Hivi hizi Pete za Ndoa, hazivuliwagi?

Hivi hizi Pete za Ndoa, hazivuliwagi?

Morning,

Natumai tuko salama wote wanajamvi. Nina kitu naomba kueleweshwa hivi, hizi pete za uchumba na ndoa ukishavalishwa ndio unatakiwa kuvaa kila siku? Yaani unalala nazo? Unaenda nazo kuoga? Unaenda nazo kupika, kufua, kuosha vyombo? Mpaka chooni?

Mfano mtu unajisikia wiki hii kupumzika, unaweza kujipumzisha kidogo? Au ndio zinapotea kwa njia ya kutatanisha kama wananzengo wanavyodai? Hebu wazoefu niambieni maana kuna jambo linanitatiza.

Have lovely weekend guys
Daaah! Kumbe umeolewa? Mbona kimyakimya sana... Hujataka kabisa kutushtua sisi wazee wa ubwabwa na vyombo tuje tusuuze roho
 
Mi navojua pete ni urembo tu wa kukuonesha kwa jamii ya mabachela kuwa umeoa au umeolewa bila kuulizwa. Wakiiona tu wanajua hili jimbo tayari lina mgombea

Ndoa ya kweli ni nadhiri mnazojiwekea nyie wenyewe na mungu wenu kuwa tushakuwa mwili mmoja mpaka pale kifo kitakapo tutenganisha. Pete inabaki tu kuwa ishara ya kile mlichoahidiana lakini pete sio ndoa

Unaweza vaa pete na ukagegeda(dwa) vile vile na mtu asiye mke/mume wako. Na pia unaweza usivae pete kabisa na kusiwe na migegedo yoyote ya nje ya ndoa

Hiki kitu cha kuitwa pete sijakiona kwenye biblia wala hata kwa mababu zetu wa kale. Ni anasa za karne hii tu
 
Mi navojua pete ni urembo tu wa kukuonesha kwa jamii ya mabachela kuwa umeoa au umeolewa bila kuulizwa. Wakiiona tu wanajua hili jimbo tayari lina mgombea

Ndoa ya kweli ni nadhiri mnazojiwekea nyie wenyewe na mungu wenu kuwa tushakuwa mwili mmoja mpaka pale kifo kitakapo tutenganisha. Pete inabaki tu kuwa ishara ya kile mlichoahidiana lakini pete sio ndoa

Unaweza vaa pete na ukagegeda(dwa) vile vile na mtu asiye mke/mume wako. Na pia unaweza usivae pete kabisa na kusiwe na migegedo yoyote ya nje ya ndoa

Hiki kitu cha kuitwa pete sijakiona kwenye biblia wala hata kwa mababu zetu wa kale. Ni anasa za karne hii tu
Kugegeda(wa) kupo pale pale wether married or not.
Ila pete ushamba tuu kwa kweli
 
Pete za ndoa mostly ni ibada za kishetani, paganism issues.
Zingekuwa zinamake sense wanandoa wasingechepuka, wasingezaa kisirisiri na michepuko yao.
Deeply kabisa mwanaume hutakiwi kuwekewa ishara kuwa umeoa. Ni mwanamke ndiye huplewa
 
Kwa kumbukumbu,
.dash dash dash XYZ.. Pokea Pete hii kama ishara ya Agano la ........ Na blah blah nyingi hapo zinaendelea. Msingi mkubwa ni ishara ya Agano. Hii ni kwa taratibu za sisi tunaoitwa waabudu jua ila wasabato hawana hizi mambo.
Swali la msingi ni katika uhalali wa kuivua, ni swala la utashi tu inavuliwa katika nini.
Mfano Tunaivua kwenye Usaliti wa (Uzinzi) sababu tukiwa nayo inatushuhudua nafsini kama ishara ya kumbukumbu la agano.
 
Amina kijana wangu wa Kiroho!Nimefurahi kukuona hapa my son in Christ hebu sasa mimi na wewe tuongee kiimani kabisa,mimi na wewe tunaongozwa na neno la Mungu,na neno la Mungu kwetu sisi ni Biblia takatifu,ila kila nikisoma kwa utashi wangu sijaona sehemu pete inaonyeshwa kama ndio itakuwa ishara ya agano la ndoa....ukiangalia ndoa zote tunazosoma kwenye neno la Mungu sijawahi ona sehemu inasisitiziwa pete au mwenzangu kuna sehemu umekutana nayo hii kitu nijuze tafadhali...
Isije tukawa tunapractise ibada za kipagani za Rome empire
lipo neno la maana sana umelisema kwenye maelezo yako linaitwa UTASHI.

utashi ni neema ya kipekee sana Mungu amemkirimia mwanadamu. Lakini kila moja wetu pia amepewa kipawa au karama ya kufanya mambo mbalimbali kwa manufaa yake na wengine.

Taratibu za Ibada na Misa kwenye haya tunayoyaita mahekalu ya Mungu ni kwa utashi wa kibinadamu yako hivyo yalivyo. Na mambo mengi ni Imaginary tu, mengine ni sahihi na mengine sio sahihi kiroho na kimwili. Na utatafuta kwa biblia but hutakuta huo utaratibu wa mavazi wala mpangilio wa Ibada inavyopaswa kua, eti kuna sehemu ya kupiga magoti, ingine kuinamisha vichwa, kusimama au kufumba macho..

Zaid sana,
katika agano la kale, ukikamatwa umeiba unakwatwa mkono au ikithibitika umefanya uzinzi unapigwa mawe hadi kufa.

Lakini kwa matashi makubwa ya kiMungu agano jipya limehuisha mambo yote na sheria kali na kuyatakatifuza kwa msamaha na hukumu nyingine za haki.

Pete ni Ishara ya upendo na utakatifu kama Ulivyo msalaba Mtakatifu.
Ni muhimu kuheshimu na kuitunza katika matashi mema na Mungu atakubariki sana,
Aimen 🙏
 
lipo neno la maana sana umelisema kwenye maelezo yako linaitwa UTASHI.

utashi ni neema ya kipekee sana Mungu amemkirimia mwanadamu. Lakini kila moja wetu pia amepewa kipawa au karama ya kufanya mambo mbalimbali kwa manufaa yake na wengine.

Taratibu za Ibada na Misa kwenye haya tunayoyaita mahekalu ya Mungu ni kwa utashi wa kibinadamu yako hivyo yalivyo. Na mambo mengi ni Imaginary tu, mengine ni sahihi na mengine sio sahihi kiroho na kimwili. Na utatafuta kwa biblia but hutakuta huo utaratibu wa mavazi wala mpangilio wa Ibada inavyopaswa kua, eti kuna sehemu ya kupiga magoti, ingine kuinamisha vichwa, kusimama au kufumba macho..

Zaid sana,
katika agano la kale, ukikamatwa umeiba unakwatwa mkono au ikithibitika umefanya uzinzi unapigwa mawe hadi kufa.

Lakini kwa matashi makubwa ya kiMungu agano jipya limehuisha mambo yote na sheria kali na kuyatakatifuza kwa msamaha na hukumu nyingine za haki.

Pete ni Ishara ya upendo na utakatifu kama Ulivyo msalaba Mtakatifu.
Ni muhimu kuheshimu na kuitunza katika matashi mema na Mungu atakubariki sana,
Aimen 🙏
Amina mtumishi...nimebubujikwa
 
Back
Top Bottom