t blj
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 7,035
- 16,705
Na kwa mtindo huu wa kufungiana akaunti , crdb inakwenda kupoteza wateja wengi sanaPerformance iko below 5%
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na kwa mtindo huu wa kufungiana akaunti , crdb inakwenda kupoteza wateja wengi sanaPerformance iko below 5%
Hii ya ndege kujaa kwenye booking nayo ni kichekesho kingine , Kama sio hujumaFanya kama unafanya booking mkuu, Ndege imejaa tayari.
Majungu!Na kwa mtindo huu wa kufungiana akaunti , crdb inakwenda kupoteza wateja wengi sana
Wacha1Mkoa wa Geita unatembelewa na mabillionare kadhaa kutoka nje kwa sababu ya kununua dhahabu. Vile vile Geita ni mkoa ambao unatakiwa kuwa na uwanja wa ndege. Watanzania mnakwama wapi kuwa na wasi wasi wa ndege zetu kwenda Geita? Mbona mikoa mingine hamuhoji? Kwa mfano Kilimanjaro, Dodoma, Dar Es Salaam, Zanzibar, Unguja nk. Wacheni wivu Geita ni sehemu ya Tanzania na lazima ivune kinachotokana na Tanzania.
Kodi silipiItafika tuu,ila ongeza juhudi katika kulipa kodi.
Hii zebra ya Burigi?
Sasa tutafikiaje malengo makubwa tuliyojiwekea kama Taifa ,yafaa utafakari uamuzi wako.Kodi silipi
Mimie nashindwa kuelewa kwa nini Tunawaombea mabaya ATCL. Kwanza chato ni miongoni mwa sehemu za tanzania. Na nyegine ni sehemu alietoka mh rais wetu wa tanzania. Kwahiyo kwanini tunaadama ATCL? Kama hamna abiria basi watasitisha. Zote tunajifanya wajuaji.Siku chache zilizopita tulimsikia Mtendaji Mkuu wa shirika la ndege la ATCL, Ladislaus Matindi akiutangazia Umma wa watanzania kuwa shirika lake la ndege, kuanzia tarehe 9/01/2021 litaanza safari zake za ndege za kwenda kijijini Chato.
Ninavyojua Mimi ni kuwa unapokuwa kwenye biashara ni lazima kwanza ufanye "feasibility study" kujua kama mpango wako utakuletea faida kabla ya kuanza kuutekekeza.
Ninajiuliza hivi hao ATCL wamefanya kweli hiyo "feasibility study" kabla ya shirika hilo kujitumbukiza kufanya safari za ndege kuelekea huko kijijini Chato?
Nina uhakika kuwa safari hizo za shirika za ndege la ATCL kuelekea Chato zitaliingizia hasara shirika hilo, sasa ni kwanini wajitumbukize kwenye huo mradi utakaowaletea hasara?
Je, shirika hilo la ATCL kufanya safari huko Chato ni katika "kujikomba" kwa Rais wa nchi hii, John Pombe Magufuli, ambaye ni nyumbani kwake huko Chato?
Kwa kuwa tunafahamu kuwa CAG wala Bunge halitakuwa na "ubavu" wa kulihoji shirika hilo kama limekula hasara, kwa kuwa shirika hilo limehamishiwa shughuli zake kwenye ofisi ya Rais, ambapo ni "marufuku" kufanya uchunguzi kwenye shughuli zozote ambazo ziko chini ya ofisi hiyo ya Rais!
Ninavyofahamu Mimi ni kuwa shirika hilo likipata hasara ya uendeshaji wake, litapata ruzuku kutoka serikalini, ambazo ni pesa za walipa kodi wa nchi hii, za kwako na za kwangu, kwa hiyo tuna haki ya kuhoji uendeshaji wa shirika hilo.
Nimekuwa nikijiuliza hivi huo ndiyo utawala bora unaozingatia sheria za nchi hii?
Tunamuomba Mtendaji Mkuu wa shirika hilo la ATCL, Stanslaus Matindi ajitokeze hadharani na kutujibia maswali haya kama shirika lake limefanya "feasibility study" ya kutosha na kujiridhisha kuwa kupeleka safari za ndege huko kijijini Chato, kutaliletea faida shirika hilo.
Baada ya muda kidogo utatuletea mrejesho mwenyewe tunakusubiri kwa hamu kubwa.Mimie nashindwa kuelewa kwa nini Tunawaombea mabaya ATCL. Kwanza chato ni miongoni mwa sehemu za tanzania. Na nyegine ni sehemu alietoka mh rais wetu wa tanzania. Kwahiyo kwanini tunaadama ATCL? Kama hamna abiria basi watasitisha. Zote tunajifanya wajuaji.
🤣🤣🤣Hii zebra ya Burigi?
Haa ha ha, si unajua sie ni mabingwa wa kutengeneza movies; sina hakika kama hua mnaruhusiwa kupiga picha humo ndaniHii ya ndege kujaa kwenye booking nayo ni kichekesho kingine , Kama sio hujuma
Nimesafiri Mara kadhaa na Atcl , kwenye booking naona ni last seats ,ila Siku ya safari mnasafiri na dege halijajaa hata nusu yake
Mimi tena kaka? Mi niliangalia tu ile booking nikakuta Ndege is almost full, hiyo ya kuzuia wana habari kuleta mrejesho, jeuri hiyo naitoa wapi?Lakini usiwazuie wanahabari kuleta mrejesho wa usemalo.
Nafikili hupajui CHATO,huwa unasoma kwenye mitandao,Ukisoma koments za JF siku hizi unatambua tunaelea kuwashinda wachangiaji wa Facebook na Instagram muda mfupi sana ujao.
Unapozungumzia uwanja wa Chato unazungumza uwanja wa Geita na Kahama.
Watanzania eneo lenye uchumi wa zaidi ya Dollar million 830 kwa Mwaka ukose kiwanja cha ndege hapa tunazumzia Uchumi au Matope?
Uwanja wa Ndege uwepo Kia Hai, na Geita ukosekane wakati Geita wa Uchimi mkubwa kuliko uchumi wa Utalii tulionao Tanzania.
Labda tatizo ni Chato, na kama Geita isingekuwa ni milima ya mawe basi hizi kelele zisinge kuwepo kwa kuwa Uwanja ungejengwa Geita district na sio Chato District Geita.
Mkoa wa Geita una uchumu mkubwa kuliko Mikoa yote Tanzania kasoro Dar es salaam na Mwanza tu.
Kimapato kuna Mikoa minane kwa pamoja haifikii mkoa wa Geita Pekee yake. ( Singida, Mara, Tanga, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Rukwa, Songwe na Njombe) au Mikoa mitano Manyara, Arusha Kilimanjaro, Tanga na Pwani.
Tujaribu kuweka ukweli kutuongoza katika michango yetu hapa JF.
Mkuu,usinichanganye na wana magamba tafadhari, please dont do it again, nakuomba. Mi nimeona kwenye system kwamba trend ya wateja ni kubwa, sasa kama system imenidanganya hilo si suala langu mkuu, hata wewe unweza tu ku apply uone simple as that.Ndege imejaa ya kwenda wapi? Yaani Mataga mnakazi kweli,
Ungekuwa unapajua CHATO usingesema kitu,
Chalinze ni mji mkubwa Sana kuliko Chato.
Kutoka Geita mpaka chato kuna miji midogo midogo inazidi ukubwa Chato. Kwa kweli kule wamebugi. Walishindwa nini kuweka Geita mjini?Huyo utafiti uliufanyia wapi?
Geita kuna mgodi mkubwa barani Africa wa Dhahabu wa Geita Gold mine yenye wafanyakazi kibao
Kuna wachimbaji Dhahabu binafsi kibao wenye mgodi
Kuna mahoteli ya kutalii kibao kuna kampuni za Tours kibao
Kuna matajiri wa mabasi na malori kibao
Kuna maofisa wa serikali wamiliki vituo vya mafuta biashara nk
Hizo takwimu zako mmmmm