Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hivi hii hali ni kutaka tu au kujisahau? Yaan kitendo Cha mwanaume kuoa tu basi na kuvaa nguo Kwa kubadilisha kunaishia hapo full shati Moja au matatu, kazini, nyumbani na la kanisani.
Kumkuta mwanaume ameoa lakini kavaa kiatu Cha ngozi kimeachama kidogo ni kawaida sana.
Nguo zile zile hadi ukiwa mbali tunajua tu, yule anayekuja ni fulani😀 sawaMwanaume unakua na nguo nyingi za kazi gani umekua zuchu?
Mwanaume ni kuwa na suruali tatu na shati nne inatosha unamaliza mwaka mmoja na nusu bila kununua nguo mpya hapo unanunua soksi tu
Hapa sasa nimekuelewa.Ndo hicho nimemaanisha mkuu
Uende nacho wapi? Hujamsikia mfame zumalidiKATAA NDOA
TUNZA KIBUNDA CHAKO
Anasemaje tena yule bibie?Uende nacho wapi? Hujamsikia mfame zumalidi
PoleniHapa sasa nimekuelewa.
Unakumbuka suggestion yangu. Kwamba mara nyingi mke anatakiwa kuwa muonaji juu ya hii mada yako. Juwa mwanaume mwenye kujitambua anakuwa na harakati nyingi sana kuhakikisha anakidhi mahitaji ya familia. Hapa ndipo wengine hawaoni umuhimu saaana wa kukimbizana na pamba. Bora tu atimize yanayohitajika zaidi.
MAJUKUMU DADA YANGU, WEE ACHA TU.🏃🏃🏃
Inahuzunisha sana mkuu... inaumiza sanaKuna siku mwaka jana tulikuwa na semina ya shirika fulani Songea.
Sasa wakati tunatoka DSM tuliwezeshwa viposho kutoka sehemu zetu za kazi.
Sasa cha ajabu tunafika tu Iringa hapo kuna njemba zikaanza kulia njaa zinaomba kukopa kela.
Kumbe kuna baadhi ya wanaume wenzetu wakipata hela huwa wanakabidhi yote kwa wake zao, kisha wanaanza kuomba upya. Yaani hata akitaka safari kubwa au castle lite ya baridi anaomba upya kwa wife. Mimi nilivyojua hivyo nikakaza hadi tunafika songea.
Nilipotambua hilo aisee nilitamani kulia.
Kabisa cute,Kuna wenzetu wanazingua balaaThat's not fair kupendeza peke yako ni ubinafsi, kwanza hata utajisikiaje unatoka na mwenzi out hana pamba kali, hanukii vizuri, si hata wewe mwenyewe utachekwa huko, pendezeni wote, usifanye mtoto wa watu akajuta kuoa bure.