Hivi kuna ulazima wa wakati Rais wa JMT anaapisha wateule wake hafla kuhudhuriwa na viongozi wakuu wote na wale wa vyombo vya dola?

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Nauliza tu maana utaratibu huu ulianza awamu ya 5 ambapo Rais wa JMT anapoapisha wateule wake viongozi wote wakuu wa serikali na wa vyombo vya dola lazima wanakuwepo.

Je, kuna ulazima wowote hawa viongozi kuhudhuria hata uapisho wa watu wadogo wadogo kama maDED na maDC?

Ni hilo tu.
 
Kwa nini hukuuliza tangu wakati huo wa awamu ya tano! Na uje uulize leo? Huu siyo unafiki kweli Bwashee!!
 
Ulikuwa ni Ushamba na Ulimbukeni wa Mwendazake.

Mwendazake alikuwa anaona Fahari sana kuzungukwa na Maaskari Muda wote, ndio.Maana hata Kisarawe kwa Yule Bi Dada alienda na CDF, IGP na Mkuu wa Usalama na ma Generali kadhaa
 
Ulikuwa ni Ushamba na Ulimbukeni wa Mwendazake.
Mwendazake alikuwa anaona Fahari sana kuzungukwa na Maaskari Muda wote, ndio.Maana hata Kisarawe kwa Yule Bi Dada alienda na CDF, IGP na Mkuu wa Usalama na ma Generali kadhaa
Wewe ulitaka aone fahari kuzungukwa na vimada?
 
Hili hata mimi najiuliza. Na akirudi safari viongozi wote wanaenda kumpokea. Angekemea hii tabia. Spika, Jaji Mkuu, Mkuu wa majeshi, IGP wanatakiwa kuonekana nae kwa nadra sana. Hasa Spika na Jaji Mkuu.

Amandla...
 
Si lazima....

Ila ni utaratibu wa nchi yetu tu ambayo hufuata nchi za jumuiya ya madola......

Ikumbukwe NCHI YETU ni ya "kipekee" kuanzia UJAMAA WAKE WA KIAFRIKA mpaka MUUNGANO WAKE wa nchi mbili....

Yako Mambo ambayo si lazima kuyaiga kwa wengine na ambayo hutupa UPEKEE na UTULIVU wetu wa kupigiwa mfano......

Mfano marekani ,wale secretaries (mawaziri wao) baada ya kuteuliwa huapa na kuapishwa bungeni tena haihudhuriwi na wabunge wote(senates) bali wale wa kamati ihusuyo wizara hiyo...mfano;Kamati ya bunge ya Mambo ya nje hushuhudia uapisho wa WAZIRI WA MAMBO YA NJE......

#StaunchSupporterOfTanzania
#DieHardFanOfCCM
 
bora hata huyu hapeleki chato
 
Siyo lazima. Ujinga huu umeanzishwa na lile zimwi tulilojichqnganya na kulipatia nchi. Bahati nzuri pacemaker imeingilia Kati.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…