Mwanamke ameajiriwa taasisi binafsi, anaingia saa moja asubuhi anatoka saa kumi na dk 40 jioni, akirudi nyumbani mume anataka apikiwe, mpaka afike kwake ni saa kumi na mbili jioni akirudi apike yaani akae jikoni apike ugali, afue uniform zake, mume aje wale walale.
Mume hana shughuli yoyote anajilimia zake bustani za mboga mboga lakini hashughuliki na chochote cha nyumbani, choo anachotumia had aje adeki mke, chumba anacholala chilia mbali nyumba kuipitisha fagio ni mwiko, nyasi zikiota bibie ajipinde mgongo alime?