Hivi ni kwanini wanaume mnaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwenu?

Hivi ni kwanini wanaume mnaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwenu?

Habari za usiku huu wana jukwaa, kabla ya yote naomba kwanza niwasihi sana wale wavivu wa kusoma nyuzi ndefu kwamba huu uzi tafadhali kabla hamjatoa comments zozote naombeni muusome wote kama ulivyo kuanzia mwanzo hadi mwisho halafu ndiyo mtoe comments maana kuna watu wana tabia ya kukurupuka kuchangia vitu ambavyo tayari vimeshafafanuliwa kwenye uzi.

Kama kichwa cha mada kinavyojieleza, leo nataka niongee na wanaume wanaoongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwao kana kwamba wanaume hawakosei kwenye jamii wakati maovu yote yanayofanywa na wanawake ni sawa tu na maovu yote yanayofanywa na wanaume lakini kabla sijaendelea naomba niorodheshe kwanza maovu yanayofanywa na wanawake na jinsi yanavyoendana na maovu yanayofanywa na wanaume.

1. Wanawake wanaochepuka wanaendana na Wanaume wanaochepuka

2. Wanawake wanaozalishwa bila ndoa/nje ya ndoa wanaendana na Wanaume wanaozalisha bila ndoa/nje ya ndoa

3. Wanawake wanaojiuza wanaendana na Wanaume wanaowanunua

4. Wanawake wasagaji wanaendana na Wanaume mashoga

5. Wanawake wanaopenda kutembea na waume za watu wanaendana na Wanaume wanaopenda kutembea na wake za watu

6. Wanawake wanaopenda kutoka na mijibaba alias sugardaddies kwa ajili ya pesa wanaendana na Wanaume wanaopenda kutoka na mijimama alias sugarmummies kwa ajili ya pesa

7. Wanawake waliopo kwenye mahusiano kwa sababu ya pesa tu wanaendana na Wanaume waliopo kwenye mahusiano kwa sababu ya mbunye tu

8. Wanawake wanaopenda kuhudumiwa (kupewa pesa, kununuliwa vitu et al) na wapenzi wao wanaendana na Wanaume wanaopenda kulelewa (kupikiwa, kufuliwa et al) na wapenzi wao

9. Wanawake wasio na utii kwa waume zao wanaendana na Wanaume wasio na upendo kwa wake zao

10. Wanawake wanaowaacha wanaume waliowasomesha wanaendana na Wanaume wanaowaacha wanawake walioanza nao kwenye umasikini

Hayo ni machache mengine mnaweza kuongezea ila nimeona nijikite zaidi kwenye maovu yanayohusiana na ngono kwa sababu ndiyo janga kubwa kwenye jamii na nilitaka niwaoneshe ni namna gani jinsia zote zina maovu yake kwenye jamii, sasa hapa najua wapo watu watakaoleta habari za kutaka usawa sijui ushindani sikilizeni niwaambie, wanawake na wanaume tutatofautiana kote lakini siyo kwenye uovu yaani tutatofautiana kwenye jinsia, nafasi na majukumu lakini tofauti zote hizo siyo sababu ya wanaume kufanya maovu vile wanavyojisikia eti kwa sababu tu wao ndiyo wako juu ya wanawake

Wapo wengine watasema eti wanaongelea sana maovu ya wanawake kwa sababu wanawake ndiyo wanaopata madhara kuliko wanaume kwamba wanaume wao linapokuja kwenye swala la mahusiano ya kimapenzi hawana cha kupoteza kabisa ila niwaambie tu kuwa bado hiyo siyo sababu ya wanaume kufanya maovu vile wanavyojisikia eti ili tu kuwakomoa wanawake sasa mbona na magonjwa ya zinaa nayo hayaangalii jinsia na yanaua wote wanawake na wanaume kwa mtindo ule ule??

Halafu pia kinachonishangaza kama kweli wanaume hamna cha kupoteza kwenye mapenzi kwanini ninyi ndiyo mnaoongoza kwa kuyalalamikia na kuyaongelea maovu ya wanawake humu mitandaoni na mitaani kila siku?? Kuna mmoja alisema eti mnafanya hivyo kwa lengo la kutusaidia sasa kama kweli mngekuwa mna nia ya kuwasaidia hao wanawake wenye hayo maovu kwanini muishie kuongea kwa mdomo tu na siyo kufanya kwa vitendo??

Eti unakuta mwanaume anasema "kuna demu jana nilimtongoza akakubali muda ule ule na akanipa mzigo muda ule ule" halafu anamalizia kwa kusema "daah wanawake wa siku hizi mnajirahisisha sana acheni umalaya la sivyo wanaume tutaendelea kupiga na kusepa au kuzalisha na kuacha" sasa mwanaume kama huyu unamuona tu ni jinsi gani alivyo mnafiki yaani anajifanya kusikitishwa na wimbi la wadada kujirahisisha wakati huo huo yeye ndiye kinara wa kuwatongoza hao wadada ili wajirahisishe sasa kama kweli huyu mwanaume angekuwa hapendi wanawake wajirahisishe kwanini asiache kuwatongoza na kuwaomba mizigo kama hana nia nao??

Namaanisha kama wanaume mna nia ya kutusaidia wanawake na mmeona kwa maneno haisaidii kwanini msifanye kwa vitendo kwa kuacha hayo mambo yanayowafanya wanawake wajirahisishe kwenu?? Halafu wanaume wengi utasikia wanasema "kwanini mwanamke ukitongozwa ukubali" badala ya kuuliza "kwanini mwanaume anatongoza pasipo na nia ya dhati" yaani wanalazimisha ionekane kama mwanaume kutongoza siyo kosa ila mwanamke kukubali ndiyo kosa wakati actually kinachoanza ni kutongoza halafu kinachofuata ndiyo kukubali au kukataa hivyo lazima tukubali kuwa mwanaume anayetongoza na mwanamke anayekubali wote wana makosa na haya yote ni kutokana na tamaduni kandamizi zilizoanzishwa na mababu zetu enzi hizo bibi zetu wakiwa hawana sauti kwenye jamii hivyo walitupiwa mizigo yote na walilazimishwa kuikubali watake wasitake nasikitika kusema kuwa mamlaka ambayo wanaume walipewa na Mungu juu ya wanawake babu zetu waliyatumia vibaya kwa bibi zetu yaani waliyatumia kuwakandamiza badala ya kuwalinda

Kitendo cha kulazimisha kwamba mwanaume akitenda dhambi ni sawa ila mwanamke akitenda dhambi ni kosa ni kinyume hata na maandiko kwa sisi tunaoamini katika Mungu na Dini yaani jamii yetu imejenga mitazamo ya hovyo inayochagizwa na mfumo dume kwamba eti maovu ya mwanaume hayatakiwi kuhojiwa wala kurekebishwa bali maovu ya mwanamke ndiyo yanatakiwa kuhojiwa na kurekebishwa halafu wanalazimisha kwamba eti ni Mungu ndiyo ametaka hivyo ni mungu gani huyo aliyesema wanaume mtende dhambi mnavyojisikia eti ili tu mjitofautishe na wanawake na muonekane mko juu ya wanawake?? Ukweli ni kwamba tofauti kati ya mwanamke na mwanaume haipo kwenye dhambi hata siku moja yaani imefikia hatua wanaume wanajisifia umalaya na tena wanakataa kabisa eti mwanaume haitwi malaya bali kidume ukiuliza hiyo ni kwa mujibu wa nani hawana majibu wanakuja na mapovu!!

Kama kila jinsia imeshindwa kubadilika kwa nafasi yake na kusubiria eti jinsia nyingine ndiyo ianze kubadilika halafu nayo ndiyo itafuata basi niwasihi tu tuache kusubiri meli kwenye uwanja wa ndege au embe chini ya mkorosho mimi naona ifike pahala jamii iache uongo na unafiki kama tumeamua kukemea maovu tukemee kwa jinsia zote na kama tumeamua kuacha yaendelee tuache kwa jinsia zote after all wanaume si hamna cha kupoteza bwana so why mjihangaishe?? Ninyi endeleeni kupiga na kusepa au kuzalisha na kuacha halafu tutaona mwisho wake maana hata hivyo pamoja na malalamiko yote haya ya wanaume kwa wanawake naona ni kama vile mnajaribu kudeki bahari au kufagia jangwa tu!!

Kwa kuhitimisha naomba niseme tu kuwa hiki nilichokiandika ni robo tu ya nilichonacho ila kwa sasa naomba niishie hapa lakini bado nina mengi ya kuandika hapa sitayamaliza ila nitajaribu kuyajibu kwenye comments kutegemeana na maoni ya wadau japo najua nitaoga mapovu ya kutosha hasa kutoka kwa jinsia ya kiume lakini sitajali nayakaribisha ila wale wazee wa kukisia maisha ya watu wale wa "wewe utakuwa na stress za wanaume siyo bure" au wale wa "wewe unapenda kujilinganisha na wanaume" maana wenzetu mkiguswa kidogo tu mnakimbilia kusema wanawake tunataka usawa au ushindani na wanaume utafikiri labda wanaume mna kitu cha ziada mmependelewa nacho yaani labda wenzetu hamfi mnapaa mbinguni moja kwa moja kama mlivyo na ingekuwa hivyo mbona ningebadili jinsia kabisa niwe mwanaume ili nisife ila tofauti na hapo sijaona cha kunifanya nitake kujilinganisha na mwanaume maana hapa duniani kinaogopwa kifo tu kwa sababu hakikwepeki ila mengine yote yanakwepeka tu na tunayoweza kupambana nayo tunapambana nayo kikubwa uhai sasa leo naomba mje na hoja tafadhali hizo kauli zenu za ushindani sijui usawa siyo hoja bali ni mihemko tu

Nipo....
Siku foreman anapopambana na meneja. Huo ulinganifu ulioufanya sio halisia, ni hulka yako ya kujilinfanisha. Jitafakari sana ujikubali nafasi yako, wala si kuleta hesabu za mlinganyo kwenye maisha. Itoshe tu kukushauri hivyo ewe mpambanaji
 
Wewe ulishawahi kumuona huyo mungu au vile viliandikwa na wanaume Kwa hisia mkajipendelea, acheni kujificha kwenye maandiko ili kukandamiza wanawake, eti mlaumu Mungu mxiiiiiew, ndio maana ili udumu na mwanamke lazima umuonee mwanamke, mabadiliko ya sasa ya wanawake kuwa huru mnabaki kulia lia umagharibi, I'm happy wanawake sasa tuna raise against all forms of discrimination na years to come tuta rule the world na nyie muanze kulia lia tu.

Ilikuwaje hicho kitabu cha dini kikaandikwa na mwanaume!?

Kwanini kisingeandikwa na mwanamke? au binadamu wa jinsia nyingine(kama yupo)?

Kwanini na nyie wanawake mkakubali kuishi kwa kukifuata kitabu hicho ambacho kiliandikwa kwa ajili ya kuwakandamizeni?

Je wewe una dini?

Kwani sasa hivi ndio mmekuja kushtuka kwamba mmekuwa mkiishi kwa kufuata mfumo(dini) unaowakandamiza?

Ina maana siku zote hizo mlikuwa wajinga kiasi kwamba mlishindwa kabisa kutambua kuwa mko chini ya ukandamizi?
Na nni nini kinachokuaminisha kwamba siku za usoni ngie wanawake ndio mta rule hii dunia ?
 
Kwa hiyo kuwa juu yetu, au kuwa mtawala ndio inawapa uhalali wa kufanya dhambi?
Au ndio mkifanya dhambi zinageuka kuwa "haki" huku zetu wanawake zinaonekana kinyaa?
Hicho ni kiburi cha asili. Hebu soma tena uelewe. You can't avoid nature, you can just control it.
 
Kuna biashara yoyote inayofanikiwa bila kuwa na wanunuzi?
Mnavyoonekana kukerwa na wanawake wanaojiuza nilitegemea kwa pamoja muungane mpinge kununua lakini sio mnanunua baadae mnakuja kuhubiri dhambi zetu.
Kwanini nyinyi msiungane kupinga kuuza. Sisi tunanunua kwa sababu zipo zinauzwa.
 
Mambo poa Manga ML.
Uzi unahusisha kila kitu, imani na uhalisia.
Ki uhalisia mkubali lawama kwamaana nyie ndo mna tulea.
Wamama wakiwaona binti zao wakiachia paja wazi ilikua ni vifinyo kwa sasa ndo kwanzaa hata chupi hamvai tutakaa sawa kweli?
 
Kuwapa wanawake wengi mimba si urijali ni lack of self control na kujielewa, kwanza hzo taasisi za wanawake zinasaidia kuinuia wanawake na Kwa takwimu za World bank Tanzania wanawake sasa wamewazidi wanaume kwenye ujasiriamali, nyie bakini na kutia mimba huku wanawake wakinyanyuka kiuchumi tu
Wow hongereni sana kumbe wanawake wa kibongo mmepiga hatua kubwa kiasi hiki kiuchumi !?

Baasi tuna haki ya kujivunia kwa maendeleo makubwa waliyonayo wanawake zetu, maana mmewazidi mpaka wanawake wa USA ambako wanaume bado ni dominant kwenye business arena.
 
Vipi kuhusu uwezekano wa hivyo mnavyoviita vitabu vya mungu kuwa siyo vitabu vya mungu bali vitabu vilivyoandikwa na wanaume?
Kwanini viandikwe na mwanaume?

Wanawake walikuwa wapi wakati wanaume wanaviandika!?

Kwanini wasingevisusia na badala yake wamekuwa wakiishi kwa kuvifuata kwa maelfu ya miaka?

Kwanini angalau hata wanawake wasingekomaa hili mwandishi wa vitabu hivyo awe neutral na pasionekane kuwa na ukandamizaji wowote?
 
Si kweli napinga huo utafiti hzo ni stereotypes tu za mwandishi na kwanini ili muonekane wanaume ni lazima mumu undermine mwanamke why?
Ili mtu awe mwanaume lazima awepo mwanamke. We unadhani wanawakw wasingekuwepo neno mwanaume lingetoma wapi?
 
Ndo uhalisia namuache kulia lia huku kuhusu wanawake kama nyie ni wanaume kweli
Who is crying by the way?
Kuna NGOs ngapi za kutetea mambo ya wanawake?
Nikimtawala mke wangu nyumbani tayari am safe sihitaji NGO yoyote. What about you? Hamjiwezi mpaka mpate NGO
 
Unamtawala ili iweje hujiamimi ur manhood ndo maana. Staki kutawaliwa na mtu najitawala mwenyewe na halmashauri ya kichwa changu. Sihitaji wakunikamilisha naji mudu mwenyewe
Who is crying by the way?
Kuna NGOs ngapi za kutetea mambo ya wanawake?
Nikimtawala mke wangu nyumbani tayari am safe sihitaji NGO yoyote. What about you? Hamjiwezi mpaka mpate NGO
 
Natutazidi sana kujiimarisha kila idara ndo tumeanza sasa mpaka tutafika juu kukomesha aina zote za discrimination. Lazima tuvuke targets zetu
Wow hongereni sana kumbe wanawake wa kibongo mmepiga hatua kubwa kiasi hiki kiuchumi !?

Baasi tuna haki ya kujivunia kwa maendeleo makubwa waliyonayo wanawake zetu, maana mmewazidi mpaka wanawake wa USA ambako wanaume bado ni dominant kwenye business arena.
 
9. Wanawake wasio na utii kwa waume zao wanaendana na Wanaume wasio na upendo kwa wake zao
Hii nukta kwa ukubwa wake unaweza kuandika vitabu na vitabu. Inaonekana umeitaja bila kujua ukubwa wake.

Naomba nikuulize maswali yafuatayo juu ya nukta hii.

1. Mipaka ya utii wa mwanamke kwa mumewe ni ipi ?
2. Kwanini umelinganisha utii na kutokuwa na upendo kwa Mwanaume kwa mke wake ?
3. Wakati gani Mwanamke huitwa si mtiifu kwa mumewe ?
4. Wakati gani Mwanaume huambiwa hana upendo na mkewe ?
10. Wanawake wanaowaacha wanaume waliowasomesha wanaendana na Wanaume wanaowaacha wanawake
Hii nukta ukiiacha hivi inaitwa upotofu au unapotosha,kwanini nasema hivyo ? Hapa ulitakiwa kusema isipokuwa kwa sababu zinazopelekea ulazima wa kuachana.

Je huko kuachana hakuna sababu ? Bila shaka zipo,hapa ulitakiwa uzitaje japo kwa uchache.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Nyaja zote za kiuchumi, kijamii, ndo mana vijana wakiume hawana mbele wala nyuma, they have nothing to show
Yaani we unachojua na kudhani material possessions will change uanamke wenu? Hahaha! No way.

Kwa idadi wanawake ni wengi kuliko wanaume. Huko makazini idadi ya wanaume outdo idadi ya wanawake. Hata mashuleni wanaohitimu wanaume ni wengi kuliko wanawake. Bungeni mpaka mpate viti maalum. Makazini manesi wengi ni KE na madoctor wengi ME, na wanaume wameanza kuvamia fani ya nursing pia. Migodini kuna wanaume wengi kuliko wanawake. Ni wapi?
Tukisikiliza report za kutoka Kisutu wanasheria kila siku majina ya ME yamedominate. Nyie mko wapi? Kwenye vicoba labda. Haya niambie ni wapi mwanaume kapitwa? Wapi?
Hivi leo wanawake na wanaume who have nothing to show?

Labda huko nchi za mbele sio hapa Tz. You women have nothing to show. Nyie mabaamedi? Wauza chiu? Ndo mseme we have nothing to show? Asalalee
 
Hatukuwa wajinga zama zimebadilika kila nyanja za maisha, ndo mana zamani watu walitembea Kwa miguu ila sikuhizi kuna magari, ndege, meli, and so on.. Hyo ya kuandikwa na mwanaume ni ilikuwa mifumo isiyo ruhusu hyo ndo mana wanawake hawakuhesabiwa ila sikuhizi wanahesabiwa na kupiga kura.

Mimi namwamini Mungu creator of everything,vinavoonekana na visivoonekana yeye ni source of life,

ila hii Kwa perspective yenu ya uonevu na kutoelewa misingi ya imani ndo mnakimbilia huko kujifichia huko kichaka sijui cha dini and whatever forms of discrimination
Ilikuwaje hicho kitabu cha dini kikaandikwa na mwanaume!?

Kwanini kisingeandikwa na mwanamke? au binadamu wa jinsia nyingine(kama yupo)?

Kwanini na nyie wanawake mkakubali kuishi kwa kukifuata kitabu hicho ambacho kiliandikwa kwa ajili ya kuwakandamizeni?

Je wewe una dini?

Kwani sasa hivi ndio mmekuja kushtuka kwamba mmekuwa mkiishi kwa kufuata mfumo(dini) unaowakandamiza?

Ina maana siku zote hizo mlikuwa wajinga kiasi kwamba mlishindwa kabisa kutambua kuwa mko chini ya ukandamizi?
Na nni nini kinachokuaminisha kwamba siku za usoni ngie wanawake ndio mta rule hii dunia ?
 
Back
Top Bottom