Kama vile wewe utaandikiaje TANU isiyo na Julius Nyerere, John Rupia, Oscar Kambona, Joseph Kasella Bantu, Kirilo Japhet, Bhoke Munanka, Paul Bomani,Patrick Kunambi, Pombeah, Mwakangale, Zacharia Madilla, James Malashi, Dominikus Misano, Stanley Kaseko na wengine wengi kama hao! Hao uliowataja walikuwa waislamu, na pengine baadhi yao walitanguliza dini yao kwanza lakini wengi wao walikuwa watanganyika walioungana na watanganyika wenzao wakristu, wahindu na wasio na dini kupigania uhuru wa nchi yao. Wanstahili heshima na kuenziwa si kwa sababu ya dini zao au kabila zao bali utaifa wao.
Oscar Kambona alikuwa Katibu wa kwanza aliyefanya kazi Full time na kulipwa mshahara kutokana na makusanyo ya ada za wanachama. Zuberi Mtemvu alikuwa part time kama walivyokuwa viongozi wengi wa mwanzo, pamoja na Mwalimu.
Amandla......
ngawetu.... Fundi mchundo. Tatizo ni kuwa simulizi hizi zimethrithishWa katika misingi ya chuki. Mfano Mohamed anAsema marhum mama yake alikuwa analia kwasababu mwanae ameonewa shule hakupewa nafasi. Juzi Mohamed kaja na habari kuwa mwanae kaonewa shuleni kwa sababu anauwezo. Na huyu mtoto naye atakua akiwa na concept hiyo hiyo.
Chuki tu hata akiona mpita njia. Mohamed anatueleza kuhusu mtoto wake alivyo kipanga huko shuleni na anavyofuatilia maendeleo yake. Hawaelezi watu wa Kilwa kuhusu sekondari iliyofungwa kutokana na wanafunzi kukimbia na madhara ya jambo hilo siku za usoni. Anachowasaidia nacho ni kuwachochea kuwa wanaonewa.
Cha kushangaza wale wanaodhaniwa wangeonelewa sana wanafanya vizuri tu na mfano ni familia ya Sykes.
Masimulizi yame base katika chuki ya mtu mmoja anayetaka kufanya chuki hiyo kama 'standard kwa taifa zima'. Kwamba Mohamed kaonewa shule basi hiyo ni 'symbol' ya dhulma dhidi ya Uislam. Haoni yule profesa aliyekwenda shule bila viatu kwasababu tu alifaulu tena jina lake ni Ramzani Mohamed. Kwamba huyu hawezi kuwa symbol ya mfanikio.
Chuki kwasababu tunaambiwa kamati kuu ya TANU ndiyo iliyovunja kamati ya watu 11 ya baraza la wazee ambalo lilikuwa na wajumbe 170. Wakati huo huo tunaambiwa Mwaikela peke yake alizuia jaribio la kuua EAMWS. Sasa hapa tujiulize kwanini mtu mmoja afanikiwe kumzuia Nyerere na watu 170+ washindwe!
Kwa mtafiti wa kweli angeanzia hapo kutafuta chanzo na si Nyerere.
Ukisoma makala za Mohamed kuna mahali ukristo upo kwa ujumla na pengine kuna ukatoliki. Vyote hivyo vinachomekwa kwa makusudi ili kuleta hisia za udini. Ni hisia hizo ndizo zilizofanya hao wazee uliowataja wasitajwe kama wapigania uhuru. Sio kuwa Mohamed hajui, la hasha lakini ni katika jitihada za kupotosha umma kwa kivuli cha dini.
Mohamed anasema wazee wake waliochangia UDSM hawaku enziwa, tukamuuliza je Bhoke alikusanya na kuhifadhi hizo pesa ameenziwa vipi? hana jibu. Fundi mchundo, tumeshaonyesha hadi wakina mama wa Kipare walivyopinga ukoloni achilia mbali huko Nyanza federation n.k. Lakini mtu akiwa umefundishwa chuki hawezi kuhubiri upendo, atatafuta njia za kweli na uongo ili mradi chuki itawale.
Ndiyo maana kuna wenzetu jamvini wanaimba nyimbo za Mohamed, lakini waulize yatokanayo na nyimbo utashangaa. Hawana majibu ila wameshashiba chuki.
Kama chuki zingekuwa zinafanyika vyumbani ahalan wahsalan, lakini zinapandwa katika jamii. Tukikaa kimya nasi tutakuwa chuki kwa jamii. Tukemee!!