Hivi ni kwanini wanaume mnaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwenu?

Hivi ni kwanini wanaume mnaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwenu?

Sawa Mkuu
Sijasoma wote ila i get your point, ipo hivi kwa ufupi sana tunaishi kwa kutegemeana hasa kwenye kitu ambacho umekizungumzia ndio husababisha lawama nyingi kwenye jamii dhidi ya Jinsia KE, me naamini tupo 50/50.
 
Huyu haujamkuta kwenye nyuzi nyingine huwa anatumia lugha za matusi balaa sema naona tu leo kaamka vizuri
Best comment in this thread!
Umeiweka point yako vizuri, umeargue kisomi kabisaaa.
Ahsante, sio wengine wanatumia matusi, kejeli, fedheha na udhalilishaji.
mbarika chukua maarifa haya kwa Jokajeusi
 
hauhisi dunia ilianza kupotea pale mmoja alipojitokeza na kusema hii aya haiko sawa? sku hizi hadi ndoa za same sex zinafungwa kwa kutumia biblia hio hio inayokataza same sex, sababu tu kuna mtu amepingana na hiko kipengele. na waumini nao wanaitikia Aameen!!
Tatizo lipo ukishindwa kujua kipi unapaswa kufanya na kipi uache kufanya, ukifanya tu kwa sababu imeandikwa hvyo utapotea.
 
Ni kweli mkuu, lakini haya mambo yanaongelewa hata mitaani na siyo mitandaoni tu yaani inaonekana wanaume wako serious kabisa kulalamikia maovu ya wanawake utadhani wao ni watakatifu au labda wenzetu maovu yao yamepitishwa
Dada mbona unayachukulia serious sana maisha ya jf? Mengi yanayoletwa humu ni kuchangamsha jukwaa tuu.

Dont take it seriously to point of giving you depression.

Unforgetable
 
Asante mkuu kwa kuukubali ukweli barikiwa
Huwa nasema kuwa ukweli utabaki kuwa ukweli tu, utapingwa, utafichwa sana lakini ndio ukweli na uhalisia ulivyo. Kuna watu n wagumu sana kuukubali ukweli hasa sisi wanaume, tutabisha, tutakataa kwa maneno hadharani lakin ndan kwa ndani unakubali na unajua fika uliosemwa n ukweli.
 
hauhisi dunia ilianza kupotea pale mmoja alipojitokeza na kusema hii aya haiko sawa? sku hizi hadi ndo za same sex zinafungwa kwa kutumia biblia hio hio inayokataza same sex, sababu tu kuna mtu amepingana na hiko kipengele. na waumini nao wanaitikia Aameen!!
Kupinga sio vibaya, me kupinga haimaanishi ndio ntakuwa muovu, Hapana nasimamia ukweli na uhalisia, kama hakuna wema duniani jaribu kuwa mwema and vice versa is true usituaminishe maandiko kwenye kila kitu.
 
Na ni biblia gani hiyo iliyomruhusu mwanaume kufanya uzinzi na uasherati??

Watu wa JF ndiyo hawa hawa wa mitaani na haya mambo yanaongelewa hadi mitaani!!
Bibilia agano la kale ilisema mwanamke malaya apigwe mawe. Hivi ulishajiuliza wanaume waliokuwa wanazini nao walipangiwa adhabu gani?

Halafu, hivi nikizini na wewe ukabaki kuwa single mama. Ni mimi ninataabika na mtoto au wewe?

Hivi nyie mkiacha kuuza, tutanunua wapi?
Mkigoma kutoa mbunye kabla ya ndoa sisi tutapata wapi?

Endelea kujilinganisha.

By the way usiyachukulie serious sana maisha ya JF
 
Mkuu hivyo ndivyo ilivyo hata ukikataa.

Walioandika hiyo Biblia ni Wanaume.

Walioandika hiyo Quran ni wanaume.

walioandika vitabu vya dini karibu zote duniani ni wanaume. Hao Budha, Hindu, Shinto, Voodoo, Bahaula, N.k. wote ni wanaume.

Huyo Mungu unayemsema anatambulika kama amebeba dhima ya Kiume. Amependelea wanaume zaidi.

Sipo Biased ila najaribu kuelezea uhalisia.

Mwanaume ndiye mtawala wakati mwanamke ni mtawaliwa.

Mtawala ndiye mtungaji wa Sheria hata katika jamii zisizo na dini zenye asili ya Abrahamu.

mtawala ndiye anaamua nini kiwe nini kisiwe akisaidiwa na Nature ambayo ndiyo watu huita Mungu.

Hiyo ni kwa habari ya Jinsia.

Kwa habari ya Rangi. Mtawala ni rangi nyeupe. Yaani wazungu kwa jamii zao.

Hao ndio hutunga sheria na hata mipaka ya nchi zetu wao ndio waliipanga na kuichora.

Wazungu huko kwao sio kwamba hawana mambo ya ajabu. Sio kwamba hawauani. Wanauana tena sana lakini kwa nini wao dunia iwapondi sana. Jibu ni moja ni kwa sababu wao ni watawala.

Lakini Muafrika akifanya uovu kidogo utaona watu wakitukana. Mara waafrika wajinga, mara waafrika ni makatili. Lakini yote ni kwa sababu Waafrika ni tabaka tawaliwa.

Mtawala hapewi lawama sana ukilinganisha na mtawaliwa.

Kama hujanielewa.

Mfano Mungu na Shetani.
Mungu ni mtawala. Yeye ndiye anaweka sheria kwa vile ni mtawala. Mungu hata akiadhibu dunia na kuiletea majanga lakini Bado watu watamsifia au kama ni kukosoa watakosoa kidogo.

Lakini shetani ambaye ni mtawaliwa hata akiua mtu mmoja utasikia watu wakimlaani sana.


Ndivyo hata kwa habari ya mwanamke na mwanaume.

Mwanaume hata akifanya umalaya huwezi sikia watu wakimtukana na kumkejeli. Hii ni kutokana yeye ni mtawala.

Lakini mwanamke fanya kidogo yaani usizini bali mkumbatie tuu hata mwanaume mbele za watu uone watu wayakavyokushukia. Watakutukana na kukupa maneno ya kejeli. Hii ni kutokana mwanamke ni Mtawaliwa.

Mtawaliwa hata afanye kizuri vipi hawezi kusifiwa. Mtawaliwa ni mtu wa kulaumiwa siku zote.

Ndio maisha hayo Marianah. Utahangaika lakini hakuna atakayekusaidia. Hata huyo Mungu hanaatakachofanya kwenye hayo malalamiko yako. Kwani yeye ndiye aliyeweka mambo yaende hivyo.

Zaidi ya yote. Tuishi kwa kupendana iwe ni tabaka tawala au Tawaliwa. Iwe ni Simba au Swala.

Kalagabaho
Machungu yatabaki kwa watawaliwa..
 
Ni kweli kabisa.
Wanyama wote wenye akili ya karibu
Binadamu ni mfano wa Mungu na siyo wanyama na wala hatukuagizwa tufuate maisha ya wanyama bali tumewekewa sheria zetu sisi kama binadamu hivyo usijilinganishe na wanyama hata siku moja binadamu tuna maisha baada ya kifo ila wanyama hawana sasa kama hadi hapo bado haujaona tofauti kubwa kati ya wanyama na binadamu basi utakuwa na tatizo mahali
 
Kupinga sio vibaya, me kupinga haimaanishi ndio ntakuwa muovu, Hapana nasimamia ukweli na uhalisia, kama hakuna wema duniani jaribu kuwa mwema and vice versa is true usituaminishe maandiko kwenye kila kitu.
Chief huwezi ukatreat maandiko kama nguo, inayokufaa unachukua, isiyokufaa unatupa kule. EITHER YOU ARE ALL IN OR YOU ARE ALL OUT.
 
Naona uzi umejijadili wenyewe , naona sina cha kuchangia , namaliza kwa kusema "Funguo inayofungua milango yote ina thamani kubwa sana , inamilikiwa na wenye pesa nyingi, ila kufuli inayofunguliwa na kila funguo ni useless utaikuta jalalani"
 
Back
Top Bottom