Hivi inawezekanaje mtu huna kazi bado unasoma Master's Degree?

Hivi inawezekanaje mtu huna kazi bado unasoma Master's Degree?

Wakuu habari za Jumapili,

Niseme, mwaka huu 2023 nimehitimu Shahada ya Umahiri ama Master's Degree kwenye fani ya uchawi na ushirikina chuo kikuu.

Kwenye kuisoma hiyo fani, kilichonishangaza sana na bado nazidi kushangaa ni kuona vijana wakisoma Shahada za Umahiri huku hawana kazi.

Najiuliza, kwa hapa Tanzania kazi zinazotangazwa zinazotaka mtu awe mahiri ni kazi ambazo lazima uwe na uzoefu usiopungua miaka 8 na kuendelea na mara nyingi kama sio zote hua ni managerial positions.

Sasa kama Shahada ya awali haijakupa kazi, haijakusaidia kupata kazi, unawezaje kwenda kusoma Shahada nyingine ya juu zaidi huku huna kazi?

Kwa mtazamo wangu, wazazi wanapoteza pesa nyingi sana kusomesha watoto wao Master's Degree ambazo wangezitumia kuwafungulia miradi ya ujasiliamali na wakapata pesa.

Leo kukuta kijana yuko mtaani na anaendesha bodaboda na ana Master's Degree ni kitu cha kawaida, unajiuliza hiyo pesa ya Master's Degree zaidi ya 10m na 2+years za kusoma, angeanza kua bodaboda si angekua mbali sana, kwanza angekua na bodaboda 5 ambazo zinamuingizia wastani wa 1.2m kwa mwezi, miaka 2 angekua na 25m+ na bado bodaboda zake ziko pale pale.

Juzi nimeenda na girlfriend wangu mahala kwa tailor, nikakuta tailor katika mazungumzo anasema ana Master's Degree ya Accountancy halafu ni fundi nguo, yeye mwenyewe anajilaumu kusoma Master's Degree bora angeaza ushonaji mapema angekuwa mbali.

Master's Degree bongo zinasomwa kwa kujifurahisha?
Sisi wengine second degree tulienda kusoma sababu ya passion ❤️😍
 
Unaposoma ni elimu ikusaidie kuishi kwa kuweza kutatua changamoto za wasiosoma. Mkisoma alafu mnarudi mtaani kulia na ambao hawakusoma ni fedheha. Someni mpate elimu....elimu ni nzuri.
Elimu ni nzuri kama pesa unazo nje ya hapo ni kujilisha upepo. Utawaamkia hadi wadogo zako siku moja na hizo elimu zako ukiwa hela huna 🤣
 
Wakuu habari za Jumapili,

Niseme, mwaka huu 2023 nimehitimu Shahada ya Umahiri ama Master's Degree kwenye fani ya uchawi na ushirikina chuo kikuu.

Kwenye kuisoma hiyo fani, kilichonishangaza sana na bado nazidi kushangaa ni kuona vijana wakisoma Shahada za Umahiri huku hawana kazi.

Najiuliza, kwa hapa Tanzania kazi zinazotangazwa zinazotaka mtu awe mahiri ni kazi ambazo lazima uwe na uzoefu usiopungua miaka 8 na kuendelea na mara nyingi kama sio zote hua ni managerial positions.

Sasa kama Shahada ya awali haijakupa kazi, haijakusaidia kupata kazi, unawezaje kwenda kusoma Shahada nyingine ya juu zaidi huku huna kazi?

Kwa mtazamo wangu, wazazi wanapoteza pesa nyingi sana kusomesha watoto wao Master's Degree ambazo wangezitumia kuwafungulia miradi ya ujasiliamali na wakapata pesa.

Leo kukuta kijana yuko mtaani na anaendesha bodaboda na ana Master's Degree ni kitu cha kawaida, unajiuliza hiyo pesa ya Master's Degree zaidi ya 10m na 2+years za kusoma, angeanza kua bodaboda si angekua mbali sana, kwanza angekua na bodaboda 5 ambazo zinamuingizia wastani wa 1.2m kwa mwezi, miaka 2 angekua na 25m+ na bado bodaboda zake ziko pale pale.

Juzi nimeenda na girlfriend wangu mahala kwa tailor, nikakuta tailor katika mazungumzo anasema ana Master's Degree ya Accountancy halafu ni fundi nguo, yeye mwenyewe anajilaumu kusoma Master's Degree bora angeaza ushonaji mapema angekuwa mbali.

Master's Degree bongo zinasomwa kwa kujifurahisha?
Usomi hauna mwisho. Soma soma soma...
Kama hauko busy na idle, soma vitabu soma tu, why not?!
 
Elimu ni nzuri kama pesa unazo nje ya hapo ni kujilisha upepo. Utawaamkia hadi wadogo zako siku moja na hizo elimu zako ukiwa hela huna 🤣
Unadhani kwanini wanasiasa wengi wanakimbilia degree za mchongo....kwamba hawana hela? Elimu ina nafasi yake hata kama utawaamkia wadogo zako,kuna namna utawasalimia kisomi
 
Unadhani kwanini wanasiasa wengi wanakimbilia degree za mchongo....kwamba hawana hela? Elimu ina nafasi yake hata kama utawaamkia wadogo zako,kuna namna utawasalimia kisomi
Wanafanya hvo ili kulamba teuzi tu

Nje na hapo huwezi kuta wanazihangaikia

Sasa wewe huna mbele wala nyuma unafukuzia mi masters ya nini
 
Mlima mpaka wakome.
Ila najua wapo manunda watasema kusoma sana ni ufala.
Na mimi kupitia mtazamo wao huo kila mara nitakuwa wale wazee wakujitapa mbele zao hasa nikiwa nimewaacha mbali
Hongera mkuu elimu ni nzuri...na mimi hii yangu ya form siksi kuna wakati ilinipa shavu katikati ya kundi la wajinga na sikuamini. Katu sitoidharau elimu. Mungu nisaidie.
 
Back
Top Bottom