Hivi Nyerere aliwahi kugombana na Kanisa Katoliki au Protestanti?

Hivi Nyerere aliwahi kugombana na Kanisa Katoliki au Protestanti?

..sidhani kama ni sahihi kusema Mwalimu Nyerere alikuwa na ugomvi na Abdulwaheed Sykes.

..Mwalimu angekuwa na ugomvi na kina Sykes basi asingemteua Abbas Sykes kuwa Gavana wa kwanza jimbo la Mashariki ambalo lilihusisha jiji la Dar Es Salaam.

..Baada ya hapo Mwalimu alimteua Abbas Sykes ktk nafasi mbalimbali za ubalozi ikiwemo ubalozi wa Canada, France, na Italy.

..Vilevile mdogo wake Dosa Aziz anaitwa Hamza Aziz alipata kuwa Mkuu wa jeshi la Polisi IGP. Kungekuwa na ugomvi kati ya Dosa Aziz na Mwalimu Nyerere, Hamza Aziz angeaminiwa ktk nafasi nzito kama IGP?

..Kuhusu uwepo wa wapigania uhuru waliosahaulika hiyo ni hoja inayosimama na wako wengi ambao hawajapata bahati ya kuwa na vijana wao wa kuwaandikia vitabu.

..Pia kuna watu walioteswa kwelikweli na utawala wa Mwalimu Nyerere, watu kama Christopher Kasanga Tumbo, James Mapalala, Bibi Titi Mohamed, na wengine.
Oscar kambona alikua mkristo ila alikosana na nyerere
Nyerere ambaye anatuhumiwa ni mdini kamwachia nchi mwinyi mwislamu kuna mambo watu wanashadadia na wana akili timamu kabisa
 
Wakuu kwema
Tunajua historia ya Tanzania, Mwalimu Nyerere aliwahi kuingia katika mgogoro au vita na iliyokuwa jumuiya ya Waislamu (East Afric Muslims Welfare Society) ambayo mgogoro huo ulipelekea jumuiya hiyo kufutwa na BAKWATA kuzaliwa

Napenda kuuliza kuwa kama aliwahi kuwa na mgogoro na Kanisa Katoliki au Waprotestanti hata kama haukuwa mkubwa kama ule wa Waislamu

Tunafahamu Magufuli aliwahi kugombana na Kanisa Katoliki na Lutheran kufuatia makanisa hayo kutoa nyaraka za kulaani watu kutekwa, na pia kuhusu alivyoshughulikia ugonjwa wa Covid

Mohamed Said
Nakumbuka kuna wakati Kanisa Katoliki lilikuwa na hofu ya kuingiza communism ujamaa ukishakomaa. Nadhani kama nakumbuka vizuri maana nilikuwa mdogo Bado baadhi ya maaskofu na mapadri walikuwa wakikosoa sera zake. Sasa sijui kama hiyo ilileta mgogogoro kati yao au la.
 
Zaidi ya kutokuwa mwizi na kutojilimbikizia mali, Mzee wa Azimio la Arusha hakuwa na jipya lolote.Blabla nyingi hakuna lolote la maana.
 
Kama unajuwa hivyo, kwa nini sasa uhoji unaowalalamikia hapo juu. Hivi unazo akili timamu kweli wewe?
Unajua nyie watu ile minyoo mnayokula kwenye nyama ya nguruwe inawavuruga akili kwahiyo siwezi kubishana na wewe.
 
Hii alone yule mujahidina Mohamed Said . Uone atakavyo ng'aka
Stux...
Umeniita ''Mujahid.''

Ahsante sana kwa kuninyanyua katika darja hiyo kubwa sana katika Uislam.
Hao Allah kawataja katika Qur'an kwa sifa nzuri sana.

Mimi siwezi kufikia makamo hayo nitajwe na Mola wangu ndani ya kitabu chake.
Natamani ningekuwa hivyo.
 
Oscar kambona alikua mkristo ila alikosana na nyerere
Nyerere ambaye anatuhumiwa ni mdini kamwachia nchi mwinyi mwislamu kuna mambo watu wanashadadia na wana akili timamu kabisa

..Watanganyika tunabaguana kwa makabila, hatubaguani kwa dini.

..mambo ya udini yameletwa na Wazanzibari waliokuja huku Tanganyika kwa wingi wakati wa Mzee Ruksa.
 
Unajua nyie watu ile minyoo mnayokula kwenye nyama ya nguruwe inawavuruga akili kwahiyo siwezi kubishana na wewe.
Haya angalia akili kama hizi.
Kwa hiyo wewe kutokula nyama ya nguruwe ni kwa sababu ya minyoo? Hivi unaishi kwenye pango gani lililojaa giza tupu bila mwanga kupenyeza!
Karne hii bado unaogopa minyoo?

Naona 'godfathe'r wenu anayewavuruga akili kuhusu wazee wake Kariakoo kaingia kwenye mada! Sijui ana lipi jipya? Kuna hadithi aliyosimuliwa na kuisahau kwa muda mrefu, leo kaikumbuka?
 
..Watanganyika tunabaguana kwa makabila, hatubaguani kwa dini.

..mambo ya udini yameletwa na Wazanzibari waliokuja huku Tanganyika kwa wingi wakati wa Mzee Ruksa.
Hadi watu wakaanza kuulizana kwa mara ya kwanza kabisa: nani achinje? Jambo ambalo kabla lilikuwa halimsumbui yeyote.
 
Wakuu kwema,

Tunajua historia ya Tanzania, Mwalimu Nyerere aliwahi kuingia katika mgogoro au vita na iliyokuwa jumuiya ya Waislamu (East Afric Muslims Welfare Society) ambayo mgogoro huo ulipelekea jumuiya hiyo kufutwa na BAKWATA kuzaliwa

Napenda kuuliza kuwa kama aliwahi kuwa na mgogoro na Kanisa Katoliki au Waprotestanti hata kama haukuwa mkubwa kama ule wa Waislamu

Tunafahamu Magufuli aliwahi kugombana na Kanisa Katoliki na Lutheran kufuatia makanisa hayo kutoa nyaraka za kulaani watu kutekwa, na pia kuhusu alivyoshughulikia ugonjwa wa Covid-19.

Mohamed Said
Nahisi hata kama si kugombana, basi kupishana mtazamo kuliwahi kutokea. Na siyo hao tu, vyema vya wafanyakazi, vya ushirika n.k. matokeo yake vyote alividhoofisha kwa kuviweka chini ya vyema vya Sasa, madhara tunayoyaona hadi Sasa, havina maamuzi ya kujitegemea bila ya ccm na pia yoga uliowajaa WaTz kwa ujumla.
 
Nyerere alipenda kujisomea, hata viongozi wa dini aliwahi kuwauliza ni wapi kwenye biblia wameandika kutoa wake wengi nu dhambi huku akitolea mfano wa baba yake.
Alibishana nao kwa hoja Ila sio hadharani
 
Unajua nyie watu ile minyoo mnayokula kwenye nyama ya nguruwe inawavuruga akili kwahiyo siwezi kubishana na wewe.
Minyoo ukisha ichemsha kwenye 100° Celsius inakumwa ni mboga kama utumbo wa kuku tu
 
Minyoo ukisha ichemsha kwenye 100° Celsius inakumwa ni mboga kama utumbo wa kuku tu
Wenyewe wanakuambia hiyo minyoo haifi labda hiyo nyama uichome iwe kama majivu sasa ikifikia hivyo hiyo nyama sijui kama itafaa tena kuliwa!
 
Wenyewe wanakuambia hiyo minyoo haifi labda hiyo nyama uichome iwe kama majivu sasa ikifikia hivyo hiyo nyama sijui kama itafaa tena kuliwa!
Nina miaka 63 sasa, nakula mdudu kuanzia nina umri wa miaka 6 sijawahi kuugua ugonjwa wa minyoo. Mnadanganywa sana. Kwetu ni Mbeya. Tena enzi hizo nguruwe walikuwa wanajitembelea kama kuku wa kienyeji wanakula chochote.

Waisalamu wajanja wamegundua, tunakula nao. Shauri yako
 
Back
Top Bottom