Hivi ukiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo utafanya nini kwa Taifa lako?

Hivi ukiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo utafanya nini kwa Taifa lako?

Hapa mnaotaman kuwa viongozi tuone experience
Ningefutilia mbali serikali ya baraza la mapinduzi na kuunganisha Tanzania kuwa nchi moja isiyo na mkoa nyonyaji kama visiwani na kuwafungilia mbali wale wote wanaotuhumiwa na CAG mbali na kuanzisha lifestyle audit kwa kila mwenye madaraka au njuluku
 
Hatua ya kwanza ni kufumua uozo wote kila kona. Nitatumia style ya Magufuli ya kutocheka na nyani.

Kikubwa wafanyakazi wa umma ukomo ni 5 years ofisini unaachia. Ukitaka kwenda senior position unaomba upya na proof kabisa kwamba umeonesha ufanisi wa hali ya juu. Utakula miaka mingine mitano kisha unaachia ngazi kwa kustaafu ukapige mishe zako. Hakuna biashara ya kuzeekea ofisini ila ntaboresha sana maslahi kuhakikisha baada ya hio miaka 5 unaweza kujiajiri maana malipo ya mshahara ntalipa hela ndefu. Ukibainika umefanya rushwa au ufisadi ni miaka 30 jela pamoja na kufilisiwa na kizazi chako hakitaruhusiwa kukanyaga kwenye ajira za umma. Watu wakaendeleze sekta binafsi.

Mahakama ijitegemee kwa kila kitu anzia budget hadi matumizi ila wembe ni ule ule. Sifugi uozo sheria ni miaka mitano mtu asepe. Judge ni miaka 10. Kila mtu akajiajiri waache wengine wapatiemo mtaji humo.

Bunge sio picnic, wabunge mshahara Million 5 ila posho ipungue hadi elfu 70 bila mkopo. Wajitegemee na mapato yao yatategemea na wanaleta maendeleo gani kwa wananchi. Wananchi ndio watafanya harambee ya kumchangia mbunge anunue gari ila kama mbunge ni mzigo basi halambi kitu. Speaker nae asimamie miongozo ya bunge ikibainika kwa namna yeyote anaegemea serikalini na kutetea maslahi ya serikali basi wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani nae apigwe chini mara moja. Hii itaondosha uchawa. Ikibainika kuna dalili za rushwa tu mahali wote ni 30 years jela.

Takukuru nawawekea organ ya kuwabana pumbu kuhakikisha majukumu yao wanayafanya effectively. Wakizingua ni jela tu haina msalia mtume. Aidha ni kufilisiwa jumla jumla na jela tu. Hamna room ya plea bargain
 
KWANZA NTAUA NA KUSAMABARATISHA MIFUMO YA WAZEE WA”REMOTE” HADHARANI ILI NITAKALOFANYA LISIPINGWE AU MIMI KUONDOLEWA PAMOJA NA KUFUMUA UPYA USALAMA WA TAIFA NA KUWAFUKUZA NA KUWAWEKA JELA UVSISIEM WALIOKO HUKO WOTE.


1.TUME MPYA YA UCHAGUZI

2.KATIBA MPYA

3.CAG KUWA NA MENO

4.TAKUKURU KUFUMULIWA NA KUSUKWA UPYA

5. DED KUTOKA KWENYE IDARA NA SI TEUZI

6.WAZIRI ASIWE MBUNGE

7.CHOMBO CHA KUDUMU CHA KUCHUNGUZA MIENENDO YA POLISI

8.MAHAKAMA NA BUNGE KUWA NA MENO

9.UKIKUTWA UNASIFISIFIA SEREKALI KIFUNGO JELA MIEZI 6

10.MKUU WA WILAYA FUTA,KUWE NA MKUU WA MKOA NA MA-DED.

11.NANUNUA GARI AINA YA PROBOX NEW MODEL SAMBAZIA RC NA MA-DED.

12.UFISADI KIFUNGO CHA MAISHA JELA.

13.URAIA PACHA RUKSA

14.WAZIRI WA MAMBO YA NJE NAWEKA MZUNGU

15.MABALOZI NATEUA WENYE UZOEFU NA SI KUJUANA

16.KUONDOA KINGA YA MASHTAKA KWA RAISI NA VIONGOZI WA JUU.

17.FUTA CHEO CHA MAKAMU WA RAISI. ABAKI PM KAMA MTENDAJI MKUU.

18.RAISI AKIFA UCHAGUZI KUIITISHWA

19.SHERIA YA KUZUIA MWANAMKE KUWA RAISI( Hili tunajuta)

20.RC ANACHAGULIWA NA WANANCHI



Mwisho kabisa keki ya taifa ni ya wote na si baadhi ya koo
Number 11 ... Hahaha
 
Haitatokea mimi kupata nafas hy bora nife na mawazo yangu mazur yenye kupendeza pengine hata lissu au kiongoz yoyote aliopo madarakan kwa sasa hakuna na hatokuja kuwaza, kama niwazavyo mimi mr bann na ninafikiri nafasi ya urais hainitoshi ni kinafas kidogo sana kwangu hiko kinafas nakiona kama kuongoza ngombe malishoni kwakwel hakinitoshi ndio mana bora nife tu na mawazo yangu kwanza moja ya sifa zangu ninauwezo wa kuwaingia watu kwenye akili zao na kuwa amrisha wafanye ninachotaka na hili naliweza hata wakiwa watu milion 30 kingine ninauwezo wa kusafiri ndani ya sekunde kumi kwenye nchi 10 vuta picha kwa uwezo huu nilionao wananchi wangapi nitawafikia ndan ya siku moja so sizan kama kinafasi cha urais kitanifaa mnaweza sema ni utani ila ndio nilivyo asanten kwa kunisoma
 
Hapa mnaotaman kuwa viongozi tuone experience
1.Wabunge wangeomba nafasi za kazi kutokana na uhitaji na sio kuchaguliwa. Kama bunge linatunga sheria basi kigezo sio kujua na kusoma tu, wawepo wajuzi wa mambo pia.
2. Ningegawa maendeleo kutokana upatikanaji wa vitega uchumi na rasilimali kwa kikanda
 
Nafuta kiswahili mambo gani ya kusoma kwa lugha ya kiswahili darasa la kwanza hadi la saba huku nasoma kiingeleza kama somo na bado kinatutoa knock out alafu mara paah form one masomo yote nasoma kwa lugha ya kiingeleza kutesana tuu huko
 
Ati Magufuli alikuwa katili? Bora yeye alimaliza miaka mitano mimi sina uakika kama naweza maliza mitatu, ila hiyo mitatu moto nitakao uwasha lazima izimwe na petrol yenyewe.

Hivi hili baraza la mawaziri lililopo nani anaweza salimika? Anyway..........hawawezi zidi watatu.

Hako ka nchi kadogo ka zanzibar hakawezi kuwa na raisi na jeshi la kujitegemea.huko naweza kuweka gavana awe ana report kwangu.
Which means katiba inabadirishwa ndani ya miezi 3 naana ninakuwa nina muda mchache wa kuishi so kila kitu nafanya fasta.
Aiiiiiiiiiii wakandarasi mlio. Lipwa na jpm miradi yote imesimama mko mnakula bata hamjamaliza nikiaposhwa tu jiondowe wenyewe.

Baba mwenye tamko kutoka mawinguni aiiiiiiiiiiiiiii unatakiwa kuhama mwenyewe kabla sijaapishwa.

Ili kutaka mizizi, naua vyama vyote kwanza nchi naiendesha kwanza bila chama chocolate cha siasa kumbuka hii clause nakuwa nishaiweka kwenye katiba ya kuondoa vyama vyote pale inapo itajika.

Wafanyankazi naomba niishie hapa naona mmejisahau deko limezidi nyodo kazini.

Vigogo nawapunguzia mishahara naajili watoto wote walioko mitaani na vyeti.

Kama ulijenga jengo hifadhi ya barabara na uliambiwa ukagoma ukajenga kwa kiburi sitowi hata notice greda linapita chwaaa.

Ahaaaaa sector ya madini sijuhi nawafanyaje wacha niishie hapa na hii ndo inaweza niondoa haraka.

Napunguza sana nafasi za kuteua watu waombe kazi wapitie kwenye interview hapa namaanisha teuzi zinakuwa chache sana.

Umeme mchi nzina ndani ya miezi 3.

Miaka mitatu mafisadi mnaweza iona mika 1000.
Hii vita si lazima iniondowe? So lazima niache ninetengeneza katiba iliyonyooka bila chenga haya mambo ati raisi kafa mtu yuko kwake hana ili wala lile anaambiwa eti yeye ni raisi hii mistake haiwezi jirudia.

Aisee kila kitu ni katiba so nitahakikisha ndo kitu chankwanza nafanya ndani ya miezi 3.
 
[mention]JamiiForums [/mention] naomba hii heading ipostiwe kwenye mitandao ya kijamii mingine ili kama kuna wezi na wabadhilifu waweze kuuona na waje waone wananchi wanavyotamani wanyongwe na wafungwe jela.

[mention]Maxence Melo [/mention] Huu uzi ni mzuri utawafanya viongozi waupitie na waone maoni ya wadau.Upostini Kwingine .

Ila mimi nahisi kama ngekuwa raisi wa nchii hii ningeuendesha kijeshi kabsaaa magufuli asingefikia mkono wangu wa chuma hata kidgo.
 
Viongozi Wa Kiafrica Ndo Wanasababisha Waafrica Wote tuonekane Hatuna Akili Kabisa Na hapo Ndo kunasababisha Tulichukie Bara hili la Giza Tatizo Kubwa ni UONGOZI MBOVU
Huo Uongozi mzuri utaukodi wapi ikiwa mliopo ndio nyie kutoka corrupt society?
 
Bodi ya Utalii, hii bodi ikitulia inaweza kuendesha uchumi wa nchi yetu!! Ningeivunja na kuajiri hata wazungu wataalam wa masoko ya utalii! Wabongo wamechemsha.

Kila kona ya hii nchi mngepishana na watalii na vijana wangepata ajira na uchumi ungesimama kuliko Dubenga!!
Kwani saizi kinashindikana nini kufanya hayo? Harafu swala la Watalii linategemea factor nyingi na zinazotegemeana.
 
Ningehamishia makao makuu ya nchi kijijini kwetu
Pia ningeifanya kanda ya kaskazin kam nchi inayojitegemea
 
Makamba wazir na baba yake ndani au kunyongwa kabisa
Nchemba kunyongwa kabisa

Makam mpango anakuwa wazir wa fedha
Rais

Majaliwa anakuwa makamu wangu wangu

Wazir mkuu namuweka bashiru

Utumishi namrudisha jafo
Mambo ya ndani polepole

Waliotajwa na cag wote jela bila mahakama
Au kunyongwa

Na nataman kuwapa nafasi wataalamu kutoka mzumbe na sua

Ud na udom wakae pembeni kwanza
 
sera nzuri kwenye kilimo na viwanda vitaboost maeneo mengine ya nchi kama,elimu,afya na ajira.

Ntaanza kwa kuweka mazingira mazuri kwenye kilimo na uwekezaji wa viwanda kwa kupunguza utitiri wa kodi na kudhibiti urasimu.

sambamba na hilo miaka miwili ya bajet 40% ya bajet ntaipeleka kwenye sekta ya kilimo ili kuweka miundombinu ya umwagiliaji kama mabwawa,mashine na vifaa vya kisasa kwaajili ya kilimo kikubwa na cha kisasa.

tz zaidi ya 80% ya mbolea tunaagiza kutoka nje ya nchi,mimi kama Rais ntahakikisha bwawa la JNHPP linazalisha umeme wa uhakika na wa gharama nafuu bila kuhujumiwa na mafisadi wa nchi sanjari na kupunguza utitiri wa kodi ili kuwavutia wawekezaji waanzishe viwanda vikubwa vya mbolea,nguo,mafuta ya kula,korosho n,k.

ili kuhakikisha dhamira yangu ya dhati kuinua kilimo na kuchochea uwekezaji inafanikiwa vizuri na kwa wakati mimi kama Rais sekta ya viwanda na kilimo vitakua chini ya ofisi ya Rais
Hizo sera nzuri mbona huzitaji? Kuondosha hizo Kodi unazoita utitiri kwanza zitapunguza Bajeti ya Serikali na hujasema utafidia wapi,pili kufuta aunkupunguza haikupi guarantee ya kupata investors Kwa mda huo huo maana inaweza chukua miaka 2 au zaidi kupata wachache..

Mpaka hapo utaendeshaje Serikali wakati mahitaji yanaongezeka?

Kwani tatizo la Kilimo Cha Tanzania ni uzalishaji au soko? Umeshafeli Hadi dakika hii 🤣🤣

Mwisho Kufuta urasimu Haijawahi kuwa rahisi maana wanaleta urasimu ni staff ambao huwezi kuwepo Kila sehemu kuwa track.
 
Sehemu kubwa ya ardhi yenye rutuba ambazo hazilimwi natengeneza mfumo inakuwa ni vijiji vya ujamaa vinakuwa chini ya Suma JKT vijana wa mjini mabishoo, wavivu, wapiga debe, wakatisha tiketi na wanaokula kwao wanasubiria ajira za serikali nawapeleka huko wakalime na kusindika mazao nchi ipate hela.
 
Nitaondoa mifumo ya kijinga ya kuteuana bila.
Nafas zote za uteuzi unafanywa leo zitakuwa wazi kwa Watanzania WOTE kulingana na sifa zilizoainishwa lakini ni lazima ujaze fomu maalumu na kujieleza kuwa ni Kwa nini unatamani kuwa katika NAFASI Fulani SERIKALINI. .Mfano waziri Wa Viwanda Wa Mambo Wa mifugo . Ni lazima useme kuwa ni Kwa nini unatamani kuwa waziri Wa mifugo. Waziri Wa Elimu unatakiwa useme maono Yako kabla ya kuapishwa Ili niyapime Kama yanatija Kwa Jamii au ni uvundo uliozieleka kukopi na kupest Kila mwaka Toka Kwa watangulizi.

NAFASI za Ukuu Wa Idara zote lazima ueleze unafaa vipi kwenye hizo NAFASI. Na Maoni ya wananchi yatazingatiwa mana Mfano unamteua MTU kuwa Mkuu Wa Polisi halafu ni MTU asiye na maono zaidi ya KUFANYA KAZI Kwa Maslahi yake muda WOTE. Ukimpa NAFASI KAZI yake ni kutengeneza mtandao Wa kukusanya pesa Kwa Wahalifu na kujilimbikizia Mali au Kupiga madili ya kuiba pesa za wale Wa chini ambazo ni stahiki zao halali. Utatumia vipi NAFASI Yako Kwa manufaa ya Umma.

Kwa Nini utoke kwenye familia maskini isiyowahi kumiliki Hata Pikipiki lakini ukiwa Wazuri unataka kutembelea gari ya Milioni 460 kutumia Kodi za Watanzania ? Je, Jamii itanifaikaje na uteuzi WAKO katika kupunguza Umaskini?

MTU kama Prof. Nalichako ,alitokea familia ya kawaida inayojua matatizo wanayopata wafanyakazi hasa wale Wa chini Kama Walimu,Mapolisi,n.k ambao mara nyingine wanahakishwa hamishwa au kupangiwa Maeneo ambayo hawawezi kujitafutia maendeleo kirahisi Wakiwa KAZINI kutokana na mazingira ya KAZI lakini anashabikia Kikokotoo kinachowafanya wafanyakazi Wa chini kuendelea kuwa chini na kuwa na maisha Duni Hata basada ya kustaafu. MTU anapangwa KAZI Mfano Mwanajeshi au polisi kule Pemba akiwa ni mzaliwa Wa Musoma ambapo Kuna ardhi ya asili heka ishirini na wakali huo huo MTU Wa Bara Hana fursa ya kupata ardhi Pemba au Zanzibar , Sasa anastasfu Badala ya kupewa pesa ZAKE zote Ili akaanzisha maisha yake kule anakotaka kutokana na KUFANYA KAZI Kwa muda Mrefu kwenye eneo lisiloruhusu kuwekeza kikamilifu na pia kubanwa na muda na majukumu na kuhamishwa hamishwa!
Cha ajabu unamteua tu MTU kama Mama ndalichako na wengine Wa ajabu ajabu bila kujua maono na mtizamo wake juu ya Jamii iliyojaa maskini 80% ikiwa imegubikwa na wafanyakazi wenye Mishahara midogo , Riba kubwa kwenye mabenki, Kodi kubwa kwenye biashara na familia tegemezi yenye Vijana wengi wasio na Ajira rasmi na fursa zinazofichwa na wale walioteuliwa Kwa manufaa Yao.

Mkurugenzi anateuliwa bila kujua Nini atakachokeenda kukifanya kwenye Jamii iliyojaa WAKULIMA na wafugaji kwenye ardhi Moja Badala yake anatumia muda Mwingi KUFANYA vikao na semina elekezi Kupiga pesa. Wanahangaika na miradi isiyokamilika.Madaraja ya matope ,yanayojengea Kila mwaka . Tumbavu kabhisa!!

Hakuna MTU atapata NAFASI ya uongozi Kama Fadhila . Hapana !!
Utachunguzwa ukiwa na historia Hata ya kimazingira ya kujihusisha na ubadhirifu,rushwa au kuhamasisha rushwa utakaa pembeni.
Sitataka viongozi Wa maigizo na KUFANYA KAZI Kwa kukurupuka.

Kama tunataka kuzuia WEZI kwenye Halmashauri hatuwezi kuchaguana Kwa kujuana. Unataka kuzuia ubadhirifu kwenye wizara ni lazima tuweke watu wenye Nia njema na waliopanda ngazi kutokea chini Kwa uadilifu na uaminifu SIO kumtoa tu MTU Sijui kutoka jalala Gani na kumpa NAFASI kubwa kwenye idara inayohusika na fedha au mipango.

Elimu itakua ya Maana tu Kwa MTU muadilifu.
Msomi anapoitumia elimu yake vibaya na kuihujumu nchi anakua mbaya mara Saba kuliko yule asiyesoma.

Nikiwa Rais Wa nchi hii nitafuta kabisa Riba kwenye mabenki Yote na kufuta mabenki ya Kizungu. Tutaanzisha Benki yenye mifumo ya Kiafrika. MTU atakatwa gharama ya mifumo ya kibenki mwanzoni tu wakati Wa kuchukua mkopo. Baada ya Hapo tutakachoangalia ni kujenga mifumo ya kurejesha fedha Kwa uaminifu Ili wengine wapate na dhamana itaambatana na wadhamini ambao ni Wanachama kwenye mabenki popote Ndani ya nchi.

MTU yeyote atakayezembea kurejesha fedha za mkopo Wa Benki Atakua na hatia ya kifungo gerezani na kufilisiwa Mali ZAKE zote. Masharti yatakua ni makali sana Kwa ajili ya kuhakikisha watanzania wanakopeshwa fedha na kujiajiri Hasa wale wanaomaliza vyuo na kujiunga kwenye vikundi na kupata wadhamini na dhamana. Lakini Riba itakua ni 0% . Miradi watakayoanzisha au kuboresha Italipa Kodi na Hazina itakua na fedha za kuwalipa wafanyakazi Wa mabenki Yote kama zilivyo huduma nyingine za Jamii. Mifumo ya Sasa ya kibenki ni mifumo ya kishetani ya kuzifanya nchi za Afrika na waafrika wanaofanya KAZI za Halili kuendelea kuwa maskini na wanaokaa kwenye viyoyozi kuwaibia pesa zao na Jasho lao kama watumwa Wa mabenki.

Pakitokea Mzungu akataka kuanzisha Benki Basi hataruhusiwa kuwa na Riba inayozidi 5%.

Kilimo na ufugaji:
Kilimo na ufugaji vitaimarishwa sana Kwa kuwekwa mitaala ya kilimo kuanzia Shule ya Msingi SIO kusubiri mpaka watu waingie Sokoine Wakiwa Tayari wamejengeka dhana kichwani ya kuwa WAKULIMA ni wale watu maskini wasiosoma na waliokosa kazi ya kuajiriwa na kukaa Ofisini.

Kila Shule itatakiwa iwe na Bustani za mboga mboga Badala ya Maua na watalima wanafunzi wenyewe Tena kitaalam . Kila Darasa kitakua na aina ya mboga ya kulima na Maji ya mvua itakua ni lazima yavunwe kwenye mashule Yote na kuhifadhiwa kwenye matenki Kwa ajili ya umwagiliaji.
Ni marufuku Shule Kununua nyanya na mchicha NJE ya Shule.
Shule zote za sekondari na msingi kuanzia Darasa la Tano wataanza kujifunza masomo ya kilimo na ufugaji. Watakaokuwa wamevuna mazao Vizuri watayauza na kununuliwa Madafatari na kalamu na vifaa vifaa vingine Ili kuwaonyesha wengine kuwa kilimo ni Ajira ya uhakika na isiyo na masharti magumu zaidi ya kutumia Akili,Maji,Mbolea ,mbegu na ardhi.

Nitaimarisha sana Tume ya watumishi Wa umma Ili Kila atakayepata fursa ya kupewa uongozi basi aweke wazi Mali ZAKE . Na akificha halafu akatokea MTU anazijua mali zilizofichwa na mtumishi Wa umma basi Yule mtoa Taarifa atazawadiwa fedha taslimu Sh. Milioni Kumi au robo ya Mali zilizofichwa . Na Mali hizo zitataifishwa.

Kiujumla nitahakikisha Elimu inaendena na mazingira ya kitanzania na fursa zilizopo kabla ya kunifundisha Mtanzania masuala ya Uingereza na Ureno ni lazima kwanza awe ameshajua kuwa dhahabu inapatikanaje na rubi ikoje na inapatikana Mikoa Gani .

Nitahakikisha Kila MAHALI panapandwa miti ya kijani Badala ya miti ya asili yenye isiyo na kijani. Miti ya asili mingi ni miti yenye Hali ya ujangwa mana Haina rangi ya kijani.
Tutapanda Miti inayoota Kwa haraka na migumu Kama miarobaini, maembe , kachungwa , Minazi n.k.

Madaraja Yote ya vijijini yatajengwe Kwa haraka na Kwa kushirikiana na wafanyabiashara na wanakijiji wenyewe.
Haiwezekani watu wakajenga kanisa au msikiti Wa bil. Moja wanashindwa kushirikiana na Serikali kujenga Daraja la kupitisha mazao Yao na wao kupita. Hiii itasaidia kuharakisha maendeleo na kiwabana watakaohujumu miradi ya umma.

Nitarudisha masomo ya Dini mashuleni Kwa Ajili ya kutengeneza kizazi chenye ujuzi Sahihi Wa Dini wanazoabudu.Hivyo watakaosoma masomo ya Dini watapata fursa ya kuingia Chuo kikuu kama wanaosoma Historia na lugha n.k.
Ni ajabu kumnyima fursa MTU anayejua Islamic knowledge au Divinity kweda chuo kikuu wakati amesoma vitabu vyenye historia ya Sheria na hukumu ZAKE na namna ya kutengeneza ushahidi.

Masomo ya Dini kuwa miongoni Mwa sifa za kujiunga na vyuo vikuu yalifutwa wakati Wa Mkapa na kutoa Mwanya Wa kujenga kizazi kisichojua Umuhimu Wa maadili na ndicho kinachotusumbua Kwa Sasa.

Itakua ni mwiko kabisa Kununua magari ya kifahari Kwa watendaji WOTE Wa Serikali isipokuwa Kwa Rais ,Makamu Wa Rais na waziri mkuu ,Spika Wa Bunge na Jaji mkuu.
Wengine WOTE ni watendaji watakua na magari ya KAZI na ya Bei ya kawaida kama Land cruizer Hard top na asiyetaka atakua amejiondoa mwenyewe mana kuna wanaotamani NAFASI ya kuwatumikia watanzania Hata Kwa kutumia Rav 4
Hizi ni sera za Kijamaa ambazo zilishashindwa kitambo Sasa ukifanya tuu hivyo haitachukua round Uchumi utaporomoka na ukiporomoka ndio hapo Sasa sijui utapata wapi pesa za Kuendesha Nchi..

Hayo ukiyoyaeleza yanawezekana kama yatafanywa gradually ila wafanyabiashara/investors wakihisi hatari yeyote umekwisha broo maana watasitisha au kupunguza uwekezaji wao matokeo yake utaanza ku struggle Kuendesha Uchumi,waulize Wachina na Cuba..

Mwisho mambo hayo ya kupanda miti,mbogamboga yatakuwa na maana kama Watoto watakuwa wanakula wao shule Sasa sijui maji ya kufanya hayo everywhere yatatoka wapi na kama ni mvua itahitaji ujenzi wa miundombinu kitu ambayo ni pesa na hizo pesa unatoa wapi Kwa Sasa upeleke maji Kwa watu na zingine ujengee Water harvesting infrastructures huko kwenye mataasisi..

Eti Madaraja ya Vijijini yatajengwa na Wanavijiji,Kwa hiari au Kwa lazima? Na kama utaleta force account labda pesa ilipwe Kwa wanavijiji ila ikirudishwa Serikalini Kwa minajiri kwamba unaokoa gharama utaishia kuua sekta ya ujenzi kama Jiwe alivyofanya..

Mpaka hapa nimeona watu wanaweza kujifunza kwamba kumbe kuongea na kupayuka Kila mtu anaweza ila kwenye vitendo Sasa ni vitu viwili tofauti,Ruto na Yule Rais wa Zambia wanalijua hili vizuri Kwa Sasa.
 
Hapa mnaotaman kuwa viongozi tuone experience
Binafsi ningekuwa na Vipaombele vifuatavyo
1.Biashara na uwekezaji,hapa ningepunguza utitiri wa Kodi,tozo nk,
2.Utawala Bora,hapa ningeifanya ugatuaji wa madaraka kwenye Mikoa na ningebadili namna ya kuwapata hao viongozi Ili mambo mengine wafanye huko huko,
3.miundombinu hasa Barabara na Bandari ndio ningefungua Kila Kona,
4.Maji,
5.Elimu yenye mkazo kwenye Uvumbuzi,ufundi na Biashara
6.Maliasili eg Madini na Utalii
7.Kilimo na viwanda,hapa Ili kukupa incentives nikikupa leseni,nakupa grace period ya Kodi miaka 2 au zaidi Ili tuu niwe na uhakika wa Soko la mazao ya Kilimo na mifugo na hasa for exports
 
Back
Top Bottom