kuhusu Uhuru. Babu yangu mmoja alikuwa ni Muislam na Mwingine alikuwa ni Mkristo na wote wawili walikuwa ni makatibu wa TANU wakati wakupigania Uhuru, kadi na risiti za TANU tumezitunza kama kumbukumbu ya familia na hatuma hata muda wa kudai Nyerere alizuia babu zetu hawa kuandikwa kwenye vitabu vya Historia ya kupigania Uhuru wa Tanganyika

Martin Luther King Jr. Malcom X. Mahtima Gandhi na wengineo walikuwa na watu wengine nyuma yao na kuandika majina ya hao wote basi itahitaji dunia nzima tuache kazi zetu ili tufanye kazi ya kuandika hadi waliokuwa wanawapikia chai mashujaa hao. Dini si kigezo cha kusema wazee wa MS historia haiwataji bali ni kwa sababu wazee hao hawakuwahi kufanya jambo lolote la kustaajabisha hata kufanya waandika Historia kuwataja kwa majina kwenye historia ya kupigani uhuru wa Tanganyika.

Jiulize ni kwa nini Historia inamtaja Chifu Mkwawa kama shujaa wa Wahehe kwani vita na wajerumani alipigana akiwa peke yake? Hao waliokufa na Kinjeketile wameandikwa wapi? Nani anajua majina ya walinzi au washauri wa Mtemi Mirambo, lini tuliambiwa Chabruma Mikuki yake ilikuwa inatengenezwa na nani? Mangi Meli maamuzi yake hayakuwa na washauri? Chifu Mazengo baraza lake la washauri lilikuwa na wajumbe wangapi. Tukubaliane kwamba kwenye kuandika Historia huchaguliwa wale tuu waliofanya mambo ambayo kwa akili ya watu wa kizazi hicho yalikuwa ni ya kufikirika tu!!
 
Mohamed Said msalie mtume,yaani Waikela kamnyoshea kidole Nyerere.Huyu ni Nyerere tunaemjua au mwingine??????

Son of Alaska,

Ndugu yangu Nyerere wala hakuwa shujaa kama watu walivyomdhania.
Angelikuwa shujaa asingelikusanya magazeti kutia moto kwa sababu tu
yametaja kuwa Waislam kwa umoja wao walipigania uhuru wa Tanganyika
pamoja nae na yeye alitiwa TANU na Abdulwahid Sykes.

Hivyo ni vitu vya kumtisha mtu? Watu walimuona shujaa kwa kuwa walikuwa
wanamuachia anasema peke yake na aliyesema anamtia kizuizini.

Hapo ndipo nilipojua udhaifu wake kuwa anaogopa Waislam na kitu chochote
kinachohusu Uislam.

Turudi kwa Bilal Rehani Waikela. Waikela ni mcha Mungu wa kweli 1970 Geofrey
Sawaya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai wakati ule kenda kumuhonga Waikela
shs: 40,000.00 fedha za serikali ya Tanzania asaidie kuingiza BAKWATA Tabora.
Waikela kazikataa.

Ule ucha Mungu wake ndiyo uliomfikisha katika daraja ile ya kutomuogopa binadamu
mwenzake sembuse adui wa Uislam na kukataa kuhongwa kuusaliti Uislam.

Tafuta DVD yake anaeleza maisha yake jinsi alivyoasisi TANU Tabora mwaka 1955 iko
Msikiti wa Mtoro.

Mohamed
 
Mimi binafsi nawaheshimu sana waislamu si kwa sababu ya dini yao bali ni kwa sababu ni binadamu wenzangu wanaostahili kuheshimiwa utu wao. Katika familia na koo zinazozaa familia yetu kuna mchanganyiko wa hizi dini mbili, Uislam na Ukristo. kuna ndugu zangu wa dini zote mbili kwenye ngazi zote mbili yaani kwenye familia yetu na kwenye ukoo wetu pia.

Wakati fulani huwa nastushwa na falsafa kama yako Faizafoxy kwamba "ndugu" zako ni waislamu wenzako. Kama dini inaua undugu si dini ya mwenyezimungu bali ina chanzo kingine kabisa. Mmoja wa babu zangu alikuwa ni Muislamu na hadi kifo chake kinatokea sikuona hata siku mmoja akiwabagua watoto wake ambao ni wakristo. Kama mungu alitaka waja wake wote wawe na dini moja basi angefanya hivyo na wala mungu wa kweli haitaji "msaada" wa mwanadamu ambaye amemuumba yeye mwenyewe kumsaidia kuieneza dini yake kwa mabavu.

Turudi kwenye mada. Hoja kubwa hapa ni kama ni kweli Nyerere yeye mwenyewe ama mtu mwingine alihusika kwenye "kuzuia" hao wazee wa Mohamed Said kuingizwa kwenye Historia ya kupigania Uhuru wa nchi hii kwa sababu ya dini zao. Babu zangu wote wawili walikuwa ni wapigania Uhuru kutoka kwenye mikoa miwili (siyo ya pwani) tofauti na Majimbo toafauti ambao siku ya kupatikana Uhuru walikesha kusheherekea. Lakini wote wawili hakuna mahali popote majina yao yametajwa kama walikuwa ni wapigania uhuru wa nchi hii.

Hata kwetu pia tunayo picha ambayo Babu yetu alipiga pamoja na Nyerere na wanakijiji wa kijiji chake wanaikumbuka siku ambayo Nyerere alifika kijijini kwao kuwaelezea kuhusu Uhuru. Babu yangu mmoja alikuwa ni Muislam na Mwingine alikuwa ni Mkristo na wote wawili walikuwa ni makatibu wa TANU wakati wakupigania Uhuru, kadi na risiti za TANU tumezitunza kama kumbukumbu ya familia na hatuma hata muda wa kudai Nyerere alizuia babu zetu hawa kuandikwa kwenye vitabu vya Historia ya kupigania Uhuru wa Tanganyika

Martin Luther King Jr. Malcom X. Mahtima Gandhi na wengineo walikuwa na watu wengine nyuma yao na kuandika majina ya hao wote basi itahitaji dunia nzima tuache kazi zetu ili tufanye kazi ya kuandika hadi waliokuwa wanawapikia chai mashujaa hao. Dini si kigezo cha kusema wazee wa MS historia haiwataji bali ni kwa sababu wazee hao hawakuwahi kufanya jambo lolote la kustaajabisha hata kufanya waandika Historia kuwataja kwa majina kwenye historia ya kupigani uhuru wa Tanganyika.

Jiulize ni kwa nini Historia inamtaja Chifu Mkwawa kama shujaa wa Wahehe kwani vita na wajerumani alipigana akiwa peke yake? Hao waliokufa na Kinjeketile wameandikwa wapi? Nani anajua majina ya walinzi au washauri wa Mtemi Mirambo, lini tuliambiwa Chabruma Mikuki yake ilikuwa inatengenezwa na nani? Mangi Meli maamuzi yake hayakuwa na washauri? Chifu Mazengo baraza lake la washauri lilikuwa na wajumbe wangapi. Tukubaliane kwamba kwenye kuandika Historia huchaguliwa wale tuu waliofanya mambo ambayo kwa akili ya watu wa kizazi hicho yalikuwa ni ya kufikirika tu!!


Umeanza kwa kunishambulia kwa kusema kwangu kuwa Waislaam wote ndugu zangu. Napenda kukufahamisha kuwa Uislaam ni dini yangu na mafundisho yake ndiyo mfumo wa maisha yangu. Kila Muislaam ni ndugu yangu, na hilo huwezi kulibadili hata upande ushuke. Turudi kwenye mada na ukitaka tupeane darsa kuhusu undugu wa Waislaam nakuomba funguwa nyuzi zingine, naona kuanzisha mjadala ambao hauhusiani na mada ni kama hila na mbinu za kutaka kututowa nje ya mada.

Kuhusu hao babu zako, walikuwa wapigania Uhuru kama ilivyokuwa kwa kila mpenda Uhuru wa siku hizo, lakini utakuta kuwa hawakuwa waasisi wa AA wala TAA wala TANU na ndio maana huna habari hata kama hawakutajwa. Wazee anaowaelezea Mohamed Said ni waasisi na sio tu wapiganiaji. Upo hapo ulipo?
 
Mimi binafsi nawaheshimu sana waislamu si kwa sababu ya dini yao bali ni kwa sababu ni binadamu wenzangu wanaostahili kuheshimiwa utu wao. Katika familia na koo zinazozaa familia yetu kuna mchanganyiko wa hizi dini mbili, Uislam na Ukristo. kuna ndugu zangu wa dini zote mbili kwenye ngazi zote mbili yaani kwenye familia yetu na kwenye ukoo wetu pia.

Wakati fulani huwa nastushwa na falsafa kama yako Faizafoxy kwamba "ndugu" zako ni waislamu wenzako. Kama dini inaua undugu si dini ya mwenyezimungu bali ina chanzo kingine kabisa. Mmoja wa babu zangu alikuwa ni Muislamu na hadi kifo chake kinatokea sikuona hata siku mmoja akiwabagua watoto wake ambao ni wakristo. Kama mungu alitaka waja wake wote wawe na dini moja basi angefanya hivyo na wala mungu wa kweli haitaji "msaada" wa mwanadamu ambaye amemuumba yeye mwenyewe kumsaidia kuieneza dini yake kwa mabavu.

Turudi kwenye mada. Hoja kubwa hapa ni kama ni kweli Nyerere yeye mwenyewe ama mtu mwingine alihusika kwenye "kuzuia" hao wazee wa Mohamed Said kuingizwa kwenye Historia ya kupigania Uhuru wa nchi hii kwa sababu ya dini zao. Babu zangu wote wawili walikuwa ni wapigania Uhuru kutoka kwenye mikoa miwili (siyo ya pwani) tofauti na Majimbo toafauti ambao siku ya kupatikana Uhuru walikesha kusheherekea. Lakini wote wawili hakuna mahali popote majina yao yametajwa kama walikuwa ni wapigania uhuru wa nchi hii.

Hata kwetu pia tunayo picha ambayo Babu yetu alipiga pamoja na Nyerere na wanakijiji wa kijiji chake wanaikumbuka siku ambayo Nyerere alifika kijijini kwao kuwaelezea kuhusu Uhuru. Babu yangu mmoja alikuwa ni Muislam na Mwingine alikuwa ni Mkristo na wote wawili walikuwa ni makatibu wa TANU wakati wakupigania Uhuru, kadi na risiti za TANU tumezitunza kama kumbukumbu ya familia na hatuma hata muda wa kudai Nyerere alizuia babu zetu hawa kuandikwa kwenye vitabu vya Historia ya kupigania Uhuru wa Tanganyika

Martin Luther King Jr. Malcom X. Mahtima Gandhi na wengineo walikuwa na watu wengine nyuma yao na kuandika majina ya hao wote basi itahitaji dunia nzima tuache kazi zetu ili tufanye kazi ya kuandika hadi waliokuwa wanawapikia chai mashujaa hao. Dini si kigezo cha kusema wazee wa MS historia haiwataji bali ni kwa sababu wazee hao hawakuwahi kufanya jambo lolote la kustaajabisha hata kufanya waandika Historia kuwataja kwa majina kwenye historia ya kupigani uhuru wa Tanganyika.

Jiulize ni kwa nini Historia inamtaja Chifu Mkwawa kama shujaa wa Wahehe kwani vita na wajerumani alipigana akiwa peke yake? Hao waliokufa na Kinjeketile wameandikwa wapi? Nani anajua majina ya walinzi au washauri wa Mtemi Mirambo, lini tuliambiwa Chabruma Mikuki yake ilikuwa inatengenezwa na nani? Mangi Meli maamuzi yake hayakuwa na washauri? Chifu Mazengo baraza lake la washauri lilikuwa na wajumbe wangapi. Tukubaliane kwamba kwenye kuandika Historia huchaguliwa wale tuu waliofanya mambo ambayo kwa akili ya watu wa kizazi hicho yalikuwa ni ya kufikirika tu!!

Kigarama,

Wazee wangu mchango wao huwezi kufananisha na yeyote katika Tanganyika.
Nimeweka uzi hapa wa maisha ya Kleist kwa muhtasari pitia usome uone ni msingi
gani aliweka kwanza kwa dini yake kisha kwa kudai uhuru wa Tanganyika.

Msingi ambao ndiyo ulikuja kutimiwa na wanae na wanasiasa wenzao katika miaka
ya 1950 kuunda TANU ndani ya nyumba ambayo yeye aliijenga 1930s.

Nyumba si ile pale Lumumba hadi leo unaiona. Abdul Sykes kadi yake na 3. Ally
Sykes kadi yake namba 2, Nyerere kadi yake na 1 na aliyetoa na ina sahihi yake
ni Ally Sykes, Dossa kadi yake namba 4 Iddi Faiz kadi yake na 25.

Unataka kweli uwafananishe watu hawa na wanachama walioingia TANU 1957 na
kuendelea?

Mchango wa wazee wangu ulikuwa wa hali na mali. Enzi zao unaingia TANU kupeleka
fedha za kuendesha chama sio kuja kuiba hela za chama.

Wazee wangu walitoa nyumba zao kufanya ofisi za TANU bila kudai kodi. Said Chamwenyewe
anapanda baiskeli kwenda Rufiji kuitangaza TANU haombi masurfu ya safari na huko anakusanya
michango na hela za kadi na zinafika salama kwa Idd Faiz Mafongo mweka hazina wa TANU.

Idd Faiz na Said Chamwenyewe wamekufa masikini. Basi hata tukiwataja mnakasikrika.

Si bure historia hii ilimtisha Nyerere kama inavyowatisha nyinyi hivi leo zaidi ya miaka
60.

Kama ukoo wa Mirambo hawakuhifadhi historia yao haina maana nami niipuuze ya
wazee wangu.

Mimi natembea kifua mbele kwa ajili ya watu hawa. Nawapenda na nawaheshimu
sana tena sana.

Sitosita kuwaeleza mashujaa hawa popote hata kama nani atakasirika.

Kuacha kuwataja ni kuisaliti nchi hii waliyoikomboa.

Mohamed
 

Son of Alaska,

Ndugu yangu Nyerere wala hakuwa shujaa kama watu walivyomdhania.
Angelikuwa shujaa asingelikusanya magazeti kutia moto kwa sababu tu
yametaja kuwa Waislam kwa umoja wao walipigania uhuru wa Tanganyika
pamoja nae na yeye alitiwa TANU na Abdulwahid Sykes.



Hakuna ushahidi wa hili ni hisia tu.
Hivyo ni vitu vya kumtisha mtu? Watu walimuona shujaa kwa kuwa walikuwa
wanamuachia anasema peke yake na aliyesema anamtia kizuizini.

Si kweli; inategemea unasema nini na hata leo wanaosema wengine wanatiwa kizuizini. Au umesahau mara ngapi kina Mtikila wametiwa pingu kwa sababu ya walichosema?


Hapo ndipo nilipojua udhaifu wake kuwa anaogopa Waislam na kitu chochote
kinachohusu Uislam.

hii si kweli; alianza kuwaogopa Waislamu lini wakati alikaa nao, kula nao, na hata kukubali kulindwa nao? Umeandika kwenye kitabu chako juu ya tukio moja ambalo kanisa alilokuwa Nyerere kaenda kusali lilindwa nje na vijana wa Kiislamu. Umeandika mara kadhaa alivyoshirikia dua mbalimbali na Waislamu na hata kulia machozi (kwenye kitabu chako kuna matukio matatu ambapo Nyerere anamwaga machozi mbele ya Waislamu!) iweje awe na chuki nao au Uislamu?

Hakuna Waislamu waliokatazwa kuabudu au kwenda msikitini au kulazimishwa kuswali msikiti fulani. Nyerere hakuwahi kuwalazimisha au hata kuwashauri washirika wake Waislamu kubadili dini ili wawe Wakristu. Lakini kinyume chake amefanya kazi vizuri na Waislamu mbalimbali. Unless of course unaposema "waislamu" humaanishi wale Waislamu waliokuwa na kukubali kufanya kazi na kupingana na kundi jingine. Kwako yumkini Waislamu ni kundi moja lisilo na tofauti au lisilopaswa kuwa na tofauti. Kwamba, Muislamu yeyote ambaye hakuwa katika hilo kundi jingine hakuwa Muislamu mzuri. Haujawahi kutoa ushahidi wowote wa nyaraka, agizo, au programu yoyote ya Nyerere dhidi ya Waislamu.

Hata hili la gazeti unalirudia mara kwa mara lakini halina ushahidi. Je, tukio hili la kukusanywa gazeti hilo lilitokea siku gani na Nyerere alikuwa wapi siku hiyo?

Turudi kwa Bilal Rehani Waikela. Waikela ni mcha Mungu wa kweli 1970 Geofrey
Sawaya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai wakati ule kenda kumuhonga Waikela
shs: 40,000.00 fedha za serikali ya Tanzania asaidie kuingiza BAKWATA Tabora.
Waikela kazikataa.

Hili nalo lipo kwenye kitabu chako lakini kama mengine halina ushahidi wowote zaidi ya maneno ya watu. Lakini si kwamba halikuwezekana lakini halina uhusiano wowote na Nyerere; Nyerere aliweza kwenda kwenye mkutano wa Waislamu na kuzungumza nao na kujadiliana nao na hata kukubali kunyoshewa kidole. Leo hii tumeshuhudia juzi Waislamu wakipewa hotuba ya Kikwete na kukataliwa mojawapo ya malalamiko yao mengi, ni Muislamu yupi amesimama kumnyoshea kidole na kumuambia juu ya dhulma? Leo hii wewe mwenyewe hujaweza kumnyoshea kidole Rais Kikwete na kumuambia juu ya dhulma hii; hujawahi kwenda kukutana naye kuwakilisha malalamiko ya Waislamu na hujaandika ni jinsi gani Waislamu wanadhulumiwa na CCM ambacho ni chama kinachoongozwa na viongozi kadhaa ambao ni Waislamu. Lakini unalalamikia Kanisa!

Ule ucha Mungu wake ndiyo uliomfikisha katika daraja ile ya kutomuogopa binadamu
mwenzake sembuse adui wa Uislam na kukataa kuhongwa kuusaliti Uislam.

Tafuta DVD yake anaeleza maisha yake jinsi alivyoasisi TANU Tabora mwaka 1955 iko
Msikiti wa Mtoro.

Mohamed

Hili yaweza kabisa kuwa kweli lakini haiwezi kuwa ukweli wote. Hulka ya mwanadamu aliyeumizwa mara zote ni kutia chumvi matatizo yake na hata kujaribu kufafanua kwanini hakuwa na makosa. Leo hii wako wapi Waislamu wasiohongwa ambao wameweza kuinyoshea mikono serikali (siyo kanisa) au kusema Kikwete anawadhulumu Waislamu? Hivi ni kweli maisha ya Waislamu leo ni bora zaidi kuliko ilivyokuwa miaka 50 iliyopita hasa baada ya vipindi ambavyo vimeongozwa na Waislamu? Je leo hii serikali ya CCM chini ya Kikwete ni rafiki mkubwa wa Waislamu kuliko CCM chini ya Nyerere?
 
mohamed said unasema Nyerere hakuwa shujaa kama watu wanavyomdhani-kichwa kimoja hicho kimewapa azimio la arusha,akawaburuza kwenye vijiji vya ujamaa,hatimaye akaweka modus operandi yake African Socialism,leo hii wewe watwambia sio shujaa,tukuelewe vipi??
 
Mnatumia nguvu nyingi sana kujibizana na watu ambao wameamua kubuni upya historia ya nchi hii.Mwanakijiji,Mag3 na wengineo nawashauri msipoteze muda wenu kujibizana na watu jobless kama Faizafoxy na ambao wako predictable watazungumza nini.Acheni waandike historia yao lakini wajue kuwa itaishia huko huko wanakoitoa.
 
mohamed said unasema Nyerere hakuwa shujaa kama watu wanavyomdhani-kichwa kimoja hicho kimewapa azimio la arusha,akawaburuza kwenye vijiji vya ujamaa,hatimaye akaweka modus operandi yake African Socialism,leo hii wewe watwambia sio shujaa,tukuelewe vipi??

Nimemsoma mzee mohamed kwa umakini sana pamoja na wanaomuunga mkono historia anayosimulia.

Nadhani hii inafanyika kwa makusudi mazima kuonyesha kwamba Nyerere hakuwa chochote wala lolote mbele ya wazee waislamu wa dsm.

Kuongezea tu katika maelezo yako ni kwamba, ilikuwaje huyu Nyerere asiye na ushujaa wowote akubalike haraka sana kwa wazee waislamu wa dsm hadi kumkabidhi dhamana kubwa kiasi kile? Ukitafakari kwa makini hali hiyo utaona upotoshaji unaofanywa kwa makusudi maalum!
 
Hakuna ushahidi wa hili ni hisia tu.


Si kweli
; inategemea unasema nini na hata leo wanaosema wengine wanatiwa kizuizini. Au umesahau mara ngapi kina Mtikila wametiwa pingu kwa sababu ya walichosema?




hii si kweli; alianza kuwaogopa Waislamu lini wakati alikaa nao, kula nao, na hata kukubali kulindwa nao? Umeandika kwenye kitabu chako juu ya tukio moja ambalo kanisa alilokuwa Nyerere kaenda kusali lilindwa nje na vijana wa Kiislamu. Umeandika mara kadhaa alivyoshirikia dua mbalimbali na Waislamu na hata kulia machozi (kwenye kitabu chako kuna matukio matatu ambapo Nyerere anamwaga machozi mbele ya Waislamu!) iweje awe na chuki nao au Uislamu?

Hakuna Waislamu waliokatazwa kuabudu au kwenda msikitini au kulazimishwa kuswali msikiti fulani. Nyerere hakuwahi kuwalazimisha au hata kuwashauri washirika wake Waislamu kubadili dini ili wawe Wakristu. Lakini kinyume chake amefanya kazi vizuri na Waislamu mbalimbali. Unless of course unaposema "waislamu" humaanishi wale Waislamu waliokuwa na kukubali kufanya kazi na kupingana na kundi jingine. Kwako yumkini Waislamu ni kundi moja lisilo na tofauti au lisilopaswa kuwa na tofauti. Kwamba, Muislamu yeyote ambaye hakuwa katika hilo kundi jingine hakuwa Muislamu mzuri. Haujawahi kutoa ushahidi wowote wa nyaraka, agizo, au programu yoyote ya Nyerere dhidi ya Waislamu.

Hata hili la gazeti unalirudia mara kwa mara lakini halina ushahidi
. Je, tukio hili la kukusanywa gazeti hilo lilitokea siku gani na Nyerere alikuwa wapi siku hiyo?



Hili nalo lipo kwenye kitabu chako lakini kama mengine halina ushahidi wowote zaidi ya maneno ya watu. Lakini si kwamba halikuwezekana lakini halina uhusiano wowote na Nyerere; Nyerere aliweza kwenda kwenye mkutano wa Waislamu na kuzungumza nao na kujadiliana nao na hata kukubali kunyoshewa kidole. Leo hii tumeshuhudia juzi Waislamu wakipewa hotuba ya Kikwete na kukataliwa mojawapo ya malalamiko yao mengi, ni Muislamu yupi amesimama kumnyoshea kidole na kumuambia juu ya dhulma? Leo hii wewe mwenyewe hujaweza kumnyoshea kidole Rais Kikwete na kumuambia juu ya dhulma hii; hujawahi kwenda kukutana naye kuwakilisha malalamiko ya Waislamu na hujaandika ni jinsi gani Waislamu wanadhulumiwa na CCM ambacho ni chama kinachoongozwa na viongozi kadhaa ambao ni Waislamu. Lakini unalalamikia Kanisa!



Hili yaweza kabisa kuwa kweli lakini haiwezi kuwa ukweli wote. Hulka ya mwanadamu aliyeumizwa mara zote ni kutia chumvi matatizo yake na hata kujaribu kufafanua kwanini hakuwa na makosa. Leo hii wako wapi Waislamu wasiohongwa ambao wameweza kuinyoshea mikono serikali (siyo kanisa) au kusema Kikwete anawadhulumu Waislamu? Hivi ni kweli maisha ya Waislamu leo ni bora zaidi kuliko ilivyokuwa miaka 50 iliyopita hasa baada ya vipindi ambavyo vimeongozwa na Waislamu? Je leo hii serikali ya CCM chini ya Kikwete ni rafiki mkubwa wa Waislamu kuliko CCM chini ya Nyerere?

Uandishi wako huwa unanchekesha, "mulitiple contradictions". Hebu tazama nilipoweka nyekundu. Punguza jazba, ukitaka raha ya mjadala uliza moja moja ujibiwe, na unaposema "si kweli" inapaswa uuweke wewe unaouona ukweli, kama alivyofanya Mohamed Said kukujibu post yako #162 kwa post yake #167 ambayo ujaipinga wala kuijibu wala kutuomba msamaha kwa kupotosha kwako ukweli. Waswahili hunena "tartiiiib".
 
Pamoja na MS kudai kwamba Historia ya AA,TAA, na TANU imepotoshwa lakini pia ukisoma kwa undani maandiko yake yanaonyesha kwamba Mwalimu alifanya juhudi za makusudi kuzuia Waislamu kupanda kielemu. Lakini kuna ushahidi wa kutosha kwamba ni Mwalimu wakati wa utawala wake ndiyo ailitaifisha shule zilizokuwa zinamilikiwa na makanisa ili watu wa dini nyingine wapate fursa za kusoma.. shule hizo zilitaifishwa bila hata wakristo kulipwa senti tano.

Shule kama Tabora Boys, Mazengo, Mkwawa, Malangali, Ilboru,Msalato, na nyinginezo nyingi za Msingi na sekondari zimesomesha waislamu wengi sana baada ya kutaifishwa na Mwalimu. Mbona hakuna mahali MS anaonyesha kwamba angalau katika hili Mwalimu "aliwadhulumu" wakristo na "kuwapendelea" waislamu?

Fikiria leo hii muhimbili, Bugando, KCMC na nyinginezo za wilaya kama si sera ya Afya za Mwalimu hali kwa ndugu zetu waislamu ingekuwaje?
 
Uandishi wako huwa unanchekesha, "mulitiple contradictions". Hebu tazama nilipoweka nyekundu. Punguza jazba, ukitaka raha ya mjadala uliza moja moja ujibiwe, na unaposema "si kweli" inapaswa uuweke wewe unaouona ukweli, kama alivyofanya Mohamed Said kukujibu post yako #162 kwa post yake #167 ambayo ujaipinga wala kuijibu wala kutuomba msamaha kwa kupotosha kwako ukweli. Waswahili hunena "tartiiiib".
Jaribu kutenganisha Uislamu na Uarabu nadhani hapo ndipo lilipo tatizo lako!! Wakati mwingine huwa nairejeza ilie hoja kwamba "mapenzi upofu" na wewe una mapenzi ya Uislamu lakini huamini katika Uislamu kwani Uislamu ni pamoja na kutafuta maarifa kutoka kwa wengine hata kutoka kwa "machina".
 
Nyumba si ile pale Lumumba hadi leo unaiona. Abdul Sykes kadi yake na 3. Ally
Sykes kadi yake namba 2, Nyerere kadi yake na 1 na aliyetoa na ina sahihi yake
ni Ally Sykes, Dossa kadi yake namba 4 Iddi Faiz kadi yake na 25
.

Sote tunaukubali mchango wa Sykes na wenzake wa Dar katika kuchangia Uhuru wa Tanganyika na kuanzishwa kwa TANU. Kinachogomba hapa ndugu yetu ni kwamba hao wazee "wetu' walifanya hivyo si kwa kusukumwa na utashi wa dini zao bali ni kwa uzalendo kwa nchi yao ya Tanganyika. Hata mwalimu naye alikuwa ni Muumini mzuri sana wa dini yake ya Kikiristo na dhehebu lake la Kikatoliki .Lakin hakuwachukia wakoloni kwa sababu walikuwa wanawagandamiza wakatoliki au wakristo wenzake, bali ni kwa sababu walikuwa wana wagandamiza watanganyika wenzake.

kuna swali nataka nikuulize kwenye hilo bandiko lako hasa kwenye sehemu nilizoweka rangi nyekundu. Kama hao wazee wako walikuwa ni Maarufu na muhimu sana kwenye TANU kuliko Mwalimu kama wewe unavyotaka tuamini, mbona ni wao wenyewe walimpa Mwalimu Kadi Namba Moja badala ya wao "Al maarufu" kuchukua kadi hiyo?

Na kwa nini kwenye maelezo yako badala ya kuanza na Kadi namba moja (ya Mwalimu) umeanza na Kadi namba tatu (ya Abdul Sykes) kisha mbili (ya Ally Sykes) na ndiyo ukaja namba Moja. Ina maana kwenye tarakimu unazozifahamu wewe namba tatu inatangulia namba mbili na moja, au ndiyo hicho kiarabu unachokipigania Irabu zake?

Na kuanzia kadi Namba 4 ya Dossa hadi Kadi namba 25 ya Idd Faiz, kuna kadi zaidi ya 21 hapo katikati, mbona Majina ya wenye hizo kadi 21 hujayataja. Kilichokufanya utoke namba 4 hadi urukie Namba 25 kimya kimya ni nini?

Unataka kweli uwafananishe watu hawa na wanachama walioingia TANU 1957 na
kuendelea?
Hakuna kutaka kufananisha bali hoja yetu ni kwamba hao watu walifanya kitu gani ambacho kilizidi kile ambacho Mwalimu alifanya? kwa Mfano ni nani kati ya hao wazee wako ambaye yeye alitaka kwenda UNO kabla ya Mwalimu Kujiunga na TAA na Mzee wako huyo ndiye badala yake akamteua Mwalimu kwenda UNO baada ya Mwalimu kujiunga TAA?

Mchango wa wazee wangu ulikuwa wa hali na mali. Enzi zao unaingia TANU kupeleka
fedha za kuendesha chama sio kuja kuiba hela za chama.
Na hakuna mahali popote pale kwenye maandiko yako ambapo umewahi kuonyesha kwamba sehemu nyingine za Tanganyika badala ya kuchangia TANU wao walikula hela zilizochangwa na wazee wa Gerezani. Mchango wa Mwalimu ulikuwa ni mkubwa sana kuliko hata hela zilizochangwa na wana TANU wengi tu, Nani wakati huo alikuwa yuko tayari kupambana na Mkoloni Uso kwa Uso?

Basi hata tukiwataja mnakasikrika.
Nani kakasirika bali sisi tusichotaka kulishwa ujinga kama makinda ya ndege.

Si bure historia hii ilimtisha Nyerere kama inavyowatisha nyinyi hivi leo zaidi ya miaka
60.
Hakuna ushahidi wowote kuonyesha kwamba Nyerere alizuia mtu kuandika historia hii unayoisimulia wewe au kuzuia andiko (Manuscriipt) kuchapwa eti kwa sababu andiko hilo linawataja kina ALLy na ABDUL SYKES kama ni watu walioanzisha TAA au TANU.

Umesikia kwamba Wamarekani kwa kushirikiana na Mayahudi ya Israel wamemuua Ghadaffi??
 
Jaribu kutenganisha Uislamu na Uarabu nadhani hapo ndipo lilipo tatizo lako!! Wakati mwingine huwa nairejeza ilie hoja kwamba "mapenzi upofu" na wewe una mapenzi ya Uislamu lakini huamini katika Uislamu kwani Uislamu ni pamoja na kutafuta maarifa kutoka kwa wengine hata kutoka kwa "machina".

Hebu usitutowe kwenye mada kwa "visa vya ..." utajaza mwenyewe.
 

Mzee Mohamed Said,Fundi Mchundo,Jasusi,FaidaFoxy,WildCard,Mzee Mwanakijiji,Mwita Maranya,Nguruvi3,Mag3 na wengine wote niliowasahau kwa bahati mbaya tafadhali sana tujiepushe na lugha za kuudhi,kejeli au matusi kwa faida ya mjadala.Niseme kweli nimejifunza mambo mengi kupitia kwenu na nina hakika wako wengi pia kupitia michango yenu wamefaidika sana.

Mkuu Ngongo, nimekuwa sikubaliani na msimamo wako katika mambo mengi lakini hapa hujakosea sana ila, haya makala ya huyu Mohamed Said si mara ya kwanza yanatokea humu ndani ya JF. Kuna mada ilikwishaanzishwa huko nyuma na katika kila mchango alioutoa Mohamed kulijaa kejeli, kebehi na dharau dhidi ya wakuja ambazo hazikuhitaji darasa kuzielewa. Hiyo ndiyo sababu mimi Mag3 sitataka nijadiliane na Mohamed Said moja kwa moja kwa sababu maandishi yake yote ukiyasoma kwa makini yamejaa dhihaka, uchochezi na misemo ambayo ni mzaliwa wa Gerezani tu angethubutu kuyatumia humu ndani ya JF.

Lakini hayo tuyaache. Wakati tunapata uhuru ulikuwa ni wakati mgumu sana kwa Tanganyika ambayo kwa hapa Afrika Mashariki ndiyo taifa lililoongoza kwa idadi ya Makabila (karibu 150). Nasita sana kujishusha kuzungumzia ukabila badala ya Utaifa lakini ili tuweze kuzijua changamoto zilizomkabili Baba wa Taifa katika harakati za kujenga umoja, mshikamano na usawa ndani ya Tanganyika kuna maamuzi mazito ilibidi yafanywe. Bila hatua alizozichukua Mwalimu hili taifa letu tunalojivunia leo lingekuwa mapande mapande na amani tunayoanza kuichezea kama anavyotaka kufanya Mohamed Said ingekuwa ndoto.

Hebu tufikirie, hivi Tanzania tungekuwa wapi hivi leo kama ingekuwa kweli kuwa ni Wazee wa Mohamed Said wa Gerezani ndio walipigania uhuru wa nchi hii wakiwa na mawazo kama ya mtoto wao Mohamed Said. Mathalani tumkubalie huyu mchochezi kwamba hivyo ndivyo ilivokuwa, sasa kwa nini walimkaribisha wakuja, mshamba, mkatoliki na mvaa kaptura kutoka Butiama na kumpa kura nyingi tu tena dhidi ya mwenzao tena mzaliwa wa Gerezani kuwa kiongozi wao. Ni namna gani mtu na akili zake timamu anashawishiwa na kuanza kuzisikiliza na kuziamini hizi porojo za Mohamed Said kama si utumwa wa akili.

Nasema na ninarudia ni mtu mpuuzi tu anayeweza kudai kafanya utafiti na kufikia hatua ya kuanza kuwabagua Watanganyika waliopigania uhuru wa nchi hii kwa kujitolea nafsi zao katika misingi ya kidini. Na hapa nataka niwe wazi, siombi msamaha kwa kuita koleo kwa jina lake kwani kilichonisukuma kujiunga na JF ni falsafa ya kumkoma nyani geledi bila kumwangalia uso. Nipo karibu na Watanzania wengi tu Waislaam kwa Wakristo na Wasiokuwa na dini na katika mazungumzo yetu wanashangaa kwa nini mtu moja ameruhusiwa kuchezea hisia ya watu wasio makini kwa kumwaga hii mbegu ya chuki miongoni mwa wananchi.

No Mohamed Said, no more free ride, nikipata nafasi nitaendelea................
 
Back
Top Bottom