Hivi ATCL kufanya safari za ndege Chato, hakutaliletea hasara kibiashara Shirika hilo?

Hivi ATCL kufanya safari za ndege Chato, hakutaliletea hasara kibiashara Shirika hilo?

Kama ulivyosema wakati ule CRDB kabla ya kufungua tawi lake huko, Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alifanya "feasibility study" na kutueleza wananchi kuwa kutaleta manufaa kwa benki yake.

Tunataka kujua je ATCL imefanya hiyo "feasibility study" kabla ya kufanya maamuzi ya kurusha ndege zake huko Chato?
Uongo unaongelea Chato ya Leo au ya miaka ipi? Hii ya sasa yenye hadi mahoteli ya Kitalii?
Chato gani unayoisema wewe au unaamgalia kwenye mitandao,otrl zilipo CHATO zipo mbili tu,nazo zinamilikiwa na mtu mmoja,alizijenga kwa kwa kiiba Kodi za Wanyonge.
 
Siku chache zilizopita tulimsikia Mtendaji Mkuu wa shirika la ndege la ATCL, Ladislaus Matindi akiutangazia Umma wa watanzania kuwa shirika lake la ndege, kuanzia tarehe 9/01/2021 litaanza safari zake za ndege za kwenda kijijini Chato.

Ninavyojua Mimi ni kuwa unapokuwa kwenye biashara ni lazima kwanza ufanye "feasibility study" kujua kama mpango wako utakuletea faida kabla ya kuanza kuutekekeza.

Ninajiuliza hivi hao ATCL wamefanya kweli hiyo "feasibility study" kabla ya shirika hilo kujitumbukiza kufanya safari za ndege kuelekea huko kijijini Chato?

Nina uhakika kuwa safari hizo za shirika za ndege la ATCL kuelekea Chato zitaliingizia hasara shirika hilo, sasa ni kwanini wajitumbukize kwenye huo mradi utakaowaletea hasara?

Je, shirika hilo la ATCL kufanya safari huko Chato ni katika "kujikomba" kwa Rais wa nchi hii, John Pombe Magufuli, ambaye ni nyumbani kwake huko Chato?

Kwa kuwa tunafahamu kuwa CAG wala Bunge halitakuwa na "ubavu" wa kulihoji shirika hilo kama limekula hasara, kwa kuwa shirika hilo limehamishiwa shughuli zake kwenye ofisi ya Rais, ambapo ni "marufuku" kufanya uchunguzi kwenye shughuli zozote ambazo ziko chini ya ofisi hiyo ya Rais!

Ninavyofahamu Mimi ni kuwa shirika hilo likipata hasara ya uendeshaji wake, litapata ruzuku kutoka serikalini, ambazo ni pesa za walipa kodi wa nchi hii, za kwako na za kwangu, kwa hiyo tuna haki ya kuhoji uendeshaji wa shirika hilo.

Nimekuwa nikijiuliza hivi huo ndiyo utawala bora unaozingatia sheria za nchi hii?

Tunamuomba Mtendaji Mkuu wa shirika hilo la ATCL, Stanslaus Matindi ajitokeze hadharani na kutujibia maswali haya kama shirika lake limefanya "feasibility study" ya kutosha na kujiridhisha kuwa kupeleka safari za ndege huko kijijini Chato, kutaliletea faida shirika hilo.
Kuna maafisa wanalinda kwa namba 1 ndio watakuwa wateja wakuu.
 
ATCL bila ruzuku toka magogoni au tuseme ikulu ya chamwino lingeshajifia kitambo.Sasa lazima wajipendekeze kwa kulipa fadhili kupeleka ndege zake Chato!
 
Uongo unaongelea Chato ya Leo au ya miaka ipi? Hii ya sasa yenye hadi mahoteli ya Kitalii?
Watalii wenyewe ni akina Magufuli, Biteko na Kalemani halafu mwisho wa siku mtakuja na zile takwimu zenu kuwa sasa Chattle ndio inaongoza kwa utalii Tanzania. 🤣 🤣🤣
 
TRC
Nenda mwanza mjini uone watu wanavyofurika kutalii Mbuga ya Chato

Yaani msukuma atoke shinyanga aende kutalii mbuga za Arusha na Moshi aache iliyo hapo jirani?

Ni afunge safari toka kigoma au kagera au Tabora aende kutalii Arusha na Moshi ?

Mbuga ni huduma ya Jamii ndio maana watu wamesogezewa karibu wawaone a jirani kwa gharama nafuu miliki wangefunga safari kulipa malaki nauli na malazi kwenda Arusha na Kilimanjaro

Baada ya kupelekwa wanyama watalii wameongezeka sana mfano mbuga ya kisiwa cha sanane Mwanza Mjini week end kunafurika watalii wa kufa mtu
Kama Watalii kutoka nchi za nje wa kufa mtu wanafurika Burigi siyo kwa kupenda Mbuga bali Covid-19 huko Chato haipo na mkombozi yuko huko lakini Arusha ni kilio tu kwa kukosa watalii. Watalii toka Ulaya kwa gharama kubwa wanakuja Tanzania kuona wanyama wa aina wachache tu ambao wangeweza kuwaona kwao kwa gharama ndogo sana. Ulaya wana karibu wanyama pori wote wa duniani kote ikiwa ni pamoja na big four wetu lakini kwa gharama kubwa wanafanya uamuzi wa kuja Serengeti au Ngorongoro bila viongozi wetu kujiuliza kwa nini. Kila eneo duniani lina wanyama wake, wanyama tunaoimba kila siku wako Afrika nzimà kusini mwa Jangwa la Sahara, Asia wana wao ikiwa ni pamoja na Tiger ambaye ni mkubwa kuliko Simba wetu, Ulaya wana wao pamoja na Dubu, Amerika wana wao pamoja na Bison kaskazini na Jaguar kusini na Australia na Kangaroo wao. Kwenye Zoo za Ulaya wanyama wote hawa na wengine wanapatikana.
 
Nenda mwanza mjini uone watu wanavyofurika kutalii Mbuga ya Chato

Yaani msukuma atoke shinyanga aende kutalii mbuga za Arusha na Moshi aache iliyo hapo jirani?

Ni afunge safari toka kigoma au kagera au Tabora aende kutalii Arusha na Moshi ?

Mbuga ni huduma ya Jamii ndio maana watu wamesogezewa karibu wawaone a jirani kwa gharama nafuu miliki wangefunga safari kulipa malaki nauli na malazi kwenda Arusha na Kilimanjaro

Baada ya kupelekwa wanyama watalii wameongezeka sana mfano mbuga ya kisiwa cha sanane Mwanza Mjini week end kunafurika watalii wa kufa mtu
🙏 😛
 
Kama ulivyosema wakati ule CRDB kabla ya kufungua tawi lake huko, Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alifanya "feasibility study" na kutueleza wananchi kuwa kutaleta manufaa kwa benki yake.

Tunataka kujua je ATCL imefanya hiyo "feasibility study" kabla ya kufanya maamuzi ya kurusha ndege zake huko Chato?
Pamoja na Kimei kuja na utafiti wake bado alipingwa na tawi likajengwa. Sijajua performance ikoje sasa hivi.
 
Mji ambao traffic light zinaongoza punda waliobeba mikokoteni kuvuka barabara.
Kuna siku nilipita hapo taa zilikua kwenye red light ilibidi tusimame magari ya upande mwingine yapite hakika muda ulipita taa ya kijani ikawaka chaajabu ni hayo magari ya upande mwingine tuliyokua tunayasubiria hayakuwepo!
 
Mleta mada

Ujinga wako ni hapo ulipoandika kijijini Chato

Chato sio kijiji ni Mji
Naona hujawahi hata fika unaandika upumbavu wako hapa
Msitukanane futa hoja kwa hoja,kama alikua hana ufahamu basi mueleweshe,
 
Uchumi wa kati, speed ya kasi, kushinda kwa kishindo, tanzania ya viwanda na mengine meengi hilo la chato kwao swala dogo sanaa
 
Kuna siku nilipita hapo taa zilikua kwenye red light ilibidi tusimame magari ya upande mwingine yapite hakika muda ulipita taa ya kijani ikawaka chaajabu ni hayo magari ya upande mwingine tuliyokua tunayasubiria hayakuwepo!
Teeh teeh.
 
Chato kuna mbuga ya wanyama kuna mahoteli ya kitalii na kampuni kibao za Tours za binafsi zenye magari ya kubeba watalii

hao wote unafikiri wapo Chato bila kufanya feasibility study kuwa business zao zitalipa?
Chato ipi unayosema ?labda Kama Dsm Kuna Chato
Hotel zipo mbili tu,Tena Mmiliki ni mmoja ,alizijenga kwa pesa za Wanyonge.
Unamjua mwenye J's Motel na Chato beach resort,
Hizo kampuni za kitalii ziko Chato ipi?
Sisi ni wenyeji hapa,Bank ya CRDB iliyolazimiahwa kujengwa kijijini haina hata wateja,NMB inasubiri hadi mwisho wa mwezi ndiyo inapata wateja,
Ungesema hata mji wa Katolo /Buseresele au Runzewe unge eleweka hiyo ni mini ya kibiashara, Chato ni Kijiji kililazimishwa kuwa wilaya, Chato huwezi kuilinganiaha hata na chalinze.

Tembea uone uaiaome kwenye mitandao.
 
TRC
Kama Watalii kutoka nchi za nje wa kufa mtu wanafurika Burigi siyo kwa kupenda Mbuga bali Covid-19 huko Chato haipo na mkombozi yuko huko lakini Arusha ni kilio tu kwa kukosa watalii. Watalii toka Ulaya kwa gharama kubwa wanakuja Tanzania kuona wanyama wa aina wachache tu ambao wangeweza kuwaona kwao kwa gharama ndogo sana. Ulaya wana karibu wanyama pori wote wa duniani kote ikiwa ni pamoja na big four wetu lakini kwa gharama kubwa wanafanya uamuzi wa kuja Serengeti au Ngorongoro bila viongozi wetu kujiuliza kwa nini. Kila eneo duniani lina wanyama wake, wanyama tunaoimba kila siku wako Afrika nzimà kusini mwa Jangwa la Sahara, Asia wana wao ikiwa ni pamoja na Tiger ambaye ni mkubwa kuliko Simba wetu, Ulaya wana wao pamoja na Dubu, Amerika wana wao pamoja na Bison kaskazini na Jaguar kusini na Australia na Kangaroo wao. Kwenye Zoo za Ulaya wanyama wote hawa na wengine wanapatikana.
WWakati CCM ikilenga kupata watalii milioni mbili Dubai isiyo na mnyama hata mmoja mwaka jana wameiingiza watalii milioni kumi na saba
Ni kweli utalii sio wanyama tuu mfano mzuri ni Zanzibar
 
WWakati CCM ikilenga kupata watalii milioni mbili Dubai isiyo na mnyama hata mmoja mwaka jana wameiingiza watalii milioni kumi na saba
Ni kweli utalii sio wanyama tuu mfano mzuri ni Zanzibar
MATAGA wanafikili utalii no wanyama tu!
Mbona Zanzibar hawana hata utalii wa panya,lakini wageni ni wengi kuliko Tanganyika.
 
Nenda mwanza mjini uone watu wanavyofurika kutalii Mbuga ya Chato

Yaani msukuma atoke shinyanga aende kutalii mbuga za Arusha na Moshi aache iliyo hapo jirani?

Ni afunge safari toka kigoma au kagera au Tabora aende kutalii Arusha na Moshi ?

Mbuga ni huduma ya Jamii ndio maana watu wamesogezewa karibu wawaone a jirani kwa gharama nafuu miliki wangefunga safari kulipa malaki nauli na malazi kwenda Arusha na Kilimanjaro

Baada ya kupelekwa wanyama watalii wameongezeka sana mfano mbuga ya kisiwa cha sanane Mwanza Mjini week end kunafurika watalii wa kufa mtu
Mbuga za arusha na moshi. Ndio top 10 africa. Ndoi mbuga zinafanya watalii waje tz. Ndio mbuga kongwe zinazofanya tz inajulikana kwa vivutio.

Hiyo burigi chato haya top 10 africa haipo. Huwez fananisha na mbuga zilizopo kwenye hiyo mikoa.
 
Mbuga za arusha na moshi. Ndio top 10 africa. Ndoi mbuga zinafanya watalii waje tz. Ndio mbuga kongwe zinazofanya tz inajulikana kwa vivutio.

Hiyo burigi chato haya top 10 africa haipo. Huwez fananisha na mbuga zilizopo kwenye hiyo mikoa.
Ni top 10 kwa kutembelewa na wageni toka nje ya nchi ndani sio kweli

Siko mbuga zina watalii wa ndani wa kufa mtu mfano mikumi national park kipindi cha sana sana train za TRC zenye mabehewa kibao hupeleka watalii

Mbuga hizo nazijua na nililipa laki saba kampuni ya kitalii kuondoka na gari ya kitalii kwenda ngorongoro unakuta kumejaa watalii wengi wa nje tu

Issue sio ku capture tu soko la nje ni ku capture la ndani pia maeneo mbalimbali
 
Back
Top Bottom