Hivi Mungu yupo au ni mipango ya watu kujipatia ajira na pesa?

Hivi Mungu yupo au ni mipango ya watu kujipatia ajira na pesa?

QURAN 4: 82
"Hebu hawaizingatii hii Qur'ani? Na lau kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani yake hitilafu nyingi '

Hebu rudia aya nilyoileta pale juu Quran 30:21-27 uangalie kama kuna uongo wowote hapo. Haya ni ambayo ni kweli katika uhalisia wa maisha yetu ya kila siku
-ni kweli Mvua inatoka mawinguni na ardhi ikipata maji inanawiri na kutoa mazao mapya
-ni kweli kuwa binadamu tumeumbwa kwa udongo scientifically proved
-ni kweli wanadamu tumetofautiana rangi na lugha na tumetawanyika duniani kote
- ni kweli binaadamu wote tunalala usiku na mchana tunatafuta riziki ya kuendesha maisha yetu
-ni kweli wanaume wanapata utulivu kutoka kwa wake zao
-ni kweli mbingu imesimama bila nguzo yeyote
aliyosema hayo ni Mwenyezi Mungu, je kuna uongo wowote hapo?
Duh
 
Taifa kubwa la Marekani kwenye dollar yao wameandika In God we trust, wewe ni nani hujavumbuwa hata vuzi la bata use na mashaka na uwepo wa Mungu?

Ungeuliza uhalali wa dini kama ni za kweli au magumashi ningekuelewa na ningekujibu dini ni project na investment za binadamu, lakini Mungu yupo.
Bila picha ya dollar?
 
Waroma 1:19 kwa sababu mambo yanayoweza kujulikana kuhusu Mungu yako wazi kabisa kati yao, kwa maana Mungu aliyaweka wazi kwao. 20 Kwa maana sifa zake zisizoonekana, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kupitia vitu vilivyoumbwa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu, hivi kwamba hawana sababu ya kujitetea
 
Waroma 1:19 kwa sababu mambo yanayoweza kujulikana kuhusu Mungu yako wazi kabisa kati yao, kwa maana Mungu aliyaweka wazi kwao. 20 Kwa maana sifa zake zisizoonekana, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kupitia vitu vilivyoumbwa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu, hivi kwamba hawana sababu ya kujitetea
Sidhani
 
QURAN 4: 82
"Hebu hawaizingatii hii Qur'ani? Na lau kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani yake hitilafu nyingi '

Hebu rudia aya nilyoileta pale juu Quran 30:21-27 uangalie kama kuna uongo wowote hapo. Haya ni ambayo ni kweli katika uhalisia wa maisha yetu ya kila siku
-ni kweli Mvua inatoka mawinguni na ardhi ikipata maji inanawiri na kutoa mazao mapya
-ni kweli kuwa binadamu tumeumbwa kwa udongo scientifically proved
-ni kweli wanadamu tumetofautiana rangi na lugha na tumetawanyika duniani kote
- ni kweli binaadamu wote tunalala usiku na mchana tunatafuta riziki ya kuendesha maisha yetu
-ni kweli wanaume wanapata utulivu kutoka kwa wake zao
-ni kweli mbingu imesimama bila nguzo yeyote
aliyosema hayo ni Mwenyezi Mungu, je kuna uongo wowote hapo?
Hii "- ni kweli wanaume wanapata utulivu kutoka kwa wake zao" sikubaliani nayo kabisa kabisa. Walau ingekuwa inasomeka kwamba "-Wanaume wameumbiwa kupata kadhia na madhila mengi kutoka kwa wake zao" ningekubali (sio nia yangu hapa kuanzisha uzi)
 
Taifa kubwa la Marekani kwenye dollar yao wameandika In God we trust, wewe ni nani hujavumbuwa hata vuzi la bata use na mashaka na uwepo wa Mungu?

Ungeuliza uhalali wa dini kama ni za kweli au magumashi ningekuelewa na ningekujibu dini ni project na investment za binadamu, lakini Mungu yupo.
Kwani Dollar ya kimarekani sio project ya kibinadamu?

Dini zikitangaza habari za Mungu uko tayari kuzipinga kusema ni za uongo kwasbabu ni project za kibinadamu

Lakini ukiona maandishi ya "In God we trust" kwenye Dollar ya kimarekani unayachukulia kwa uzito bila kuzingatia nayo ni sehemu ya project za binadamu.

Vipi kama walioandika hayo maandishi kwenye Dollar waliyatoa kwenye vyanzo vya dini ambazo hauko tayari kuzikubali?

Huoni kwamba kwa mujibu wako hiyo itaaminisha kuwa Mungu hayupo kwasbabu vyanzo vyote vilivyotaja habari zake ni project za watu?
 
Hii "- ni kweli wanaume wanapata utulivu kutoka kwa wake zao" sikubaliani nayo kabisa kabisa. Walau ingekuwa inasomeka kwamba "-Wanaume wameumbiwa kupata kadhia na madhila mengi kutoka kwa wake zao" ningekubali (sio nia yangu hapa kuanzisha uzi)
Kabisa
 
Uzuri haulazimishwi yaani unatoa kwa hiyari..., tatizo ni wale wanaongaganiza michango na harambee..., kwa hao sio poa au wengine vitisho vya kutokuzikwa au kupewa huduma
 
Ogopa hiyo kauli,Tajiri wa Titanic alisema meli yake haitazamishwa hata na Mungu, safari ya kwanza ikazama.

Fikiria shahawa zinakua mtu, mbegu inaota, unavuta hewa free.
Umeishi wapi siku zote hizo mpaka uje leo kuuliza kuhusu uwepo wa Mungu? uko serious kweli? Kahoji mambo mambo mengine usiendelee kuhoji mambo yaliyokuzidi kimo. Kasema vitabu vitakatifu. Tafuteni shughuli za kufanya muepuke kuhoji vitu vya ajabu ajabu. Ungekuwa unajishighulisha usingepata muda wa kuhoji mambo km haya
 
......alimwambia Musa kuwa hakuna mwanadamu anaweza kumuona akaishi......
Kwa mantiki hiyo, mtu atakapokoma kuwa mwanadamu (akishakufa) i.e akawa ni Roho, hapo ndipo atamwona Mungu. Nimefurahi sana kwa kauli hii.
Mkuu, sioni kama baada ya kifo kuna existence maana muhubiri 9:5,6,10 inasema wafu hawajui lolote..sasa watamuonaje ilhali hawajui kitu!
 
Mwenyezi Mungu, Muumba wa Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo mbinguni na ardhini yupo ndugu yangu; usiahadike na hii pumzi aliyokupa ukamkufuru kwani baada ya kufa utaenda kukutana nae.

QURAN 30: 20-27
20. Na katika Ishara zake ni kuwa kakuumbeni kwa udongo. Kisha mmekuwa watu mlio tawanyika kote kote (duniani)

21. Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri.

22. Na katika Ishara zake ni kuumba mbingu na ardhi, na kutafautiana lugha zenu na rangi zenu. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa wanao jua.

23. Na katika Ishara zake ni kulala kwenu usiku na (kuutumia) mchana katika kutafuta kwenu fadhila (riziki) zake. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao sikia.

24. Na katika Ishara zake hukuonyesheni umeme (wa radi) kwa kukutieni hofu na tamaa (ya mvua). Na hukuteremshieni maji kutoka mawinguni, na kwa hayo huifufua ardhi baada ya kufa kwake. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanao zingatia.

25. Na katika Ishara zake ni kuwa mbingu na ardhi zimesimama kwa amri yake. Kisha atakapo kuiteni mwito mmoja tu, hapo mtatoka kwenye ardhi. (mtafufuliwa kutoka makaburini)

26. Na ni vyake Yeye vilivyopo mbinguni na vilivyopo katika ardhi. Vyote vinamtii Yeye.

27. Na Yeye ndiye aliye anzisha uumbaji, kisha ataurudisha mara nyengine(kwa kuwafufua wafu). Na jambo hili ni jepesi zaidi kwake. Naye ndiye mwenye mfano bora katika mbingu na ardhi. Na Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima."
Nyie waslam mnazingua asee nyie Mungu wenu mnaemwita Allah anawapanga sana asee,kuna vitu mkiulizwa huwa hamjibu kwasabb Muhammad aliwaacha bila maelezo
 
Mkuu elliclassic sina evdence ya mkoNOni kuwa MUSA alikuwepo lakin meng yanaonyesha kuwa bible iko accurate,na sio fictious mfano kuinuka na kuanguka kwa empire mbalimbal kama roman, greek, medo-persian etc zingatia haya yalikuwa tayar yameandikwa ndpo yalitokea, , pia ayubu 26:7 inasema dunia ipo suspend pacpo na k2 wakat watu waliamni dunia iko suspended na mgongo ya tembo.
 
Back
Top Bottom