Hivi hawa watu wanalipwa na hizi redio?

Hivi hawa watu wanalipwa na hizi redio?

aisee ,hawa wa kutuma sms sishangai sana mana ni rahisi ukiwa unajua ratiba za vipindi kwenye radio tofauti tifauti kazi yako ikawa ni kutuma tuh na wala husikilizi ivyo vipindi
Clouds utaratibu wao ulikuwa mzuri sana!
Huhitajiki kusikiliza vipindi vyote..

Mfano: ukituma text asubuhi kwenye power breakfast, watakuwa wanakunotify nini kinafuata robo saa kabla ya kipindi kinachofuta kuanza!

Kwahiyo ukipata notification hata kama huna redio, we unajilipua tu na text!

Kipindi kikianza wanaosikiliza, lazima wakusikie.

Changamoto kubwa ni majina yaleyale kujirudia daily!!!
 
Kuna kipindi nilikuwa nikisikiliza radio hukosi simu au message za hawa watu katika kipindi chochote;

1. Mwalimu Kennedy mpemba kutoka Kahama hasa kwenye DW
2. Hamisi full migebuko kutoka kigoma
3. Daudi wa kota
4. Salma Msangi kutoka Dodoma
5. Kuna mwingine Filbert japo jina la mwisho nimesahau hutuma sana DW
Filbert Kyauke
 
Lawena Nsonda,toka mimi mdogo,nasasa naelekea 40,yupo tu,sijui ana umri gani kama siyo 60s huko,sijui.
 
Lawena Nsonda,toka mimi mdogo,nasasa naelekea 40,yupo tu,sijui ana umri gani kama siyo 60s huko,sijui.
Mm huyu filbert Jonathan wa DW ...toka nikiwa primary
 
Bila kumtaja Mwita Maranya RFA hii thread itakuwa haijakamilika.

Washamba wa kanda ya ziwa wanawekewa kipindi SAA 8 za usiku hakuna kulala na kweli mikulima inakesha redioni kutuma salaam.
Wanaweza kuwa wavuvi labda ndio maana hawalali
 
Kazi ipi ya kufanya na kutuma txt radioni kila muda labda ulinzi
Kesho ukiamka saa 4 tembea na mguu kilometre kama 7 huku akiangalia watu walio kazini madukani nk nakuhakikishia 90% utawaona wanachezea simu na wakk job

Mimi kutwa mzima naperuzi JF, nimetoka Twitter, IG nk na nipo Job....suala eti huna kazi ya kufanya silielewagi kabisa
 
Back
Top Bottom