Hivi inawezekanaje mtu huna kazi bado unasoma Master's Degree?

Hivi inawezekanaje mtu huna kazi bado unasoma Master's Degree?

Nimemuonya shemeji yangu amemaliza digrii ya public administration akakaa mtaani kujaribu kufuga kuku ameshindwa eti Sasa anamrubuni Mzee atoe kibunda Cha korosho akasome masters ! Akili zinatoka mbali sana
 
Kama ana Degree ya Accountancy asome CPA hiyo CPA ni marketable than masters
Kama ana Degree ya Law ni Bora asome law school awe Wakili,
Wote wanasota tu, cpa, masters, degree. Graduate asiye na bahati ya kazi na hana uwezo wa kujiajiri kwa kiwango cha elimu yake hata umpe level gani ya elimu haitampa kipato.
 
Wakuu habari za Jumapili,

Niseme, mwaka huu 2023 nimehitimu Shahada ya Umahiri ama Master's Degree kwenye fani ya uchawi na ushirikina chuo kikuu.

Kwenye kuisoma hiyo fani, kilichonishangaza sana na bado nazidi kushangaa ni kuona vijana wakisoma Shahada za Umahiri huku hawana kazi.

Najiuliza, kwa hapa Tanzania kazi zinazotangazwa zinazotaka mtu awe mahiri ni kazi ambazo lazima uwe na uzoefu usiopungua miaka 8 na kuendelea na mara nyingi kama sio zote hua ni managerial positions.

Sasa kama Shahada ya awali haijakupa kazi, haijakusaidia kupata kazi, unawezaje kwenda kusoma Shahada nyingine ya juu zaidi huku huna kazi?

Kwa mtazamo wangu, wazazi wanapoteza pesa nyingi sana kusomesha watoto wao Master's Degree ambazo wangezitumia kuwafungulia miradi ya ujasiliamali na wakapata pesa.

Leo kukuta kijana yuko mtaani na anaendesha bodaboda na ana Master's Degree ni kitu cha kawaida, unajiuliza hiyo pesa ya Master's Degree zaidi ya 10m na 2+years za kusoma, angeanza kua bodaboda si angekua mbali sana, kwanza angekua na bodaboda 5 ambazo zinamuingizia wastani wa 1.2m kwa mwezi, miaka 2 angekua na 25m+ na bado bodaboda zake ziko pale pale.

Juzi nimeenda na girlfriend wangu mahala kwa tailor, nikakuta tailor katika mazungumzo anasema ana Master's Degree ya Accountancy halafu ni fundi nguo, yeye mwenyewe anajilaumu kusoma Master's Degree bora angeaza ushonaji mapema angekuwa mbali.

Master's Degree bongo zinasomwa kwa kujifurahisha?
Au mtu anatoka 1st Degree anaunganisha na Masters.

Sasa sijui anaenda kusoma kumaster kitu gani.
 
Unajua hakuna mtu mwenye uhakika kwamba akifanya nini atafanikiwa. Kila mtu anajaribu. Kuna watu drs la saba wana mafanikio kuna drs la saba ni mafukara wa kutupwa. Kuna mtu masters ndo imempa +advantage akapata kazi nzuri kuna mtu diploma ndo imempa kazi nzuri.

Jamani. KILA MTU APAMBANE KWA LILE AMBALO ANAONA LINAWEZA KUMPA MAISHA ANAYOYATAKA, TUSIWE WACHAWI KUKAA NA KUTAFUTA WANAOKOSEA MAISHA TUWAITE WAJINGA. MAISHA HAYANA NJIA YA UHAKIKA YA MAFANIKIO.
 
Back
Top Bottom