Hivi mnawezaje kuwapeleka watoto wenu wa kike wakafanye kazi za ulinzi?

Ni kweli tu maskini lakini kuna kazi nyingine za kimaskini kwa wanawake tofauti na ulinzi tuwatafutie kazi nzuri nzuri watoto wetu wa kike

Kuna mwingine binti mbichi tu wa form4 anampeleka huko wakati option zipo nyingi tu kwa umri huo
 
Sasa sheria inasema wanawake wasachiwe na wanawake wenzao, nani atawasachi kusipokua na wanawake walinzi ?
Swali zuri na fikirishi pia

Jibu ni kuwa sheria zinatungwa kufuata matakwa ya jamii hazijakuwepo kama biblia au quran kuwa zifuatwe tu bila kurekebishwa kwa hapo tutarekebisha kulingana na uhitaji
 
Simaanishi wasifanye hapana maisha ni magumu mkuu inabidi lakini hasa kazi za ulinzi ni ngumu na mshahara kidogo sana....... Plus mazingira yake...

Niseme tuu hivyo Mr
Tuwachagulie kazi nzuri watoto wetu wa kike zipo nyingi tu tofauti na ulinzi
 
Unataka kuwasagia kunguni wale wooote (Ke)walio huko JW; Magereza; Polisi; ; Wanyama pori; Uhamiaji n.k. wasitishe Ajira kwa kisa ni mtoto wa kike?.
Utakuwa hujawatendea haki. Mpe kazi, akishindwa badilisha weka mwanaume.
 
Tuwachagulie kazi nzuri watoto wetu wa kike zipo nyingi tu tofauti na ulinzi
Mara nyingi nimekuwa nazungumza nao hasa agemates au wadogo nawashauri wajikite kwenye ufundi cherehani, mapishi, ususi na urembo, zaidi hizi akiwekeza kujifunza, akawa na mtaji ama akaajiriwa ni salama zaidi kwao
 
Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
 
Mara nyingi nimekuwa nazungumza nao hasa agemates au wadogo nawashauri wajikite kwenye ufundi cherehani, mapishi, ususi na urembo, zaidi hizi akiwekeza kujifunza, akawa na mtaji ama akaajiriwa ni salama zaidi kwao
Unawapa ushauri mzuri sana na hizo ndio kazi za kike
 
maneno yako hayana tofauti na ya yule mama wa vijisenti vya mboga au wakati ule wakazi wa kigamboni tulipoambiwa tulishindwa kulipia kivuko tupige mbizi...
Fungua code mkuu
 
Unataka kuwasagia kunguni wale wooote (Ke)walio huko JW; Magereza; Polisi; ; Wanyama pori; Uhamiaji n.k. wasitishe Ajira kwa kisa ni mtoto wa kike?.
Utakuwa hujawatendea haki. Mpe kazi, akishindwa badilisha weka mwanaume.
Kwa watoto wa vigogo sina shida nao hao ni vitengo maalum hao course nzima ya jkt ni maselule na vyeti wanapewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…