Hivi ilikuaje hadi urafiki wa baba na jirani yake tolu kuvunjika?

Hivi ilikuaje hadi urafiki wa baba na jirani yake tolu kuvunjika?

Mjomba wa gorofa la nne aliandaa mpaka fimbo za kumchapa Tolu akizingua. Tolu akawa mpole kama paka wa dukani.
Ila Tolu naye kama Kigogo tu maana hata msiba ulipotokea alijisahaulisha kama hajui mpaka juzi alipomtuma kitukuu chake kuja kutoa pole.

#4 alimtibulia tolu madilu ya madini kwa mapapaa wa Congo.

#4 mpenda haki. Tolu mwizi. N32 walikuwa vijana wa tolu.

#4 na tolu wanaelewana vipi kwenye hali hiyo?
 
Kuna kipindi funguo la geti letu ilisumbua,inasemekana hata vibaka walieeza kulifungua kwa kutumia vijiti!! Basi baba akamsimulia rafiki yake tolu wakiwa kilabuni,saa hiyi baba amelewa chakari,ila tolu alikuwa timamu kabisa,si unajua tolu huwa anachanganya maji mengi kwenye gongo ili aobekane kama anakunywa sana? Cha ajabu halewi,sasa si ndiyo tolu akamwahidi baba kumpa wachonga funguo mahiri kutoka mtaani kwake ili wamchongee funguo ya "maana"!baadaye baba aliporudi nyumbani na kutueleza adhma yake hiyo ya kuwapa mafundi wa tolu kazi ya kutuchongea fungup la geti mjomba alikuwepo,na akamkazia baba macho na kumwambia asithubutu kuwapa kazi hiyo mafundi wa Tolu,basi tolu AKAJA kesho yake akiwa na mafundi wake!! Baba akawatimua mafundi ila akamwambia tolu asiondoke kwanza hadi waongee,hapo ndiyo baba akamchana tolu kuwa hawaitaji mafundi wake,maana wale mafundi huwa wanapewa maagizo ya kuchonga funguo mbili,moja wanampa Tolu na nyingine wanampa mteja,so tolu akitaka kuingia kwetu muda wowote anachukua tu ile funguo ya pili na kuzama ndani!! Baba akakumbuka stori aliyopigiwa kilabuni jinsi jirani yake Papaa anavyoteseka kwa kuibiwa vijiko kila mara,tena siku nyingine anawakuta kabisa waizi wa vijiko wakiwa ndani,wakiulizwa mnataka nini ndani kwangu wanasema "hata sisi tulizaliwa hapa,ila tulitoka kidogo na sasa tumeamua kurejea" basi baba akaamua kumpiga ban tolu mazima!! Hata tolu akimsalimia yeye akawa anakaushia kikamanda,mwisho tolu aka maindi na kuamua kufanya yake,maana alijua kabisa kuwa baba ataenda mbele na kumshtua hata papaa kuhusu mwizi wa vijiko vyake!! Basi ndiyo ikawa hivyo!! Binamu ameshamwonya Mama asijipitishe pitishe kwa tolu,naamini mama atazingatia hilo, sasa hivi tunafurahia ulanzi wetu bila bugudha,tolu anatumaindi kiaina ila anawaza kama baba alimshtua mama kuhusu ilw ishu,kwa hiyo ametulia tu,ila tuombe Mungu tusiishiww chumvi na mama aende kuomba kwa tolu!! Maana hilo ndilo analosubiri Tolu! Ngoja nimalizie tumbaku yangu.
 
Na baada ya Mzee kututoka, tolu hakuonekana hata katika sala za kumuhifadhi baba yetu.

Baada ya miezi mawili tolu alianza kutuma wajumbe kuja kumuona mama mwenye dhamana ya kuongoza familia yetu.

ANGALIZO: Mama anatakiwa kuwa makini sana na tolu, anauwezo mkubwa na team yake siku hizi imeimarika vilevile tolu ni mshirika mzuri wa mataifa ya njema yenye nguvu na yanayoitolea macho familia yetu.

YANGU NI HAYO TU KWA LEO.
 
Na baada ya Mzee kututoka, tolu hakuonekana hata katika sala za kumuhifadhi baba yetu.

Baada ya miezi mawili tolu alianza kutuma wajumbe kuja kumuona mama mwenye dhamana ya kuongoza familia yetu.

ANGALIZO: Mama anatakiwa kuwa makini sana na tolu, anauwezo mkubwa na team yake siku hizi imeimarika vilevile tolu ni mshirika mzuri wa mataifa ya njema yenye nguvu na yanayoitolea macho familia yetu.

YANGU NI HAYO TU KWA LEO.
Tolu katuma salamu za rambirambi miezi takribani miwili na nusu baada ya msiba wa baba
 
Yale mawe ya yule mmasai kule mererani yalipigwa kizembe Sana na tolu. Halafu ule ununuzi wa zile Costa kwa cash tolu alihusika moja kwa moja ..kwa mzee wetu na ujuaji wake akapigwa K.O ndo maaana hakuwa na hamu na tolu Tena.
 
Tolu hanaga urafiki wa kudumu.ni opportunist na mjanja mjanja.mr tabasamu anaeishi mtaa wa nne alimshtukia mapema sana. ugonvi wao haukuanzia kwenye ushauri kama walivyodai.tatizo mwendazake alikua na kaushamba flani ndo maana aliingia miguu miwili kwa tolu.
Mwendazake hakutegemea kushikilia ufunguo wa nyumbani na mmliki ..Yani kwa ufupi hakujiandaa kuwa kama baba mwenye nyumba. Ndio maana Tolu alimwingiza mkenge Sana.
 
aise we jamaa,ni mchochezi kweli[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787].talu alitaka kumuingiza kwenye Rada zake,mzee baba!,mwanzo baba hakushtuka akaanza kujaa mdogomdogo,Kuna siku tall si akajisahau kuwa alikuwa ametega chambo,mzee akasanuka !weeee ukawa ndo mwisho wa urafiki wao,kila mmoja akawa anaishi na mwenzie kwa kujihami!!
 
PAKA ana ng'ata na kupuliza.
Mzee wa chalinze anamjua vizuri

Hao wote walikuwa wajeshi na tena wenyewe wanawaita DMI.

Waswahili wa Pemba wanaojuana kwa vilemba.

Kwenye mchuano huo tulikuwa tumelamba dume tukamaliza vifua mbere!
 
Back
Top Bottom