Hivi kweli kuna biashara ya kuingiza faida kuanzia milioni 100 na kuendelea kwa siku/wiki/mwezi?

kiongozi million 100 ndogo sana kwa wafanya biashara watu wanaingiza milioni 500 kwa siku ijekuwa iyo 100.
Kwa biashara gani hiyo mkuu ebu weka na mfano basi tujue maana kariakoo hakuna biashara ya faida ya mil20 kwa siku
 
Watu wengine hata reasoning kidogo tu hawana watu wamewekeza kwenye uchimbaji madini lakini hiyo mil100 anaingiza ndani ya mwez na sometimes inafeli na niuwekezaji mkubwa. Sasa kariakoo kunauwekezaji gani hapo wa kuingiza mil100
 
Hujui biashara kijana wewe so unajua faida iliyopo kwenye semi ya nondo wew..tufautisha mauzo na faida...hakuna kitu kinachoitwa faida ya siku. Mwenzio faida anaihesabu pale mzigo unapoisha anatoa import taxes ambazo ni kama pasu kwa pasu na faida bado gharama za uendeshaji wa biashara na mishahara. Kinachobaki sio haba kwa kapuku kama wewe ila ni kilio kwa tajiri. Biashara haiko kama unavyodhani na usione semi zinapakia mizigo mingi hapo hailipiwi cash ni mwendo wa mali kauli sasa unapozungumzia faida ya mil100 kwa siku nakuona kichaa. Hizo ni faida za viwanda.
 
Hapa inshu sio mtaji mkubwa,kwani kwa biashara yenye kuleta faida ya milioni 100 kwa siku lazima uwe mkubwa sana!!inshu ni MAUZO hapa ambayo yatakuletea faida hiyo,unaweza kuwa na mtaji mkubwa(stock) lakini mauzo yakawa madogo!!hebu niambie kwa biashara za kariakoo yupi anaweza kuwa na mauzo ya milioni 800-bilioni moja kwa siku?!!ndii aweze kupata faida hiyo??hata kwa wanaouza mitambo kama ya ujenzi wa barabara hawezi kuwa anauza kila siku!!kwani hao ndio unakuta akiuza item moja tu milioni 2!!
 
Wachana na Biashara za Kariakoo, fanya biashara ya mazao makavu.

Utazungusha hata billion 5 kwa siku bila shaka yoyote ile.
 
Biashara ya mizigo ni nzuri
 
Biashara ya spare upate eneo zuri
 
Biashara ya pembejeo inalipa Sana aiseee
 
Kumbuka huwezi kuingiza faida ya milioni 100 kwa muda ulosema kwa mtaji wa milioni mia mbili au hata milioni mia tatu au nne. Kwanza capital, pili aina ya biashara, tatu idadi ya wateja iwe large scale.
Nimeshuhudia kuna watu wanaingiza faida milioni mia tano kwa siku pale Kariakoo. Biashara ya simu za jumla wale ma agent waloingia ubia na viwanda vya simu China. Unakuta wafanyabiashara wote wanachukua mzigo kwake na kila Pisi moja unakuta faida elfu 5 tu na viswaswadu unakuta faida hadi buku tu. Sasa kwa siku anauza katoni nyingi sana za smartphone na viswaswadu brands zote itel, tecno, infinix, samsung n.k Na katoni moja mara nyingi ina simu 60pcs au 40pcs.
 
Umeambiwa kariakoo wewe

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…