Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
HIVI UNAMCHUKULIAJE MTU WA NAMNA HII?
Anaandika, Robert Heriel
Hivi unamchukuliaje mtu ambaye kazaliwa mjini lakini hajasoma? Yaani kuna shule na vyuo vya kutosha lakini yeye hajasoma, yaani Hana hata elimu ya diploma wakati vyuo hivyo amezaliwa amevikuta. Hivi mtu wa namna hiyo unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu ambaye anajiita Muislam safi lakini haijui Quran na yupo comfortable 😂😂, au Mtu kujiita Mkristo Safi alafu hajui hata Biblia na wala hajui abc za Ukristo na yupo Comfortable kabisa. Hivi watu wanamna hii wewe unawachukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu anayejifanya anajua Sana kingereza na kujivunia nacho alafu wakati huohuo ukimuambie azungumze lugha mama yake hajui. Mtu WA namna hiyo unamchukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu anayeishi kijijini lakini Hana Shamba analolimiliki, mtu wa namna hiyo unamchukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu ambaye kavaa vizuri na yupo smart Kwa nje lakini mahali anapoishi ukiingia ndani utabaki mdomo wazi. Mtu wa hivyo unamchukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu kasoma mpaka degree na kahitimu vizuri lakini anakuambia Hana kazi. Na yupo comfortable kabisa. Unamchukuliaje? Je utaungana naye au utamuona katika jicho jingine?
Unamchukuliaje mtu anayeishabikia CCM alafu maisha yake ni dhoofu ilhali, yakifukara na yasiyo na matumaini. Unamchukuliaje mtu huyo?
Unamchukuliaje mtu anayekuona huna kazi ya maana lakini umemzidi kipato/maisha😂😂.
Yaani yeye anahangaika kila siku lakini maisha yake ni yaleyale.
Unamchukuliaje mtu ambaye anakuona mshamba, ananyuka viwalo na kujipenda lakini anakuja kukukopa kila iitwapo leo, au unamdai yeye au mke wake. Unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu anayejivunia kuishi mjini wakati huko mjini Hana la maana analolifanya zaidi ya kugeuzwa MSUKULE au mtumwa wa wenye navyo. Unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu unayemheshimu na kumuona anaakili lakini analishwa na mkewe. Au anaendeshwa endeshwa na mkewe?
Unamchukuliaje mtu anayeshauri watu namna ya kuwa Tajiri wakati huohuo yeye mlo mmoja tuu unamshinda. Mtu wa namna hiyo unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu ambaye anadharau makabila ya watu wengine au kudharau watu wengine ambao Wana sifa za ndugu zake au wazazi wake?
Mfano, mtu anadharau watu wasio na vipato au wenye kazi za kuvuja jasho ilhali mama yake mzazi au Baba au dada au Kaka zake wanafanya kazi hizohizo, mtu wa hivyo unamchukuliaje?
Mwisho, tuache kudharau wengine Kwa sababu za kijinga.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Hivi unamchukuliaje mtu ambaye kazaliwa mjini lakini hajasoma? Yaani kuna shule na vyuo vya kutosha lakini yeye hajasoma, yaani Hana hata elimu ya diploma wakati vyuo hivyo amezaliwa amevikuta. Hivi mtu wa namna hiyo unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu ambaye anajiita Muislam safi lakini haijui Quran na yupo comfortable 😂😂, au Mtu kujiita Mkristo Safi alafu hajui hata Biblia na wala hajui abc za Ukristo na yupo Comfortable kabisa. Hivi watu wanamna hii wewe unawachukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu anayejifanya anajua Sana kingereza na kujivunia nacho alafu wakati huohuo ukimuambie azungumze lugha mama yake hajui. Mtu WA namna hiyo unamchukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu anayeishi kijijini lakini Hana Shamba analolimiliki, mtu wa namna hiyo unamchukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu ambaye kavaa vizuri na yupo smart Kwa nje lakini mahali anapoishi ukiingia ndani utabaki mdomo wazi. Mtu wa hivyo unamchukuliaje?
Hivi unamchukuliaje mtu kasoma mpaka degree na kahitimu vizuri lakini anakuambia Hana kazi. Na yupo comfortable kabisa. Unamchukuliaje? Je utaungana naye au utamuona katika jicho jingine?
Unamchukuliaje mtu anayeishabikia CCM alafu maisha yake ni dhoofu ilhali, yakifukara na yasiyo na matumaini. Unamchukuliaje mtu huyo?
Unamchukuliaje mtu anayekuona huna kazi ya maana lakini umemzidi kipato/maisha😂😂.
Yaani yeye anahangaika kila siku lakini maisha yake ni yaleyale.
Unamchukuliaje mtu ambaye anakuona mshamba, ananyuka viwalo na kujipenda lakini anakuja kukukopa kila iitwapo leo, au unamdai yeye au mke wake. Unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu anayejivunia kuishi mjini wakati huko mjini Hana la maana analolifanya zaidi ya kugeuzwa MSUKULE au mtumwa wa wenye navyo. Unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu unayemheshimu na kumuona anaakili lakini analishwa na mkewe. Au anaendeshwa endeshwa na mkewe?
Unamchukuliaje mtu anayeshauri watu namna ya kuwa Tajiri wakati huohuo yeye mlo mmoja tuu unamshinda. Mtu wa namna hiyo unamchukuliaje?
Unamchukuliaje mtu ambaye anadharau makabila ya watu wengine au kudharau watu wengine ambao Wana sifa za ndugu zake au wazazi wake?
Mfano, mtu anadharau watu wasio na vipato au wenye kazi za kuvuja jasho ilhali mama yake mzazi au Baba au dada au Kaka zake wanafanya kazi hizohizo, mtu wa hivyo unamchukuliaje?
Mwisho, tuache kudharau wengine Kwa sababu za kijinga.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam