Hivi lengo la Hamas lilikuwa ni nini ile Oktoba 7, 2023?

Hivi lengo la Hamas lilikuwa ni nini ile Oktoba 7, 2023?

Ni kweli wapalestina wanadhulumiwa na wanaonewa sana kwa miaka mingi, ila uamuzi wa Hamas kufanya tukio lile Oct 7 haukuwa sawa
Kwahiyo hata Ukraine wanakosea kujitetea dhidi ya Russia sababu watamprovoke aiharibu Kyiv kwa nuclear?
 
Lengo ilikuwa ni kuifuta Islael katika uso wa Dunia..
Yale makombora zaidi ya 1000 yangetua yote Islael wangeweza kufa maelfu kwa maelfu - na wao HAMAS wakisaidiwa na Iran wangetumia muda huo huo kuitawala.

HAMAS kosa lao kubwa ni kutojua uwezo wa Islael kijeshi, na kama walijua basi ni wapumbavu kupita kiasi.
Ni kweli maisha ya GAZA hayayarudi tena, leo taifa la parestina limekuwa la kwanza kwa idadi ya watu wasio na viungo vya mwili Duniani.
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda sasa bila kupata majibu.

Kwa nini Hamas walianzisha chokochoko ambayo msukosuko wake hawawezi kuustahimili?

Wapalestina wa Gaza wanapaswa kuilaani kabisa Hamas na kuipinga kwa hali zote.

Ndiyo, Wapalestina hao wa Gaza walikuwa wanaishi kwenye mazingira magumu sana, kwa hisani ya Israel.

Lakini kabla ya Oktoba 7, hali haikuwa mbaya kama ilivyo hivi sasa.

Sasa hao Hamas wakijua kabisa uwezo wao pamoja na ule wa adui yao, kwa nini waanzishe songombingo ambayo walijua kabisa hawawezi kuimudu?

Labda walikuwa wakiichukulia poa Israel.

Viongozi wa Hamas ni wapumbavu sana. Gaza haitorudi kuwa Gaza tena.

Ndo matatizo ya kuongozwa na watu wapumbavu.

In the end, was it all worth it? I think not.
Kusema ukweli hata mimi nilijiuliza sana nini hasa lilikuwa lengo la walichokifanyq maana walio kwenda kuchokozwa ni zaidi ya walivyo wafikiria. Sasa imebadilika na kuwa kilio cha kuonewa.
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda sasa bila kupata majibu.

Kwa nini Hamas walianzisha chokochoko ambayo msukosuko wake hawawezi kuustahimili?

Wapalestina wa Gaza wanapaswa kuilaani kabisa Hamas na kuipinga kwa hali zote.

Ndiyo, Wapalestina hao wa Gaza walikuwa wanaishi kwenye mazingira magumu sana, kwa hisani ya Israel.

Lakini kabla ya Oktoba 7, hali haikuwa mbaya kama ilivyo hivi sasa.

Sasa hao Hamas wakijua kabisa uwezo wao pamoja na ule wa adui yao, kwa nini waanzishe songombingo ambayo walijua kabisa hawawezi kuimudu?

Labda walikuwa wakiichukulia poa Israel.

Viongozi wa Hamas ni wapumbavu sana. Gaza haitorudi kuwa Gaza tena.

Ndo matatizo ya kuongozwa na watu wapumbavu.

In the end, was it all worth it? I think not.
Sinwar ndie alikuwa mastermind wa huu mpango.

Lengo lake lilikuwa ni kuipiga tukio Israel, tukio kubwa ambalo litawafanya wayahudi waingie vitani kuipiga Gaza.

Wakishafanya hayo, waliamini nchi za kiarabu na makundi yote ya wapigania haki na uhuru wa wapalestine watasimama na Hamas kuipiga Israel. Iran, Hezbola, Houth nk watajiunga katika hii vita ya kuifuta Israel.

Lilikuwa kosa kubwa na mahesabu mabovu. Wameipoteza Gaza yote.
 
Hammas walivamia Israel wakitokea Gaza.
Mandela alivamia nchi gani?
Kwamba hujui kipindi cha Apartheid nchi iligawanywa kwa maeneo ya wazungu, Waafrika na cape coloureds? Kingine Palestina sio recognised kama nchi tokea iwe occupied na Israel so wakivamia Israel haina tofauti na Mandela kuvamia makazi ya wazungu.
 
Kwamba hujui kipindi cha Apartheid nchi iligawanywa kwa maeneo ya wazungu, Waafrika na cape coloureds? Kingine Palestina sio recognised kama nchi tokea iwe occupied na Israel so wakivamia Israel haina tofauti na Mandela kuvamia makazi ya wazungu.

Mbona hata hapa nchini kuna maeneo yamegawanywa mahususi kwa watu Fulani.

Nazungumzia nchi kuvamia nchi nyingine.
 
Lengo ilikuwa ni kuifuta Islael katika uso wa Dunia..
Acha uongo, lengo ilikua kujikomboa. Huwezi futa taifa kwa mabomu 1000 tena sio Anti Ballistic missiles.
Yale makombora zaidi ya 1000 yangetua yote Islael wangeweza kufa maelfu kwa maelfu - na wao HAMAS wakisaidiwa na Iran wangetumia muda huo huo kuitawala.
Why elfu 1? Wakitaka kuifuta si Iran inarusha nuclear tu hapo Tel Aviv kwani kigumu kipi?
HAMAS kosa lao kubwa ni kutojua uwezo wa Islael kijeshi, na kama walijua basi ni wapumbavu kupita kiasi.
Kumbe ukitaka kudai uhuru lazima uangalie uwezo wa mkoloni? Kwamba Mandela naye alipaswa kuogopa nguvu ya kijeshi ya makaburu ambao walikua mpaka na miradi ya nuclear? Hivi kina Nyerere na Mandela wangeogopa silaha za wazungu!! Tungepata uhuru?
Ni kweli maisha ya GAZA hayayarudi tena
Kwanini yasirudi? Kwani ni mara ya kwanza wao kulipuliwa? Au hujui miaka 70 sasa Gaza inapigwa mabomu tu kila kukicha.

Vipi Ukraine haijaharibiwa na Putin? Au nao walifanya makosa kujitetea dhidi ya uvamizi wa Russia?
 
Mbona hata hapa nchini kuna maeneo yamegawanywa mahususi kwa watu Fulani.

Nazungumzia nchi kuvamia nchi nyingine.
Sasa hao Israel hawaitambui Palestina kma nchi bali huitambua kama mamlaka tu!! Kwahiyo ni sawa tu na labda ceuta na merilla zivamie mainland Spain utasema ni nchi imevamiwa na nchi?

Pilj, Hapa nchini hakuna maeneo ya makazi ambayo yanakataza watu weusi wasiingie. Kwamba mweusi hutakiwi kuingia CBD ya ilala??
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda sasa bila kupata majibu.

Kwa nini Hamas walianzisha chokochoko ambayo msukosuko wake hawawezi kuustahimili?

Wapalestina wa Gaza wanapaswa kuilaani kabisa Hamas na kuipinga kwa hali zote.

Ndiyo, Wapalestina hao wa Gaza walikuwa wanaishi kwenye mazingira magumu sana, kwa hisani ya Israel.

Lakini kabla ya Oktoba 7, hali haikuwa mbaya kama ilivyo hivi sasa.

Sasa hao Hamas wakijua kabisa uwezo wao pamoja na ule wa adui yao, kwa nini waanzishe songombingo ambayo walijua kabisa hawawezi kuimudu?

Labda walikuwa wakiichukulia poa Israel.

Viongozi wa Hamas ni wapumbavu sana. Gaza haitorudi kuwa Gaza tena.

Ndo matatizo ya kuongozwa na watu wapumbavu.

In the end, was it all worth it? I think not.
Kwa kujibu wa media za Uturuki lilimnukuu marehemu yahya Sinwalli kuwa waliivamia Israel ili kuleta mzozo wa ghaza kwenye agenda za kimtaifa

USSR
 
Nilisema mahali fulani humu jukwaani, narudia: Wapalestina waliobaki wanapaswa kutathmini sana kuhusu siasa zao za ndani na aina ya washirika walionao.
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda sasa bila kupata majibu.

Kwa nini Hamas walianzisha chokochoko ambayo msukosuko wake hawawezi kuustahimili?

Wapalestina wa Gaza wanapaswa kuilaani kabisa Hamas na kuipinga kwa hali zote.

Ndiyo, Wapalestina hao wa Gaza walikuwa wanaishi kwenye mazingira magumu sana, kwa hisani ya Israel.

Lakini kabla ya Oktoba 7, hali haikuwa mbaya kama ilivyo hivi sasa.

Sasa hao Hamas wakijua kabisa uwezo wao pamoja na ule wa adui yao, kwa nini waanzishe songombingo ambayo walijua kabisa hawawezi kuimudu?

Labda walikuwa wakiichukulia poa Israel.

Viongozi wa Hamas ni wapumbavu sana. Gaza haitorudi kuwa Gaza tena.

Ndo matatizo ya kuongozwa na watu wapumbavu.

In the end, was it all worth it? I think not.
walijipanga kwa miaka mingi tu, trained mno, na mle ndani kulikuwa na wanajeshi hadi wa iran, wale walikosa vifaa tu ila walikuwa makomandoo wazuri mno kwa vita. Lengo lao ilikuwa kuvamia israel, kuanza kuua, vita ianze, hamas apige kutokea gaza, hezbollah awasaidie kutokea lebanon, na iran amalizie ili isrel ifutike.ndio maana adui wa Mungu ayatollah alikuwa anaongea wazi kitambo kwamba kuna siku mzayuni atafutika kwenye ramani pale. bahati mbaya, matokeo yakawa tofauti, myahudi ameuwa karibu magaidi wote wa hamas, kauwa makamanda wa kutosha wa iran, hezbollah aliyekuwa na malaki ya silaha akaingia, viongozi wake wakuu wote wameshauza sasaivi, ikabaki kutazamia ceasefire, iran kaenda kuwaambia waache vita wapokee ceasefire.

matokeo: majengo kadhaa ya israel yamebomoka na watu kadhaa wameuawa, ila upande wa gaza, haikaliki, imeteketezwa yote. hakuna sehemu gaza bom halijatua. na kwa hezb, majengo yote wanayomiliki yavunjwa, wamepata hasara ambayo hawakutegemea.

way forward: mzayuni anajiandaa tukio kama lile lisijetokea tena, anajenga silaha bora, na kununua zingine. Israel haitakuja kufutika milele. kwa sababu pale Yerusalem ndio mji wa Mungu.
 
Itikadi kali ndio ipi? Hamas ni chama cha siasa hao wanaopigana ni wing inaitwa Al Qassam brigade
Acha kujitoa ufahamu. Hicho chama cha siasa kina mlengo upi? Hizi millitary wings zinapambana chini ya mwamvuli wa chama kipi kama siyo Hamas?
Na iweje hamas ambacho ni chama cha kisiasa cha kiislamu ndo kipambanie uhuru wa nchi ambayo inaundwa na dini tofauti?
Je, ANC na Mandela ni wapi walitumia itikadi za kidini au ANC na chenyewe kilikuwa chama cha kidini hadi uwalinganishe na Hamas?
 
Laiti Hamas wangepiga vizuri mahesabu yao, leo hii pengine akina Sinwar, Haniyeh, Nasrallah, Deif, na wengineo wangekuwa bado wako hai.

Pia, pengine hata Assad angekuwa bado ni Rais wa Syria.
 
Hicho chama cha siasa kina mlengo up
Kulikua na uchaguzi 2006 wa wabunge na chama kilichoshinda Gaza ni Hamas na kuwaangusha vyama vingine kama Fatah etc. Kwahiyo Hamas ni chama cha siasa kama to republicans au Democrats.
Hizi millitary wings zinapambana chini ya mwamvuli wa chama kipi kama siyo Hamas?
Ndio nakwambia military wing inaitwa Al qassem Brigade, ni sawa tu na ANC ilivyokua na military wing ya Umkhonto we Sizwe, au CCM na green guards.
iweje hamas ambacho ni chama cha kisiasa cha kiislamu ndo kipambanie uhuru wa nchi ambayo inaundwa na dini tofauti?
Hamas sio chama cha kiislamu ni chama cha kisiasa kilichosajiliwa rasmi na kina wabunge kabisa na mawaziri. Unaposema ni chama cha kiislam ni kutokana na usajili upi huo?
Je, ANC na Mandela ni wapi walitumia itikadi za kidini au ANC na chenyewe kilikuwa chama cha kidini hadi uwalinganishe na Hamas?
Mie siongelei udini naongelea UGAIDI, hao ANC walikua wanatega mabomu na kulipua majengo kwenye maofisi ya wazungu na wakati mwingine kuuwa hata waafrika wenzao lakini Mandela tunamuita shujaa sio gaidi ndio maana nashangaa huu undumila kuwili ni kwa faida ya nani?
 
Laiti Hamas wangepiga vizuri mahesabu yao, leo hii pengine akina Sinwar, Haniyeh, Nasrallah, Deif, na wengineo wangekuwa bado wako hai.
Oooh kumbe ni bora utunze uhai wako kuliko kupigania uhuru wa generations za baadae..... kwahiyo Mkwawa na Kimathi walitakiwa waangalie uhai wao sio kupigania uhuru? Typical coward.

Pia, pengine hata Assad angekuwa bado ni Rais wa Syria
Assad anahusiana nini na Hamas? If anything hawa waasi ndio watakua hatari zaidi kwa Israel kuliko Assad aliyekua toothless neighbor.
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda sasa bila kupata majibu.

Kwa nini Hamas walianzisha chokochoko ambayo msukosuko wake hawawezi kuustahimili?

Wapalestina wa Gaza wanapaswa kuilaani kabisa Hamas na kuipinga kwa hali zote.

Ndiyo, Wapalestina hao wa Gaza walikuwa wanaishi kwenye mazingira magumu sana, kwa hisani ya Israel.

Lakini kabla ya Oktoba 7, hali haikuwa mbaya kama ilivyo hivi sasa.

Sasa hao Hamas wakijua kabisa uwezo wao pamoja na ule wa adui yao, kwa nini waanzishe songombingo ambayo walijua kabisa hawawezi kuimudu?

Labda walikuwa wakiichukulia poa Israel.

Viongozi wa Hamas ni wapumbavu sana. Gaza haitorudi kuwa Gaza tena.

Ndo matatizo ya kuongozwa na watu wapumbavu.

In the end, was it all worth it? I think not.
Screenshot_20241208-173758_Chrome.jpg
 
Back
Top Bottom